Ludovick bojo!
Acha kutonesha vidonda hivyo. Tunataka kwa pamoja kuanza kurasa mpya hayo yaache. Tujenge litaifa letu kwa umoja wetu katika vyomba vyetu.
--------------------------------------------
On Sat, 2/13/16, Joseph Ludovick <josephludovick@gmail.com> wrote:
Subject: Re: [wanabidii] Kina nani wanaompinga Magufuli?
To: wanabidii@googlegroups.com
Cc: "Telesphor Magobe" <tmagobe@gmail.com>
Date: Saturday, February 13, 2016, 11:44 PM
Mama Nkya
wewe mwenyewe haukubali kukosolewa. Tulikuambia kuwa
ulijiongoza vibaya wakati wa Lowassa. Haukukubali kusikiliza
hata jambo moja.
Leo unasema wengine wakubali kukosolewa.
On Feb 13, 2016 7:02 PM,
"'Thomas Joseph' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
wrote:
Duh@
Nkya
Sent
from Yahoo Mail on Android
On Sat, Feb
13, 2016 at 18:52, Telesphor Magobe<tmagobe@gmail.com>
wrote: Asane
dada Ananilea Nkya! Kuogopa kukosolewa ni kasoro kubwa mno
kwenye uongozi wa nchi. Kama nilivyosema kwenye mchango
wangu wa kwanza ni kwamba hata kama mtu anafanya vizuri
akikosolewa na kukubali kukosolewa atafanya vizuri
zaidi. Kama angeridhika tu na hali yake asingeweza
kufanya vizuri zaidi! Hivyo, kumkosoa rais si kumkatisha
tamaa wala kutomtendea haki kwa vile bado ana muda mrefu
mbele yake! Bali ni kumsaidia afanye vizuri zaidi na
akishafanya vizuri zaidi, akikosolewa tena
ata'sustain' hiyo hali ili asirudi nyuma. Hali hii
ndiyo huwa inaleta maendeleo. Huwa wakati mwingine nachangia
kitu kilichotokea kwangu. Huwa nasema kuwa nilipoanza maisha
nilikuwa sina kitanda, meza ya chakula, TV, kabati la vyombo
na pia nilikuwa na pair moja tu ya viatu etc. House help
wangu akawa amepeleka habari kwa neighbours. Hivyo, baadhi
ya akina mama wakaanza kusema: "mtu mwenyewe analala
chini, hana meza ya chakula, ana viatu pair moja tu, hana
TV...etc." Mwanzoni iliniumiza, lakini nikaona
walichokuwa wanakisema siyo uwongo. Nilichofanya ni
kuorodhesha walivyosema sina, kisha kila nikipata hela
nilikuwa nanunua kimoja baada ya kingine na hatimaye wale
waliokuwa wakinicheka walijikuta nimewaacha nyuma
kimaendeleo. Ningekasirika na kuanza kujibizana nao leo hii
nisingekuwa na vitu nilivyoweza kununua baada ya kutafakari
kuwa sina na navihitaji pia. Hivyo, kwa kunisema, neighours
wangu walinisaidia/challenge na nilivyokubali nikapiga
hatua. Lakini ni kwa sababu mimi mwenyewe nilikubali kuwa
waliyosema kuhusu mimi yalikuwa kweli. Kujitambua ni hatua
muhimu sana katika maendeleo.
2016-02-13 17:34 GMT+03:00
'ananilea nkya' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Magobe
umetuweka sawa. Nakubaliana nawe asiyekubali kukosolewa pia
asikubali kusifiwa. Kwa maoni yangu kukosoa na kusifia vyote
vina mchango kwenye maendeleo. Lakini kiongozi wa umma
anayeweza kuleta maendeleo makubwa ni yule ambaye kwanza
yeye mwenyewe anafiriki sana (ana original ideas zake siyo
siyo za kukopa) na yuko tayari kukosolewa na wengine
wanaofikiri tofauti naye---maana bila kukosoana tena kikweli
kweli bila unafiki--maendeleo ya kweli yawe ni ya mtu
binafsi ama ya taifa hayawezi kupatikana. Binafsi huwa
nawapenda sana wakosoaji makini wenye moyo wa uzalendo
maana hao ndio wamekuwa wajenzi wakubwa wa taifa letu.
Wasifiaji mara nyingi ni walinda maslahi binafsi na
wamepungukiwa kitu kimoja muhimu katika uongozi unaoweza
kunufaisha walio wengi--ujasiri.
Ananilea Nkya
E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com
--------------------------------------------
On Sat, 2/13/16, Telesphor Magobe <tmagobe@gmail.com> wrote:
Subject: Re: [wanabidii] Kina nani wanaompinga
Magufuli?
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Saturday, February 13, 2016, 7:58 AM
Hakuna
anayempinga! Kuna wanaomkosowa. Kupinga na kukosowa
hakuna
maana sawa. Kukosowa ni kusema namna kitu kichenye
matokeo
mabaya kingeweza kufanywa kwa namna tofauti na kuleta
mafanikio chanya, au kitu kizuri kingeweza kufanywa kwa
namna nyingine na kuwa kizuri kuliko au kitu kizuri
kuliko
kingeweza kufanywa kwa namna ambayo kingekuwa kizuri
zaidi
ya vyote. Kama kuna watu wanaoweza kumsifia rais kwa
yale
anayofanya, kuna watu wanaweza pia kumkosowa kwa yale
anayofanya. Kama kumkosowa rais si sahihi kwa vile
ameanza
kazi muda si mrefu na bado ana miaka kadhaa ya kumpima,
basi
hata kumsifia si sahihi kwa mantiki hiyohiyo. Kwa
upande
mwingine, kupinga ni kuonyesha kuchukizwa na kitu
kinachofanyika na kutaka kisifanyike.
2016-02-12 13:58 GMT+03:00
'lang'itomoni lokomoi' via Wanabidii
<wanabidii@googlegroups.com>:
NI wazi kuwa
siyo watu wote ni mashabiki wa uongozi na aina ya uongozi
wa
Rais Magufuli. Ni
wazi siyo wote walifurahia kuchaguliwa kwake na kwa
hakika
si wote wanafurahia
kile ambacho kinajulikana kama Operesheni Tumbua
Majipu.
Ni kufanya
makosa
kudhania kuwa watu wote wanafurahia au wanapaswa
kufurahia
operesheni hii au
kuchaguliwa kwa Magufuli. Wapo wenye kumpinga, na
wengine
wameshajitokeza wazi
kumpinga. Hili kwa kweli siyo la kushangaza na lenyewe
tu
siyo habari.
Swali kubwa
ambalo linaweza kuwa habari ni kuwa hawa wenye kumpinga
ni
kina nani na ni kwa
nini. Je wote wenye kumpinga wanampinga kwa sababu
wanataka
kitu kingine au
wanampinga kwa sababu wanaona hawana jinsi isipokuwa
kumpinga?
Je, wenye kubeza
serikali hii na uongozi wa Magufuli wanafanya hivyo kwa
sababu wanafurahia au
wanatamani ule uongozi uliopita au wanatamani uongozi
mwingine ambao haupo na
haujawahi kuwepo bado?
Kwa maoni
yangu, wenye kumpinga Magufuli wako kwenye makundi
mbalimbali, makundi ambayo
ama yanaunganishwa na baadhi ya mambo.
Kundi la
wapinga mabadiliko haya si yale
Kundi hili
naweza kusema ndio kundi lenye watu wengi wenye
kumpinga
Magufuli na ambao
watajitokeza wengi wakijionesha wanafanya kwa nia
njema.
Hawa ni wale ambao
mgombea wao alishindwa na Magufuli na ahadi zile za
mabadiliko ya mtu mmoja
yakakataliwa ndiyo yanasumbua kwa sababu bado hawaamini
kuwa
mtu wao (siyo
mabadiliko yao tu) alikataliwa.
Kundi hili,
haliwezi na halitakuwa na sababu ya
kushabikia mambo yanayofanywa na Magufuli hata akifanya
nini.
Hawa mara
nyingi ni watu ambao hawachelewi kuhamisha magoli.
"Kama kweli
Magufuli
anatumbua si tuone kama atatumbua Bandari" wanasema.
Bandari wanatumbuliwa na
wao wanarudi "ah ile mbona rahisi sana kama kweli
anataka
kutumbua Bandari si
atumbue Uhamiaji tuone"; uhamiaji kunatumbuliwa na
hawa
(hawakiri kuona
kilichotokea bandari wala uhamiaji) wanarudi na goli
jingine; "ah mbona yule
kaonewa kama kweli ye mwanamme si aiguse Takukuru";
Takukuru inaguswa mwisho
wanakuja na kusema "Vipi escrow". Na itakapoguswa
hawatakubali bado watatafuta
goli jingine na jingine. Hawa ni wa mabadiliko yale;
mabadiliko ya kuzungurusha
mikono na hawako tayari kuacha kuzungurusha
mikono.
Tukumbuke
neon kubwa la hawa wakati wa kampeni lilikuwa "CCM
iondoke
kwanza mengine
baadaye". Tatizo ni kuwa yale mengine yameanza
kutokea
sasa wakati CCM iko
madarakani na hili ni gumu sana kulipatanisha.
Walijiaminisha kuwa yale
"mengine" hayawezi kutokea CCM ikiwa madarakani na
kwamba yanayotokea ni
kinyume (antithesis) cha fikra zao zote na ndoto zao.
Hawa
hawawezi kumuunga
mkono Magufuli wala kushabikia mabadiliko haya.
Kundi la
wakosoaji hawa
Lipo kundi
jingine la wakosoaji 'hawa'. Hawa ni wakosoaji wa
serikali. Hawa ni watu ambao
kwao serikali ni ya kushukiwa wakati wote. Ni kundi
zuri
sana kwenye utawala wa
kidemokrasia kwani kundi hili halipendi geresha na
mazingaombwe; ni kundi
ambalo linawaangalia wanasiasa kama viongozi wa ngoma;
wanajua wanafanya
burudani na kuhakikisha watu wanapokea kwa kiitikio na
manyanga. Wakosoaji
"hawa" wao
wanaweza kufurahia mabadiliko lakini wakati huo huo
wanayashuku
mabadiliko hayo; hawaamini nia za wanaotaka kuleta
mabadiliko na hawachelewi
kutafuta kasoro ili waweze kusema "aha si unaona
amefanya
hivi tena".
Kundi hili
nalo kama kundi lile la mwanzo halitakoma; litaendelea
kumshuku Magufuli,
litaendelea kuhoji ukweli wake na malengo yake na
halitochelewa kulia "kavunja
katiba" "kaingilia Bunge" "kaingilia
Mahakama"
"dikteta n.k". Ni kundi ambalo
lipo kama mwiba wa lazima ili serikali isije kufikiri
au
kuishi bila
kuangaliwa.
Kundi la
waathirika wa haya
Kuna kundi
na ninaamini litazidi kuwa kubwa zaidi kwa siku
zinavyokwenda; hili ni kundi la
waathirika wa mabadiliko haya. Wale watu wanaopoteza
nafasi
zao na watu ambao
wanaaanza kuguswa na mabadiliko haya hawawezi kamwe
kuwa
mashabiki wa yule
ambaye amesababisha jamaa, ndugu, mabodi au marafiki
zao
kuanza kuwa na maisha
magumu.
Kwa kadiri kwamba
Magufuli anaanza kulazimisha uchumi wetu
kujirekebisha ndivyo ambavyo wapo watu wengi ambao
walikuwa
wamezoea kuishi
maisha fulani na sasa maisha hayo hayapo tena; na kama
baadhi ya mishahara na
posho zitakavyofutwa – kama inavyotarajiwa – kwenye
Bunge la bajeti ni wazi
kuwa Magufuli atapoteza mashabiki na marafiki wengi; na
kwa
vile hawa wanaweza
kuwa wengi, kundi hili litazidi kumpinga na linaweza kuwa
na
watu wengi ndani
ya serikali na ndani ya chama tawala.
Makundi haya
matatu naamini ndio makubwa na yataendelea kuwepo kwa
kadiri
ya kwamba Magufuli
anaendelea na ajenda yake ya kusafisha utumishi
serikalini,
kubana matumizi
yasiyo ya lazima na kurejesha nidhamu na heshima kwa
Watanzania.
Siyo wote
watafurahia na si wote watasimama na kuunga mkono. Nina
uhakika hata wale ambao
walipiga makofi kushangilia kutumbua majipu wanaweza leo
hii
wasiwe tena wa
kwanza kushangilia hasa baada ya wao wenyewe
kutumbuliwa.
Bado kazi kubwa
inakuja na ngumu zaidi lakini kama alivyosema Rais –
"hakuna namna nyingine".
Nina uhakika
pamoja na watu wengi wenye kumpinga bado wapo wengine
wengi
ambao nao
wataendelea kuunga mkono na kumtia shime kwa sababu
tunajua
kushindwa kwake ni
hasara kwa taifa na vizazi vijavyo.
Hili tusiliruhusu
litokee. -
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole
responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and
hence
statements and facts must be presented responsibly.
Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to
the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving
emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole
responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and
hence
statements and facts must be presented responsibly.
Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to
the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving
emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 comments:
Post a Comment