Sunday, 6 December 2015

[wanabidii] KESI RUFAA YA TALAKA DHIDI YA MTEMBEI YAAHIRISHWA

Habari za asubuhi,

Tafadhali pokea CODES hapo chini



<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/12/Wooden-Gavel.jpg"><img class="size-full wp-image-152593" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/12/Wooden-Gavel.jpg" alt="wooden gavel and books on wooden table,on brown background" width="640" height="345" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Na Mwandishi wetu</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>KESI ya rufaa ya madai ya talaka dhidi ya mfanyabiashara na Mkurugenzi wa shule ya  sekondari ya St Mathew, Thadei Mtembei imeahirishwa baada ya wakili wa Mtembei, Mussa Kyoboya kudai mrufaniwa yuko India kwa matibabu.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Temeke, Tarimo.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Katika kesi hiyo, mpeleka rufaa, Magreth Mwangu  anawakilishwa na wakili Chacha Mrungu. Kesi hiyo ilikuja mahakamani juzi ambapo mrufaniwa alitakiwa kupeleka majibu ya rufaa.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Hata hivyo, wakili wake alisema majibu hayako tayari kwani kuna vipengele ambavyo alitakiwa kusaini, lakini ilishindikana kutokana na kuwa nchini India kwa matibabu. Kesi hiyo imepangwa kuendelea Desemba 16 mwaka huu.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Awali, kesi hiyo ilisikilizwa katika  Mahakama ya  Mwanzo Kizuiani mbele ya hakimu  Rajab Tamaambele, ambapo Mwangu na watoto wake walionekana hawana haki, kwa madai sio mke halali na watoto hao ni wa zinaa kutokana na kuzaliwa nje ya ndoa.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Katika madai ya msingi, Mwangu anataka talaka, mgawanyo wa mali na matunzo ya watoto.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Katika sababu za rufaa, mrufani alieleza kusikitishwa na maamuzi yaliyotolewa na Mahakama ya Mwanzo Kizuiani Septemba Mosi mwaka huu, kwa hakimu kukosea kisheria kwa kutosaini nakala ya hukumu ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa saini za wazee wa baraza.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Sababu nyingine ni Mahakama kukosea kisheria kwa kunyang'anya haki ya watoto kwa kutotoa matunzo ya watoto kwa mama, ambaye anaishi na mrufaniwa kwa miaka 20 na kuvunja Sheria ya Mtoto Namba 21 ya mwaka 2009. Maamuzi ya Mahakama ya Kizuiani yalishindwa kufuata sheria kwa wazee wa baraza kushindwa kutoa maoni yao.</strong></span></p>

--
Zainul A. Mzige,
Operation Manager,
MO BLOG,
+255714940992.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment