Tuesday 1 July 2014

Re: [wanabidii] FALSAFA YA ACT-TANZANIA NI UNYERERE.

ACT-Tanzani ni nini? Nipo gizani!
 
God created men in LOVE ,let us live with LOVE


On Tuesday, July 1, 2014 11:29 AM, 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:


Sina uhakika kama waTanzania wanaoweza kudanganywa kwa kuamini ACT tanzania kuwa inataka (achilia mbali kuweza) kuufufua uNyerere. Ni kweli chama kama hicho kinatakiwa. na naamini siku moja kitaundwa. lakini pia naamini watu wa kukiunda wako shule ya msingi na wengine matumboni mwa baba zao. mpaka wahamie matumboni mwa mama zao wazaliwe. Ndani ya CCM kuna watu wanatamani hilo lakini hawawezi hata kupata nafasi wala ruhusa ya kufanya hivyo.

Hii itatokea baada ya madhara makubwa ya RUSHWA. hapo ndipo waTanzania wataamua na kulitaka azimio la Arusha. Wakati CCM ilipowarudhisha Kinana na Mangula tulifikiri huo ni mwanzo wa kuelekea huko. Sasa wameisha kuwa maadui wa njia hiyo.
CHADEMA licha ya kutokuwa na mwelekeo wa ujamaa lakini sera zao zilielekea zingeweza kuzaa mwelekeo huo. Sasa wananyang'anywa mwendo huo kwa kuvurugwa.
ACT ni wzkala tu wa maadui wa utaifa wetu. Kwamba wanajua au hawajui hiyo nayo ni siri iliyo sirini


On Tuesday, July 1, 2014 9:05 AM, Abdalah Hamis <hamisznz@gmail.com> wrote:


Falsafa ambayo ina lengo la kulifufua azimio la Arusha(maana limekufa na hakuna chama chochote cha siasa isipokuwa ACT chenye nia la kulifufua)

NA

kuliboresha azimio hilo hata lipate kuendana na hali halisi ya Tanzania ya sasa. ACT-TANZANIA tunaamini kurudi katika misingi ya azimio la arusha, misingi ambayo juu yake ndipo zilipoinuliwa kuta za Tanzania iliyootwa na Mwalimu Nyerere na Shekhe Karume ndio njia pekee na suluhisho la kudumu la kuondokana na maadui wetu kama vile umaskini, maradhi, ujinga, rushwa na upungufu kama si ukosefu wa uzalendo katika nyoyo za watanzania waliowengi. Kupitia azimio la Arusha lililoboreshwa, ACT-TANZANIA inadhamiria kutengeneza umma utakao kuwa tayari kufa kwaajili ya nchi yao, umma utakaofikiria cha kulifanyia taifa lao na si umma wenye uhodari wa kudai haki tu bila kutekeleza wajibu wao kwa taifa lao.

ACT-TANZANIA inaamini mwananchi hawezi kupata uhalali wa kudai haki zake hata zile za msingi kama mwananchi huyo hatekelezi wajibu wake. Mfano mzuri; wazee wetu walianza kwanza kutekeleza wajibu wao kwa kumfukuza mkoloni na Sultani kabla hata hawajaanza kudai haki zao toka kwa serikali za kizalendo. Kwa vyovyote vile bila ya utekelezaji wa wajibu wa kumtoa mkoloni na Sultani kusingekuwa na serikali za kizalendo abadani.

Hii ina maanisha nini? Hii ina maanisha kuwa siku zote utekelezaji wa wajibu ndio huanza na udaiji wa haki hufuata. Kama ndivyo, kwanini kuitoa CCM madarakani na kuingiza ACT-TANZANIA usiwe wajibu wako? Kwanini usiipe nafasi falsafa adhimu ya mwalimu Nyerere ikatunge sera za kulikomboa taifa hili toka kwenye maadui niliowainisha hapo juu kwenye viwanja vya Ikulu yetu takatifu? Cha kuzingatia, unyerere si kutunga sera zilizochini ya falsafa ya mwalimu nyerere tu lakini pia ni kuzitekeleza sera hizo bila kusigana na maadhui ya falsafa tajwa.

Kwa swali lolote kuhusiana na ACT-TANZANIA tafadhali waweza kuniuliza hapa au kwa namba zangu hizo chini.

ACT-TANZANIA, TAIFA KWANZA.
MABADILIKO NA UWAZI, CHUKUA HATUA.
Njano5.
0784845394.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


0 comments:

Post a Comment