Saturday 19 October 2013

[wanabidii] UWANJA WA NDEGE MWANZA/BUKOBA

Poleni sana kwa yaliyowafika mie pia nilipata tatizo la kuzungushwa bukoba hadi kufikia kuanguka ndege ya Auric kisa tumetoka mwanza jioni tukijua tunakwnda bukoba tukiwa angani pilot alitwambia anakwenda rubongo kuchukua abiria tukaishia kufika bukoba saa 2 usiku na hakukuwa na taa sitasau tulizunguka sana na hatimaye pilot kuamua kutua popote akabahatisha near ukuta wa bukoba na watu walijua tumetumbukia ziwani hakukuwekwa habari yeyote kwa kweli manager huyu wa mwanza achukuliwe hatua kama sio kufukuzwa ni mara nyingi shida hizi zinatokea, kwani mashirika haya ya ndege ni ya kika nani why not precision ni fast jet na auric mtatuua tunaokaa kanda ya ziwa,
 
Binafsi niliposalimika na kurudi nilimwandikia katibu mkuu wa wizara nikajibiwa kwamba wanashughulikia hadi leo sijapata jibu tena licha ya kufuatilia Auric wakasema niwape gharama nilizotibiwa bima yao italipwa, hivi mnayaona haya wahusika, kweli watanzania tunapelekwa tu
 
 
 
Julieth Mulungi Mutabiilwa P. O. BOX 13755 TEL 255 22 754 279974 MUHIMBILI NATIONAL HOSPITAL Office: 255 22 2151599 Fax: 255 22 2150534 DAR ES SALAAAM TANZANIA EAST AFRICA
From: MaryGlady Heri <mglady2@gmail.com>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Saturday, October 19, 2013 9:50 AM
Subject: Re: [wanabidii] Ndege ya fastjet yarudi Dar kwa kushindwa kutua Mwanza baada ya taa kuzimika

Ndio tatizo la fast jet no customer care information is power,wangewaarifu abiria kuwa uwanja hatuuoni hakuna taa kwa hiyo tunajaribu kuzungudika ili kuona kama umeme unaweza kurudi isipowezekana basi tunarudi dar kwani abiria wange cool down! but they always don't day anything! am in Love with Precision no matter what delays,cancellation but WE ARE WHY WE FLY


2013/10/19 Mwema Felix <mwema.felix@gmail.com>
Jovias
Wasafiri waliogopa bure kwani ndege haikuwa na tatizo. Uzuri kwenye ndege huwa wanachukua mafuta ya "dharura".


2013/10/19 Jovias Mwesiga <ngonzy@gmail.com>
Tunataka kwenda mbinguni bila kufa hahaha. Poleni wasafiri angalau mlipata nafasi ya kumkabidhi muba wenu maisha yenu siku hiyo ni jambo jema
On Oct 18, 2013 3:28 AM, "Abdalah Hamis" <hamisznz@gmail.com> wrote:
KUZIMIKA kwa taa katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza juzi kulisababisha ndege ya fastjet kushindwa kutua na kulazimika kurejea jijini Dar es Salaam.

Inaelezwa kwamba ndege hiyo iliyopaswa kutua saa 2 usiku kwenye uwanja huo ikitokea jijini Dar es Salaam, ilishindwa
 kutua na kulazimika kuzunguka hewani mara tano, hali inayodaiwa kuleta taharuki miongoni mwa abiria.

Habari zinadai kuwa kukosekana kwa umeme katika uwanja huo kulisababisha kutokuwapo kwa mawasiliano, hivyo kuzua tafrani kubwa kwa baadhi ya abiria.

Baadhi ya abiria waliosafiri na ndege hiyo waliieleza Tanzania Daima kwamba wengi walikumbwa na hofu ya kuzama katika Ziwa Victoria.

"Tuliogopa sana baada ya kuona ndege imeanza kuzunguka zunguka angani, na tukahofia kuwa huenda tukatumbukia ziwani, maana uwanjani haukuwa na umeme.

"Nilianza kusali huku mapigo ya moyo yakinienda mbio sana. Maana rubani angeweza kushuka ziwani kwa kuona taa za wavuvi," alisema abiria mmoja ambaye hakutaja jina lake.

Hata hivyo, baadhi ya abiria na wadau wengine wa usafiri, akiwamo Mbunge wa Nyamagana jijini Mwanza, Ezekiel Wenje na Meneja wa Shirika la Bima la Jubilee Mkoa wa Mwanza, Jared Owando, walieleza kusikitishwa na taarifa za kukatika kwa umeme kwenye uwanja wa ndege.

Walisema kwamba, kitendo hicho kinapaswa kudhibitiwa, ikiwa ni pamoja na uongozi wa uwanja huo kuwajibika kikamilifu, ili tatizo hilo lisijirudie tena, kwani hali hiyo ni hatari katika usalama wa abiria na ndege kwa ujumla: "Siku hiyo mimi nilifika Mwanza mapema usiku na ndege ya Precision kutoka Dar. Lakini baadaye nikaarifiwa kwamba kuna ndege imelazimika kurejea Dar es Salaam kwa sababu uwanja una giza. Sasa najiuliza, hakuna jenereta uwanjani hapo?" alisema Jared.

Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza, Easter Madale, alipoulizwa jana kwa njia ya simu kuhusiana na tatizo hilo, alikiri kutokea hitilafu ya umeme hivyo ndege hiyo kupata usumbufu ikiwa angani, na kusema hilo ni tatizo la kawaida: "Ni kweli siku hiyo kulikuwa na hitilafu ya umeme, hivyo mawasiliano yakakosekana! Umeme ulikatika na jenereta la TCAA halifiki huku kwetu…na sisi hapa jenereta yetu ni ndogo haina nguvu sana," alisema meneja huyo.

Miaka kadhaa iliyopita iliwahi kutokea ajali mbaya, baada ya ndege ya mizigo kutoka Ulaya iliyokuja kubeba samaki kutumbukia ndani ya Ziwa Victoria, kutokana na kukosekana kwa umeme na mawasiliano uwanjani hapo.

--- via Tanzania Daima

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.


0 comments:

Post a Comment