Thursday 24 November 2016

Re: [wanabidii] MCHUNGAJI ANTHONY LUSEKELO USIRUDIE TENA KUFANYA USHETANI HUU

Bahati mbaya hatuelewi nia ya andiko hilo na uwezo wa kiroho wa dada huyu. Pengine uchanga wako kiroho uliakufa kuamini ulichoamini na kutoamini unachokiona pole. Ahika neno ulilojifunza ili kesho usilalamike kwamba hukujua kwa kumwangalia mchungaji wako alifanyaje badala ya alihubiri nini kulingana na maandiko matakatifu

On Nov 24, 2016 23:48, "'Stephen Ruvuga' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Sidhani kama tunapaswa kuhukumu kwa sababu hatuna uwezo wala mamlaka hayo. Hata hivyo kwa ujumla tunapaswa kujifunza kitu; hatupaswi kuabudu binadamu wenzetu, tunapaswa kumwabudu Mwenyezi Mungu tu.

Kwa sababu ya kukata tamaa kwetu, mifadhaiko, matatizo na changamoto mbalimbali za maisha tumeacha njia sahihi na kuchukua njia ya mkato kwa kugeukia binadamu wenzetu na kuwaabudu tukiamini kwamba wana uwezo wa Kimungu!

Watu wajanja wanaojiita kila jina (manabii, mitume, wachungaji, nk nk nk) nao wametumia matatizo yetu na kukata tamaa kwetu kama mtaji wao kwa kutuhadaa ili watuvune. Wengine kwa kiburi, wanajipa uwezo wa Kimungu na kujitangaza kila mahali kwamba wanaponya watu, wanafufua waliokufa, nk nk nk!! Hata Yesu Kristu mwenyewe alipofanya maajabu ya kuwaponya na kuwafufua watu aliwaambia wasitangaze neno hilo! Leo tunashuhudia matangazo kila upande ikitangaza uwezo wa miujiza, kuponya na kufufua!! Lakini hao wafu, viwete, vipofu, viziwi tunaowajua kwa uhakika wapo hivyo hivyo. Badala yake watu "anonymous" na "abstract" ndiyo mifano na mashuhuda wa miujiza hiyo!

Kuna taarifa zinazoashiria kwamba kuna watu wanaolipwa ili kutoa ushuhuda wa uongo kwamba waliponyeshwa kimiujiza.

Tumeona utabiri wa wahubiri maarufu ukienda kombo, ikidhihirisha kwamba wahubiri hao si miungu kama tunavyoamini bali ni binadamu wenzetu tu wanaocheza na akili zetu. Kwa mfano, utabiri wa hivi karibuni juu ya ushindi wa Clinton uliofanywa na TB Joshua ulivyoenda kombo. Kwa mujibu wa BBC, bado waumini wake wakatetea upungufu huo na kudai kwamba TB Joshua hakukosea kwani Clinton alipata kura nyingi za moja kwa moja (popular votes), na hivyo ubashiri ulikuwa sawa!!!

Kuna wahubiri kadhaa duniani waliowaongoza wafuasi wao hata kukatisha maisha yao wakiwahadaa kwamba ndiyo njia ya kwenda mbinguni! Kibwetere wa Uganda ni mfano mmoja tu . Jim Jones, kiongozi wa Peoples' Temple aliua wafuasi wake 918 ambao waliamini ni nabii wao!

Bila kuingilia imani ya yeyote yule, biashara na hadaa inayoendelea kwa mgongo wa kidini inapaswa kutuamsha na kutufanya tutafakari upya njia zetu za kiimani ili kuchuja nabii yupi ni wa ukweli na yupi wa uongo anayetutumia kama mtaji wa kujitajirisha yeye binafsi huku akitumia matatizo yetu na kukata tamaa kwetu kama daraja la kutuvuna!

Ni wakati wa kuamka!


Sent from my Samsung mobile


From: Victor Mwita <victormwita@gmail.com>;
To: <wanabidii@googlegroups.com>;
Subject: Re: [wanabidii] MCHUNGAJI ANTHONY LUSEKELO USIRUDIE TENA KUFANYA USHETANI HUU
Sent: Thu, Nov 24, 2016 1:10:38 PM

Huenda ni watu wengine kujifanya ni watu wa kiroho sana lakini kumbe wakiwa mitaani ni watu kama wengine tu


On 24 Nov 2016 16:05, "Telesphor Magobe" <tmagobe@gmail.com> wrote:
Hakuna lolote. Wanaotangaza maovu ya wenzao wao wanayaficha yao. Tukianza kuviziana na kuchukua video na kuzileta humu hakuna mtakatifu hapa!

2016-11-24 14:01 GMT+03:00 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Katabazi.
Ukiwa msomi, muelewa wa haki za binadamu (kwa taaluma yako ya sheria) na huku ukijua kuwa huyu jamaa ana watu wanaomuona kaqma " mungu" kwa kumwita majina kama katapila na mengine mengi, ukijua kuwa watu hao waliyahama makanisa yao wakidhani sasa wanamfuata Mungu kwa mtu kama huyo (kwa hiyo waumini hao ni victims). Ulikosaje kupiga picha ya video ukaweka humu potelea kote ufungwe lakini uwasaidie watu hao??? Umekosea sana. Majuzi niliandika makala humu watu wakaogopa kuijadili (isheheni vifun gu vya biblia vinavyokataa viongozi wa kihuni wanaojitokeza kwa njia ya ibada na kupotosha watu) pengine kwa kudhani huyu jamaa anamhubiri Mungu. Huoni kuwa hapo umeuzuia upanga wa Bwana usimwage damu (Yeremia 48: 10). Nyoka hupigwa kichwa sio kiwiliwili.

