Zainul Mzihge,
Usikubari taarifa yoyote ile kuhusu kupungua ukeketaji mpaka iwe imekamilika kukuonyesha mbinu ya utafiti iliyotumika. Ukeketaji kupungua inawezekana lakini inaweza kuwa hadithi za alinacha. Kuna hoja nyingi yafuatayo:
(i) Aina ya utafiti uliofanyika ulioonyesha kuwa ukeketaji umepungua. Amethibitishaje kwa kutumia mbinu hiyo ya utafiti? Amehoji makundi ya ngariba wakamwambia hawakeketi au amehoji wanawake au wasichana wakamwambia hawajakeketwa (respondent biased research). Na ni wa umri gani? Hii itakupa majibu ya uongo False Negative kumbe ni positive kakeketwa ila mila haimruhusu kukubali na pia anaogopa sheria na ni aibu kumwambia mtu mwingine si wa mila yako kuwa umekeketwa ukijua mila hii haikubaliki na wengine na serikali pia.Ngariba anaogopa sheria kama atasema bado anaendelea kukeketa na kukupa idadi ya aliowakeketa kijijini au makisio ya wangapi kwa mwaka hapo alipo na kwingineko.
(ii) Unaweza ukahoji kundi la wanaokeketwa na ngariba ukapata False Positive results (wamekubali kukeketa na kukeketwa lakini sio kweli kwa wote). Wapo wanaotegemea kama akisema ndio nimekeketwa au ninakeketa kutokana na kipato ninapata hela, mbuzi, nguo kama malipo nikikeketa na kutambulika na kuheshimiwa kimila. Nikiacha sina pa kupata pesa. Anasema YES ili awemo katika kundi la kupata msaada unaokuja na serikali kama muathirika aliyekeketwa au mkeketaji wapewe hela za ujasiriamali. Kwa Ngariba wengine hata akisema ameacha kukeketa na kukabidhi vifaa vya ukeketaki-MUONGO, anavyovingine kaficha nyumbani au kiunoni kwa mila nyingine.Anaendelea kukeketa. Tunasema ukeketaji umeisha lakini wakienda kuzaa hata umri mdogo-wamekeketwa.
Katika mila nyingine ngariba wa Kike huvaa kiunoni visu au vifaa vyake vya aina yake aliyonayo iwe kisu, kibati, kisu gome, mkasi, nyembe etc kwani mtu akikitia uchawi (Imani zao) kila anayemkeketa au kumtahiri atakufa. Ukimkuta mtoni anaoga-cha kwanza hakimbilii chupu au nguo ajisetiri bali ni kukimbilia mkanda wake wa kuvaa kiunoni wenye kisu na dawa za kukeketea. Kuna binadamu waongo. Alikabidhiwa kazi ya ungariba kama mwanamke au mwanaume kwenye mizimu na mikoba ya mila. Kuacha anaogopa mizimu itamdhuru (Kwa wale wenye mila hizo). Hurithishana babu, mwana na wajukuu. Au Bibi, mtoto, mjukuu, kilemwbwe. Ni ukoo wa mangariba au wakeketaji au ukoo wa uganga wa aina fulani ya matibabu kwa wanawake, wanaume, au wa jumla. Kuna paediatricians, gynaecologists, waganga wa wanaume na waganga wa mifupa, pumu, vichwa kuuma aina mbalimbali hatamigraine, ulemavu na ganzi, kufunga choo etc. Kila ngariba mke au mume ana mganga wake ambae humsaidia kazi zake na madawa ya vidonda. Wengine wanaokeketwa walishaanza ngono wana magonjwa mbali mbali na madonda kuharibika mganga huja kuwatibu. Uchafu wa mazingira na nguo wavaazo huwapa fungus mganga huja kumletea dawa.
(iii). Kuhoji aliyekeketwa na mumewe kama kaolewa au ana mwenza na kuhoji watoto na kumuhoji mzazi wake pia. Ina maana unaunganisha respondents. Dodoso yako unaiweka namba na code ya muunganisho. List ya watoto anakupa na unamuuliza mzazi kati ya hao nani kakeketwa kwa wanawake. Ukienda shule kuwahoji alishakwambia wanasoma shule gani na darasa gani unaita watoto wa kuhoji unampata na kuweka note ya jina la wazazi atakutajia. Unamuuliza kama kakeketwa kisha unaangalia kulinganisha na wazazi walivyosema. Kituko utakachokipata ni kwamba-Wazazi huwa wakweli kwa vile ni watu wazima hawana woga wanajua mengi wanayowafundisha watoto ni uongo (asipokeketwa hataolewa, hatozaa, mizimu itamdhuru etc). watoto wanazingatia hayo kuwa akisema kakeketwa atadhurika hiyo ni mila na ni siri kwa makabila yanayotahiri kwa kificho sio yale yanayotahiri wasichana hadharani. False negative itakuwa stastically significant different. Wazazi watasema watoto wao wametahiriwa 50% watoto husika hawatosema wametahiriwa wachache tu watasema wametahiriwa 3-8% mpishano wa asilimia 3-50 (47%) ni mkubwa mno. Watoto wanasema uongo kiasi kikubwa kuliko wazazi.
(iv) Kabla sijajaza kurasa kama kawaida yangu (Soma tu kama unaona ya maana wacha kusoma kama unaona kuonglea ukeketaji ni ujinga) ni kwamba Methodology ya maana (kuacha nyingine zilizopo) ni Patient Blind Research Methodology. Hii ni medical research. Baada ya kufanya Interview ya Respondents wa kabila, mila me na ke umri mbali mbali na walioolewa, kuhoji wakunga wa jadi, wazee wa mila etc-ni kutumia madaktari au wauguzi kuchunguza FGM wanapopima Watoto wa Kike umri mbali mbali, kuchunguza Wanawake watu wazima umrimbali mbali wakati wanapimwa hospitali wanapokwenda kupata matibabu. Unakuwa na fomu ambayo inaonyesha Umri, jinsia, Kabila, kijiji anakoishi, Elimu yake, Ndoa na kabila la wazazi au mume kama kaolewa. utajaza aina ya ukeketaji aliofanyiwa kama kakeketwa (manual za aina hiyo zipo muuguzi awe ameshafundishwa kuziainisha au kuzijua). SIRI. Mgonjwa asijue kama anachunguliwa uke kutafitiwa kama kakeketwa. Mradi amesema huko chini kuna matatizo anaumwa na itabidi ukuangalie, utamuangalia (Chungu kaona kivuno-utapata nafasi ya utafiti). Anayepima Mama wajawazito na watoto budi amuangalie mama chini na kuwapekua watoto wanaokwenda kliniki-hii ni rahisi kwake maana budi waangaliwe kiafya Atajaza kadi na fomu yake ya utafiti. Kama mgonjwa atakuwa mcheshi, huru, asijejali na kuongelea mambo unayoyaona basi utapata nafasi ya kumuuliza yeye mzaramo lakini mbona kapitia hiyo tohara? Atakueleza kwa nini. Mwingine wakati wa kuzaa atapata matatizo atakwambia usimshone baada ya kumuongeza njia kwani kakeketwa anapata tabu kila anapozaa anaongezwa njia basi mwache apone hivyo donda hilo likishonwa atakuja kukatwa tena usimshone! huwa wanawaambia wauguzi hivyo eti litajiunga lenyewe tu. Patiend Bliend Reserch itakupa Exact number ya FGM kwa umri wa wanawake. Hii itakuwa tofauti sana na respondent interview 80-100% ya wanawake watu wazima na wasichana watakuwa wamekeketwa wale wa mila za FGM na 50-82% ya wasio na mila ya ukeketaji Wameketwa. Ukiangalia uwepo wa ukeketaji kuanzia miradi yako ya kutokomeza ukeketaji uone kama kuna MABADILIKOOOO!- Budi uangalie WALE WALIOZALIWA wakati wewe UMEANZIISHA MRADI NA MIAKA KADHAA tumeme10 BAADA ya Mradi au elimu ya kuacha ukeketaji. Kwani wale wa umri wa kukeketa na akina mama watu wazima walishakuwa wamekeketwa! Ukeketaji utawezaje kshuka wakati mijitu mizima na wasichana walisha kupitia mila? Lazima itakuwa 75% plus waliokeketwa. Umemuhoji nani au wale wale na ndio uliwachungulia pia lakini hao miaka yote hiyo wapo hivyo? Labda mimi Elimu yangu ya research haifai!
Inafaa -Cross-tabulate vitu na weka trends kwa umri pale ambapo elimu ilianza kwa kuchukua makundi ya waliozaliwa wakati huo wakakua kufika umri fulani ili uangalie Impact kwa hao wapya waliolelewa na wazazi walioelimishwa.
Utaweza kukuta FGM ktk famila moja watoto wakike wapoi ambao hawakukeketwa na wapo waliokeketwa kutokana na -ndoa za makabila mchanganyiko. Wazazi hugawana watoto kila mmoja akacheze kwao. Yule wa mila ya kukeketa anamkeketa wa mila siyo anamcheza tu hamkeketi hana mila hiyo. Waliokeketwa mila si yao-Mchumba, mume, wakwe wamemwoma akeketwe ili kulida hadhi ya familia. Akina wifi ndio influential sana. Mwingine -kakeketwa na nurse aliyelipwa hela wakati wa kujifungua amkate. yeye anaona anaongezwa njia azae au anasikia uchungu wa kuzaa tu sio wa kukeketwa. Wapo waliowengi vijijini ambako huduma ya afya si nzuri ukeketaji ni medical solution. Kwamba hao hawana mila ya ukeketaji-ila aliumwa magonjwa ya chini fungus akavimba sana, gono na mavidonda chini, vagina warts (madole yalitoka katika labias yanatisha haya) gynaecologist akamwambia aende kwa ngariba wa kike akayaondoe hayo ya nje. Hivyo, wengi wa mila isiyotahiri waliotahiriwa/kukeketwa wasio an mila hiyo ni kutokana na sio ndoa za mchanganyiko makabila bali na kukosa matibabu husika ya magonjwa ya chini. Lakini hata akikikeketwa kuondoa fungus, vagina warts-bado ndani ya damu,maumbile ya ndani ya uke maradhi hayo yapo na partner ataathirika nayo.
Kwa Hiyo kwenye FGM kwa wahojiwa kuna Over-reporting, Under-reporting and Correctly reporting. Hivyo-Tanzania isijidanganye na FGM kupungua popote pale bila ya Patient Blind Research. Pia, kutokana na uchafu wa mazingira watu kuoga maji machafu, wasichana na wamama kuvaa matambara machafu, michepuko, ndoa za makabila tofauti kuongezeka, utaalamu na vifaa vya kukatia hata ganzi kuwepo, njaa ya madaktari na wauguzi, usafiri kuwepo na wanawake kuwa na uwezo wa kumleta ngariba DSM au miji mingine aje kukeketa kisiri (hata Ulaya watu huchangizana na Ngariba Ke akaenda kukeketa)-FGM inaweza kuwa imeenea kwani inatumika kama Preventive method ya magonjwa kama haya unayoyaona ktk picha moja attached. Kama huna external genitalia yataota wapi? FGM inatumika kama Alternative Treatment ya Infectious Diseases za kwenye uke-ona ugonjwa wa madole yalivyojaa ukeni. Bila ya kufanya zahanati, vituo vya Afya na District Hospitals hasa kutibu maradhi ya sehemu za siri kwa kuwa na dawa za kumeza na kupaka-FGM itaendelea kwani uchafu wa mazingira na michepuko vimeongezeka. Na FGM imeanza baada ya hunting and gathering cultur watu walipoanza kilimo na ufugaji. wakangudua sio tu kuzuia maradhi bali pia kukata na kushona uke kuzuia kubakwa na kuanza zinaa mapema. Pharaonic Circumcision kwa wanawake. Unakatwa, unashonwa. Kwa Misri-anayekeketa ni KINYOZI wa NYWELE.
Fika WRDP NGO- Mlalakua DSM P.O BOX 35108 DSM- tumefanya tafiti hizi za FGM, tumewakilisha haya mikutano ya FGM na ya Wizara ya maendeleo na kusambaza makala zetu isipokuwa sio wote wanaokubali tuelezayo kuwa-lazima elimu ya madhara ya FGM itolewe kwa wote, Mfumo wa afya uboreshwe kutibu maradhi husika yanayosababisha watu wakeketwe, usafi wa mwili na mazingira, vivalo vya chini ndio kwa wasichana na wanawake viwe nadhifu ndipo maradhi hayo yapungue. Hata mijini ukekeaji hufanyika kama tiba. Elimu ya FGM itolewe kwa wanaume wa mila za kukeketa sio kwa ngariba tu kwani huko ndio wenye Fistula waliowengi (wamama na visichana waolewao umri mdogo ni wengi hutokea) na kuhudumiwa CCBRT na kwingineko kushonwa VVF na RVF.
Adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzie-wamama wa kimasai, kigogo na makabila mengine wanaokeketa-huvinyosoa vidoto vya kike ukeni vikiwa vichanga ili wasishitakiwe na wasichana wakikeketwa kwa nguvu wakiwa wakubwa hutoa siri kwa mwalimu shuleni au kwa NGO (baadhi yao) na waliowatendea hivyo kushitakiwa. Mzazi asiyetaka mwanae akeketwe0shangazi hufanya mpango wa siri. Akienda likizo kwao anakamatwa kwa nguvu anakeketwa. Ngariba kuvizia watoto wakiwa shamba kuwakamata na kukeketa na kuwatoza waazzi faini. Mzazi akitaka kushitaki-anatishiwa uchawi na mkunga na wazee wa mila watatambika adhurike na anaaibisha ukoo na kabila kwa kutokeketa. Mizimu inagoma mengi kutokana na tabia yake hiyo. Imani potufu zinatumika kuhalalisha udhalilishaji huu. Bado tuna mengi ya kufanya sio Loliondo tu bali nchi nzima.
KAMA KAWA.
--------------------------------------------
On Fri, 13/11/15, zainul mzige <zainul.mzige21@gmail.com> wrote:
Subject: [wanabidii] UKEKETAJI WAPUNGUA WILAYA YA NGORONGORO
To:
Date: Friday, 13 November, 2015, 8:06
Habari za asubuhi
tena,
Tafadhali pokea CODES hapa chini
<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0842.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150508"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0842.jpg"
alt="IMG_0842" width="640"
height="427" /></a><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000080;"><em><strong>Mwakilishi wa
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro
ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii, Teresia Irafay
akifungua warsha ya wiki moja ya mafunzo juu ya elimu ya
Afya ya Uzazi na Maadili iliyojumuisha wakunga wa Jadi,
Waganga wa tiba asili, viongozi wa dini, waandishi wa habari
na wahamasishaji afya jamii iliyowaleta pamoja wadau
mbalimbali katika ngazi ya vitongoji, vijiji na wilaya
kujifunza namna ya kufanya kazi shirikishi ili kuleta
mabadiliko katika jamii inayofanyika katika hoteli ya
Domel-Wasso, tarafa ya Lolilondo katika wilaya ya Ngorongoro
mkoani Arusha. (Picha zote na Zainul Mzige wa <span
style="color: #0000ff;"><a
style="color: #0000ff;" href="http://www.modewjiblog.com">Modewjiblog</a></span>).</strong></em></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Na
Mwandishi wetu,
Loliondo</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>IDADI ya
wanawake wanaokeketwa Loliondo wilaya ya Ngorongoro
imepungua kufikia asilimia 75 kwa mwaka
huu.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Hayo
yameelezwa na Mratibu wa Afya ya Uzazi na Mtoto, Loliondo,
Bi. Nailejileji Joseph katika mahojiano maalum na mwandishi
wa habari hii kwenye warsha ya wiki moja ya mafunzo juu ya
Elimu ya Afya ya Uzazi na
Maadili.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Warsha
hiyo inajumuisha wakunga wa Jadi, Waganga wa tiba asili,
viongozi wa dini, waandishi wa habari na wahamasishaji afya
jamii.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Wadau hao
wanatoka ngazi mbalimbali ya vitongoji, vijiji na
wilaya.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Lengo la
warsha hiyo ni kujifunza namna ya kufanya kazi shirikishi
ili kuleta mabadiliko sahihi katika jamii inayofanyika
katika hoteli ya Domel-Wasso, tarafa ya Lolilondo katika
wilaya ya Ngorongoro mkoani
Arusha.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Bi
Nailejileji alisema idadi ya ukeketaji Loliondo inaonyesha
kupungua hadi kufikia 57% mwaka 2015 ikilinganishwa na 87%
mwaka 2014 kwa wanawake waliojifungulia
hospitalini.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Alisema
kwamba matokeo hayo yamefanikiwa kutokana na mkakati maalum
unaofanyika shuleni kwa kuanzisha vituo vya kirafiki kwa
vijana vinavyolenga kutoa elimu na hamasa kuhusu masuala ya
ukeketaji.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Aidha
mafanikio hayo ni miongoni mwa jitihada za Shirika la Elimu,
Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kueneza hamasa shirikishi
katika jamii, kuelezea ukubwa wa tatizo, athari zinazotokana
na ukeketaji kwa kuwashirikisha wazee wa kimila wa jamii ya
Kimasai (Laigwanan) kuchukua hatua zipasazo kukomesha
ukatili huu dhidi ya
wasichana.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0843.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150509"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0843.jpg"
alt="IMG_0843" width="640"
height="427"
/></a></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Wazee wa
kimila wa kimasai ni watu wenye kuheshimika na kusikilizwa
kwenye jamii pale wanapotoa matamko mbalimbali yanayopelekea
kuleta mabadiliko katika jamii ambao wanaonekana kuwa na
uwezo mkubwa katika kukomesha ukeketaji na ndoa za utotoni
kwa watoto wa kike ambao huozwa baada ya kufanyiwa ukeketaji
mwezi Desemba kila
mwaka.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000000;"><strong>Changamoto hizo zinachangiwa
kwa kiasi kikubwa na kile kilichoonekana na washiriki kuwa
ni mila na tamaduni zilizojengeka katika jamii ya Kimasai
kwa vijana kupokea amri kutoka kwa wazazi wao hata kama
jambo hilo halina tija katika
jamii.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000000;"><strong>Wakichangia dhana ya mtoto
na kijana ni nani, majukumu yao na wana haki gani katika
jamii, wadau hao wa jamii ya kimasai walisema kuwa mtoto ni
kati ya umri 0-18 na kijana ni yule anayeanzia miaka
18-35.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000000;"><strong>Wakizungumzia kuhusu haki
walisema kwamba mtoto ana haki za kupata huduma muhimu kama
kupata elimu, kupata matunzo bora, kuishi kwa usalama au
kulindwa, kuwa na afya bora na kuheshimiwa mawazo
yake.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Lakini ,
hata hivyo walisema kwamba, kutokana na tamaduni
iliyojengeka miongoni mwa vijana kujifunza na kuiga malezi
kutoka kwa wazazi wao, imekuwa ni changamoto kubwa
kuhamasisha vizazi kupiga vita mila na desturi
zinazoathiri
wanawake.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0854.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150511"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0854.jpg"
alt="IMG_0854" width="640"
height="427"
/></a></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000080;"><em><strong>Afisa Elimu ya
Afya na Ukimwi kutoka Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni
(UNESCO), Mathias Herman akizungumza kwenye warsha ya wiki
moja ya mafunzo juu ya Elimu ya Afya ya Uzazi na Maadili
iliyojumuisha wakunga wa jadi, waganga wa tiba asili,
viongozi wa dini, waandishi wa habari na wahamasishaji afya
jamii iliyowaleta pamoja wadau mbalimbali katika ngazi ya
vitongoji, vijiji na wilaya kujifunza namna ya kufanya kazi
shirikishi ili kuleta mabadiliko katika jamii inayofanyika
katika hoteli ya Domel-Wasso, tarafa ya Lolilondo katika
wilaya ya Ngorongoro mkoani
Arusha.</strong></em></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Hata
hivyo walisema pamoja na kwamba mabadiliko huchukua muda
mrefu, lakini yanaweza kufanikiwa ikiwa wanawake wa kimasai
wenyewe watayavalia njuga masuala yanayowahusu katika jamii
na yanayohatarisha maisha
yao.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong> "Ndio
mila na tamaduni zipo na kuna msemo unaosema kwamba mkataa
kwao ni mtumwa, lakini zipo tamaduni ambazo ni hatarishi na
anayeathirika kwa kiasi kikubwa ni wanawake na
wasichana,"alisema Nailejileji
Joseph.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Mazingira
waliyokulia Wanawake wa jamii ya Kimasai yamejenga ukimya
miongoni mwao na kuona kwamba changamoto zozote zinazotokea
ni jambo la kawaida na
hazizungumziki.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Kwa mfano
ndoa za utotoni kwa wasichana wa Kimasai ni mwendelezo wa
tamaduni hatarishi unaotokana na majukumu ya mtoto au kijana
katika jamii ya kupokea anachoamrishwa na wazazi bila
kuelewa athari zinazoweza kumpata mtoto wa kike wa jamii
hiyo.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_08491.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150523"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_08491.jpg"
alt="IMG_0849" width="640"
height="427"
/></a></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>"Mimi
nalea mjukuu na binti yangu yaani mama wa huyu mjukuu. Binti
yangu amepata ulemavu wa maisha baada ya kujifungua huyu
mtoto akiwa na umri wa miaka 13,"alisema Bi. Noorkidemi
Kitupei mkazi wa kijiji cha Ilopolum, tarafa ya Loliondo.
Binti huyu (jina linahifadhiwa) ni mke wa tatu kuolewa na
mume wake akiwa katika umri mdogo baada ya baba yake
kuamrisha
aolewe.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000000;"><strong>Changamoto nyingine kama
hiyo ilimpata binti mmoja wa kimasai aliyeolewa akiwa na
umri wa miaka 13 baada ya kupigwa na kuumizwa mkono na
kuachiwa kovu kubwa sana na mumewe baada ya Ngómbe mmoja wa
mume wake kupotea, mume wake alichukua jukumu la kumpiga
karibia kumpa ulemavu wa mkono baada ya kumuuliza binti huyo
kwanini Ngómbe huyo amepotea na kujibiwa kwamba alikuwa
amelala.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color: #000000;"><strong>Kwa
mujibu wa Mratibu huyo wa afya ya uzazi visa kama hivyo
vinaendelezwa kwa sababu hamasa bado ni ndogo katika jamii
ya kimasai na wadau wachache wanaobahatika kupata mafunzo au
kwa woga unaotokana na muendelezo wa tamaduni hatarishi
zimekuwa hazihamasishwi na haziwafikii
walengwa.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000000;"><strong>Inategemewa kwamba kituo cha
redio cha jamii Loliondo FM kitatoa mchango mkubwa wa
kuhamasisha jamii masuala mbalimbali ya kijamii na
kimaendeleo.</strong></span></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0856.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150513"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0856.jpg"
alt="IMG_0856" width="640"
height="427"
/></a></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000080;"><em><strong>Mtaalamu wa
Masuala ya Vyombo vya Habari Jamii na Mkufunzi kutoka
Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose
Haji Mwalimu (katikati) akiteta jambo na Mwakilishi wa
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro
ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii, Teresia Irafay
(kulia) wakati warsha hiyo ikiendelea. Kushoto ni Afisa wa
UNESCO, Hamidun
Kweka.</strong></em></span></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0923.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150515"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0923.jpg"
alt="IMG_0923" width="640"
height="427"
/></a></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000080;"><em><strong>Pichani ni
mjumuiko wa wakunga wa Jadi, Waganga wa tiba asili, viongozi
wa dini, waandishi wa habari na wahamasishaji afya jamii
wanaohudhuria warsha hiyo inayoendelea wilayani
Ngorongoro.</strong></em></span></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0887.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150518"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0887.jpg"
alt="IMG_0887" width="640"
height="427"
/></a></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0868.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150519"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0868.jpg"
alt="IMG_0868" width="640"
height="427"
/></a></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0892.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150516"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0892.jpg"
alt="IMG_0892" width="640"
height="427"
/></a></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000080;"><em><strong>Afisa Elimu ya
Afya na Ukimwi kutoka Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni
(UNESCO), Mathias Herman (wa pili kushoto) akiendesha
mafunzo ya uelewa juu ya dhana ya Utamaduni kwa mifano hai
katika warsha hiyo ya wiki inayofanyika katika hoteli ya
Domel-Wasso, tarafa ya Lolilondo katika wilaya ya Ngorongoro
mkoani Arusha. Kushoto ni Mshiriki ambaye ni mkalimani wa
lugha ya kimasai, Joseph Ndaika na kulia ni wanawake wa
kimasai wanaoshiriki warsha
hiyo.</strong></em></span></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_1035.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150517"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_1035.jpg"
alt="IMG_1035" width="640"
height="427"
/></a></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000080;"><em><strong>Mtaalamu wa
Masuala ya Vyombo vya Habari Jamii na Mkufunzi kutoka
Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose
Haji Mwalimu (kulia) akifafanua jambo kwa washiriki wakati
wa kuhakiki kazi za vikundi katika warsha hiyo inayoendelea
wilayani Ngorongoro mkoani
Arusha.</strong></em></span></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0957.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150520"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0957.jpg"
alt="IMG_0957" width="640"
height="427"
/></a></p><p
style="text-align: center;"><span
style="color:
#000080;"><em><strong>Washiriki wa
warsha hiyo wakiwa kwenye kazi za
vikundi.</strong></em></span></p><p
style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0975.jpg"><img
class="aligncenter size-full wp-image-150522"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/11/IMG_0975.jpg"
alt="IMG_0975" width="640"
height="427" /></a></p>
KAWAIDA
Mwakilishi wa
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro
ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii, Teresia Irafay
akifungua warsha ya wiki moja ya mafunzo juu ya elimu ya
Afya ya Uzazi na Maadili iliyojumuisha wakunga wa Jadi,
Waganga wa tiba asili, viongozi wa dini, waandishi wa habari
na wahamasishaji afya jamii iliyowaleta pamoja wadau
mbalimbali katika ngazi ya vitongoji, vijiji na wilaya
kujifunza namna ya kufanya kazi shirikishi ili kuleta
mabadiliko katika jamii inayofanyika katika hoteli ya
Domel-Wasso, tarafa ya Lolilondo katika wilaya ya Ngorongoro
mkoani Arusha. (Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).Na Mwandishi wetu,
LoliondoIDADI ya wanawake
wanaokeketwa Loliondo wilaya ya Ngorongoro imepungua kufikia
asilimia 75 kwa mwaka huu.Hayo yameelezwa na Mratibu
wa Afya ya Uzazi na Mtoto, Loliondo, Bi. Nailejileji Joseph
katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hii kwenye
warsha ya wiki moja ya mafunzo juu ya Elimu ya Afya ya Uzazi
na Maadili.Warsha hiyo inajumuisha
wakunga wa Jadi, Waganga wa tiba asili, viongozi wa dini,
waandishi wa habari na wahamasishaji afya
jamii.Wadau hao wanatoka ngazi
mbalimbali ya vitongoji, vijiji na
wilaya.Lengo la warsha hiyo ni
kujifunza namna ya kufanya kazi shirikishi ili kuleta
mabadiliko sahihi katika jamii inayofanyika katika hoteli ya
Domel-Wasso, tarafa ya Lolilondo katika wilaya ya Ngorongoro
mkoani Arusha.Bi Nailejileji alisema
idadi ya ukeketaji Loliondo inaonyesha kupungua hadi kufikia
57% mwaka 2015 ikilinganishwa na 87% mwaka 2014 kwa wanawake
waliojifungulia hospitalini.Alisema kwamba matokeo
hayo yamefanikiwa kutokana na mkakati maalum unaofanyika
shuleni kwa kuanzisha vituo vya kirafiki kwa vijana
vinavyolenga kutoa elimu na hamasa kuhusu masuala ya
ukeketaji.Aidha mafanikio hayo ni
miongoni mwa jitihada za Shirika la Elimu, Sayansi na
Utamaduni (UNESCO) kueneza hamasa shirikishi katika jamii,
kuelezea ukubwa wa tatizo, athari zinazotokana na ukeketaji
kwa kuwashirikisha wazee wa kimila wa jamii ya Kimasai
(Laigwanan) kuchukua hatua zipasazo kukomesha ukatili huu
dhidi ya wasichana.Wazee wa kimila wa kimasai
ni watu wenye kuheshimika na kusikilizwa kwenye jamii pale
wanapotoa matamko mbalimbali yanayopelekea kuleta mabadiliko
katika jamii ambao wanaonekana kuwa na uwezo mkubwa katika
kukomesha ukeketaji na ndoa za utotoni kwa watoto wa kike
ambao huozwa baada ya kufanyiwa ukeketaji mwezi Desemba kila
mwaka.Changamoto hizo
zinachangiwa kwa kiasi kikubwa na kile kilichoonekana na
washiriki kuwa ni mila na tamaduni zilizojengeka katika
jamii ya Kimasai kwa vijana kupokea amri kutoka kwa wazazi
wao hata kama jambo hilo halina tija katika
jamii.Wakichangia dhana ya mtoto
na kijana ni nani, majukumu yao na wana haki gani katika
jamii, wadau hao wa jamii ya kimasai walisema kuwa mtoto ni
kati ya umri 0-18 na kijana ni yule anayeanzia miaka
18-35.Wakizungumzia kuhusu haki
walisema kwamba mtoto ana haki za kupata huduma muhimu kama
kupata elimu, kupata matunzo bora, kuishi kwa usalama au
kulindwa, kuwa na afya bora na kuheshimiwa mawazo
yake.Lakini , hata hivyo
walisema kwamba, kutokana na tamaduni iliyojengeka miongoni
mwa vijana kujifunza na kuiga malezi kutoka kwa wazazi wao,
imekuwa ni changamoto kubwa kuhamasisha vizazi kupiga vita
mila na desturi zinazoathiri
wanawake.Afisa Elimu ya Afya
na Ukimwi kutoka Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni
(UNESCO), Mathias Herman akizungumza kwenye warsha ya wiki
moja ya mafunzo juu ya Elimu ya Afya ya Uzazi na Maadili
iliyojumuisha wakunga wa jadi, waganga wa tiba asili,
viongozi wa dini, waandishi wa habari na wahamasishaji afya
jamii iliyowaleta pamoja wadau mbalimbali katika ngazi ya
vitongoji, vijiji na wilaya kujifunza namna ya kufanya kazi
shirikishi ili kuleta mabadiliko katika jamii inayofanyika
katika hoteli ya Domel-Wasso, tarafa ya Lolilondo katika
wilaya ya Ngorongoro mkoani
Arusha.Hata hivyo walisema pamoja
na kwamba mabadiliko huchukua muda mrefu, lakini yanaweza
kufanikiwa ikiwa wanawake wa kimasai wenyewe watayavalia
njuga masuala yanayowahusu katika jamii na yanayohatarisha
maisha yao. "Ndio mila na tamaduni
zipo na kuna msemo unaosema kwamba mkataa kwao ni mtumwa,
lakini zipo tamaduni ambazo ni hatarishi na anayeathirika
kwa kiasi kikubwa ni wanawake na wasichana,"alisema
Nailejileji Joseph.Mazingira waliyokulia
Wanawake wa jamii ya Kimasai yamejenga ukimya miongoni mwao
na kuona kwamba changamoto zozote zinazotokea ni jambo la
kawaida na hazizungumziki.Kwa mfano ndoa za utotoni
kwa wasichana wa Kimasai ni mwendelezo wa tamaduni hatarishi
unaotokana na majukumu ya mtoto au kijana katika jamii ya
kupokea anachoamrishwa na wazazi bila kuelewa athari
zinazoweza kumpata mtoto wa kike wa jamii
hiyo."Mimi nalea mjukuu na
binti yangu yaani mama wa huyu mjukuu. Binti yangu amepata
ulemavu wa maisha baada ya kujifungua huyu mtoto akiwa na
umri wa miaka 13,"alisema Bi. Noorkidemi Kitupei mkazi wa
kijiji cha Ilopolum, tarafa ya Loliondo. Binti huyu (jina
linahifadhiwa) ni mke wa tatu kuolewa na mume wake akiwa
katika umri mdogo baada ya baba yake kuamrisha
aolewe.Changamoto nyingine kama
hiyo ilimpata binti mmoja wa kimasai aliyeolewa akiwa na
umri wa miaka 13 baada ya kupigwa na kuumizwa mkono na
kuachiwa kovu kubwa sana na mumewe baada ya Ngómbe mmoja wa
mume wake kupotea, mume wake alichukua jukumu la kumpiga
karibia kumpa ulemavu wa mkono baada ya kumuuliza binti huyo
kwanini Ngómbe huyo amepotea na kujibiwa kwamba alikuwa
amelala.Kwa mujibu wa Mratibu huyo
wa afya ya uzazi visa kama hivyo vinaendelezwa kwa sababu
hamasa bado ni ndogo katika jamii ya kimasai na wadau
wachache wanaobahatika kupata mafunzo au kwa woga unaotokana
na muendelezo wa tamaduni hatarishi zimekuwa hazihamasishwi
na haziwafikii walengwa.Inategemewa kwamba kituo
cha redio cha jamii Loliondo FM kitatoa mchango mkubwa wa
kuhamasisha jamii masuala mbalimbali ya kijamii na
kimaendeleo.Mtaalamu wa Masuala
ya Vyombo vya Habari Jamii na Mkufunzi kutoka Shirika la
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu
(katikati) akiteta jambo na Mwakilishi wa Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia
ni Afisa Maendeleo ya Jamii, Teresia Irafay (kulia) wakati
warsha hiyo ikiendelea. Kushoto ni Afisa wa UNESCO, Hamidun
Kweka.Pichani ni mjumuiko
wa wakunga wa Jadi, Waganga wa tiba asili, viongozi wa dini,
waandishi wa habari na wahamasishaji afya jamii
wanaohudhuria warsha hiyo inayoendelea wilayani
Ngorongoro.Afisa Elimu ya Afya
na Ukimwi kutoka Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni
(UNESCO), Mathias Herman (wa pili kushoto) akiendesha
mafunzo ya uelewa juu ya dhana ya Utamaduni kwa mifano hai
katika warsha hiyo ya wiki inayofanyika katika hoteli ya
Domel-Wasso, tarafa ya Lolilondo katika wilaya ya Ngorongoro
mkoani Arusha. Kushoto ni Mshiriki ambaye ni mkalimani wa
lugha ya kimasai, Joseph Ndaika na kulia ni wanawake wa
kimasai wanaoshiriki warsha hiyo.Mtaalamu wa Masuala
ya Vyombo vya Habari Jamii na Mkufunzi kutoka Shirika la
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu
(kulia) akifafanua jambo kwa washiriki wakati wa kuhakiki
kazi za vikundi katika warsha hiyo inayoendelea wilayani
Ngorongoro mkoani Arusha.Washiriki wa warsha
hiyo wakiwa kwenye kazi za
vikundi.
--
Zainul A.
Mzige,Operation
Manager,MO BLOG,www.modewjiblog.com+255714940992.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 comments:
Post a Comment