Friday, 6 November 2015

Re: [wanabidii] HONGERA UKAWA MPEIPA NCHI SOMO

Mashaka Makama,
Nakukushukuru sana kwa kusoma andiko langu:
Hata hivyo ili niweze kukujibu swali uliloniuliza endapo mimi ni mwanaharakati au mwanasiasa nahitaji kwanza unieleze kwa mtazamo wako:
1) Mwanaharakati ni nani?
2) Mwanasiasa ni nani?
3) Uchochezi ni nini?
4) Je andiko langu lina uchochezi gani?
5) Je ni kosa la jinai (uchochezi) sisi wananchi wa Tanzania kuandika uchambuzi kususu siasa za nchi yetu?
6) Je siasa za Tanzania ni mali binafsi ya watu maalum kama wewe tu na wananchi wengine wakijihusisha wanakuwa wanafanya kosa la jinai?

Ananilea Nkya
 E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com

--------------------------------------------
On Fri, 11/6/15, 'Mashaka Makana' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Subject: Re: [wanabidii] HONGERA UKAWA MPEIPA NCHI SOMO
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Friday, November 6, 2015, 3:16 PM

Mama Nkya unanichanganya! Wewe ni mwanaharakati
au mwanasiasa? 

Sent
from Yahoo Mail on Android From:"'ananilea
nkya' via Wanabidii"
<wanabidii@googlegroups.com>
Date:Fri, Nov 6, 2015 at 17:00
Subject:[wanabidii] HONGERA UKAWA MPEIPA
NCHI SOMO

HONGERA UKAWA MPEIPA NCHI
SOMO

Na Ananilea Nkya

Baada ya uchaguzi mkuu
kukamilika,  Watanzania  wote  wanaopigania mabadiliko 
ili  kila baada ya uchaguzi nchi  yetu ipate uongozi 
uongozi
utakaowezesha  mamilioni ya Watanzania wanaoteseka kwa
umaskini kuondokana na umaskini  wao,  bila shaka
watavipongeza  vyama  vinanyounda  Umoja wa Katiba ya
Wananchi UKAWA.

UKAWA
wametoa somo kubwa kwa nchi yetu kuhusu changamoto kuu
zinazokabili nchi yetu kufikia uchaguzi huru na wa haki kama
nitakavyoeleza katika  makala hii.

Aidha wanachama na viongozi wa CCM ambao
waliamua kuchukua maamuzi magumu  kuondoka katika chama
hicho  na kuungana na UKAWA katika kupigania mabadiliko nao
wanastahili pongezi kubwa.

Miongoni  viongozi hao ni  Edward Lowassa
aliyekuwa mgombea Urais  CHADEMA –UKAWA ---ambaye
ushawishi wake wa kisiasa umeacha historia  ya aina yake
katika uchaguzi wa vyama vingi Tanzania.

Wengine Mzee Kingunge Ngombale Mwiru, Waziri
Mkuu mstaafu Mheshimiwa  Fredrick Sumaye na Waziri wa Mambo
ya Ndani mstaafu Lawrence Macha.

Viongozi
hawa  wamejitoa mhanga kukubali kujishusha na kuwa sehemu
ya harakati za  wananchi  kutafuta mabadiliko ya
kunufaisha walio wengi.

Tena  wamejitoa  bila kujali  kudhalilishwa
kwa matusi  na kunyanyaswa na vyombo vya dola kama
wanavyonyanyaswa wananchi  wa kawaida.

Ninaamini  ni watu wasioitakia mema Tanzania
na wasiojali maslahi ya Watanzania wengi ndio pekee
watawabeza viongozi  hawa kutokana na uamuzi wao wa
kuungana na wana mabadiliko.

Lakini  Watanzania  wanaoelewa vema  mchango
wa  uongozi  katika harakati za ukombozi watawapongeza na
kuwatia  moyo viongozi hawa waliojitoa mhanga na kuthamini
mchango wao katika kupigania  maslahi ya Watanzania  walio
wengi  maana bila  viongozi  kujitolea ili kuleta 
mabadiliko, mabadiliko hayawezi kupatikana.

Zaidi ya yote  vyama
vinavyounda UKAWA ambavyo ni 
NLD,  NCCR-Mageuzi, CHADEMA Nna CUF  vinastahili pongezi
kubwa kwa sababu  umoja wao katika uchaguzi wa mwaka huu
umetoa somo jipya katika siasa za  vyama vingi Tanzania.

Jambo moja kubwa  ambalo
UKAWA wamewathibitishia Watanzania  ni kwamba vyama vya 
upinzani vikishirikiana kwa dhati  na kujiandaa vema 
kupata viongozi makini  na wenye dhamira ya kweli  ya
kuleta  mabadiliko kweli  ya kunufaisha mamilioni ya
Watanzania maskini,  wanashinda  uchaguzi kwa kura
nyingi.

Jambo muhimu zaidi
sana  ambalo UKAWA  wametoa  somo kwa Watanzania katika
uchaguzi huu  ni kwamba  nchi yetu bado ina safari ndefu 
kufikia uchaguzi HURU NA WA HAKI unaowesha mshindi
kutangazwa mshindi na si vinginevyo.  Je amani inaweza
kutamalaki kwenye jamii yetu  kama uhuru na haki kwenye
uchaguzi vitaendelea kuchezewa kwenye uchaguzi?

Swali
hili  msingi wake  ni mgogoro ulipo sasa  kuhusu
kutotangazwa kwa  matokeo ya  mshindi katika uchaguzi  wa
Urais Zanzibar  na  UKAWA kutokukubali matokeo  ya
Urais.

UKAWA  katika
uchaguzi huu wametoa somo kwamba kuna matatizo makubwa
matatu  yanayokwamisha uchaguzi huru na wa haki 
Tanzania. Mambo hayo ni haya:
1)   
Walioko madarakani  kutokuwa na dhamira ya dhati (political
willingness)  kuona mfumo wa siasa za vyama vingi
ukistawi  na kuleta manufaa kwa  mamilioni ya Watanzania
wanaoteseka kwa umaskini nchini. Dhamira inakosekana
kutokana walioko madarakani kunufaika na  kuwepo kwao
madarakani.
2)    Mifumo ya  kisheria
na kitaasisi iliyokuwa inatumika kutawala wakati wa mfumo wa
chama kimoja cha siasa kuendelea kutumika katika mfumo wa
vyama vingi hivyo kunufaisha chama kilikuwa madarakani.
3)   
Vyombo vya dola kutumika kisiasa kunyanyasa  wananchi 
wanapodai haki  ya uchaguzi huru na wa haki.

Hivyo  matatizo haya 
yasipotafutiwa ufumbuzi wa  kikatiba  kabla ya uchaguzi
mwingine 2020 tbila shaka  idadi ya wapiga kura 
ikapungua  sana  uchaguzi ujao kutokana na wanachi kukata
tamaa kwamba uchaguzi hauna manufaa yoyote kw amaisha
yao.

Lakini kibaya zaidi
tusishangae  umaskini  ukiongezeka  mara dufu 
miongoni  mwa  mamilioni ya Watanzania tuendako  maana 
hata kama  serikali  ya Rais John Magufuli itafanya kazi
kubwa na kuweza kukuza uchumi  kutoka asilimia saba (7%)
ilivyo sasa na kufikia asilimia  kumi na tatu (13%) huenda
uchumi huo usiwanufaishe Watanzania wengi wanaoteseka kwa 
umaskini.

Hii ni kutokana 
Katiba na mifumo ya kiutawala iliyopo nchini hivi sasa 
kutoa mwanya kwa watawala
kujitajirisha  zaidi wao wenyewe kwa fedha  na mali za 
za nchi  huku  mamilioni ya Watanzania  wakibaki maskini
wa kutupa.

Kwa hiyo  kazi
kubwa aliyonayo Rais Dr John Magufuli, UKAWA,  vyama
vingine vyote vya siasa  na Watanzania wote  ni kutafakari
hatma ya mamilioni ya Watanzania wanaoteseka kwa umaskini 
kwa kuzingatia  hayo matatizo  matatu niliyoyaainisha hapo
juu.  Mungu Ibariki Tanzania.
 
Note: Ninaridhia anayetaka kuchapisha andiko
hili afanya hivyo lengo likiwa ni kujifunza tuijenge nchi
yetu nzuri Tanzania.






Ananilea Nkya
 E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda

wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata
Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to
this Forum bears the sole responsibility for any legal
consequences of his or her postings, and hence statements
and facts must be presented responsibly. Your continued
membership signifies that you agree to this disclaimer and
pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message
because you are subscribed to the Google Groups
"Wanabidii" group.
To unsubscribe
from this group and stop receiving emails from it, send an
email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.



--

Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

 

Kujiondoa Tuma Email kwenda

wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma

 

Disclaimer:

Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.

---

You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.

To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment