Tuesday, 20 May 2014

Re: [wanabidii] KASHFA YA ESCROW ISITUVURUGE

Basi Happiness. Usiangaike


Sent from Samsung Mobile



-------- Original message --------
From: 'Happiness Katabazi' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
Date:
To: wanabidii@googlegroups.com
Subject: Re: [wanabidii] KASHFA YA ESCROW ISITUVURUGE


Asante kwa kusoma ila namimi sikubaliani na mtazamo Wenu ila na heshima.minataka Kuonyesha nimekosea para gani.ili Niobe kweli nimekosea.mkieleza kijumlajumla siwawezi.ni kweli nimesema sikubali wala sikatai Kuwa tuhuma zilizoibuliwa na rafiki yangu Kafulila Kuwa ni za uongo au ukweli kwasababu Tayari serikali na Bunge kupitia Mh.makinda na Pinda wameishaigiza TAKUKURU na CAG wafanyeni uchunguzi, Ndio kwanza wapo Kwenye uchunguzi lakini baadhi yenu mmeishatoa hukumu.Misio wa hivyo naheshimu Sheria na vyombo husika kwasababu vimeanzishwa KWA Sheria za nchi,papara ya nini.tusubiri ripoti ya uchunguzi Ndio tutafanikiwa ni kweli au uongo.kwani ni uongo hapa nchini Hakuna wanasiasa uchwara ambao wanapenda kudandia Gari KWA Mbele?Najiamini Makala yangu ipo sahihi anayepinga aichambue nimekosea wapi.ni kweli inawezekana Ina matatizo proof leading but in law we sa that is human error ,I will go and make a correction.

Sent from my iPad

On May 20, 2014, at 9:56 AM, "'Jovi kamuntu' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Hapiness Katabazi,

Kama Happiness alikuwa ana cha kuandika ungeacha tu. Kwasababu makala yake imeenda mbele na kurudi nyuma. Hapingi wala hakubali

Mimi sikuelewa huyu Happiness ana maana gani.
 
Jovin Bifabusha

DIRECTOR
KWF
P. O. Box 313
Skype: jovin.bifabusha
Karagwe, Tanzania
+255 784 709200
On , 'jabir yunus' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:


Kasoro ya kuumiza ktk makala ni kutumia haki yake vibaya.
 
Ameamua kueleza kwa kuzingatia aspect ya UTASHI wa SHERIA, ila amepita akichomeka vijembe vilivyoleta aspect ya vijembe vya kisiasa vya kukandia upinzani.
 
Sikubali kinachosemwa kaandikiwa makala. Hapana. Ni mali yake aliyoiandika mwenyewe. Sema binafsi sijapenda kusoma makala iliyojaa typographical errors za kizembe.
 
Kwako Mpiganaji, soma tena na tena kabla hujatia kitu chako mtandaoni. Wanakusoma watu!
 
Jabir+

From: 'Julius Mtatiro' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Monday, May 19, 2014 1:06 PM
Subject: Re: [wanabidii] KASHFA YA ESCROW ISITUVURUGE

Obvious, hii makala mwandishi ameandikiwa na ina malengo maalum. Haiwezekani leo hapa Tanzania mwandishi wa habari mzoefu kama Happiness Katabazi akaanza kujinasibu kuwa kelele za wanaharakati na viongozi mbalimbali juu ya ESCROW ni za kutunga.

Nchi hii ina safari ndefu mno na wengi wetu wanatumika kuitafuna hadi itakapokwisha.

-----------------------------------------------------
Julius Sunday Mtatiro,
Deputy Secretary General, 
The Civic United Front (CUF),
Tanzania Mainland, 
P.O Box 10979, 
Dar Es Salaam - Tanzania. 

Office Tel;   +255222862506,                  
Phone;       +255717536759
Email;        juliusmtatiro@yahoo.com 
Twitter;       https://twitter.com/Julius_Mtatiro 
Face book; https://www.facebook.com/julius.mtatiro 
Website;    https://www.cuf.ot.tz/
    

On 19 May 2014, at 9:00, "'Happiness Katabazi' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

KASHFA YA ESCROW ISITUVURUGE

Na Happiness Katabazi
MIONGONI wa Wimbo unaotamba hapa nchini ni Homa ya Dengue na kile kinachoitwa eti ni vigogo wa serikali  wanaotuhumiwa kuhusika Katika kashfa  ya ufisadi  wa Sh Bilioni 200  Katika Akaunti ya Baraza la Usuluhishi la Migogoro ya Kibiashara (ESCROW) ya Benki Kuu (BoT).

Makala yangu itazungumzia Wimbo huo wa pili wa kashfa ya ESCROW ambayo  Mbunge wa Kigoma Kusini(NCCR-Mageuzi), David Kafulila amedai Kuwa ndiye yeye ameiibua kashfa hiyo  ambapo  aliwataja wahusika wakuu wa kashfa hiyo Kuwa ni  Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospter   Muhongo na Katibu Mkuu wake, Eliachim Maswi, Waziri wa Fedha Saada Mkuya, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Benno Ndullu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Jaji  Frederick Werema na Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba.

Kafulila alisema  kuwa ufisadi huo ni lazima mbivu na mbichi zifahamike, na kwamba haungi mkono uamuzi wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wa kuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuchunguza suala hili kwa kuwa linagusa mamlaka kubwa katika dola, badala yake iundwe Kamati Teule ya Bunge.

Muda mfupi baada ya Kafulila kutoa tuhuma hizo Bunge, hakukubaliana na ombi la Kafulila lililotaka iundwe Kamati Teule ya Bunge na badala yake akaiagiza TAKUKURU na OFISI ha CAG Ifanye uchunguzi wake ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo.

Kwa jicho la Sheria tuhuma zilizotolewa na Kafulila zitabaki Kuwa tuhuma, na Kafulila atahesabika kwanza Kuwa yeye ni mtoa  taarifa za tuhuma hizo.Hivyo kitendo Cha Kafulila kunukiliwa na Gazeti hili toleo la Jumatano ya wiki hii Kuwa   uamuzi huo wa Pinda una Mashaka makubwa na kwamba tuhuma hizo zinahusu viongozi wakubwa wa dola hivyo eti ni Vyema  Kamati ya Teule ya Bunge iundwe uchunguze siyoni Kama Ina mantiki.

Kwani TAKUKURU imeanzishwa chini ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana Rushwa ya Mwaka 2007 Namba 11/2007.Na kifungu Cha 7 Cha Sheria hiyo kimeanisha Kazi za Takukuru na miongoni mwa Kazi za Takukuru ni kufanya uchunguzi makosa ya kula Njama Kutenda kosa, kuchunguza tuhuma za makosa ya rushwa yanayowahusu maofisa wa serikali.

Aidha OFISI ya CAG nayoilianzishwa na inayo majukumu yake mengi tu ikiwemo ya kukagua mahesabu Katika Fedha za serikali na imekuwa Ikitimiza majukumu yake na kutoa taarifa zake kwa umma.

Na Taasisi hizo zimeanzishwa kwa mujibu wa Sheria zilizotungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kafulila ni miongoni mwa wa Bunge wa Bunge Hilo.

Sasa Inashangaza  Kama siyo kutisha kusikilizwa  mtunga  Sheria Huyo Akisema uamuzi huo wa Pinda una Mashaka kwasababu yeye alikuwa akitaka Bunge iunde Kamati Teule.

Kama Kafulila alikuwa Hana Imani na Takukuru, CAG ni kwanini alitoa tuhuma hizo bungeni akitaka mbivu na mbichi sijulikane? Kumbe anaamini Takukuru, CAG ni wa chafu ni kwanini aliibua tuhuma hizo tena akitaka uchunguzi ufanyike? Hivi MWISHO wa siku alifikiri Takukuru, CAG hazitausishwa Katika uchunguzi huo

Tuhuma hizo zinahusu Fedha za serikali , Ofisi  ya ya CAG lazima ili usiishie mAana ipo pale kwa kutazama matumizi ya Fedha za serikali zimetumika Kama iliyokusudiwa?

Maana hata Kama Kamati Teuli ya Bunge ingeundwa Mwisho wa siku ripoti hiyo ya uchunguzi wa Kamati Teuli ya Bunge Ingepelekwa Takukuru au Polisi ili zichunguze kuona je kuna ushahidi wa kutosha wa kuweza kuwafungulia Mashitaka watuhumiwa? maana Polisi  na Takukuru Ndio wenye majukumu hayo Kimsingi.

Pia Itakumbukwwa kashfa ya wizi Katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), iliibuliwa Bungeni, Kamati ya Teule ya Bunge haikuundwa Matokeo yake Rais Jakaya Kikwete alitenda TIMU ya Uchunguzi wa tuhuma hizo ambayo ilishirikisha polisi, Wanasheria toka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na tasisi nyingine za serikali ambayo ilikuwa na Ofisi zake Mikocheni ambapo ili fanyakazi yake vizuri  Mwisho wa siku Uchunguzi huo ulimfanya Mkurugenzi wa Mashitaka , Dk.Eliezer Felelshi Kufungua jumla ya Kesi 12 za EPA m Novemba 4 Mwaka 2008  ambapo hadi sasa jumla ya Kesi Nne zimetolewa hukumu na baadhi ya washitakiwa walipatikana na hatia za makosa waliyoshitakiwa na wengine waliachiwa Huru kwasababu ushahidi haukuwagusa.

Mfano mwingine ni tuhuma za mkataba wa kampuni ya Richmond Ambapo kelele zilipigwa na wabunge hadi Kamati Teuli ya Bunge ikaundwa Mwaka 2007 na Mwanzoni Mwaka 2008 Kamati Teuli ikabainika kulikuwa na ouzo Katika mkataba huo na kumtaka Aliyekuwa waziri makuu Edward Lowassa ajipime na Kamati hiyo ikaamuru Wamiliki wa kampuni hiyo Naeem Gire na Mohamed Gire na baadhi ya Maofisa wa serikali wawajibishwe  Hali iliyosababisha Lowassa kuwajibika Kuwajibika kwa kujiudhuru   wadhifa  huo ambao alidumu nao kwa Kipindi  kifupi sana.

Baada ya ripoti ya Kamati hiyo kusomwa, baadhi ya wabunge kwasababu wanazozijua wa kaanza  kuishinikiza Takukuru iwashitaki watu Hao Hali iliyosababisha Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru , Dk.Edward Hosea na baadhi ya wabunge kuingia Kwenye malumbano Kwani Hosea alikuwa akitaka Takukuru iachwe ifanyekazi yake kwa  Uhuru na siyo kuingiliwa na wanasiasa Hali iliyosababisha kila kukicha kukimbia wabunge hao wakawa wanaishambulia  Takukuru na Kumbe wabunge Hao walikuwa wa mama  zao chafu za kuaribiana kisiasa.

Wananchi ambao walikuwa hawaelewi Njama hiyo waliwaunga mkono wabunge Hao wengine ambao walipachika jina la ' wabunge wanaopambana  na  ufisadi", Leo hii wanasiasa Hao wapo  kimya utafikiri ufisadi ndani ya nchi hii umekwisha.Dhambi sana.

Mwisho wa siku Takukuru iliamua kumfungulia Kesi ya Kutoa taarifa za uongo Kwenye Kikao Cha Tenda Cha Tanesco kuhusu uwezo wa kampuni ya Richmond, mshitakiwa alikuwa ni Neem Gire Mwaka Juzi Hakimu Mkazi wa Mahakama Ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Waliarwande Lema alimuoa Gire Hana Kesi ya Kujibu  na Mkurugenzi wa Mashitaka DPP- Dk.Feleshi hakulidhika na uamuzi huo anakimbilia Mahakama Kuu Ambapo Jaji Lawrence Kaduri alitenga uamuzi huo na akaamuru jarada la Kesi hiyo lirudishwe Mahakama ya Kisutu na Gire aanze kujitetea na Gire naye kupitia Wakili wake Alex Mgongolwa hawakubaliani na uamuzi wa Mahakama Kuu, wamekimbilia Mahakama ya Rufaa.

Kwa  hiyo binafsi naweza Kusema Kuwa sikubali Kuwa tuhuma ni za kweli na sikatai Kuwa tuhuma hizo zilizoibuliwa na Kafulila  Kuwa ni za uongo Katika Hatua hii ya awali.

Nasubiri   vyombo vyenye mamlaka ya kufanyia uchunguzi  zitakapotoa  ripoti za uchunguzi wake.

Kwani tuna Mifano hayo ambayo inafunza kupitia wanasiasa wetu ambao Walijifanya ni mabingwa wa kuibua kile wanachokiita ufisadi  wakati Sheria zote za Tanzania ikiwemo  Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya Mwaka 2002 , haina kosa linaloitwa ufisadi. Sijui wenzetu hawa kosa la ufisadi wanaotaka watu washitakiwa nalo sijui wanakipata katika kifungu gani na cha sheria gani.

Mbunge Zitto Kabwe aliuaminisha umma Kuwa Ana ushahidi kuhusu Majina na namba za Akaunti za watu walioficha  Fedha nje ya nchi na baadhi ya watu waliomua mini, lakini siku zote njia ya muongo ni Fupi, Mwanasheria  Mkuu wa Serikali Jaji Werema aliliambia  Bunge Kuwa Zitto ni muongo aliwasilisha kumuita  Ofisini kwake na akamtaka atoe ushahidi chini ya kiapo  , Zitto akasema hana ushahidi, na hadi Leo kimya kabisa utafikiri Zitto  siyo yeye Aliyokuwa akibwatuka  majukwaa na kujinadi Kuwa anaushahidi wa Majina ya walioficha Fedha nchini Uswiss.

Pia kuna wanasiasa wengine ambao Walijitapa ndani na nje ya Bunge Kuwa wanaushahidi wa Majina ya watu walioiba fedha kwenye akaunti ya EPA kupitia kampuni ya Kagoda hadi Leo hii hawajaenda kutoa ushahidi thabiti Katika vyombo hisika, Wanaishia kubwatuka majukwaani na kuwaaminisha Ujinga huo baadhi ya  waandishi wa Habari ambao hawajui kilichopo nyuma ya tuhuma zinazoibuliwaga na baadhi ya wanasiasa.

Wiki iliyopita Spika Anna Makinda  Mara Tatu wakati akiendesha Bunge aliwataka baadhi ya wabunge waache kutumia na baadhi ya watu walionje 

0 comments:

Post a Comment