Tuesday, 22 April 2014

Re: [wanabidii] NILICHOONGEA NA WAANDISHI WA HABARI LEO JUMATATU 21/4/2014

Hawa madogo tunawaona na kuwasikai kwenye vyombo vya habari, ni mkusanyiko wa ama watoto wa walio madarakani wanaoenjoy matunda ya nchi hii wakiambatana na vijana wenye njaa. Ebu angalia wanavyojichanganya kwa maneno

"Power tends to Corrupt, and absolute power corrupts absolutely. Great men are almost always bad men"

Yakimaanisha kuwa; "Madaraka yana tabia ya kuwaharibu walio nayo, na wenye madaraka makubwa Zaidi huharibika Zaidi kwa kuwa hata watu wema hugeuka kuwa wabaya wakishakuwa na madaraka"


Hapa wanachoeleza ni kitu gani? Kwani hao UKAWA wanamadaraka gani?  Wao wenyewe wanaojiita wazalendo wako upande wa waliomadarakani au wasiokuwa madarakani?  Munachofanya ni kuwalinda walio madarakani kwa kuwaunga mkono mkitumia fedha zetu. Mungekuwa wajanja musingenukuu maneno hayo hapo juu, inaelekea hamjui munachokifanya



2014-04-22 6:26 GMT+03:00 Fred Hans Kipamila <fhkipamila@yahoo.com>:
Unakataa matusi kwa kutukana wenzako kwa kuwa bwana wako unamuona bora zaidi kuliko wa wenzako. Nani kakupa jeuri hiyo ya kutukana wenzio kama si ulevi wa madaraka aliyokupa bwana wako? Sisi sote ni Watanzania wa Tanganyika na Zanzibar tueshimiane. Anapokosea mwenzetu tumwambie umekosea kwa staha na si kwa matusi. Najua unapata jeuri kwa kuwa mmetengeneza tabaka la watwana na waungwana ambamo mtoto wa muungwana ndiye atarithi madaraka ya baba yake. Kama wewe ni muungwana omba radhi ila kama ni mlevi nyamaza kwa jeuri
--------------------------------------------
On Mon, 4/21/14, Abdalah Hamis <hamisznz@gmail.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] NILICHOONGEA NA WAANDISHI WA HABARI LEO JUMATATU 21/4/2014
 To: wanabidii@googlegroups.com
 Date: Monday, April 21, 2014, 4:51 AM

 NILICHOONGEA
 NA WAANDISHI WA HABARI LEO JUMATATU 21/4/2014Leo
 Nitatumia maneno makali kidogo ili tuelewane kiurahisi.
 Wapinzani wa Nchi hii ni "BAPHOON". Maana ya
 BAPHOON ni Watu au Kundi la Watu linalotumika Kwa Maslahi ya
 Mataifa Mengine Kuangamiza Taifa Lao. Wako Tayari Hata
 Kuchukua Mabomu na kulipua Nchi yao Wenyewe. Hawa ndio
 wanaojiita UKAWA (THE BAPHOON)Imani
 namba Tano na namba nane za Chama Cha Mapinduzi kwa pamoja
 zinasema:Cheo
 ni Dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa
 faida yangu na Nitasema Kweli Daima Fitna kwangu
 Mwiko.Kwa
 tafsiri ya Imani ya Chama tunakubaliana na maneno ya
 Mwanahistoria wa zamani wa Uingereza Lord Acton aliyewahi
 kusema;"Power
 tends to Corrupt, and absolute power corrupts absolutely.
 Great men are almost always bad men"Yakimaanisha
 kuwa;"Madaraka
 yana tabia ya kuwaharibu walio nayo, na wenye madaraka
 makubwa Zaidi huharibika Zaidi kwa kuwa hata watu wema
 hugeuka kuwa wabaya wakishakuwa na madaraka"Na
 sisi Vijana Wazalendo tunasema;
 "Watu wenye Madaraka Makubwa Wakiharibiwa na hayo madaraka
 hulewa hayo madaraka na kuanza hata kutukana kudharau
 waliowapa madaraka hayo. Lakini wenye madaraka makubwa
 wanaojua kuwa madaraka yao ni dhamana, kwanza huwa wapore na
 wanyenyekevu na hubeba dhamana kubwa ambayo wao huona
 madaraka hayo ni Mzigo wala si zawadi."Wapo
 wanaodhani kuwa Vyama vya Upinzani vipo kwa ajili ya Maslahi
 ya Taifa. Wapo wanaodhani Vyama vya Upinzani ndio mkombozi
 wao. Na wapo wanaodhani muarobaini wa matatizo ya taifa hili
 ya kiuchumi, kijamii na kisiasa ni vyama vya Upinzani.
 Ukweli halisi wamepotoka sana. Vyama vya Upinzani vipo kwa
 maslahi yao tu na vimekuwa ni dhaifu kiasi haviwezi
 kuaminiwa kupewa dhamana ya Uongozi wa Taifa hili.Hatuna
 haja ya kuwaambia BAVICHA waombe radhi kwa matamshi yao
 yasiyo na adabu waliyoyatamka jana dhidi ya Rais wa Jamhuri
 na Waziri Mkuu kwa sababu tunajua wanadhani wako sahihi.
 Lakini tunajua wanajua hawako sahihi na wanafanya hivyo ili
 kuwaridhisha mabwana zao ambao wanawatumia wao kutengeneza
 mitaji yao kisiasa. Wao wanabaki tu kama kigenge fulani
 ambacho kama kikiachwa kikue na uwongo wake mwishowe
 kitaaminiwa na hapana shaka nchi hii ipo siku itaongozwa na
 Vichaa.Tuelewe
 Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ndiyo Lulu pekee
 iliyobaki Afrika ambayo imeundwa na sisi wenyewe , kwa hiari
 yetu wenyewe baada ya kukomboa sehemu zake mbili kutoka
 katika Ukoloni. Haiwezekani tuache Muungane uchezewe tu na
 wachache wetu ambao kinachowasukuma ni Uroho tu wa
 madaraka.Tulipoanzisha
 Mfumo wa Vyama vingi, tulidhamiria kuwa na vyama vyenye
 nguvu za dhati ambazo ama zingekuwa kubwa kuliko CCM ili
 kuweza kuiwajibisha serikali sawasawa nayo iwajibike moja
 kwa moja kwa ujenzi wa taifa. Miaka 21 baada ya kuwa na
 mfumo wa vyama vingi, tumekuwa na vyama legelege ambavyo
 havina dira wala mwelekeo badala yake vimejikita katika
 uchochezi na ulaghai. Hali hii inatupa wasiwasi kama kweli
 hivi ni vyama vya siasa ama ni vikundi tu vya harakati
 vinavyofanya siasa. Watanzania wako tayari kuamini Upinzani
 lakini si kwa miaka hii ya karibuni,ni mpaka tutakapopata
 vyama vyenye nia thabiti ya kuleta maendeleo ya nchi hii
 huku vikithibitisha kwamba vitadumisha muungano wa nchi
 mbili serikali mbili na kuheshimu Katiba ya Nchi.Chama
 Cha Mapinduzi kinabaki Imara na Msimamo thabiti wa Kuendelea
 na Jamhuri Muungano wa nchi mbili na Serikali Mbili. Azimio
 la kutaka serikali tatu si mara ya kwanza sasa. Azimio kama
 hili lilikuwepo Mwaka 1993 kwa hoja Binafsi ya Wabunge 55
 (G55) iliyopelekwa na Mh. Njelu Kasaka Mbunge wa Chunya. Kwa
 kikao Cha Bunge cha August 24-27, Bunge liliridhia mchakato
 wa kuanzisha serikali ya Tanganyika. Lakini kwa Uthabiti wa
 CCM ambao ni imara sana sasa kuliko mwaka 1993, kilisimamia
 mfumo wa kubaki na Muungano wa Nchi mbili na Serikali Mbili.
 Msimamo wa CCM wa Mwaka 1993 ni thabiti sana sasa, hatuwezi
 kufufua Tanganyika isipokuwa tutatumia mfumo uliopo kutatua
 kero za Muungano zilizopo. Changamoto kubwa zinazotukabili
 ni za kiuchumi kuliko zilivyo za kijamii na muungano wetu
 sana una nia thabiti ya kijamii kuliko uchumi.Demokrasia
 imechukua njia hadi sasa hata mifumo ya demokrasia imeanza
 kupuuzwa. Nasema inapuuzwa kwa sababu hata Vichaa sasa
 wanaweza kuamka tu na kutoa matamko yasiyo na kichwa wala
 Miguu. BAVICHA ni Vijana wadogo sana ambao hawawezi kuamka
 na kutoa matamko waliyoyatoa ila kwa kutumwa na Bwana zao.
 Na hao Bwana zao wanafadhiliwa na Mataifa ya nje ambay
 hayataki kuona siku moja AFrika inaungana na kuwa taifa moja
 kubwa. Namna pekee ya kufanikisha uovu huo mkubwa dhidi ya
 Afrika, ni kuibomoa Tanzania, na wenzetu hawa wapinzani
 wamekubali kutumika kama vibaraka wa kudidimiza
 Afrika.Hatuoni
 Sababu ya Kukaa Kimya, Sitanyamaza kufumbia macho Ujinga
 huu. Nani kawatuma BAVICHA kutoa Matamko dhidi ya Rais na
 Waziri Mkuu? Nani kawadanganya kuwa eti Mchakato wanaoutaka
 UKAWA ndio Mchakato wanaoutaka Wananchi?Unamsikiliza
 Mh. Lipumba, amejawa maneno kinywani mwake ya uchochezi tu
 wa kidini na ubaguzi wa wazi kabisa. Hizo zote ni hila
 ambazo kama zisipodhibitiwa kwa kuelezwa ukweli wake kama
 hivi, taifa litaangamia. Tumedhamiria kupambana na hili,
 hatutakaa kimya Mpaka watanzania watuelewe na wawapuuze
 wapinzani kwa lugha zao za uchochezi.Kwa
 Nini wakatake kufanyia Mkutano Zanzibar kibanda Maiti na Si
 Dodoma maana wote walikuwepo hapa? Hivi wapi ni Karibu,
 Iramba kwa Tundu Lisu au Zanzibar (Unguja Kibanda Maiti)?
 kuna Umbali gani Hai kwa Mbowe au Tabora kwa Lipumba au
 Vunjo kwa Mbatia ukilinganisha na Zanzibar? Hawa waheshimiwa
 wasitake kulaghai Umma, kuna ajenda wameibeba ambayo
 hawataki kuisema. Warudi Bungeni waje wajenge hoja maana
 Katiba haitapatikana Majukwaani bali kwa kukamilisha
 Mchakato Bungeni na ndicho CCM tutakachofanya. Tunaendelea
 na Bunge na tunakamilisha Mchakato hata wasiporudi.Ikiwa
 wao ni vyama vya kidemokrasia na nia yao ni kujenga
 demokrasia, kwa nini hawataki kukaa meza ya Mazungumzo? kwa
 nini wakimbie mkutano halali wa kidemokrasia wasikae hapo
 wajenge hoja hapo badala yake wanakimbilia eti kwenye
 mikutano ya hadhara? Hapo kuna walakini na demokrasia
 wanayohubiri. Anayehubiri demokrasia lazima awe wa kwanza
 kukaa meza ya mazungumzo. Mumewasikia wakitoa matamko kwamba
 hawako tayari kukaa meza ya mazungumzo na serikali wala CCM,
 hawa ni washari na wanatangaza shari na kisha wanatafuta
 huruma ya wananchi. Hiyo siyo demokrasia ni Vurugu. Uhuru
 bila mipaka i vurugu na Demokrasia bila Utaratibu nayo ni
 vurugu.Tunazo
 tetesi kuwa hivi vyama vinafadhiliwa na wasiotaka kuiona
 Afrika ikiungana na kuwa jumuiya moja kubwa yenye nguvu.
 wanatafuta ucku na Mchana kuisambaratisha Afrika na namna
 pekee ye kuisambaratisha Afrika ni kuisambarataisha Tanzania
 kwa maana Tanzania ndiyo kinara wa Umoja wa Afrika. Kutumiwa
 kwao na Ukibaraka wao uendelee lakini tuko imara sana
 kulinda Muungano wetu. Hawa ni BAPHOON.Lugha
 za kichochezi za wapinzani wananchi wamezisikia. Wamemsikia
 Prof. Ibrahim Lipumba akiweka matabaka ya watu kwa sababu za
 Kidini, wamemsikia Tundu Lisu akipandikiza chuki dhidi ya
 Mwalimu Nyerere na waasisi wa Muungano, Mumewasikia viongozi
 wa CUF, NCCR Mageuzi, wakifanya juhudi za kufitinisha
 watanzania kwa kauli zao ovu. Ufitini wa aina yoyote, uwe wa
 kidini, kikanda, kikabila au haiba ya watu hauna budi
 kupigwa vita kubwa na kila Mtanzania mpenda amani.Wakumbuke,
 Chuki wanazozijenga sasa, itafika mahali zitakomaa na
 zikishakomaa zitaanza kuwa mwiba mkali kwao wao wenyewe. Kwa
 maana wakifanikiwa kupanda mbegu ya chuki miongoni mwa
 watanzania kwa namna yoyote ile, hakuna namna ambayo hao
 waliowapandikiza chuki watawapenda wao. Chuki yao itawala
 wao wenyewe na itaangamiza taifa. Hatuwezi kuacha hili
 litokee tukiangalia kwa macho yetu.Taifa
 halitajengwa na watu waoga wala waongo na wafitini.
 Watanzania wenzangu tujikite katika kujenga uchumi na
 kujiletea maendeleo kwani tukiendelea kuwasikiliza
 "BAPHOON" hawa na kuacha shughuli zetu za
 kiuchumi, ni kujipotezea fursa tulizo nazo kwa faida ya
 wengine. Hawa wanawasumbua nyie mwasikilize, wao shughuli
 zao za NIGHT CLUBS, GUEST HOUSE ZAO, BAR ZAO, CASINO ZAO,
 DALADALA ZAO, MAHOTEL, na BIASHARA ZAO NYINGINE zinaendelea
 kuwaingizia Pesa na wanachofanya ni kuwajaza matumaini ya
 uwongo huku wao wanajaa MAPESA. Kwa kuwa wameamua kutumika
 na mataifa ya nje kuhujumu nchi yao, bado wanalipwa kwa kazi
 yao ya UFITINI. Mapato yao hayayumbi na wala
 hayatayumba.Ewe
 Mtanzania Mwenzangu, Shtuka, Achana na BAPHOON.Mungu
 Ibariki TanzaniaPaul
 C. Makonda
 Katibu Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM
 Mjumbe Bunge Maalum la Katiba




 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.



--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment