Katika kipindi cha miaka kumi iliyopita tumeweza kupiga hatua kubwa katika sekta ya elimu nchini. mafanikio tuliyoyapata ambayo ni matokeo ya kuongezeka kwa shule, idadi ya wanafunzi, idadi ya walimu, vitabu na vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Katika kipindi hicho, Shule za msingi zimeongezeka kutoka shule 14,257 mwaka 2005 hadi kufikia shule 16,343 mwaka 2014.
Hii imefanya idadi ya wanafunzi kuongezeka kutoka milioni 7.54 hadi kufikia milioni 8.23. Kwa upande wa shule za sekondari, idadi yake imeongezeka kutoka shule 1,745 mwaka 2005 hadi kufikia shule 4,576 mwaka 2014. Hali kadhalika, idadi ya wanafunzi wa shule za sekondari imeongezeka kutoka wanafunzi 524,325 mwaka 2005 hadi kufikia wanafunzi 1,804,056 mwaka 2014.
Jumla ya walimu wote wa msingi na sekondari idadi imeongezeka kutoka 153,767 mwaka 2005 hadi 301,960 mwaka 2015. Katika kipindi hicho, vyuo vya ufundi vimeongezeka kutoka 184 mwaka 2005 hadi 744 mwaka 2015. Wanafunzi wa elimu ya ufundi nao wameongezeka kutoka 40,059 mwaka 2005 hadi 145,511 mwaka 2015. Kwa upande wa elimu ya juu, wanafunzi wa vyuo vikuu wameongezeka kutoka 40,719 mwaka 2005 hadi 200,986 mwaka 2014.
Hii ni kutokana na kuongezeka kwa vyuo vikuu na vyuo vikuu vishiriki vimeongezeka kutoka 26 mwaka 2005 hadi 52 mwaka 2015. Upanuzi huu mkubwa katika udahili wa wanafunzi wa vyuo vikuu umewezekana kutokana na kuongezeka kwa bajeti ya Bodi ya Mikopo ya wanafunzi na kuruhusu wanafunzi wa vyuo vikuu vya binafsi navyo wapatiwe mikopo. Bajeti iliongezwa kutoka shilingi bilioni 56.1 mwaka 2005 hadi shilingi bilioni 345 mwaka 2015 na kunufaisha wanafunzi 98,000 mpaka sasa.
Mafanikio haya ni matokeo ya kutoa kipaumbele cha kwanza kwa elimu katika bajeti ya serikali. Leo hii bajeti ya sekta ya elimu ndiyo kubwa kuliko zote nchini ambayo sasa imefikia shilingi trilioni 3.4 ikilinganishwa na shilingi bilioni 669.5 mwaka 2005.
Kweli kabisa Lowasa unautaka urais lakini kuwa mkweli, katika elimu awamu ya nne imejitahidi na atakae kuja anapaswa kuendeleza pale palipofikiwa lakini si kubeza kama unavyofanya wewe,
" Hayo ni kwa ufupi. Wahariri wakuu katika media zote kupitia Jukwaa la Wahariri walikuwepo, na Absalom Kibanda (New Habari) na Nevil Meena (Free Media) ndio walikuwa waratibu wakuu wa mkutano huu."
teh teh teh tehhhh mbio zimeanza pale, kipenga kinalia watazamaji wenzangu.....
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 comments:
Post a Comment