Tuesday, 25 March 2014

Re: [wanabidii] MAKABILA YA TANZANIA - TRIBES OF TANZANIA

Kama umeshawahi kukaa na makabila yanayotaniana katika kikao kimoja ukaona vituko vyao au yanayochukiana lakini ukakuta wanakunywa pombe pamoja na kuongozana wakiwa wamelewa na kuanguka na kuinuka wakibebana ndio utafahamu ya kuwa-magomvi mengine hasa ya wakulima na wafugaji ni ya kutegeneza. yanaweza yakamalizwa kama kuna utawala bora, uwazi na ukweli. Utaona kuwa watanzania ni watu wanaopendana ila kuna vikasoro vidogo tu vya kumaliza.

Ukifika vijiji vya ngerengere vijana wa-kimasai wamezaa sana mtu ana mtoto kijiji A hadi Z kazaa na wakwere, wakutu. Mparakuyo Maasai kaoa Mkwere. Ila si rahisi Mkwere, Mkutu, Msambaa kuoa Mmasai labda wawe wasomi waliokutana vyuoni-makazini. Huko Chalinze, Ngerengere vijijini mwenye hela ni mfugaji na ndiye mwenye maduka mengi ya bidhaa za rejareja, pikipiki za kukodisha huko ngerengere, Magindu wilaya ya Bagamoyo. Wadada wanawagombania hawa maana wanafedha. lakini haimaanishi vijana wa makabila wengine hawana mabibi (wapenzi wa kike wa siri) kwa makundi ya wafugaji. Ipo, inafurahisha utakapowaona wanapigana ukope na kula chenga kuelekea muelekeo fulani lakini wao hawajui kama unawafuatilia kuangalia mahusiano.

Ukifika Mkomazi vijiji vya ndani vilivyopakana na mbuga upande wa tambarare Same Kusini na wilaya ya Lushoto au upare na usambaani usidhanie wamama wote waliovaa nguo za kimasai wote ni wamasai wengine ni wapare na wasambaa waliolewa na Parakuyo Maasai.

Unakaa kikao na wafugaji Parakuyo Maasai na Wasambaa kila mmoja anaelewa na kuongea lugha ya mwenzake lakini wakikaa kuongea Mmasai anaongea lugha yake Msambaa anamjibu kwa kisambaa. Wewe mtafiti au mwezeshaji unayetaka kuelewa wanaongea kuhusu nini ktk kikaochao cha kawaida unakosa pa kuibia maana wao wanaongea kilugha chake. Ukiuliza wanakuambia yeye hataki kuongea lugha yangu nami sitaki kuongea yake nisiwe mtumwa wake lakini tunaongea tunaelewana maana yeye anajua lugha yangu nami ninajua yake.

Ukienda mwambao wa bahari ya Hindi-pangani Tanga, Bagamoyo, Saadani, Mafia-Wapemba (wagunya na makabila mengine ya wavuvi toka Pemba) wengi wameoa au wana nyumba ndogo hata kama huko kwao hawajui. Akija kuvua na kushusha mzigo wa biashara ya samaki anako kwa kufikia.

Inafurahisha halafu unajiuliza-kwa nini huwa tunagombana? Mfugaji kulishia mazao mifugo yake, mapikano kugombea ardhi/maeneo na kukatana mapanga, kutaka kujitenga Kisiwa na Bara badala ya kurekebisha mapungufu tukaishi salama.

Ethocentrism tu ndio inatupa tabu-kikabila kimoja, rangi ya mmoja kujiona bora kuliko mwengine bila ya kuangalia mapungufu yake ndio vitatupa utata mpaka katiba ituwie ngumu kuikamilisha.
Mungu ibariki TZ.

On Wednesday, 26 March 2014, 5:40, Gaston Kikuwi <kikuwigg@gmail.com> wrote:
Tena umenikumbusha

Kuna kabila la Wandonde ambao walikuwa kabila moja na wangoni.  Baadae wakasambaratika na kukimbilia maeneo ya mkoa wa Lindi pamoja na wandendeule.  Hao waliitwa Ndendeule kwa kuwa walikuwa hwataki sana maswal ya kupigana pigana vita.  Kwa hiyo wakiulizwa tu wanajibu " NDENDEBHULE"  nimefanya nini, wakaitwa hivyo.

Asante sana kwa kujuzana


2014-03-25 7:43 GMT+03:00 Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>:

 
Wangindo-Wako Mkoa wa Lindi na Morogoro (Liwale na Ilonga-Mahenge:
-Sawa kabisa wapo maeneo haya hata wangoni.Wangindo ni kabila kuu maeneo mengine ya Mkoa wa Morogoro wilaya ya kilosa. hawa waliletwa kulima mashamba ya katani na miwa-kama manamba. Utawakuta Muhenda (njia ya Mikumi-Kilosa kijiji kabla hujafika Ulaya na Zombo) wapo Kidogobasi-kabla ya Rwaha eneo la ndani ukitoka Kidodi miwa linalopakana na Mikumi National Park kuelekea Kilombero.
Wangoni na ngoma yao'Kitoto' ndio ngoma kuu ukifika Rwaha-Kidodi. Sababu hawa walifika kivita wakati wakitoka South Africa na kupanda na vita vyao vya Zulu-Mfekane lakini walipata kipigo na kisago kikubwa hapo Milima ya Kidodi kwa Wavidunda waliokuwa wakiishi milimani juu (kuna vijiji 3 kwa sasa Vidunda, Chonwe, Udunghu). Hawa ni shina moja na Wahehe, Bena, Benamanga. historia yao ya vita wanadawa ya kienyeji ambayo wakiitumia nyie adui mtauana mmoja baada ya mwingine atabakia mmoja akasimulie kwao ilikuwaje. Ndi sababu wajerumani waliwachomea moto mapangoni kwani ilikuwa hakuna mbinu ya kuwapata wakalime kama manamba. Bora wafe kuliko kuonewa, kiburi pepo za hasira daima hupanda kichwani hakieleweki kitu. Kwa mila za zamani, ukipigwa ukishindwa unabaki kumfanyia kazi bosi, unaolewa na kuwa mtumwa hapo au kibarua. Hivyo wangoni walibaki kwa Chief Gwira na kuwa wanamfurahisha kwa kucheza dansi ngoma yao ya kitoto ndio ikawa ngoma kuu ktk mihadhara ingawaje nao wavidunda wanayo yao zinazochezwa kwa nyakati na makundi mbalimbali-soma hans Cory na Bieldman. Ni Chief Towegale Kiwanga (aliyekimbilia Ulanga baada ya maelewano korofi ya udugu kati yake, Ngwira, Mkwawa) tu ndiye aliyekuwa rafiki mzuri wa wajerumani kiasi cha wao kutaka kumpeleka Ujerumani akasalimiane na Bismack (Soma Benas of the River, personal communication with Kiwanga2).

Ukifika Vijiji vya Kisanga, Madizini, Ihombwe huko utakuta-Wanyamwezi ambao kwa sasa ni Wasagala. hawa walikuwa wakipitisha watumwa huko awali. Lakini baada ya mashambulio ya awali ya wajerumani kunyonga watawala wilaya ya Kilosa kutokana na kiburi chao, kukawa kwa wasagala hakuna mtawala. wanyamwezi walikuja kujipachika utawala kwani muingereza alikuwa nan indirect rule na machifu walikuwa na nafasi hivyo Mnyamwezi akatawala akawa Msagala Msagala na msagala original ni Msagala Wakwiva.

Makabila mengi nchini yamekuja wakati tofauti na kwa sababu tofauti. Nilishangaa kumkuta bibi wa kinyakyusa vijiji vya mashamba ya katani Mwakiyumbi-Hale Tanga aliniambia alifika akiwa 9 years (kwa makisio) na mpaka 2005 alikuwa hajui kuongea Kiswahili sawasawa ilibidi kupata mkalimani. Baadhi ya makabila walishikilia lugha yao ili wasionekane watumwa ktk maeneo ya kazi/makazi nje ya kwao kwa kuongea lugha za wenzao. Kuna Warundi maeneo mengine walioletwa/kuja kutafuta kazi wakilima vibarua wamekaa karne.

Wadoe (Wadoezi) walio maeneo ya kati ya Tanga na Bagamoyo ni Wanyamwezi waliomsaidia Chief Pazi kuwapiga Wakamba waliokuwa wanawinda Paa kwa ajili wa Wazigua na mila zao za kumtoa mtoto baada ya siku 40 toka kuzaliwa na kufanya mila kwa kumuweka ktk ngozi ya paa,. Huko porini wakiwinda walimbaka mtoto wa kike ukoo chief wakampa mimba. alitafuta watu wa kupiga/kuwaua wakamba Mnyamwezi aliyekuwa akipitisha misafara ya watumwa akakubali kwa mkataba wa kupewa kitambaa cha bafta cha yadi 10 cha kupiga kilemba. baada ya kuwaua wakamba akabakizwa mmoja walimkata masikio na kuyatafuna aende akasimulie kwao-Pazi hakuwa na bafta (Pure cotton toka India) ya kuwapa. Akawapa ardhi wakae. Wakaitwa Wadoe (maana yake Wadoezi wasiotaka kurudi kwao).

Na wala majina ya makabila mengine sio halisi inatokana na mazingira fulani. Mfano hao Wadoe na Wasagala wanyamwezi. Pia wavidunda (ni la kupanga waingereza kabila hasa ni 'Temekwira'. Unauliza wale walioko milimani?-wale wakidunda? Yes- Mzungu anajibu basi hao wataitwa  'Wavidunda'. Benamanga badala ya Bena. Manga maana yake ni mchanganyiko wa kitu halisi na kinginecho. wamekwenda bondeni na kuchanganyika na makabila mengine (Benamanga; mmanga alicjichanganya).

Ninachangia Gaston.



On Tuesday, 25 March 2014, 6:00, Gaston Kikuwi <kikuwigg@gmail.com> wrote:
Kuna makabila mengine umeysahau

(i) Wangindo-Wako Mkoa wa Lindi na Morogoro (Liwale na Ilonga-Mahenge
(ii) Wandwewe pia wako katika mkoa wa Morogoro
(iii) Wanyamanyafu-Wako katika mkoa wa Mbeya

Congratulation


2014-03-24 12:10 GMT+03:00 Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>:
Mimi nimechangia tu kwa waikoma. Mbona vikabila vingi. Unafika Nata-wanata; Isenye-waisenye etc. hata wavidunda ni kabila dogo la sasa watu labda laki 4 kwani asilimia 90% ya kabila hili liliuawa kwa kuchomwa mapangoni walikokimbilia kwa kugoma kufanya forced labour ya mjerumani.


 



On Sunday, 23 March 2014, 14:40, F Kitigwa <kitigwa@gmail.com> wrote:
mbona mmesahau WASIMBITI?


2014-03-23 13:32 GMT+03:00 Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>:
Nichangie-Waikoma ni wasonjo. Nimefanyakazi kwao kwa miaka 2. Historia yao ni kuwa walipokuwa hunters and gatherers walifika hadi Ikoma Robanda wakimfuata Nguu-Nyumbu. Wanawinda wanyama wadogo na nyumbu ndio mwenyewe mkate wa kila siku. Nyama ikinyooshwa na kuanikwa 'Kimoro' na mtoto analalia chini ya kitanda cha kamba juu ngozi na akila nyama usiku na muda wowote akitaka. hakuna iron deficiency kwao kutokana na ulaji nyama. Muikoma ni mpiganaji vibaya sana kwa kutumia mishale ya sumu. Mfugaji wa kimasai na yeye mpambano wake mmasai atatimka tu. Nimeshughudia mengi katika jamii hii ya waikoma. Ninasikitika tu mabadiliko ya uwekezaji pamoja ni ya maendeleo lakini ningependa jamii zetu nyingine ziwe na maendeleo bila athari mbaya.

Kule Ndani Loliondo wasonjo walianzisha baadae kilimo cha umwagiliaji, wakajijengea maboma kujilinda na wamaasai waliokuwa wakiingia, kupigana nao  kuwaondoa (ugomvi umedumu hadi leo). Hivyo kufuga kukawa kugumu wakaanzisha agro-pastoralism na irrigation system yao imeandikwa sana. Sonjo ni wakazi wa awali kutoka central africa Maa groups (maasai group la Serengeti, Loita, Parakuyo, Purko) walikuja baadae baada ya hawa wasonjo na Mang'ati. Maasai wakawaondoa mang'ati ndani ya serengeti na kuwasukuma ziwa jirani (jipe kama sijasahau). Ugomvi wa mang'ati na Serengeti Maasai ulimalizwa kimila 1994s kama wa waikoma na Wamasai kutoka mbuga ya serengeti umemalizwa miaka ya majuzi-kimila kwa kunyonyesheana watoto. waikoma wanafuga na kilimo ktk eneo lao ni kigumu kuna limestomes. Wanazingatia mila vibaya sana, hawazaani sana kutokana na matatizo sitoyaandika hapa. Wachaga nao wana makundi ya aina nyingi waliotoka maendeo mbali mbali nchi nje ya TZ. Huenda wakafanana mambo fulani na mengine yakapishana. Pia Wapare-wapo waliotoka taita na wapo waliotoka Ethiopia. Makabila mengi ya TZ yanaingiliana namna hii na unaweza kuwatofautisha watu wa kabila moja kwa mila zao za namna fulani (kundi hili linafanya hiki hili hapana), lafudhi, nywele, rangi, wajihi (kimo), matambiko/imani, mila na destruri kwa ujumla.

Ndio hivi biashara ya utumwa na utawala wa wakoloni, climate change na kuleta wahamiaji ambao walichanganyika TZ na makabila waliyoyakuta. wakoloni mfano wajerumani walileta  wabaluchi, waingereza walileta wahindi; waajemi walikuja wenyewe na kuinunua kilwa na kuitawala na kuacha koo zao zilizounda makabila. Mchanganyiko wa wengine wanapojiona weupe huwafanya wajione bora kuliko wengine na kusahau historia na kudiriki hata kutaka nchi zijetenge lakini hana kwao ni wa hano hano na pengine alizaliwa katika njia zisizo halali-kimila. Vurugu huwa kubwa na ubaguzi na kuja kutesa watu kama inavyotokea Sudan na nchi nyingine afrika zenye watu wanaobaguana.





 



On Sunday, 23 March 2014, 12:18, KIM <dekleinson@gmail.com> wrote:
Waisenyi
Wangoreni
Hawa wote ni vikabila vidogo vidogo ambavyo ni jamii za mikurya kama waikoma.

Sent from my Xperia™ smartphone

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.



--
Gaston G Kikuwi
SIDO Small Business House
Bibi Titi Mohamed Road
Block B, 3rd Floor Room No:-34
P O Box 15877, Dar es Salaam-Tanzania
Tel:- +255 22 2152 359
Cell:-+255 784 546 122
       +255 713 294 318
       +255 768 633 685
e-mail:-kikuwigg@gmail.com


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.



--
Gaston G Kikuwi
SIDO Small Business House
Bibi Titi Mohamed Road
Block B, 3rd Floor Room No:-34
P O Box 15877, Dar es Salaam-Tanzania
Tel:- +255 22 2152 359
Cell:-+255 784 546 122
       +255 713 294 318
       +255 768 633 685
e-mail:-kikuwigg@gmail.com

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


0 comments:

Post a Comment