Tuesday, 25 March 2014

[wanabidii] Re: [Wanazuoni] BUNGE MAALUM LA KATIBA; TUMETOKA WAPI, TUKO WAPI NA TUNAKWENDA WAPI

A story is told of a king who had no heir and one day he decided to find one among his subjects. He invited 10-year-olds to the palace and told them his desire. 
He gave them a simple assignment to test their readiness to take the mantle — each was to plant a seed, nurture it and after two or so weeks the children were to go back to the king with their seedlings. 
The excited children and parents planted the seeds and watered them but after a week, they had not germinated! The parents shared their frustrations and they conspired to buy seeds similar to the king's and continue with the assignment. One boy's parents refused to play ball insisting that he had to nurture the seed given by the king. 
When the boys went before the king, they were all excited about their healthy seedlings, which they held in pride. The king praised them for a job well done. 
And when it came to the boy whose seed was dead, the king asked, "What happened?" Trembling, the boy explained that he did everything but the seed did not germinate. The king held the boy's hand and announced to his subjects, "Behold, the king's heir!"
Honest boy 
The others complained aloud. How and he had no seedling? The king explained that he had actually given them boiled seeds to plant and among them all, the boy with no seedling was the only honest one! 
This story is relevant to nearly every member of political opposition parties in Zanzibar and Tanzania mainland. Every one wants the best in life and somehow believes that the easiest way to achieve this is through dishonest means.
 
Benn Haidari
Klintvägen 16 C 36
22100 Mariehamn
Åland
Suomi-Finland
Author of Modern Zanzibar Cuisine
Tel/Home: +358.18.13665
Mobile: +358.457.3424826


On Wednesday, 26 March 2014, 7:18, valencemeriki2002 <valencemeriki2002@yahoo.com> wrote:
 
Ndugu Mtatiro nashindwa kuelewa hii lugha ya "tukakaa kimya". Jambo linapotokea and you keep quite umekubaliana nalo na litakuwa sheria. Kwanini msilipinge hadi litakapo rekebishwa? Unasema muda mwafaka , ni lini huo muda utafika na unadhani mambo yatakuwa yanawasubiri?. Ni lazima mchukue hatua SASA.


Sent from my iPhone



-------- Original message --------
From: mruahdeo@yahoo.co.uk
Date: 26/03/2014 6:36 AM (GMT+10:00)
To: Wanazuoni@yahoogroups.com
Cc: wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
Subject: Re: [Wanazuoni] BUNGE MAALUM LA KATIBA; TUMETOKA WAPI, TUKO WAPI NA TUNAKWENDA WAPI


 
Salim,
Ilikuwa ni CUF ya Lipumba lakini tofauti na wakati ule alikuwa amezungukwa na watu wenye busara, sio hii KAFU ya akina Lipumba na Mtatiro na akina bwege. Hakuna maana nyingine ya chama cha kishkaji zaidi ya hiyo unayoijua. Kwa miaka mitano tu kundi la CUF ya akina Mtatiro limeitoa kule kwenye chama chenye kuleta ushindani hadi kufikia kuwa wasindikizaji katika kila chaguzi ndogo zaidi wameongeza matamko.


From: Salim Khatri <skhatri@orcis.com>;
To: <Wanazuoni@yahoogroups.com>;
Cc: wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>;
Subject: Re: [Wanazuoni] BUNGE MAALUM LA KATIBA; TUMETOKA WAPI, TUKO WAPI NA TUNAKWENDA WAPI
Sent: Tue, Mar 25, 2014 5:25:51 PM

 
Deogratius,
Naomba ufafanue maana halisi ya maneno "chama flani cha kishikaji"...
Na kilipokuwa chama kikuu cha upinzani "bungeni" kilichokuwa kinashirikisha vyama vingine vya upinzani kuunda upinzani rasmi bungeni (tofauti kabisa na hichi cha sasa), ilikuwa CUF ya nani kama siyo Lipumba? Ama kulikuwa na mwenyekiti mwengine unayemjua wewe ambaye sisi wengine hatumjui?
On Mar 25, 2014 4:17 PM, "deogratius mruah" <mruahdeo@yahoo.co.uk> wrote:
 
Hii tabia ya kutumia lugha za vitisho na kulalamika haijawahi na wala sioni siku za karibuni kama itakuja kuwasaidia hawa wanaojiita wapinzani nchini. Mle sahani moja, mpambane hadi kieleweke na mtumie ukubwa wenu ( as opposed to utoto CCM wanaodhani mnao) bila kuhakikisha mnapata uwakilishi mkubwa mtaendelea kuwa walalamikaji tu. Na kwa mfumo wa demokrasia ya uwakilishi hii inapatikana kwa kuchaguliwa na wananchi kwenye sanduku la kura. Na kwa CUF ya Lipumba na Mtatiro hili ni ndoto maana wanarekodi mbaya sana kwenye uongozi maana ni kipindi chao CUF imeporomoka kutoka chama kikuu cha upinzani hadi kuwa chama flani hivi cha kishikaji. 
 


Deogratias Mruah
International Development Consultants
Cell: +255 713 399 700


On Tuesday, 25 March 2014, 15:37, Yona Maro <oldmoshi@gmail.com> wrote:
 
Na Julius S. Mtatiro

BUNGE MAALUM LA KATIBA; TUMETOKA WAPI, TUKO WAPI NA TUNAKWENDA WAPI.
1. Wajumbe wengi(asilimia 81) kati ya wale 201 walioteuliwa na Rais Kikwete ni viongozi na wanachama waandamizi wa CCM. Tukavumilia na kukaa kimya.
2. Kwenye kutengeneza kanuni za Bunge Maalum CCM walipambana kila kukicha kupitisha kanuni zitakazotetea MFUMO wao - tukatumia nguvu kubwa kuwazuia lakini tulifanikiwa kidogo sana -Tukakaa kimya.
3. Katika kuanza kuzitumia kanuni, Mwenyekiti wa Bunge Maalum kwa shinikizo la wazi la CCM alikiuka kanuni bila aibu, ikapangwa kuwa hotuba ya Jaji Warioba ianze ili aje Rais wa nchi baadaye, jambo hili ni kinyume kabisa na kanuni. Suala hili likaleta mvutano mkubwa sana tukaamua KUJIFANYA HATUTAKI MAKUU, tukaliacha - Tukakaa kimya.
4. Jambo hili lilipokubalika, CCM wakamshinikiza Mwenyekiti wa Bunge Maalum amnyime jaji Warioba muda. Mwenyekiti akatangaza kuwa atampa dkk 60 tu, tukakataa, siku jaji Warioba alipokuja kuwasilisha tukalikwamisha ili aongezewe muda, baada ya mashauriano ya baadaye, ikakubaliwa apewe saa nne.
5. Baada ya uwasilishaji wa Rasimu wa Warioba, Rais Kikwete alikuja na kuivunjavunja na kuweka misimamo ya chama chake dhidi ya maoni ya wananchi yaliyomo kwenye rasimu ya katiba. Tukamsikiliza Rais kwa nidhamu kubwa na kuvumilia hatua yake ya juu ya kupinga hadharani rasimu ya katiba ambayo imetokana na maoni ya wananchi ambayo ameyakusanya baada ya kuiunda tume ya Warioba. Tukakaa kimya.
6. Ikumbukwe kuwa hata kwenye kuchagua Mwenyekiti wa Bunge la Katiba CCM walipigania nafasi hiyo na kushinda. Nafasi ya Makamu Mwenyekiti pia waliipigania wakachukua. Tukakaa Kimya.
7. Jana Mwenyekiti wa Bunge la Katiba aliteua kamati za uandishi na kamati ya Kanuni. Kamati zote hizi mbili, kila moja, mwenyekiti na makamu mwenyekiti walioteuliwa wote ni viongozi wa CCM, Tukakaa kimya. Wenyeviti wa kamati hizi wote wanaingia kwenye kamati ya uongozi ya Bunge Maalum. Tumekaa kimya.
8. Juzi CCM walipokutana kwenye kikao cha wajumbe wa CCM waliamua kuteka kamat zote 12 zitakazojadili sura za Rasimu ya Katiba.
Jana tulipokwenda kwenye uchaguzi wa viongozi wa kamati, wateuliwa wote wa CCM walishinda akiwemo HAMAD RASHID na Dr. Francis Michael ambao pia wamejivika joho la kusimamia maoni ya wananchi huku ukweli halisi ni kuwa wapo ili kusmamia matwaka na Maslahi ya CCM.
Ikumbukwe kuwa, wenyeviti wa kamati hizi 12, wote ni wajumbe wa kamati ya Uongozi ambayo ndiyo dira itakayoongoza kila jambo linaloletwa katika bunge Maalum.
9. Leo, Mwenyekiti wa Bunge Maalum ameteua wajumbe watano ili kuingia kwenye kamati ya uongozi kama kanuni zinavyoelekeza. Jambo la ajabu ni kuwa, kati ya nafasi hizo 5, nafasi 4 zote amewateua wajumbe ambao ni viongozi waandamizi wa CCM akiwemo mwakilishi wa walemavu Amon Mpanju.
Mjumbe mmoja wa walemavu amesimama na kupinga uteuzi wa mwakilishi wao palepale.
Prof Lipumba amesimama na kukataa uteuzi huo, ameeleza si wa haki hata kidogo. Ameeleza alijiunga na siasa ili kutafuta haki za wananchi na umoja wa kitaifa na si vinginevyo. Lipumba amesema kuwa hawezi kutumika kama mhuri.
Kama CCM wana nia njema wasingehodhi nafasi zote katika mchakato wa katiba.
10. Hoja kubwa ya CCM kuchukua nafasi zote za uongozi wa bunge maalum ni "eti" wao ni wengi. Hoja ya ajabu sana hii! Kama hoja ni nani au kundi gani lina idadi gani basi nafasi hizi zingegawanwa kwa mantiki hiyo. Vyama visivyo CCM peke yake vina wajumbe zaidi ya 130, kama hoja ni wingi vyama hivi peke yake vingepewa nafasi 5 kwenye kamati ya uongozi. Badala yake tumepewa nafasi 1 tu a Prof. Lipumba ambayo ameikataa kwa sababu si nafasi ya haki.
11. Tuko hapa kwenye Bunge Maalum kutafuta katiba ya wananchi wa Tanzania, hatuko hapa kutafuta katiba ya chama chenye wabunge wengi kuliko vyama vingine kama anavyosema Mwenyekiti wa Bunge Maalum Samwel Sitta. Ili tupate katiba ya watanzania wote lazima chama chenye wabunge wengi kitambue wingi wao, na kiutumie wingi huo kuunganisha makundi muhimu yenye idadi ndogo ili kutafuta katiba yenye maridhiano na inayokubalika na makundi madogo na makubwa ndani na nje ya Bunge Maalum.
12. Michakato mingi ya kutafuta katiba mpya inaonesha kuwa vyama vilivyoko madarakani huwa ni chanzo kikubwa cha kuvuruga mchakato wa katiba. Na sbb kubwa ya kuvuruga mchakato husika huwa ni chama dola kutaka kuhodhi na kulinda maslahi yake dhidi ya maslahi ya wananchi. Pamoja na uzoefu huu, bado CCM hawataki kujifunza, wanataka kushinda bila kujali wananchi watapata nini.
ANGALIZO;
Masuala hayo 12 yanaonesha wazi kuwa CCM hawana kabisa nia ya kuona nchi inapata katiba inayokidhi matakwa ya wananchi. CCM wanataka kuchukua kila kitu, wanataka kupata kila kitu, wanataka kuhodhi kila kitu, hawajali wananchi wamesema nini.
Wasidhanie kuwa tulioko hapa Dodoma ni watoto wadogo, tutachukua hatua, hatua stahili kwa wakati muafaka. Idadi yao na wingi wao havina maana katika na juu ya maslahi ya taifa na matakwa na maoni ya wananchi.
MWISHO;
CCM watambue kuwa TUTAKULA nao sahani moja, hatutatumiwa kuwa mhuri wa Maslahi ya chama chao na kwamba katiba mpya siyo hisani yao, ni matakwa halisi ya watanzania na serikali na chama kinachoongoza dola lazima kitii maoni ya wananchi na matakwa ya misingi ya kdemokrasia, na kwa sababu mchakato huu umeshaanza lazima ufike mwisho. "Jini likitoka kwenye chupa, halirudi"(hadithi za Alfu Lela Ulela).

--

Yona Fares Maro

Institut d'études de sécurité - SA




.

__,_._,___


0 comments:

Post a Comment