Thursday 1 October 2015

Re: [wanabidii] 2015: NI KURA YA MAAMUZI MAGUMU

Natamani kungekuwa na mbadala kwenye haya mabadiliko...Mimi binafsi watu waliotumua mfumo mbovu kutufikisha hapa haijalishi wanaahamia wapi...hao sio jibu wala mabadiliko tunayoyataka. Nakubali wananchi wamechoka na mfumo mbovu Wa ccm lkn majibu sio cdm chini ya EL

On 10 Sep 2015 15:40, "'ananilea nkya' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Ndugu Kim,

Neno mabadiliko  katika muktadha wa uchaguzi  Tanzania mwaka  huu 2015 linatumika kumaanisha wananchi kuchagua  serikali mpya  tofauti na serikali ya CCM iliyoko madarakani ambayo ilikataa kuandika Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi.

Katiba Mpya itaweka misingi ya kuzuia serikali kuwa chanzo  ufisadi wa  fedha za umma, watawala kujitajirisha na kuwatajirisha  wawekezaji kutoka nje  kwa kutumia rasilimali za nchi yetu  huku mamilioni ya wananchi wakibaki masikini wa kutupa.

Mfano ufisadi wa   mwaka jana 2014 wa Tegeta escrow bilioni 306, ufisadi wa  Richmond bilioni 172 mwaka  2008 na ufisadi wa EPA bilioni 133 mwaka 2005 na hakuna aliyefikishwa mahakamani.

Mabadiliko ya  kupata serikali  inayoongoza na  vyama vingine tofauti na CCM  ikiandika Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi ---Katiba hiyo  itaweka misingi  ambayo pamoja na mambomengine madaraka ya Rais yatapunguzwa—kuzuia Rais kuwa Mungu mtu.

Kadhalika madadiliko  yataweka mihimili  isiyoingiliana  ya utawala—serikali—bunge na mahakama HIvyo  serikali  ikifanya ufisadi kama ule wa Tegeta escrow na EPA  watawala hawatakwepa mkono wa sheria  kama walivyokwepa.

Kadhalika mabadiliko   yatazuia   watawala wachache  wakijitajirisha kwa kutumia fedha za wananchi  kujilipa mishahara mikubwa, mafao na marupurupu wakati  watumishi wengine wa umma madaktari, wauguzi, walimu, polisi na wananchi wengi wakibaki maskikini.

Pia Katiba Mpya  itaweka misingi mizuri  ya kuwepo usawa wa kijinsia katika uongozi hasa 50 kwa 50 wabunge wanawake na wanaume  majimboni badala ya hili changa la macho ambalo baadhi ya vyama vinajidai eti kwa kuweka wagombea wanawake ni usawa wa jinsia.

Je inawezekana kuwa  na usawa wa jinsia endelevu kama haijaandikwa kwenye Katiba ya nchi? Kama kweli serikali CCM walikuwa wanataka nchi iwe na usawa wa jinsia katika uongozi ni kwa nini waliikataa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi ambayo ilikuwa imependekeza utaratibu mzuri kabisa wa kupata asilimia 50 kwa 50 ya wanawake na wanaume bungeni kutoka majimboni?

Hivyo mabadiliko  wanayoyataka wananchi wanaosumbuliwa na umaskini hapa nchini   wao wenyewe wananchi  wamejipanga kuweka msingi wake hapo hapo tarehe 25 Oktoba 2015 kwa  kuiondoa CCM madarakani   na kuweka  serikali ya vyama vinavyounda UKAWA (CUF, NCCR Mageuzi, CHADEMA  na NLD) ambavyo  vilipigania  Katiba Mpya inayotokana na  maoni ya wananchi na vimeahidi  kwamba  wakichaguliwa Katiba Mpya  ya wananchi itaandikwa.

Hivyo yeyote anatumia neno mabadiliko kwenye kampeni zake ajuwe  akichaguliwa atatimiza yaliyobebwa katika tafsiri hii.  Kinyume chake hayo siyo mabadiliko wanayoyataka wananchi.   Mungu ibariki Tanzania.


Ananilea Nkya
 E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com

--------------------------------------------
On Thu, 9/10/15, De kleinson kim <dekleinson@gmail.com> wrote:

 Subject: Re: [wanabidii] 2015: NI KURA YA MAAMUZI MAGUMU
 To: wanabidii@googlegroups.com
 Date: Thursday, September 10, 2015, 2:45 PM

 Kwanza
 MABADILIKO ni nini?
  Tukisema TUNATAKA MABADILIKO, maana yake ni
 nini? ya wapi? kwenye nini? yatamgusa nani? yatatuchukua
 muda gani? yatatokea tokeaje?
 Mabadiliko yaweza kuwa baya kwenda zuri au zuri
 kwenda baya, dogo kuwa kubwa au kubwa kuwa dogo, nyembamba
 kuwa pana au....

 Its all about "different" "utofauti wa hiki
 kilichopo". nikikosea nisahihishwe. mie sio mtaalam wa
 lugha!!
 Mnazi awaye yeyote iwe wa Chama au mtu, aandike
 akituelezea vizuuri na kwa ufasaha jinsi watakavyoleta
 MABADILIKO nchini. i mean ameshawishikaje kuwa mnazi wa
 flani/chama flani kuamini watafanya MABADILIKO ndani ya kila
 mmoja wetu ili tukuamini na kukufuata popote ulipo!! Wanazi
 wote hapa mkae mkijua nyie ni mawakala wa HAO mnaowasemea!!
 kwa sababu sie hatumjui yule/wale vizur zaidi yako, umeamua
 kuwa agent wake/wao ina maana unayajua ya kwake/kwao! Latin
 proverb "if you host a guest, host his dog"
 Tukibaki kuainisha MAHITAJI YA NCHI na
 MTU/CHAMA chenye SULUHU yake bila kuijadili, kuchambua na
 kuitafakari SULUHU yenyewe kwa kina, hatuna tofauti na mtu
 anaeajiri bila vyeti na interview. Akiulizwa kwa nini? ati
 " ameahidi ataongezea kampuni faida ndani ya miaka
 5" ****!!! Its the question of HOW not WHO!!! WHO will
 come later to filter HOW!!
 Watanzania tumelogewa wapi??? tunashindwa na
 hesabu ndogo ambazo tunazifanya kwenye maisha ya kila
 siku!!!!!????? Mpaka inakera.



 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment