Tuesday 29 October 2013

[wanabidii] UCHAGUZI 2015 – WAGOMBEA WAFUATE DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA

Ndugu zangu

Nilikuwa naona ni wakati sasa kwa wagombea mbalimbali wa nafasi za udiwani , ubunge na urais katika uchaguzi mkuu wa 2015 kama kweli utakuwepo wanadi sera zao kulingana na malengo ya taifa ambayo imeelezwa vizuri katika dira ya maendeleo ya taifa 2016 .

Mfano tukiongelea suala la miundombinu kwa ujumla mgombea ajue masuala ya miundombinu kwa ujumla na vile ambavyo iko kwenye dira ya maendeleo na kile ambacho kimeshafanyika halafu yeye atueleze atatekelezaje akipewa fursa hiyo kwa njia ya kura , kwenye masuala ya afya hivyo hivyo , michezo , elimu ya juu , ulinzi na usalama , mawasiliano ETC .

Hatutapenda kuona kiongozi anaingia madarakani na kuondoa miradi ya maendeleo ambayo imeanzishwa na mtangulizi wake wakati iko kwenye dira ya taifa ya maendeleo .

Watanzania tuseme Tanzania kwanza vyama baadaye na tuanze hivi kwa kuainisha ni nini tunataka kwa maendeleo yetu hawa wagombea waje kutueleza watakavyotekeleza tu na mwisho wa siku kwa sababu tunajua tunachotaka tutaweza kuwahoji .

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

0 comments:

Post a Comment