------------------------------ --------------
On Thu, 11/24/16, 'Happiness Katabazi' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] MCHUNGAJI ANTHONY LUSEKELO USIRUDIE TENA KUFANYA USHETANI HUU
 To: "WANABIDII" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Thursday, November 24, 2016, 10:59 AM



 MCHUNGAJI
 ANTHONY LUSEKELO USIRUDIE TENA KUFANYA USHETANI
 HUU
 Na
 Happiness Katabazi
 MITHALI
 20: 1 Katika Biblia inasema : " Mvinyo hudhihaki ,kileo
 huleta ugomvi; Na akosaye kwa vitu hivyo Hana
 Hekima".
 Nimelazimika
 kutumia nukuu hiyo ya Biblia Kuonyesha matendo ya kishetani
 yaliyotendwa Jana hadharani na Kiongozi wa Kanisa la
 Maombezi nchini lenye masikani yake Ubungo Kibangu Dar Es
 Salaam,Anthony Lusekelo yana baraka  za kitabu cha
 Mithali 20:1 Katika Biblia Kwani matendo Yale aliyoyatenda
 ambayo nimeyaanisha Katika ndani ya makala hii ya
 lithibitishwa mtumishi Huyo wa Mungu Hana
 Hekima. 
 Jana
 23/11/2016   nikitoka nyumbani kwetu saa 11 asubuhi
   Sinza  C nakuelekea  University of Bagamoyo
 eneo la Kawe Beach Dar es Salaam  Ambapo chuo hicho
 kimepakana na Ofisi ya Redio Times kwaajili ya kukamilisha
 mambo yangu ya kitaaluma.
 Hatua
 chache kabla ya kufika chuoni hapo ni kama nyumba  Tatu
 kurudi  nyuma  kuna Ukumbi unaitwa Mtana Multipose
 Hall  na katikati kuna barabara ya vumbi
 inayotenganisha nyumba zilizopo upande wa kushoto na kulia
 .Ni barabara ndogo ambayo Dereva hawezi geuza Gari
  hadi aende Mbele zaidi.
  Upande
 wa kulia wa ukumbi huo wa Mtana Multipose Hall kuna nyumba
  ya ghorofa ambayo inalimdwa na walinzi wa makampuni ya
 Ulinzi  ambao walinzi Hao  ni Waaafrika na
 wanaishi pia raia wa kigeni .
 Nyumba
 ina namba  KAW / MZN/ 1348  ambayo imebandikwa
 katika ukuta wa geti la nyumba hiyo na mabango ambayo
 yanayoonyesha nyumba hiyo inalindwa na kampuni ya ulinzi
 nyuma ya nyumba hiyo ni  Bahari ya Hindi .
 Saa 12: 32 asubuhi nilipita Katika njia
 hiyo nikiwa nimepanda usafiri wa aina ya Bajaji kwaajili ya
 kwenda Chuoni kukamilisha mambo yangu ya kitaaluma
  nilipofika  katika eneo la nyumba hiyo yenye
 namba KAW /MZN / 1348 inayotenganisha
 nyumba zilizojengwa  upande wa kulia na kushoto na
 Kabla ya kufika chuoni ambapo ni mwisho kabisa ya barabara
 hiyo nyembamba nilikuta Gari limesimama katikati ya barabara
 yenye namba za usajili  T126 DFN  huku watu kama
 nane  wakiwa wamesimama pembeni ya Gari Hilo huku
 wakimtazama mtu mmoja aliyekuwa akiongea kwa sauti ya juu
 nje ya geti ya  nyumba hiyo.
 Mimi
 nilipofika karibu nione kuna nini na kwanini Gari limeziba
 njia na nani Kaziba njia Yule anayeongea kama kuna ugomvi
 ninani niliposogea Karibu nikabaini aliyekuwa anafoka ni
 Mchungaji Anthony Lusekelo  maarufu " Mzee wa
 Upako.
 Nilishtuka
 nikamtaka Dereva anishushe Mara Moja licha safari yangu
 ilikuwa haijafika mwisho licha ni Hatua Chache kufika chuoni
 Kwangu ili niwahi kwenda kumsihi Mchungaji Lusekelo aondoke
 eneo lile Mara Moja Kwani yeye ni kiongozi wa Kiroho na
 Mtumishi wa Mungu haifahai , kujibizana na watu tena
 hadharani Kwani mwisho wa siku anayedhalilika ni
 yeye.
 Nilimkaribia
 Mchungaji Lusekelo na kumshuhudia kwa macho yangu akiwa
 anatoa lugha za matusi na zisizofaa kwa wakazi wa nyumba
 Namba KAW / MZN/ 1348 huku akiwa amesimama nje ya geti la
 nyumba hiyo ambayo wanaishi pia Raia wa kigeni huku
 akisikika akisema wamezidi kumchokoza kwa kumuita yeye ni
 Mlevi.Nilihisi  kuchanganyikiwa kabisa maana sikuamini
 nilichokuwa nilikushuhudia.
 Mzee
 wa Upako ni miongoni wa wapenzi wa makala zangu  
  na zaidi ya Mara Tatu alishanipigia simu kunipongeza
 kwa ujasiri wangu wa kuandika makala zenye Lengo la Kujenga
 nchi na Akawa anasema ananiombea kwa Mungu azidi kunilinda
 ili niendelee kuandika.
 Namimi
 pia nimekuwa nikifuatilia   mahubiri yake kupitia
 Televisheni ya Chanel Ten , Mara kwa Mara ila sikuwahi
 kubahatika kuonana ana kwa ana na yeye hadi Jana saa 12
 asubuhi nilipomuona akiwa Katika Hali ile ambayo siyo ya
 binadamu wa kawaida .
 Ambapo
 nilimsabahi nikamwambia Mimi ni Muhumini wake na ni
 mwanafunzi wa Univeristy of Bagamoyo chuo ambacho kipo
 nyumba ya pili kutoka nyumbani kwake .
 Licha
  ukweli ni kwamba Mimi siyo muumini  wa Kanisa
 lake . Nililazimika  kuficha jina langu ili asinijue
 kwani ningemtajia jina langu tu lazima angenifahamu kuwa
 mimi ni Mwandishi wa habari ' Mkonoko ' ambaye
 amekuwa akiwasiliana namimi na kunipongeza kwa makala zangu
 kwasababu  angekosa amani kwasababu Angejua waandishi
 wamemuona.
 Kwa
 mujibu wa wale watu Saba  niliyowakuta eneo la tukio
 saa 12 asubuhi walinieleza Mzee wa Upako asubuhi hiyo
 alikuwa anatoka alikokuwa atatokea ndiyo muda huo alikuwa
 akirudi nyumbani kwake ndipo aliposimamisha Gari lake Hilo
 Mbele ya geti ya nyumba ya jirani yake yenye Na.KAW/MZA 1348
 ambapo ndani ya geti Hilo kuna walinzi alianza kujibizana na
 walinzi akidai wamekuwa wakimkebehi yeye hafai Kuwa
 Mchungaji kwasababu ni Mlevi kupita kiasi.
 Nilimsii
 sana hadi saa Moja asubuhi ikanikuta eneo Hilo la tukio huku
 Mvua ikitunyeshea nikimwomba anisikilize  aache
 kutukana,kufoka Katika eneo la nyumba ya watu kwasababu yeye
 ni mtumishi wa Mungu anajidhalilisha ,na anavunja
  Sheria za nchi Kwani kutoa lugha chafu ni kosa la
 jinai,na pia kuziba njia ili watu wasipite kwasababu eti
 anaugomvi na wale watu siyo ustaarabu na anavunja Haki za
 watu wengine za kwenda Kokote watakako .
 Sasa
 yeye Mzee wa Upako kwa kitendo Chake kile kuegesha Gari
 katikati ya barabara ile nyembamba ni kuvunja Haki za watu
 wengine wanatumia usafiri wa Magari Katika barabara ile
 wasiende wanakotaka kwenda kwaajili yake na kweli
 alifanikiwa Kuzuia Magari  yasipite eneo Hilo kwa zaidi
 ya muda Kadhaa huku Mvua ikinyesha na wengine wakichelewa
 kwenda Katika shughuli zao kwa muda .
 Baadae
 alinisikia huku akiwa ameloana maana Mvua ilionyeshea
 alikuwa akisikika akinuka Pombe  huku akiyumbayumba
 akafungua Gari lake akatoa Kikapu kilichokuwa kinachupa za
 Maji ya Kunywa ,kavaa viatu Vya wazi  na kashika miwani
 huku akiwa amekunja suruali.
 Nikamsaidia
 Kubeba miwani na funguo wa Gari tukaelekea  
  nyumbani kwake ambapo ni jirani kabisa na eneo la
 tukio huku tukinyeshewa na Mvua tutafika nyumbani kwake saa
 Moja asubuhi tukafunguliwa  geti na vijana wake
 nikamuingiza hadi ndani ya geti la nyumba yake  na
 vijana wake wakanihoji nimetoka na baba Yao wapi asubuhi ile
 maana ndiyo baba Yao anarudi nyumbani muda ule tangu
 alivyoondoka Juzi (Jumanne) .
 Nikawajibu
 nimetoka aye nyumba za Mbele alikuwa akigombana kwa maneno
 ndiyo nikamuondoa eneo la tukio nakumleta nyumbani kwake
 hapo kama msamalia Mwema.
 Vijana
 wake wakatukaribisha  Mimi na baba Yao ( Mchungaji
 Lusekelo)  .Mzee wa Upako huku akiendekea kuongea kwa
 sauti ya juu akaingia ndani na kile kikapu na Mimi nikampa
 ile miwani niliyokuwa nimeishika ,akaingia nayo ndani Kisha
 akarudi ndani ya uwa wake   akaanza  Kuwaeleza
 vijana wake Kuwa yeye hata siku Moja hataki
 kudharauliwa,kuonewa  na atapambana  .
 Wakati
 huo Mimi ule funguo wa Gari bado nilikuwa nimeishikilia
 kwaajili ya kutaka niwape wale vijana wake waende kukichukua
 lile Gari lilokuwa eneo la tukio walilete nyumbani wa Mzee
 wa Upako ili wananchi wengine waweze kutumia ile
 barabara.
 Mzee
 wa Upako baada ya kumfikisha nyumbani wake aliniambia
 anaishukuru sana kwa kumfikisha nyumbani salama  na
 akaniambia ananiheshimu sana Mimi ni kama binti yake ila
 nimsamehe sana yeye anarudi eneo la tukio kwaajili ya
 kuendelea kupambana na wale majirani ambao ni
 Wazungu.
 Nilimsii
  sana Aiingie ndani akaoge,alale  kwanini yeye
 mwenyewe ndiyo ameniambia muda ule wa asubuhi ndiyo alikuwa
 akirudi nyumbani kwake akitokea katika matembezi yake ya
 jioni lakini akakakata akaanza Kuwaeleza vijana wake
 amedhihakiwa kwa kuambiwa yeye hafai Kuwa mtumishi wa Mungu
 Kwani ni Mlevi sana wakati mtumishi wa Mungu hapaswi Kuwa
 Mlevi na kufanya vurugu.
 Vijana
 wake wale walivyokosa akili na busara wakaungana na uamuzi
 mbovu wa baba ya I wa kurudi eneo la tukio wakati Mvua
 ikinyesha kwaajili ya kwenda kuendelea Kujibu
 mapigo. 
 Kwa
 zaidi ya Mara Sita nikawabembeleza  wale vija na wake
 waache upumbavu huo Mzee wa Upako ni mtu mashughuli nchini
 na kiongozi wa kidini wasiruhusu tena baba Yao kurudi tena
 eneo la tukio kwenda tena kufanya Fujo siyo vizuri Kwani
 mwisho wa siku Atakayedhalilika ni baba Yao.
 Nikawataka
 wale vijana wasikilize ushauri wangu wamfungie ndani Baba
 yao ( Mchungaji Lusekelo ) a kalale Kwani anaonekana
 amechoka sana hajapumzika maana kanieleza alfajiri ile ndiyo
 alikuwa akirudi nyumbani kwake.
 Ili
 Mimi niwapatie ule ufunguo wa Gari la baba Yao ili wao
 vijana ndiyo waongozane na Mimi   nikawaonyeshe eneo la
 tukio na Gari lilipoegeshwa Katikati ya barabara ,wale
 vijana walinijibu ' uwa hawatakagi
 Ujinga'.
 Haraka
 sana wakanitaka niwape funguo nikawapa , huku Mzee wa Upako
  akiiondoka hapo ndani kwake kurudi Katika eneo la
 tukio Kujibu mapigo huku Mzee wa Upako akiwa miguu peku
 ,vile viatu vyake Vya wazi ( Open Shoes ) vyenye rangi
 nyeusi Nikiwa nimevishika Mimi wakitembea Mwendo haraka na
 vijana wake ambapo njia nzima Mzee wa Upako alikuwa akifoka
 na matope miguuni.
 Na
 alipofika tena eneo la tukio la wale vijana wake huku Mimi
 Nikiwa nimebeba Open Shoes zake ambazo nimezipiga picha
 .
 Tayari
 kulikuwa kumeishapambazuka watu wamejaa anaendelea kufoka
 Magari hawawezi kupita kwasababu Mchungaji Lusekelo aligoma
 kuondoa Gari lake katikati ya barabara huku akisema aondoi
  Hilo Gari hadi Rais John Magufuli na RPC Simon Sirro
 waje ndiyo wataliondoa Hilo Gari.
 Nilisikitika
 sana Kwani jitihada zangu za Kuzuia Mchungaji Lusekelo
 asidhalilike  Mbele ya umati wa watu kadri kunavyozidi
  kupambazuka Kwani watu walizidi kujaa na kumshuhudia
 Vituko alivyokuwa akivifanya huku akilindwa na vijana wake
 ambavyo Mtumishi wa Mungu hapaswi kuvifanya.
 Nikahamua
 kukaa Mbali kujifanya natuma SMS Katika simu yangu Kumbe
 napiga  picha vile viatu vyake alivyoniachia ,na Gari
 yake iliyokuwa imageshwa katikati ya barabara Mbele ya geti
 la nyumba Na.KAW/MZA 1348 ambapo tukio Hilo la aina yake
 lilitokea hadi saa mbili asubuhi Jana .
 Hata
 Hivyo wale wale vijana wake alinishitukia  napiga picha
 tukio lile walitaka kunipiga kisa nampiga picha baba Yao
 .
 Kwa
 makusudi  Niliamua kukanusha Kuwa sijapiga picha na
 kusingizia Mimi Nina matatizo ya macho hivyo nilikuwa Nasoma
 SMS lazima simu niinue juu na nisogeze  karibu na macho
 yangu.
 Mmoja
 wa kijana wake akanitishia kunipiga ikabidi nimbadilikie
  na kumtaka kwanza anikome, cha pili jeuri ya kunipiga
 Hana,Tatu sikumtuma baba yake arudi alfajiri aanze kufanya
 vituko vile vya kujidhalilisha,nne nikamwambia yule kijana
 ni shetani mwenye Mkia  ndiyo maana wameshindwa
 Kumfungia ndani  Mzee wao ( Mchungaji Lusekelo ) aache
 kufanya Fujo Mbele ya umati wa watu wakati wana nguvu za
 kumzuia na baba Yao Huyo ni kiongozi wa kiroho anajishushia
 heshima.Akawa mpole.
 Akageuka
 pembeni nikawaweka mkono wangu nyuma kiaina ,nikairusha
  simu yangu kwa nyuma Kwenye  majani na kulikuwa
 na majani yanaunyevu unyevu wa Maji ya Mvua   ili hata
 akianza kunipiga na kunilazimisha nimpe simu ,ashindwe
 kuipata simu.

 Kijana
 Yule ambaye alioneka ni mtu wa mazoezi na
 misuli alivyoona sijamuogopa Akaamua kuondoka
 nilipokuwa nimesimama mimi na akasogea  eneo la
 tukio na kumshuhudia Mzee wao  Mchungaji Lusekelo
 akizidi kufoka nikageuka nyuma haraka nikaokota simu yangu
 nikaenda kusogea Mbali nikampa mwanamke mmoja anayefanyakazi
  chuoni kwetu anishikie tukasogea mbali
 na  aneo la tukio ,tukasimama  mbele ya geti
 la Redio Times na kuendelea   Kutizima  Sinema
 yote ilivyokuwa ikiendelea ambayo Mwongozaji wa Sinema
 alikuwa ni Mchungaji Lusekelo.
 Kumbe
 vile vitendo vilivyokuwa vikifanywa na Mchungaji Lusekelo
 Jana Mbele ya Hadhara viliwakera   wakazi wa eneo hilo
 na watumiaji wa eneo hilo  licha ni la makazi ya watu
 lina Ofisi  pia na chuo wakaamua kupiga simu polisi kwa
 siri .
 Baada
 ya muda mfupi polisi wa Kituo cha Kawe walifika eneo la
 tukio na kushuhudia tukio hilo na kuondoka na Mchungaji
 Lusekelo na kwenda kumuifadhi ndani ya kituo hicho kwa muda
  kwa saa Kadhaa.
 Hata
 hivyo taarifa toka ndani ya Kituo hicho zilieleza Kuwa licha
 ya Mchungaji Lusekelo kuifadhiwa ndani ya Kituo hicho
  aliendelea kutoa lugha zisizo na staha kwa baadhi ya
 Askari Polisi ambao walikuwa wakimshangaa Kuwa imekuwaje
 yeye ni mtumishi wa Mungu halafu amekunywa Pombe kiasi kile
 na anatoa lugha zisizo na staha .
 Hata
 hivyo mchana wa jana kuna taarifa ambazo hazikuwa
  zimethibitishwa  Kuwa Mchungaji Lusekelo
 alihamishwa pale Kituo cha Polisi Kawe na kupelekwa Katika
 Kituo kingine.
 Kwa
 mujibu maelezo hayo ya tukio Hilo la ' Sinema ya
 Bure' nililolishuhudia kwa macho yangu yaliyokuwa
 yanafanywa  na Mchungaji Lusekelo huku akiwa Katika
 Hali isiyokawaida kwa zaidi ya saa mbili ya kufoka na kutoa
 lugha chafu na kuleta Usumbufu Katika eneo la nyumba ya
 jirani yake  limenifundisha mambo mengi ikiwemo Mimi
 Leo kukubaliana ule usemi usemao ' Mungu adhihakiwi'
 Kwani ukimdhihaki atakuumbua hadharani.
  Mchungaji
 Lusekelo ni muhubiri maarufu nchini na ana waumini wengi
 sana nchini ndani na nje ya nchi na wamekuwa wakimuamini na
 hata serikali ya sasa inayoongozwa na Rais John Magufuli
 Inamuamimi na hata Rais Magufuli Mwenyewe siyo Siri
 anamuamini mtumishi huyu wa Mungu Mchungaji wa Lusekelo na
 alishampongeza Lusekelo kwa Kazi nzuri anayoifanya ya kutoa
 huduma ya Kiroho kwa Watanzania ambao ni waumini wake
 .
 Juni
 5 mwaka huu, Rais Magufuli alipofanya ziara ya kushitukiza
 katika kanisa hilo ambapo alienda kwaajili ya kusali katika
 kanisa linaloongozwa na Mchungaji Lusekelo na Rais Magufuli
 akatumia fursa hiyo kuzungumza kanisani hapo eneo la Ubungo
 Kibangu na akamwagiza sifa Lusekelo Kuwa anafanyakazi nzuri
 ya Kiroho.
 Magufuli
 akasema kwa  mamlaka aliyonayo ameishaagiza mamlaka
 zake zianze mchakato wa Kujenga barabara Inayopita Katika
 Kanisa la Mzee wa Upako ili waumini na wananchi wa eneo
 wasiendelee kupata tabu kwasababu barabara ile ni Mbaya
 sana.
 Hata
 hivyo baadhi ya wananchi  walipinga uamuzi huo wa Rais
 Magufuli na walidai uamuzi huo ni wa upendeleo waziwazi na
 wakukurupuka.
 Licha
 ya Lusekelo ya Kuwa na heshima kubwa nchini hadi Rais
 Magufuli Akaamua kwenda kusali kanisani kwake lakini Jana
 alishindwa kutunza Umaarufu wake,heshima yake aliyokuwa nayo
 Katika Jamii kama kiongozi wa Kanisa lenye waumini Wengi
 Akaamua kuporomosha matusi hadharani ,kuyumbayumba wakati
 amesimama Na kutembea Mithili ya mtu aliyelemewa na kilevi.
  Uzuni.
 Vituko
 vile alivyovifaya Jana Mchungaji Lusekelo pia vimenifundisha
 Mimi binafsi Kuwa kuanzia Jana niache tabia ya Kuwa mgumu
 kuamini /kunisha baadhi ya  taarifa za mambo
  machafu yanayodaiwa kufanywa na baadhi ya watumishi wa
 Mungu.
 Miezi
 mitatu iliyopita kuna watu watatu  toka vyombo Vya
 Ulinzi na Usalama walinieleza Huyo Mchungaji Lusekelo ni
 Mlevi mzuri tu wa Pombe aina ya Konyagi na wakati mwingine
 anavyokuwa madhabauni anavyokuwa na kitaulo anajifuta jasho
 mara kwa mara ni zile pombe kali zinakuwa zinachemka mwilini
 zinamfanya ajisikie jasho na walishamnasa katika matukio
 zaidi ya Mara Tatu  akiwa hoi kwa kilevi ,kwakeli
 nilikuwa mgumu kuwakubali maelezo hayo kwasababu kwanza
 sikuamini na niliwaona wale maofisa ni wazushi .
 Ila
 Jana asubuhi nilichokiona kilichokuwa kikifanywa na Mzee wa
 Upako Mbele ya umati watu ,na alivyokuwa ananuka pombe ya
 kuyumbayumba nilikubaliana na Yale waliyonieleza watu wale
 na nikachukua simu nikamupigia mmoja baada ya mwingine na
 kuwaambia kweli waliyonieleza Leo Mungu amenileta eneo la
 tukio nithibitishe Yale waliyonieleza Kuwa Mzee wa Upako
 naye anakunywa Pombe.
 Hata
 hivyo mama yangu Mzazi kwa zaidi ya Miaka mitatu  sasa
 tukikaa wote sebuleni tukiwa tunaangalia Kipindi cha
 Mchungaji Lusekelo kinachorushwa na Channel Ten ,mama
 amekuwa akiniambia huyu Mzee wa Upako ana michanganyo yaani
 alikuwa anamaanisha  Kuwa licha ni Mchungaji ila bado
 anafanya mambo ya kidunia ambayo Mungu hayapendi.
 Basi
 mama akisema hivyo namwambia aache hiyo tabia ya kumsema
 Mzee wa Upako kwasababu Hana ushahidi.Mama anasema haya
 anafunga mdomo ila ipo siku Mungu atamuanika hadharani ndipo
 nitakapoamini.
 Kweli
 kupitia tukio la Jana aliyofanya Mchungaji Lusekelo
 ,Nimelazimika kukubaliana na maneno ya Mama yangu Mzazi
 kuhusu Mzee wa Upako Kuwa licha ni mtumishi wa Mungu bado
 anafanya matendo ambayo Mungu hayataki  mfano
 Fujo, kutoa lugha zisizonastaa,kulipa kisasi wakati Mungu
 anatutaka tusamehe ,tusi lipe kisasi kwa watesi wetu lakini
 Mchungaji Lusekelo alishindwa kuwasamehe watesi wake na
 Akaamua Kupambana na maneno makali huku alipokuwa Kaipamba
 nao wakiwa wanamtazama hawamjibu.
 Lusekelo
 ni binadamu kama Sisi ila tofauti yetu na yeye amejipambanua
 kama mtumishi wa Mungu ambaye ni kiongozi wa Kiroho hivyo
 Hakupaswa kufanya Yale yote aliyoyatenda Jana ambayo
 niliyashuhudia kwa macho yangu ambayo kwa kiasi Fulani
 yalinivuruga  akili na akili zangu za kawaida Jana
 mchana.
 Maana
 sikutengemea kumkuta kiongozi wa dini akiwa Katika Hali kama
 ile aliyokuwa nayo Mzee wa Upako na kufanya matendo Yale
 ambayo uwafanywa  na watu wasiyo na hofu na Mungu
 na hawajashiba  neno la Mungu.
 Hata
 hivyo Fedhea iliyomkuta Jana Mchungaji Lusekelo pia naweza
 Kusema licha Mimi nilikuwa anajitahidi kumuokoa Lusekeo as
 izidi  Kuaibika Mbele ya watu Wengi Kumbe Mungu
  naye aliamua kuruhusu mtumishi wake Huyo wa Mungu
 afedheheke  Mbele ya watu Wengi ili watu wa mjue Kuwa
 mtumishi Huyo wa Mungu ambaye Kutwa anahubiri  
 neno la Mungu naye Si Msafi  na kwamba anayefanya Mambo
 ambayo Mungu ameyakataza.Na kweli Mungu Jana kumdhalilisha
 kweupe Lusekelo. Mungu anatisha.
 Nilikuwa
 najiuliza hivi ndiyo mmoja wa waumini wake angepata fursa ya
 kushuhudia Vituko alivyokuwa akivifanya Mchungaji Lusekelo
 Jana au kama Alikuwepo muumini Akawa anashuhudia tukio lile
 ,wamejisikiaje? 
 Hata
 hivyo tukio la Jana pia limenifanya nikubaliane na Kauli ya
 Rais Mstaafu Jakaya Kikwete alipokuwa madarakani alisema
  hivi : ' Kuna baadhi ya viongozi wa dini Si wa
 safi,ni wachafu na wengine wanauza dawa za
 kulevya'.
  Nimuulize
 Mchungaji Lusekelo hivi kupitia tukio
 lile  ,atapata wapi tena ujasiri wa kusimama
 madhabau ni kuwataka waumini wake wasitumie vileo,wasilipize
 Ubaya kwa Ubaya ,wasiingie Katika vita ya maneno na watesi
 wao?
 Sikutaka
 kuandika makala hii ila ni mejikuta nikijiuliza ni kwanini
 Mungu alipenda nikutane na Mchungaji Lusekelo kwa mara ya
 kwanza ana kwa ana akiwa katika hali ile na akiwa anafanya
 matendo yale ya kishetani?
 Kwanini
 Mungu asingepanga nikutane na Mchungaji Lusekelo akiwa Mzima
 ananukia harufu  ya mafuta mazuri badala ya halufu ya
 kileo na akiwa anafokea na kutoa lugha chafu dhidi ya jirani
 yake na kuziba njia na kusababisha kuziba njia kwa muda na
 hali ya sintofahamu ?
 Na
 Kwanini Mungu hakuruhusu waandishi wa habari wengine wapige
 asubuhi ile jana katika eneo hilo ili washuhudie tukio Lile
 isipokuwa mimi Mwandishi wa Habari Mimi Happiness Katabazi
 peke yangu?
 Nikahitimisha
  kwa Kusema Huyo  ni Mungu ndiyo aliyesababisha
 mimi nikutane na Mchungaji Lusekelo ambaye kwa zaidi ya
 miaka minne tumekuwa tukiwasiliana kwa simu ila jana
 nikakutana naye ana kwa ana na ndiyo  ananisukuma
 niandike makala hii ambayo imeanika   matendo hayo ya
 kishetani yaliyotendwa na Mchunga Kondoo wa Bwana  (
 Lusekelo)  ili watu waumini wake na watu wengine wajue
 matendo yanayotendwa na Lusekelo  nje ya
 madhabau.
 Na
 wao wenyewe wapi me Je  Mzee wa Upako ambaye ni kinara
 wakulusha ' Madongo' Je anastahili kuendelea
 kuaminiwa Kuwa kiongozi wa kidini na Baba wa Kiroho wa
 waumini wake ?
 Nikajikuta
 nachukua Kompyuta na kuacha kwenda GYM kufanya mazoezi ya
 viungo  Jana jioni nikaa chini hadi saa Kumi alfajiri
 wa usiku wa kuamkia Leo nilipomaliza kuiandika.
  Kwa
  kupitia makala hii ambayo itamfedhehesha Lusekelo kwa
 kiasi Fulani  na Imani kwa baadhi ya watumishi wa Mungu
 itazidi kutiliwa Shaka lakini neno la Mungu litasimama
 .
  Uenda
 makala hii  akiisoma anaweza kujirudi na asirudie tena
 Kutenda matendo yasiyompendeza  Mungu Kwani yeye
 Lusekelo ni mtumishi Mungu anapaswa asitende mat endo ya
 kishetani kama Yale  aliyoyafanya  badala yake
 abaki na kazi moja ya kumtumikia Mungu tu .Na ni aomba iwe
 hivyo.
 Kwani
 hata EZEKIELI 3:19 Katika
 Biblia inasema , " Lakini ukimwonya mtu Mbaya ,wala
 yeye hauachi ubaya wake, wala njia yake Mbaya ,atakufa
 Katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako.
 Hivyo
 kupitia kitabu maneno hayo yaliyopo Katika kitabu cha
 Ezekiel ,Mimi nimeitimiza wajibu wangu kwako wewe Mtumishi
 wa Mungu Lusekelo kukuonea ili uache michanganyo ya mambo ya
 kidunia badala yake Ubaki na jambo Moja tu la kumtumikia
 Mungu.
 Mchungaji
 Lusekelo Kumbuka  Biblia inasema Mungu wetu ni Mungu
 mwenye wivu na hataki michanganyo.
 Ukiamua
 kumtumaini / kumtumikia basi Ufuate mafundisho yake na
 uyatii  maandiko yake Kwani Mungu anauwezo wa kukuinua
 na kukushusha  pindi Akiamua.
 Lusekelo
 Mungu ameinua huduma yako lakini sasa umeanza kurudi nyuma
 una michanganyo kama hiyo.Siyo vizuri .Mungu
 hapendi. 
 Nina
 Hakika ungekuwa mzima usingetenda matendo ya kishetani
 uliyoyatenda Jana asubuhi Mbele ya kadamnasi .
 Au
 ulivamiwa na mapepo ndiyo ya kakutuma  utende ushetani
 ule ambao ulikufedheesha ?Kwa lugha nyepesi ulikuwa umelewa
 .Aibu sana mtu wa Mungu.
 Ingia
 ndani tubu kwa Mungu wako atakusamehe songa Mbele ila tu
 wale watu wote waliokushuhudia Jana ukiwa Katika Hali ile na
 kufanya vitendo vile Vya kishetani siyo rahisi tena kuiamini
 huduma ya Kimungu unayoitoa.Nisamehe sana.Licha Nitaendelea
 kukuheshimu na kukupenda.
 Kama
  kweli Mchungaji Lusekelo umeitwa na Mungu umtumikie
 ,sikutegemea kabisa mimi binafsi au umati ule watu huku
 ukiwa umelewa Pombe na huku hujavaa viatu   ukifanya
 ushetani ule hadharani tena asubuhi asubuhi.
 Inatisha.
 Mchungaji
 Luseleko kama kweli umeweza Kutenda ushetani huo wa
 kuporomosha matusi hadharani ,nakuwa Katika Hali ile
 isiyoyakawaida ambayo unafahamu Mungu hataki matendo Yale
 ,Kesho wewe utashindwa kuingia tamaa ya kufanya mambo
 yasiyompendeza Mungu kama kwenda kufanya matendo ya
 kishirikina ili uwapumbaze waumini wako waendelee kuamini
 Kuwa ni mtumishi safi wa Mungu Kumbe unatenda matendo sirini
 yasiyompendeza Mungu?
 Hivi
 Leo hii watu wakikurushia vijembe Kuwa Sadaka zinazotolewa
 na waumini wako pia unazitumia Katika ulevi ,Utakataa au
 utasema wanakuonea wivu?
 Pombe
 inavishawishi Vingi sana na inaweza kumshawishi mtu
 aliyekunywa kufanya chochote anachokisia ikiwemo hata
 kufanya  zinaa.
 Hivi
 ule ushetani ulioutonda Jana  wewe Mzee wa Upako
 ,wakiibuka watu wakisema unywagi Pombe tu pia hata dhambi ya
 uzinzi unatenda ,utakuja kukataa useme wakuzushie?

 Pole
 waumini wa Kanisa linaloongozwa na Mchungaji Lusekelo Kwa
 makala hii Kwani nafahamu baadhi yenu itawakwaza ila ndiyo
 mvumilie ukweli ndiyo huo niliyoohushudia Mimi kwa macho
 yangu nanilitahidi kumsitili kiongozi wenu ili asidhalilike
 bila mafanikio na mwisho wa siku nilichoambulia nikutaka
 kupigwa na vijana wake .
 Ila
 roho yangu nyeupe na wala makala hii haina Lengo la kuwazuia
 muache kumuabudu Mungu kupitia Kanisa linaloongozwa na
 Mchungaji Lusekelo.
 Namimi
 ni madhaifu yangu sikatai ila bado sijafikia Hatua ya kama
 alifikia Lusekelo ya Kuwa mtumishi wa Mungu halafu kufanya
 matendo hayo ambayo kila Mara amekuwa akisimama madhabauni
 Kukataza waumini wake wasiyafanye kwasababu Mungu
 ameyakataza Kumbe yeye Anayafanya .
 Lengo
 la Makala hii ni Kuonyesha Mchungaji Lusekelo ambaye
 anasimamaga madhabau ni anakemea dhambi Kumbe na yeye
 anatenda baadhi ya dhambi.Mtaamua wenyewe.Ila nawashauri
 sote tumuombee maana sote sisi ni binadamu Hakuna Mkamilifu
 .
 Ila
 kuna utofauti wa upokewaji wa Jamii wa baadhi ya matendo ya
 dhambi yanayofanywa hadharani na viongozi wa kidini na
 matendo hayo hayo ya dhambi yakifanywa Na mtu ambaye siyo
 kiongozi wa kidini.
 Mtumishi
 wa Mungu akitenda  dhambi za aina hizo alizozitenda
 Mzee wa Upako Jana za kutukana ,ulevi Jamii zitaipokea kwa
 uzito wa aina yake na kwa Mshangao mkubwa sana.
 Hakuna
 ubishi Mchungaji Lusekelo umefedheheka Jana tena sana Katika
 eneo unaloishi Kawe Beach Karibu Univeristy of Bagamoyo na
 Redio Times .Kaa utulie,maana Hasira ya Mungu Jana
 imekushukia ,tubu Mungu atakusaidia uondokane na shetani wa
 Kupenda Konyagi na aina nyingine za Pombe Kali.
 Mchungaji
 Lusekelo kama utashindwa kuachana na anasa za Dunia basi
 achana na Kazi ya Mungu ili uwe huru kufanya mambo ya anasa
 kuliko Jumapili na siku za katikati ya wiki Una
 Simama  madhabauni unaubiri neno la Mungu Kumbe
 ukitoka madhabauni unaenda kufanya mambo yasiyompendeza
 Mungu ukiwemo Kunywa Pombe.
 Mchungaji
 Lusekelo jana kweli ilikuwa ni mara yako ya kwanza kunywa
 pombe kwa kiwango kile hadi zikakutuma kufanya matendo yale
 hadharani ambayo Mungu hapendi?
 Je
 Mchungaji Lusekelo jana ni mara yako ya kwanza kurudi
 nyumbani kwako saa moja asubuhi ? Maana miminilikufika
 nyumbani kwako saa moja asubuhi huku nikiwa nimekubeba
 baadhi ya vitu vyako kama funguo wa gari ,miwani  huku
 wewe ukiwa umebeba Kikabu chenye chupa za maji ya kunywa
 ;
  Baada
  ya kufanikiwa kumuondoa Kwenye eneo la tukio la ugomvi
 uliotokea na Kisha baada ya kukufikisha ndani ya nyumba yako
 wewe na vijana wako wewe ukatoka miguu pekupeku bila kuvaa
 viatu maana viatu ulikataa kuvaa nimevishika mkononi mkarudi
 tena eneo la tukio huku ukiwa Ujavaa viatu unakanyaga matope
 na Mvua inatunyeshea unafoka Katika nyumba ya jirani yako
 kuishinikiza walinzi wakifungulie Mlango uwaonyeshe
 Kazi?
 Nakupenda
 kwasababu unapenda kuzungumza ukweli na mimi naupenda ukweli
 .
 Hivyo
 nakushauri jirekebishe ,tubu kwa Mungu wako, na ukipata muda
 omba msamaha majirani zako kwa Usumbufu uliowasababishia
 Jana asubuhi wakuwazibia njia wenzio wasiende makazini na
 Magari Yao kwasababu Lako ulilipaki katikati ya barabara
 kumalizima tangu saa 12 asubuhi hadi saa mbili  huku
 ukisikia hutaliondoa Hilo Gari Hali RPC Sirro,Rais Magufuli
 waje kuliondoa. Nilikushuhudia ukiyasema haya sina Sababu ya
 kunisingizia .
 Pia
 Hao vijana wako unaoishi nao hapo ndani baadhi yao wana
 akili mbovu wote watatu waliotufungulia geti kwasababu wao
 waliochangia kukurudisha tena   eneo la ugomvi Matokeo
 yake  ukaenda kudhalilika zaidi wakati Mimi
 nilifanikiwa kukuondoa  mapema eneo la tukio mapema na
 watu walikuwa  wachache na Magari yalikuwa hawajaanza
 kupita Wingi Katika njia ile .
 Vijana
 Hao kama wangekubali ana na ushauri wangu niliyotoa wakati
 nome kufikisha ndani kwako wa kukuingiza ndani na kukufungia
 na Kisha wao vijana ndiyo ni wapeleke eneo la tukio niwape
 ufunguo wa Gari la Baba Yao Mchungaji wa Luseko wafike eneo
 la tukio wachukue Gari walioleta nyumbani bila kujibizana na
 watu kwani lakini walinipuuza Matokeo yake ndiyo hayo umati
 ulifurika ukakushuhudia ukibwatuka .
 Polisi
 wa Kituo cha Kawe Dar es Salaam wakaitwa na wasamalia wema
 kwa siri wa kakukuta  eneo la tukio ukibwatuka
  wakakupeleka kituoni ukiwa bado pombe hazijakuisha
 ukaifadhiwa  Kituo hapo kwa muda  ukasababisha
 hata Polisi ambao walikuwa hawafahamu Kuwa unakunywa Pombe
 wakajua,wakakudharau maana matendo yako ya Jana
 yalitukanisha pia watumishi wa Mungu .
 Mchungaji
 Lusekelo na wale vijana wako mngeuzingatia ule ushauri wangu
   Kuwa uende ndani ukaoge kisha ukalale  ile saa
 Moja asubuhi maana ulikuwa umechoka ungefanikiwa kukwepa
 Kadhia na Fedhea hiyo.
 Mchungaji
 Lusekelo wewe ni mtumishi wa Mungu ,jiheshimu ,usijaribu
 kumgeuza Mungu Kuwa ni Mwanasesele labda aoni mambo
 unayoyafanya Gizani.Mungu siyo Mwanasesele anatuona yote
 tunayoyafanya hadharani na Gizani Akiamua kukuumbua
 anakuumbua na wewe Jana ni Mungu Yule ndiyo aliyekuumbua
  hadharani kwakuonyesha wewe ni mtumishi wa Pombe,
 Haukulala nyumbani umerudi nyumbani kwako asubuhi, umeenda
 kufanya Fujo nyumbani kwa jirani na matusi ukayamwaga na
 ukawakera watumiaji wa barabara hiyo.Pole sana.

 Na
 kukubaliana  na maneno haya yaliyoandikwa
 Katika  MITHALI 20: 1 Katika Biblia inasema :
 " Mvinyo hudhihaki ,kileo huleta ugomvi; Na akosaye
  kwa vitu hivyo Hana Hekima".
 Kwasababu
 maneno hayo yametimia kwa Lusekelo ambaye alikuwa amepata
 kileo amefanya ugomvi na alipofanya ugomvi Jana
 alithibitisha umati ule wa watu  Hana Hekima Kwani
 Angekuwa na Hekima asingekubali kufanya ushetani ule
  ambao umefedheesha Vya kutosha.
 Naitimisha
 kwa kutoa ushauri wa viongozi wa dini akiwemo Mchungaji
 Lusekelo kama mmeamua kumtumikia Mungu basi mmtii Mungu
 kweli kweli Kwani sisi waumini wenu tunamuamini Mungu na
 Nyie viongozi wa dini sasa mnapokuwa mnafanya mambo ya
 kishetani Mnatupa wakati mgumu na kutuvuruga akili na
 kusabisha Kondoo mnaowachunga kutawanyika na wengine
 wanaamua kurudi kwa shetani. Mungu alishasema ole wake
 Mchunga Kondoo anayetawanya Kondoo wake .
 Matendo
 kama hayo aliyoyafanya Mchungaji Lusekelo ndiyo
 yanayowatukanisha viongozi wa dini nakufanya wasiaminike
 Kumbe siyo viongozi wote hawana uadilifu wapo waadilifu na
 wameitwa kumtumikia Mungu na kuna viongozi ambao wao
 hawajaitwa kumtumikia Mungu na makanisa ni Biashara
 inayowaingizia picha .Mtalaaniwa lazima.
 Mungu
 Ibariki TanzaniaChanzo:
 Facebook: Happy KatabaziBlogg: www.katabazihap py.blogspot.com0716 774494.24/11/2016.

 Sent from my iPad



 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googleg roups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegr oups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/op tout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegr oups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegr oups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/op tout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@ googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@ googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/ optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment