Wednesday, 23 April 2014

Re: [wanabidii] BUNGE LA KATIBA NI " KOMEDI" ?

Huyu mwandishi anatwambia Katiba mpya siyo hitaji muhimu sana kwa sasa? Kawaulize wanaokomaa na serikali mbili hadi mate yanawatoka watamwambia kwa nini ni itaji muhimu sana sasa kwao. Kwa waliozoea kushika utamu katiba ni chombo muhimu sana kinachotumiwa na watawala kutawala watawaliwa.

Kwa mwananchi wa kawaida katiba si rahisi kuona kama katiba ni kitu muhimu sanalakini tukumbuke kwamba katiba ndo mwongozo wa kila kitu na hata hayo madawa na huduma nyingine vitaweza kupatikana kwa utaratibu mzuri kama tutakuwa na mwongozo mzuri. Kimsingi kwa wewe na mimi hata nchi ikitawaliwa na jeshi hatuna tatizo kubwa wenye shida ni hao wanaoshika utamu (viongozi) watakosa KUCHUMA KAMA WALIVYOZOEA


2014-04-23 8:52 GMT+03:00 'lucas haule <kisacha2003@yahoo.com>' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Ni;ianza kwa kushangaa, watawala walipoanza kutukana viongozi wa tume badala hoja zilizomo. Nimeona siasa za kizanzibar zikianza kuchomoza na kudakwa na wabara.
Namshukuru dr Migiro nilimwona akikwepa kujadili kwa mtindo huwo.
Kwakuwa picha zinachukuliwa watoto na wajukuu zetu watahukumu kwa hilo.
--------------------------------------------
On Tue, 4/22/14, 'ananilea nkya <ananilea_nkya@yahoo.com>' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: Re: [wanabidii] BUNGE LA KATIBA NI " KOMEDI" ?
 To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Tuesday, April 22, 2014, 10:48 PM

 Historia 
 itahukumu  watawala  wetu -wanawake na
 wanaume  kwa kusambaza sumu ya maneno ya kulipasua
 taifa letu vipande vipande.
 Tusubiri.   Ananilea Nkya
  E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com
     On Saturday, April
 19, 2014 1:42 PM, Happiness Katabazi
 <katabazihappy@yahoo.com> wrote:
     BUNGE LA KATIBA NI
 " KOMEDI" ?

 Na Happiness Katabazi
 HAKUNA Ubishi kuwa siku hizi ukitaka kucheka, kukereka na
 kupunguza msongo wa mawazo uliyonayo, ukitaka kujifunza
 maneno machafu mapya, huna budi kufungulia Televisheni ya
 Taifa (TBC1), na kuanza kuangalia mijadala ya Bunge la
 Katiba la Tanzania linavyoendeshwa na jinsi wajumbe wa bunge
 hilo wanavyochangia kwa kutumia lugha za matusi,
 zisizonastaa na zinazopolomosha heshima ya bunge hilo na
 jamii yetu ya Tanzania.

 Na Baadhi wananchi wengine wamekuwa wakisema uenda kabla ya
 bunge hilo
  kuanza , baadhi ya wajumbe wanakunywa kwanza 'viroba'
 ndiyo wanaingia ndani ya bunge na kuanza kuchangia mjadala
 kwa kutoa lugha za kejeli, uzushi, kuzomea na kugonga meza
 ovyo.

 Nimeyasema hayo kwasababu tayari baadhi ya wananchi wameisha
 lipachika bunge la Katiba kuwa ni 'Komedi'. Kwa wajumbe
 wa bunge hilo ambao ni watu wazima wenye umri wa zaidi ya
 miaka 18 , baadhi yao wameshindwa kujiheshimu na kuchunga
 kauli zao wakati wakichangia mjadala wa mchakato wa kupata
 Katiba Mpya

 Kila kukicha tumesikia wabunge hao wengine wakiwa na umri
 mdogo wamekuwa wakiwatolea maneno ya 'shombo' wajumbe
 wenzao ambao wamewazidi umri kwa kisingizio kuwa wajumbe hao
 wenye umri unaowazidi na kuwapita hata wazazi hao wamekuwa
 wakilidanganya bunge, na baadhi ya wajumbe wa bunge hilo
 ambao wanaumri mkubwa nao wamekuwa wakiwatolea maneno
 yasiyofahaa wajumbe wenzao wenye umri mdogo wachangiapo
 mjadala huo.

 Mila na tamaduni zetu ni mkubwa
  anamheshimu mdogo na mdogo anamheshimu mkubwa lakini
 kupitia bunge letu la Katib a'Komedi', niwazi wajumbe wa
 bunge hilo wanauzika utamaduni huo na kufanya sasa jamii ya
 watanzania waanze kuishi kwa kutumia utawawa Kambare kwani
 baba,mama ,mtoto wa kambare wote wanandevu hakuna wa
 kumbabaisha mwenzie.

 Nia ya Rais Jakaya Kikwete ya kutaka Tanzania iandike Katiba
 mpya ni njema, ila sasa tunashuhudia baadhi ya wajumbe wa
 bunge hilo hawataki nia hiyo ikamilike kwa kila siku kuibua
 mapingamizi na hoja zisizokuwa na kichwa wa miguu hali
 inayosababisha hivi sasa  heshima ya bunge hilo
 kuporomoka na kuona ni kheri tubakie na Katiba ya zamani ya
 mwaka 1977 licha ina mapungufu yake kuliko kuletewa Katiba
 mpya ambayo inaendelea kuandikwa na baadhi ya wajumbe
 waliokosa adabu, wanatumia lugha za matusi, uzushi kwa
 kisingizio kuwa eti wanataka serikali mbili wengine wanataka
 serikali tatu.

 Kwa wale tuliopata kuisoma rasimu ya pili ya Katiba,
  mtakubaliana na mimi rasimu hiyo imeandikwa vitu vingi sana
 siyo Muungo wa Serikali mbili, Serikali tatu, wala hati ya
 Muungano pekee.Imeandikwa vitu vingi lakini hatuoni kama
 baadhi ya wajumbe wanajipa muda wa kuisoma rasmi hiyo yote
 na kufahamu kilichoandikwa.

 Leo hii baadhi ya wajumbe wanaibuka wanasema hati za
 Muungano mara zimegushiwa, mara hazipo kwa sababu hiyo
 hakuna muungano.Na mbaya zaidi wanaongea uzushi ndani ya
 bunge hilo hawatoi vielelezo.Tuwaulize wajumbe wa aina hii
 hivi siku hati za Muungano zilivyokuwa zinatengenezwa na
 waliozitengeneza na zikasainiwa na Marehemu Baba wa Taifa
 Julias Nyerere na Rais wa Zanzibar, Abeid Aman Karume
 walikuwepo?

 Mapema wiki hii  Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue
 alifanya mkutano wake na waandishi wa habari na kuwaonyesha
 hati za Muungano na kusema hati hiyo ni halisi na kwamba
 Rais Jakaya Kikwete amesikitishwa na uzushi huo kwamba hati
 hazipo, na lugha za kejeli na
  matusi.

 Minashangaa sana huyo Balozi Sefue anavyosema Rais Kikwete
 eti amesikitishwa na vitendo hivyo.

 Naye Rais Kikwete amenukuliwa juzi akisema kuwa anakerwa na
 lugha za kejeli , matusi nakuwakejeri waasisi wa taifa
 hili.

 Ni najiuliza Kwa hiyo rais Kikwete akishasikitika ndiyo hao
 wajumbe wazushi, wanaotoa lugha za kejeli ndiyo wataacha
 tabia hiyo ambalo linaporomosha heshima ya bunge hilo mbele
 ya jamii?

 Kwa hiyo Rais Kikwete akisikitishwa na lugha hiyo za kejeli
 zinazotolewa na Hao  baadhi ya wabunge la Katiba, ambao
 watu tunaofikiri sawa sawa HIvi sasa kutokana na vitendo Vya
 kishenzi na kijani  vinavyofanywa  ndani ya Bunge
 na Hao wajumbe  HIvi huo mchakato wa kuwapata wajumbe
 wale ulifanywa na watu wenye akili timamu  au wahuni
 tu?

 Maana aingii akilini kabisa kuna baadhi ya wajumbe ambao
 tangu serikali hii iingie madarakani Desemba 21 mwaka 2005 ,
 wamekuwa wakipinga kila kinachofanywa na
  serikali hii kiwe kizuri au kibaya na wazushi wakubwa,
 lakini cha ajabu Rais Kikwete akawateua baadhi ya wanasiasa
 hao sijui akidhani kwa kuwateua ndio atawafurahisha na
 wataacha kuzua uongo?

 Matokeo yake wajumbe hao wenye tabia hiyo baada ya kufika
 ndani ya bunge hilo ndiyo kwanza wameendelea na tabia zao ya
 uzushi, kulazimisha mambo wanayoyataka wao tu na wanataka
 watu wote waamini yale wanayoyaamini wao na kuzua taftari ma
 maneno ya shombo ndani ya bunge jambo linalosababisha hivi
 sasa heshima ya bunge hilo kuanza kuporomoka kwasababu ya
 vitendo vya kiuni kufanywa na baadhi ya wajumbe ambao
 wengine ni wateuli wa rais Kikwete.

 Wahenga waliwahi Kusema " Mtoto umleavyo ndivyo
 akuwavyo". Msemo huu umethibitika kwamba Katika Utawala
 wa serikali awamu ya nne imekuwa ikiwa lea na wakiwa
 kukumbatia baadhi ya wanasiasa na wanaharakati ambao
 wamekuwa wakitoa maoni Yao kupitia vyombo Vya Habari,
 mikutano ya adharani kuzulia uongo na kuwachafua
  mahasimu wao kisiasa, vyama Vya siasa na wakati mwingine
 serikali.

 Sasa tabia hiyo chafu ya kuzua maneno ya uongo ndiyo
 Imefikia mahali sasa wajumbe wa Bunge la Katiba kufikia
 Hatua ya Kusema Hati ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
 Mara imegushiwa Mara haipo wakati ipo.

 Kwa hiyo tabia hii Chafu iliyoota mizizi sasa Kwenye vinywa
 na Fikra Kwa baadhi ya wanasiasa wetu uchwara ya uzishi,
 upotoshaji kwa kiasi kubwa nadiriki Kusema imelelewa na
 kukumbatia sana na Utawala wa serikali awamu ya NNE ambayo
 Katika Utawala awamu ya NNE ndiyo wanasiasa Wengi uchwara
 hapa nchini ndiyo wamekuwa walitumia mbinu hiyo ya uzishi na
 uongo Katika hotuba zao kuwadanganya wananchi Katika Mashaka
 mbalimbali.

 Na uthibitisho wa hili ni kitendo Cha baadhi ya wajumbe wa
 Bunge Hilo kusimama ndani ya Bunge Kusema eti hati ya
 Muungano haipo , wengine imegushiwa Kumbe hati hiyo ipo.

 Mbona serikali hii imeishawahi kuyafungia baadhi ya magazeti
 kwa kile
  ilichodai kuwa magazeti hayo yamekuwa yakiandika habari
 ambazo zinaleta uchochezi na uhasama katika jamii?.

  Kwanini baadhi ya wajumbe wa bunge hilo kwa ushabiki wao wa
 kijinga tu wa kundi moja linataka serikali mbili jingine
 linataka serikali tatu lifikie sehemu ya kufanya vitendo vya
 kulidhalilisha bunge letu mbele ya walipa kodi?

 Hata kama hati zilizotolewa na Balozi Sefue ni halisi au
 zimegushiwa hao walisema hati za muungano hazipo na
 zimeghushiwa  wanaweza kuzitambua? .Tukubaliane
 kimsingi si kila nyaraka ya serikali inatakiwa kuwekwa
 wazi.Nyaraka zingine hazistahili kuwekwa adharani.

 Siku zote wananchi wataendelea kuzieheshimu na kuziogopa
 mahakama licha mahakama zetu nyingi hazina mazingira mazuri
 ya ofisi kwasababu mahakimu na majaji wanaoendesha kesi
 wanajiheshimu wawapo mahakamani wakiendesha kesi.Wakati kesi
 zikiendeshwa hutakuta mtu akipokea simu, wala kuchati wala
 kupigana picha na kisha picha kuweka kwenye simu
  wakati kesi zikiendelea.

 Lakini hivi sasa tunashuhudia baadhi ya wajumbe wa bunge la
 Katiba wakati bunge hilo likiendelea wakitumia Ipad na simu
 zao kuchati na kupigana picha.Hivi tujiulize muda wa
 kufuatilia kwa makini hoja zinazotolewa na wajumbe wenzao
 wanaupata wapi?Maana muda wote wapo bize na simu?

 Na nina mshangaa sana huyu Mwenyekiti wa Bunge la
 Katiba,Samuel Sitta ambaye ni msomi wa sheria anashindwa
 kupiga marufuku ufedhuli huu ambao nao  unaporomosha
 heshima ya bunge hilo ambalo hivi sasa huku mitaani limepewa
 jina la utani la 'Komedi'.

 Kwa uhuni huu unaofanywa na baadhi ya wajumbe wa bunge la
 Katiba wa kuibua hoja za uzushi, kejeli,matusi ambazo
 zimesababisha baadhi ya wajumbe hao wamekosa adabu wanaacha
 bila kuchukuliwa hatua, kunanifanya sasa nione ni kheri
 tuendelee kutumia Katiba ya zamani ya mwaka 1977 ambayo ni
 kweli ina mapungufu ambayo yanaweza kurekebishwa kuliko kuja
 kutumia hiyo Katiba mpya
  ambayo  inaendelea kutengenezwa na hawa baadhi wajumbe
 ambao wakati wanaitengeneza walikuwa wakitumia lugha chafu
 na uzushi.

 Katiba Mpya sio itaji muhimu sana kama lilivyoitaji la
 serikali kutoa hela kununua madawa mengi kuweka
 mahospitalini, kujenga miundombinu,kutengeneza wodi za
 kuzaliwa wa kinamama, kutoa elimu kuhusu ugonjwa wa UTI
 ambao hivi sasa umeanza kuwa tishio kubwa hapa nchini.

 Kama kweli tunataka kutengeneza hiyo Katiba mpya, wale
 wajumbe wa bunge hilo ambao kisheria sisi tunasema wao siyo
 wa mwisho wa kutengeneza Katiba mpya ,wajiheshimu na
 watimize jukumu lao hilo kwa nidhamu bila kuvunja heshima ya
 bunge hilo na kupotosha jamii.

 Ni ajabu sana wajumbe wa bunge la Katiba kutaka kuparurana
 kuhusu mchakato wa kupata Katiba mpya, wakati sisi tuliosoma
 somo la Katiba tumefundishwa kuna hatua kadhaa za kufikia
 kutengeneza Katiba mpya. Hatua ya kwanza ni Tume kukusanya
 maoni ya wananchi, tume kuyaweka kwenye maandishi
  maoni hayo(rasimu), Bunge la Katiba kuijadili rasimu husika
 kama bunge linavyofanya sasa, kisha yaliyojadiliwa na Bunge
 yapelekwe kwa  kwa wananchi wayapigie kura za ndio au
 hapana.

 Sasa nyie wajumbe mnaotaka kuparulana kwa kisingizio cha
 kutaka serikali mbili, mara tatu make mkijua bunge siyo
 chombo cha mwisho ya kutengeneza Katiba mpya.

 0716 774494
 www.katabazihappy.blogspot.com
 Aprili 19 Mwaka 2014.


 Sent from my iPad

 --
 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

 Kujiondoa Tuma Email kwenda
 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
 Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

 Disclaimer:
 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and
  hence statements and facts must be presented responsibly.
 Your continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 ---
 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.
 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.





 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.



--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment