Saturday, 3 May 2014

Re: [wanabidii] Re: [Mabadiliko] SERIKALI INAWADHIHAKI WAFANYAKAZI!

George
Una mawazo mazuri nakuunga mkono, nimkumbushe ryoba kwamba wakati wa utawala wa kibaguzi nchini Africa Kusini pamoja na kwamba walimu waliokuwa wakifundisha shule za weusi wenzetu walikuwa wananyanyaswa na makaburu bado waliendelea kuwafundisha watoto wa walalahoi wenzao. Ili nchi iweze kupata ukombozi wa kweli ni vyema walimu wakajitahidi kuwafundisha watoto wa walalahoi wenzao ili wajitambue. Ukizingatia kwamba watoto wa wakubwa hawasomi kwenye shule za kata ni rahisi kuwafundisha watoto wa walalahoi kujitambua ili nao wawafundishe wazazi wao kujitambua. Mchango wenu walimu tunauthamini sana na hivyo jitoe kulikomboa taifa lililo utumwani mwa ukoloni mamboleo wa mweusi kwa mweusi


2014-05-03 10:42 GMT+03:00 'LINGONET Lindi' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
mfumo wa wakusajili walimu ndio unaowatesa,kuchukua waliofanya vibaya katika mitihani na kuwafanya walimu ni vigumu kutetea haki ya na kujenga umoja kwa sababu wanaona wameingia kwa fadhila za utawala ndio chanzo cha kukosa umoja na mgawanyiko miongoni mwao leo hii.walimu walioingia kwa uwezo wao wanashindwa kuwashawishi walimu walioingia kwa fadhila za viongozi kujenga umoja na mshikamano wa kweli
--------------------------------------------
On Sat, 3/5/14, 'george ramadhani' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] Re: [Mabadiliko] SERIKALI INAWADHIHAKI WAFANYAKAZI!
 To: "mabadilikotanzania@googlegroups.com" <mabadilikotanzania@googlegroups.com>, "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Saturday, 3 May, 2014, 8:35

 Ryoba,Msipofundisha
 kabisa mtakuwa mnawakomoa watoto wa wakulima na watumishi wa
 umma wa kima cha chini wakiwemo walimu! Wataendelea
 kutawaliwa milele kwa sababu ya ujinga!Watoto
 wa wakulima na watumishi wa umma wa kima cha chini
 wanahitaji kufundishwa kwa bidii, ndipo watakapopata ufahamu
 wa kujitambua wao ni nani na wanapaswa kufanya nini ili
 kuondokana na utawala
  wa kifisadi! Mtu anapokuwa mjinga inakuwa rahisi
 kutawaliwa kwa sababu hakuna anachojua kuhusu uendeshaji wa
 serikali kifisadi. Kashfa kama za EPA, Richmond/Dowans,
 Rada, Twiga hai, biashara ya pembe za ndovu, madawa ya
 kulevya, Mabilioni yaliyofichwa Uswis nk,
 zisingeweza kuibuliwa na watu wajinga.Endeleeni
 kupigania haki zenu kama walimu na watumishi wa umma kwa
 ujumla lakini msiache kuwafundisha watoto wetu, mtakuwa
 mnawajengea mazingira ya kutawaliwa milele.

   

     On Friday, May 2,
 2014 7:25
  PM, 'Ambokege Benard M' via Mabadiliko Forum
 <mabadilikotanzania@googlegroups.com> wrote:




 Kaka Ryoba napingana na wewe
 kuwa mbele za Mungu makosa yote yako sawa. Si kweli,
 kilicho  sawa ni adhabu za makosa hayo.

 Nawasilisha!



 From:
 'Gikaro
 Ryoba' via Mabadiliko Forum
 Sent:
 ‎5/‎2/‎2014 0:40
 To:
 wanabidii@googlegroups.com;
 Mabadiliko
 Subject:
 [Mabadiliko] SERIKALI
 INAWADHIHAKI WAFANYAKAZI!



 Katika biblia hakuna kosa lililo dogo wala kubwa
 kuliko lingine. Makosa yote ni sawa mbele za Mungu. Jambazi,
 mchawi, fisadi, kibaka na mzinzi, wote watapata hukumu iliyo
 sawa sawa. Dhana hii ni tofauti na jinsi tunavyoichukulia
 hapa duniani ambapo kila mtu huadhibiwa kulingana na uzito
 wa kosa alilotenda.
  
 Kosa kubwa kuliko yote hapa Tanganyika ni kuendelea
 kuikumbatia serikali dhaifu na ya kifisadi inayoongozwa na
 CCM. Serikali hii 'sikivu' imeshindwa kabisa kuboresha
 maisha ya wafanyakazi katika nchi hii. Kila mwaka tunaambiwa
 serikali haina fedha huku tukishuhudia ufisadi wa kutisha,
 matanuzi ya kipuuzi ya viongozi wa serikali, kulipana posho
 kubwa kubwa, misamaha ya kodi, ufisadi na maovu mengine kama
 haya yakitendwa na serikali ya CCM kila kukicha. Yote haya
 yanafanyika kwa gharama za wananchi na mwisho wa siku
 wananchi wameendelea kuishi maisha ya kusikitisha wakati
 nchi ikiwa imebarikiwa kuwa na rasimali kedekede kama vile
 almasi, misitu, tembo, twiga, dhahabu, tanzanite na utajiri
 mwingine chekwa!
  
 Kitendo cha serikali ya CCM kugoma kuongeza
 mishahara ya watumishi kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015 ni
 uhaini, ugaidi na uuaji ambao haukubaliki hata kidogo.
 Watumishi wa umma wamekuwa wakiishi kama yatima katika nchi
 hii huku kikundi kidogo cha mafisadi wasiozidi 50
 wakiendelea kutumbua rasimali za taifa na kuishi kama vile
 wako peponi. Ni lini hasa serikali hii ya kijangili itaacha
 kuwadharau, kuwanyonya na kuwaonea wafanyakazi katika nchi
 hii kwa kuthamini mchango wao katika maendeleo ya
 taifa?
  
 Mwaka wa jana tumeshuhudia serikali hii ikigoma
 kupunguza kodi ya mishahara na badala yake ikapunguza kwa 1%
 tu, kiwango ambacho ni sawa na bure. Tumeshuhudia wajumbe wa
 Bunge Maalum la Matusi (BMM) wakilipwa mamilioni ya shilingi
 kwa ajili ya kutukana tu na kazi hiyo ya kutukana wameifanya
 kwa muda mrefu hadi imebidi waongezwe muda mwingine wa
 kuendelea kutukana na kukejeli maoni ya wananchi. Pesa kama
 hizi zinazopotea bila sababu ya msingi, zingepaswa zitumike
 kuboresha mishahara ya walimu. Walimu tumekuwa tukiishi kama
 wakimbizi. Huwezi kuamini kwamba mshahara wa mwalimu mwenye
 shahada hauzidi Tsh 300,000 kwa mwezi. Kila mtu ni shahidi
 kwamba wajumbe watukanaji wa bunge la katiba wanalipwa zaidi
 ya kiasi hicho cha pesa kwa siku wakati mwalimu
 anayeeelimisha taifa hulipwa chini ya kiwango hicho kwa
 mwezi na wakati mwingine
  kukaa zaidi ya miezi 6 bila kulipwa mshahara. Jamani, usawa
 wa binadamu upo wapi katika nchi hii?
  
 Natoa wito kwa wafanyakazi wote, hasa walimu,
 kujitahidi kuwahi kufika kazini. Mkifika kazini tieni saini
 kwenye vitabu vya mahudhurio, kisha endeleeni kupiga soga
 mpaka muda wa kazi unapoisha mrudi majumbani kwenu. Ndio.
 Hatuwezi kila siku tuwe tunatumiwa na mafisadi kama ngazi ya
 kupandia na kuning'inia madarakani huku sisi tukiendelea
 kuishi maisha ya dhiki. Ifike wakati walimu tujitambue na
 tukatae kunyonywa na mafisadi ilhali tunao uwezo wa kukataa
 unyonyaji huu. Mkakati huu wa kutofundisha utasaidia
 kuzalisha wajinga na wajinga wakishakuwa wengi itakuwa sio
 rahisi kutawalika. Hapo ndipo sasa wafanyakazi tutakapoanza
 kuthaminiwa. Malipo yetu yataboreshwa na tutakuwa
 hatucheleweshewi mishahara. Ule utaratibu wa kufundisha
 chini ya kiwango umeonekana kwamba haulipi tena. Kufundisha
 chini ya kiwango huzalisha watu wenye elimu
  nusu ambao ni rahisi kutawalika. Ni bora sasa tuanze
 mapango mpya (BRN) wa kutokufundisha kabisa ili tuzalishe
 vilaza halisi wasiotawalika tupate
 kuheshimiana.
  
 SOLIDARITY FOR EVER!






 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment