Wednesday, 30 September 2015

Re: [wanabidii] Lowassa akikumbuka kutubu, atasema na hili

Mia mbili tu? Si angejenga kwa pesa za narafiki zake maana ametumua nyingi zaidi kuutafuta huo ukubwa.
Lakini hats kama 200m in kitu gani kstika ujenzi?
Nakumbuka CHADEMA walizipinga shule hizi lakini na muungwana mmoja akawa anasema yeye kwao shule in kila kijiji na wala sio kata!


Walewale

On Oct 1, 2015 6:21 AM, "'Paschal Leon' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
kama chanzo ni Raia Mwema, unarudia hapa ili nini? Kwani watu ni malofa hata gazeti hawanunui?



On Wednesday, September 30, 2015 11:14 PM, 'francis kinyawela' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:


Pamoja na yote hayo nakumbuka Mh Lowassa ndiye aliyeaamuru fedha zilizokuwa kwenye Fixed Deposit account ya Manispaa ya Ilala takribani milioni mia mbili zikajenge shule za Kata. Sijui kama kuna Mh. mwingine alisema hivyo.


From:"'lang'itomoni lokomoi' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
Date:Wed, Sep 30, 2015 at 22:18
Subject:[wanabidii] Lowassa akikumbuka kutubu, atasema na hili


Lowassa akikumbuka kutubu, atasema na hili

KWA muda mrefu nimekaa kimya kusikiliza watu wakizungumza, na hasa mgombea urais kupitia Chadema anayeungwa mkono na vyama vinne, vya NCCR-Mageuzi, CUF na NLD chini ya umoja wao maarufu kwa jina la Ukawa, Edward Lowassa, na wapambe wake kuhusu ujenzi wa shule za sekondari za kata.

Kinachozungumzwa ni kwamba Lowassa ndiye mwanzilishi wa shule hizo huku baadhi ya vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 23, wakitangaza kuwa bila Lowassa wasingepata nafasi.

Vijana hao wanafikiri hivyo kwa madai kuwa ni Lowassa ndiye aliyekuna kichwa kubuni wazo hilo la kuanzishwa kwa shule za kata ambazo wana Ukawa walipokuwa katika Bunge la Tisa na hata la 10 walikuwa wakiziita shule za yeboyebo kwa madai kuwa hazifai kwa lolote lakini baada ya Lowassa kuingia Ukawa, sasa ni kete yao
kisiasa.

Maneno ya Lowassa na wapambe wake kuwa ndiye aliyefanya kazi hiyo ni kupotosha ukweli na kufuta historia halisi ya nani hasa mbunifu wa wazo hilo, mwezi Machi mwaka 2006.

Chimbuko la shule za kata
Kiini cha wazo la kuanzishwa kwa shule za kata kinahusisha historia ndefu tangu utawala wa awamu ya kwanza chini ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, kupitia tume ya kupitia mfumo wa elimu ya Tanzania aliyoiunda Novemba, mwaka 1980, na kuanza kazi rasmi mwanzoni mwa mwaka 1981.

Tume hiyo ilijulikana kama Tume ya Jackson Makweta, kama Mwenyekiti na Katibu wake alikuwa ni Musel Muze, na miongoni mwa wajumbe wa tume hiyo ni pamoja na maprofesa watatu na wajumbe wengine takriban tisa.

Sitaki kwenda kwa undani kuhusu kazi au hadidu rejea za tume hiyo kwa leo, lakini mojawapo ya mapendekezo ya msingi yaliyozaa wazo la kuanzishwa kwa shule za kata ni taarifa ya tume hiyo iliyokuwa na kurasa 354 nje ya viambatanisho, iliyolenga kufanyia marekebisho mfumo mzima wa elimu wa nchini, kwa kupanua kwanza elimu ya sekondari.

Katika mapendekezo hayo mojawapo ya hatua iliyopendekezwa na Tume ya Makweta ni kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 1985, kila tarafa iwe na shule ya sekondari na baadaye kila kata ziwe na shule ya sekondari. Pia tume ilipendekeza baada ya miaka mitano, yaani mwaka 1990 upanuzi wa elimu ya juu uanze rasmi kwa kasi.

Katika pendekezo hilo, Tume ya Makweta iliitaka serikali kupandisha 'ngazi' vyuo vya ufundi vilivyokuwa maarufu kipindi hicho kama Dar Tec, Arusha Tec, Mbeya Tec, Musoma Tec kuwa vyuo vikuu, ili kuongeza nafasi ya elimu ya juu na kufanya Tanzania iendane na mataifa mengine katika elimu ya juu.

Kwa kuwa wakati huo kulikuwa na chuo kikuu cha umma kimoja tu, Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) na tawi lake dogo la Morogoro, tume pia ilipendekeza tawi hilo lipanuliwe kuwa chuo kikuu kinachojitegemea kazi ambayo ilizaa matunda ya kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), mwaka 1984.

Yapo mengi yaliyojiri katika taarifa ya Tume ya Makweta iliyowasilishwa kwa Rais Julius Nyerere, mwezi Machi mwaka 1982, ikiwamo kuhakikisha Kiswahili na Kiingereza ndizo ziwe lugha rasmi za kutumia kufundisha katika ngazi zote ili kuwezesha Tanzania kwenda sawa na mataifa mengine. Kwa kuwa sitaki kujadili kazi na utekelezaji wa tume, kwa ujumla sitakwenda mbali zaidi ya hapo kwa kuwa iko siku nitaandika juu ya utekelezaji wa maoni ya tume hiyo kwa wakati muafaka.
Mkapa na mapendekezo ya ya Makweta

Alipoingia madarakani Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, mwaka 1995 alianza kutekeleza kwa vitendo maoni ya Tume ya Makweta kwa kubuni Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) na Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES).

Kwa wale wanaojua watakumbuka kuwa MMEM ililenga kupanua nafasi za shule za msingi na kuboresha mazingira ya shule ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa vitendea kazi huku MMES, pia ikiwa na lengo hilo kwa shule za sekondari.

Ili kutekeleza azma yake kwa ufanisi mkubwa Rais Mkapa kama kiongozi wa nchi alielekeza kuwepo kwa awamu ya kwanza ya mipango hiyo yaani MMEM na MMES, ambapo awamu ya pili iliangukia katika serikali ya awamu ya nne.
Kikwete na ujenzi wa shule za kata

Baada ya Serikali ya Awamu ya Tatu kukamilisha kazi yake na kukabidhi kijiti cha kuongoza nchi kwa Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais Jakaya Kiwete, Novemba 2005, Edward Lowassa aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huku Waziri wa Elimu akiteuliwa Magareth Sitta na Naibu wake akiwa Mwantumu Mahiza (wote hao wakiwa ni walimu).

Mwezi Machi mwaka 2006 kulifanyika mkutano wa watendaji wa serikali katika Hoteli ya Blue Peal, Ubungo jijini Dar es Salaam.

Katika mkutano huo, kama ilivyo kwa ratiba ya wakubwa Lowassa baada ya kufungua mkutano husika iliwadiwa wakati wa kunywa chai, Naibu Waziri wa Elimu Mahiza, alifanya kile kinachoitwa ujasiri kwa kumwomba Waziri Mkuu wakati huo kumsikiliza kidogo ili amweleze shida yake kwa niaba ya waziri wake.

Katika maeelezo yake Mama Mahiza alimwambia Lowassa kuwa; "Sisi katika Mkoa wa Dar es Saalam tuna shida, tuna watoto waliofaulu lakini hawana nafasi ya kuendelea na masomo sasa tunaomba kutoa wazo la kuwapatia nafasi lakini inahitaji ushauri wako mheshimiwa."

Baada ya maelezo hayo na ufafanuzi wa kina kidogo, Lowassa alimtaka Waziri na timu yake kufika ofisini kwake kesho yake saa nane mchana ili wamweleze kwa undani ni mikakati gani waliyokuwa nayo kuhakikisha watoto hao wanaendelea na elimu ya sekondari, baada ya kufaulu lakini hawawezi kusoma kutokana na ufinyu wa nafasi za sekondari kipindi hicho.

Nataka niweke wazi kuwa wakati huo, Mkoa wa Dar es Salaam ulikuwa na shule za sekondari za serikali tatu tu. Leo mkoa huo una shule za sekondari 112.
Ufaulu ulikuwa ni watoto 33,775 sawa na asilimia 71.2 kati ya 47,459 waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2005 ufaulu uliotokana pia na maboresho ya MMEM huku MMES yakiwa bado hayajatekelezwa vya kutosha kwenda sambamba na ongezeko la ufaulu.

Kati ya wanafunzi 33, 775 waliofaulu ni watoto 25,457 tu ndio waliopata nafasi ya kuendelea na masomo hivyo kufanya wanafunzi 8,300 kukosa nafasi ya kuendelea na masomo. Sitaki kueleza kwa undani mjadala uliokwepo kabla ya Mahiza kumvaa Lowassa kuhusu hali hiyo lakini nitagusia tu kwa ufupi.

Kabla ya Naibu Waziri Mahiza kumvaa Lowassa, aliwaita wabunge watatu wa majimbo kupitia CCM Mkoa wa Dar es Salaam ambao wote bado wapo, Abbas Mtemvu Jimbo la Temeke, Iddi Azan Jimbo la Kinondoni na Mussa Azan Zungu Jimbo la Ilala, na kuwaambia hali halisi kuwa watoto zaidi ya 8,000 wamefaulu lakini wamekosa nafasi ya kuendelea na elimu ya sekondari na hapo, Mahiza akawaeleza kuwa atamvaa Lowassa kumpa wazo la kuondokana na tatizo hilo.

Jibu la Lowassa kwa Mahiza
Baada ya maelezo hayo ya Mahiza kwenye chai, walipotoka hapo walikwenda moja kwa moja kujifungia ofisini yeye na wataalamu karibu wote wa ngazi ya juu hadi usiku wa manane, na kuingia tena alfajiri kwa ajili ya kuandaa kile ambacho Waingereza wanakiita "paper" ya kwenda kwa Waziri Mkuu Lowassa saa nane mchana.

Takwimu zinaonesha kuwa saa 8 kamili mchana Magret Sitta, Mahiza na watalamu wao walitinga kwa Lowassa kuwasilisha paper ya nini tatizo na ni nini wanachotaka kufanya kukabiliana na tatizo.

Walichowasilisha kwa Lowassa
Kwanza walitoa takwimu za ufaulu wa wanafunzi wa shule za msingi kwa nchi nzima wakiainisha kila mkoa kuanzia waliofanya mtihani, waliochaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari na waliokosa nafasi kutokana na ukosefu wa shule za sekondari.

Pili walitoa takwimu maalumu kwa Mkoa wa Dar es Salaam peke yake kutokana kuwa na idadi kubwa zaidi huku serikali nzima ikiwa katika Jiji hilo kubwa Afrika Mashariki. Walitumia mfano wa Dar es Salaam kutaka kujenga hoja yao ambayo kiini chake kilikuwa ni Mahiza kutaka kufanya mambo mawili.

Jambo la kwanza alilopendekeza Mahiza kwa Lowassa ni kuomba kubadilishwa kwa sheria ili Wizara ya Elimu na Ufundi iruhusiwe kutumia fedha za MMES awamu ya pili (MMES 2) kujenga shule mpya za sekondari kwa haraka ili wanafunzi wote waliokosa nafasi waendelee na masomo badala ya fedha hizo kutumika kuboresha shule za zamani na kuwalipia ada watoto wanaotoka katika kaya masikini.

Pili alipendeleza wananchi wachangie kufyatua matofaili na kukusanya mawe, halmashauri za wilaya zichangie usafiri huku serikali kuu kupitia MMES 2 ikipeleka fedha kwa ajili ya mabati, saruji na misumari kukamisha madarasa hayo.

Wakati huo MMES awamu ya pili ilikuwa na lengo la kujenga shule 1,600 katika kipindi cha miaka mitano nchi nzima hatua ambayo bado isingesaidia kutatua tatizo kubwa lililokuwa limekumba taifa kwa wakati huo licha ya idadi hiyo kuwa ndogo mno kwa mahitaji ya nchi.

Mahiza alipata ujasiri huo kwa kuwa wakati huo alikuwa amemaliza kujenga shule ya sekondari ya sayansi kuanzia kidato cha tano hadi cha sita, ikiwa na vitu vyote Bagamoyo, kwa mfumo wa ushirikiano kati ya serikali na wananchi hivyo alikuwa na uzoefu kuhusu kile alichopendekeza kwa Lowassa.

Shule kama hiyo aliyojenga Mahiza zilitakiwa kujengwa katika kanda zote 11 za
elimu nchini japo leo sitaki kujadili kama zipo kweli au imebakia hiyo ya Mahiza peke yake.

Kutokana na 'paper' hiyo Lowassa aliguswa na mpango huo na kutoa ruhusa kwa Wizara ya Elimu kuanza kutekeleza mpango huo japo ilimchukua muda mrefu kumwelewa Mahiza.

Kwa ufupi huo ndio mwanzo wa ujenzi wa shule za sekondari za kata, sasa swali langu la msingi hapa ni je, kati ya Mahiza kwa maana ya Wizara ya Elimu na Lowassa, nani aliyeanzisha shule za sekondari?

Nataka Lowassa atuambie ukweli kuhusu hili na akiwa kama mkristo mzuri atubu katika hili. Lakini pia awaombe radhi Watanzania kwa kujitwalia sifa isiyomhusu bila kuwataja wahusika wakuu.

Lowassa angesema kuwa yeye ni miongoni mwa watendaji wa serikali walioshiriki kuhimiza ujenzi huo wala isingekuwa shida na wala nisingediriki kushika kalamu yangu inayopatika kwa nadra siku hizi kutokana na kubanwa na majukumu mengine ya kitaifa, kuandika juu ya hili.

Najua, natambua na nasema wazi kuwa mwaka 2007 baada ya Bunge la mwezi wa pili, Lowassa kama Waziri Mkuu alimsaidia Rais Kikwete kuratibu mgawanyiko wa mawaziri wote nchi nzima kusimamia uamuzi wa Wizara ya Elimu kuhakikisha shule hizo za kata zinakamilika na watoto wote waliofaulu kupata nafasi ya kuendelea na masomo wanapata fursa hiyo.

Uamuzi huo pia ulitokana na malalamiko kutoka kwa wabunge wengi kuwa watoto wamefaulu hawana pa kwenda, mimi nilikuwepo bungeni na anayenipinga akachukue hansard (kumbukumbu rasmi) za Bunge na orodha ya waandishi wa habari waliokuwapo wakati huo bungeni.

Lakini nikimnukuu Lowassa na mpambe wake namba mbili Frederick Sumaye, ambaye alikuwa waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 10, alisema wazi kuwa hakuwa na nguvu ya kufanya lolote ndio maana walishindwa
kufanya mabadiliko wanayotaka sasa.

Sasa swali langu kwa Lowassa kama kweli hiyo ndio hali halisi kumbe hata usimamizi wa mawaziri kwenda mikoani ilikuwa amri ya Rais Kikwete na si yeye?
Na kama sivyo basi yeye Lowassa na Sumaye watueleze wazi kuwa kama walikuwa na mamlaka makubwa ya kuanzisha vitu kama hivyo na vikafanikiwa kumbe yale yote wanayodai walishindwa ilikuwa ni uzembe wao, hivyo Lowassa hafai kuwa Rais kwa kuwa alishindwa?

Na kama sivyo basi, mafanikio ya shule za kata tumpe Mwantumu Mahiza/ Wizara ya Elimu na Rais Kikwete kama kiongozi wa nchi, aliyetoa kibali cha kubadilishwa kwa sheria, taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za MMES -2. Mimi nasubiri Ikulu ya sasa kabla ya kuingia Rais mpya, basi Rais Kikwete ampe Mahiza tuzo ya ubunifu na kutekeleza maoni ya Tume ya Makweta vinginevyo mnaficha ukweli wa historia.

Tusisahau kuwa moja ya pendekezo la Tume ya Makweta ambayo Mahiza alisaidia ubunifu katika utekelezaji ni upanuzi wa elimu juu yaani vyuo vikuu kuanzia mwaka 1990. Kazi hiyo imefanyika na leo kila mmoja anashuhudia nafasi ya elimu ya juu. Sasa tunapigania ubora wa elimu na si nafasi ya elimu.

Nimalizie makala yangu kwa kusema tufanye siasa kwa lengo la kuomba ushindi lakini tuwaambie Watanzania ukweli tukimhofia Mungu tunayemtaja kuwa yuko pamoja nasi kila siku, kwani iko siku tutajibu kila neno tunalotamka.

Tusisahau kuwa kadri tunavyotumia udhaifu wa Watanzania walio wengi kutojua kufanya utafiti wa mambo muhimu na kuwaaminisha uwongo kama huo kwa maslahi ya kwenda Ikulu, ndivyo tunavyozidi kubomoa taifa badala ya kujenga kwa kuwa
tutakuwa na wananchi wengi wasiojua ukweli kuhusu nchi yao na matokeo yake ni kukosekana kwa uzalendo kwa kuwa hawajui historia halisi ya mambo mbalimbali ya kimaendeleo yanayowahusu.

Siasa za uwongo, za ubinafsi kama hizi ndizo zinatufanya tuamini kuwa Kenya na Uganda wanatuzidi kwa kila kitu jambo ambalo si kweli. Nimeshuhudia mara nyingi wataalamu kutoka Kenya na Uganda wakitiririka Mamlaka ya Mawasiliamo Tanzania (TCRA) kuja kujifunza vitu na mbinu mbalimbali kuhusu uendeshaji masuala ya mawasiliano na teknolojia mpya hapa kwetu.

Nimeshuhudia vijana wa Tanzania wakibuni mbinu za kisasa jinsi ya kutumia teknolojia kama Maxmalipo inayoongoza, lakini leo ukimuuliza kijana wa Tanzania kuhusu ubunifu huo, atakwambia ukitaka kujua mambo mengi kuhusu teknolojia nenda India au Afrika Kusini. Kisa kajazwa uongo na wanasiasa wanaojitafutia ufalme. Tuache siasa za uongo tuseme ukweli, tujenge taifa madhubuti kwa maslahi yetu sote. –

Chanzo Raia Mwema
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
Read More :- "Re: [wanabidii] Lowassa akikumbuka kutubu, atasema na hili"

[wanabidii] INTERNATIONAL DAY OF OLDER PERSONS, SUSTAINABLE CITIES FOR ALL AGES

Habari za asubuhi,


Tafadhali pokea CODES hapa chini


<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/10/UNFPAs-Executive-Director-Dr.-Babatunde-Osotimehin..jpg"><img class="aligncenter wp-image-146690" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/10/UNFPAs-Executive-Director-Dr.-Babatunde-Osotimehin..jpg" alt="UNFPA's Executive Director, Dr. Babatunde Osotimehin." width="618" height="348" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>UNFPA's Executive Director, Dr. Babatunde Osotimehin.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">Population ageing and urbanization are major global issues of the 21<sup>st</sup> century. While cities are growing, their share of residents aged 60 years and over is also rising. Rapid urbanization is challenging both national and local governments in developing inclusive and integrated cities.</span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">Today, as we observe the International Day of Older Persons, we must ensure that cities respond to the needs of persons of all ages and that older persons are as much a part of urban life as their younger counterparts.</span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">This year's theme of <em>Sustainability and Age Inclusiveness in the Urban Environment </em>fits in perfectly with the objectives of the recently adopted 2030 Agenda for Sustainable Development: <strong>leave no one behind</strong>! Together, we must ensure that older persons are fully integrated in cities' economic, social, political and cultural life.</span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">What can we do to make our cities more inclusive? We can start by ensuring that both younger and older generations are included in the urban planning process and their issues, needs and concerns are equally taken into account.</span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">We need an approach to urban planning that focuses on well-being throughout the life cycle. We should invest in young people today by promoting healthy habits, ensuring education and jobs, and providing access to health services and social security coverage for all workers. This is the best investment to improve the lives of young people, help stem the increasing tide of out-migration, and improve the lives of future generations of older persons.</span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">At the same time, we must provide affordable and accessible health-care services, lifelong learning and retraining opportunities, and flexible employment for older persons to improve their well-being and facilitate their integration into the fabric of communities.</span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">Strengthening human capital by ensuring empowerment, education and employment of all citizens will yield a high return on investment and will help countries reap a demographic dividend that can lift millions out of poverty. Creating hope and opportunity for young people to develop their full potential can drive progress in the years to come and, ultimately, result in a second demographic dividend of healthier, wealthier and more productive older persons.</span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">Today, we call on policymakers and urban planners to work together to ensure an inclusive urban environment for all ages. This means paying particular attention to the important pillars of urban living, such as housing, transportation, basic social services, and health care, to make them age-friendly. It means creating an ageless society, characterized by an urban physical environment that facilitates personal mobility, safety and security. It means creating an urban social environment that encourages respect, social inclusion, and participation. And it means protecting natural resources, preparing for natural disasters, and reducing risk so that current and future generations look forward to a sustainable future.</span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">Today, we call on urban leaders to ensure the protection of the human rights of all urban residents, including the elderly who are more vulnerable, and to enforce zero tolerance of discrimination, neglect, violence and abuse of older persons.</span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">Ensuring sustainability and age inclusiveness in the urban environment means creating a society for all ages where the voices of all generations are heard and where the needs of both young and old are met. It means empowering young and old to fully participate in the economic, social and political life of their communities. It means gathering data on city residents and their needs and working to ensure that they are adequately met. It also means sharing experiences about what makes a city a great place to live in for both young and old.</span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;">Age-friendly cities are not just elderly-friendly. They are better for everyone. </span></p>

KAWAIDA




--
Zainul A. Mzige,
Operation Manager,
MO BLOG,
+255714940992.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
Read More :- "[wanabidii] INTERNATIONAL DAY OF OLDER PERSONS, SUSTAINABLE CITIES FOR ALL AGES"

Re: [wanabidii] Kigwangala's facebook

Muganda

Sijasema majimbo nimesema mikoa. Hata kama hutaki lakini ukweli ndio huo Zitto alithubutu kuzunguuka na dk. Slaa uthubu ambao kina Lissu na Mbowe hawana.

Muganda punguza kupenda sana kwani kupenda sana ni ugonjwa na kupenda kuliko pindukia zaidi ni utumwa.

On Sep 30, 2015 10:33 PM, <emuganda@gmail.com> wrote:
Fadhil, kwanza si kweli kwamba Zitto alizunguka na Dr. Slaa katika majimbo zaidi ya 15. Tunachokumbuka ni kwamba Zitto alimkapenia Kikwete Kigoma. Mkapa amefuatana na Magufuli
Bukoba, je hiyo ni dalili ya kuzidiwa? Tumemsikia Nape anamkampenia Magufuli je nako ni kuzidiwa? Wote uliowataja wanasubiri tu kuapishwa. Lema anekatazwa na wananchi wa Arusha wala asihangaike na kampeni.
em

Sent from my iPhone

On Sep 30, 2015, at 1:26 PM, fadhil fadhil <fadhil.fadhil96@gmail.com> wrote:

MUGANDA

asingezidiwa asingewaomba mbowe na Mbatia wawaachie majimbo watu wengine wawafanyie kampeni ili wazunguuke nae,  hilio aliliweza Zito pekee aliyezunguuka na dk. Slaa mikoa zaidi ya 15 baada ya kina mbowe kukimbilia majimboni mwao na kumuacha Dk.Slaa kama wanavyomuacha Lowassa.

On Sep 30, 2015 8:10 PM, "Emmanuel Muganda" <emuganda@gmail.com> wrote:
Fadhil,
Kazidiwa kitu gani? Juzi nimemwona Hai na Mbowe, na pia nimeona umati wa Tanga na Muheza.
Nadhani akina Kigwangala ni kama yule fisi anayemwona binadamu anatembea na kufikiria mkono utaanguka wakati wowote.
em

2015-09-30 13:00 GMT-04:00 fadhil fadhil <fadhil.fadhil96@gmail.com>:

Kiuhalisia lowassa kazidiwa waliotarajiwa kumsaidia kina Lissu, mnyika,  msingwa pamoja na kafulila wote wana hali mbaya majimbini,

Mzee wa watu Kajikatia tamaa matapeli wamemuingiza mjini. Aliwategemea slaa na lipumba ambao dhamira zao zimewasuta.

Kwii kwii kwiiiiiii

On Sep 30, 2015 7:50 PM, "Emmanuel Muganda" <emuganda@gmail.com> wrote:
Do you guys write just for the sake of writing something or something is loose in your heads?
em

Mgombea wa Urais kupitia UKAWA analia lia kumuomba Mbowe aje aongeze nguvu kwenye kampeni zake, inamaanisha nini? Kwangu ni vitu vitatu ama vinne vifuatavyo: cha kwanza, mgombea wa Urais wa UKAWA anahisi kama ametelekezwa na Mwenyekiti wa Chama chake na kwamba ana hisia kuwa Mbowe amepoteza imani ya ushindi, cha pili, Mbowe amebanwa sana jimboni na hivyo karudi kuimarisha jimbo ili asijekosa yote na kwamba haamini tena kama kuna uwezekano wowote ule wa kushinda Urais kwa mwaka huu. Hivyo, bora nusu shari kuliko shari kamili; cha tatu, mgombea wa Urais wa UKAWA hana imani na wanaomfanyia kampeni (akina Zero, Mgeja, Msindai, Masha et al) na yeye mwenyewe hana msuli wa kujifanyia kampeni (hotuba alizokuwa akitoa walau kwa dakika 6 sasa zimekuwa za dakika 1: 08 [ya jana]), na ya nne, ukweli kwamba hatutegemei mgombea wa Urais aanze kulia lia jukwaani mbele ya hadhara ya Hai kumtaka Mwenyekiti wa chama chake aje kwenye kampeni za Urais kuongeza nguvu huku angeweza kulizungumza hilo kwenye vikao vyao vya ndani vya tathmini (CP) inamaanisha kuwa Mwenyekiti amesusa na pengine ni kwa sababu alichokitarajia kutokana na mazungumzo yao hakijatokea...

Acha yote haya yatokee, kwa vyovyote vile, hili moja ni la uhakika, kwamba, kampeni ya CCM imeimarika, mgombea wake Ndg.‪#‎MagufuliMtendaji‬ anaendelea na ‪#‎HapaKaziTu‬, ana ‪#‎Magufulika‬, na sisi wapambe wake tunamagufulika tu kumuunga mkono, nayo imekuwa viral, na hii inaashiria mafanikio makubwa zaidi ya haya yanayojionesha kwenye tafiti mbalimbali; wakati huo huo kampeni ya UKAWA iko hoi bin taabani na mgombea wake amechoka sana mpaka anachanganyikiwa kiasi cha kupotea podium pamoja na mengine ya kusikitisha na kufedhehesha yanayomtokea, na mpaka kufikia mwisho wa kampeni, CCM itakuwa ina uhakika wa ushindi wa zaidi ya asilimia 70!

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
Read More :- "Re: [wanabidii] Kigwangala's facebook"

Re: [wanabidii] Lowassa akikumbuka kutubu, atasema na hili

kama chanzo ni Raia Mwema, unarudia hapa ili nini? Kwani watu ni malofa hata gazeti hawanunui?



On Wednesday, September 30, 2015 11:14 PM, 'francis kinyawela' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:


Pamoja na yote hayo nakumbuka Mh Lowassa ndiye aliyeaamuru fedha zilizokuwa kwenye Fixed Deposit account ya Manispaa ya Ilala takribani milioni mia mbili zikajenge shule za Kata. Sijui kama kuna Mh. mwingine alisema hivyo.


From:"'lang'itomoni lokomoi' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
Date:Wed, Sep 30, 2015 at 22:18
Subject:[wanabidii] Lowassa akikumbuka kutubu, atasema na hili


Lowassa akikumbuka kutubu, atasema na hili

KWA muda mrefu nimekaa kimya kusikiliza watu wakizungumza, na hasa mgombea urais kupitia Chadema anayeungwa mkono na vyama vinne, vya NCCR-Mageuzi, CUF na NLD chini ya umoja wao maarufu kwa jina la Ukawa, Edward Lowassa, na wapambe wake kuhusu ujenzi wa shule za sekondari za kata.

Kinachozungumzwa ni kwamba Lowassa ndiye mwanzilishi wa shule hizo huku baadhi ya vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 23, wakitangaza kuwa bila Lowassa wasingepata nafasi.

Vijana hao wanafikiri hivyo kwa madai kuwa ni Lowassa ndiye aliyekuna kichwa kubuni wazo hilo la kuanzishwa kwa shule za kata ambazo wana Ukawa walipokuwa katika Bunge la Tisa na hata la 10 walikuwa wakiziita shule za yeboyebo kwa madai kuwa hazifai kwa lolote lakini baada ya Lowassa kuingia Ukawa, sasa ni kete yao
kisiasa.

Maneno ya Lowassa na wapambe wake kuwa ndiye aliyefanya kazi hiyo ni kupotosha ukweli na kufuta historia halisi ya nani hasa mbunifu wa wazo hilo, mwezi Machi mwaka 2006.

Chimbuko la shule za kata
Kiini cha wazo la kuanzishwa kwa shule za kata kinahusisha historia ndefu tangu utawala wa awamu ya kwanza chini ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, kupitia tume ya kupitia mfumo wa elimu ya Tanzania aliyoiunda Novemba, mwaka 1980, na kuanza kazi rasmi mwanzoni mwa mwaka 1981.

Tume hiyo ilijulikana kama Tume ya Jackson Makweta, kama Mwenyekiti na Katibu wake alikuwa ni Musel Muze, na miongoni mwa wajumbe wa tume hiyo ni pamoja na maprofesa watatu na wajumbe wengine takriban tisa.

Sitaki kwenda kwa undani kuhusu kazi au hadidu rejea za tume hiyo kwa leo, lakini mojawapo ya mapendekezo ya msingi yaliyozaa wazo la kuanzishwa kwa shule za kata ni taarifa ya tume hiyo iliyokuwa na kurasa 354 nje ya viambatanisho, iliyolenga kufanyia marekebisho mfumo mzima wa elimu wa nchini, kwa kupanua kwanza elimu ya sekondari.

Katika mapendekezo hayo mojawapo ya hatua iliyopendekezwa na Tume ya Makweta ni kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 1985, kila tarafa iwe na shule ya sekondari na baadaye kila kata ziwe na shule ya sekondari. Pia tume ilipendekeza baada ya miaka mitano, yaani mwaka 1990 upanuzi wa elimu ya juu uanze rasmi kwa kasi.

Katika pendekezo hilo, Tume ya Makweta iliitaka serikali kupandisha 'ngazi' vyuo vya ufundi vilivyokuwa maarufu kipindi hicho kama Dar Tec, Arusha Tec, Mbeya Tec, Musoma Tec kuwa vyuo vikuu, ili kuongeza nafasi ya elimu ya juu na kufanya Tanzania iendane na mataifa mengine katika elimu ya juu.

Kwa kuwa wakati huo kulikuwa na chuo kikuu cha umma kimoja tu, Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) na tawi lake dogo la Morogoro, tume pia ilipendekeza tawi hilo lipanuliwe kuwa chuo kikuu kinachojitegemea kazi ambayo ilizaa matunda ya kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), mwaka 1984.

Yapo mengi yaliyojiri katika taarifa ya Tume ya Makweta iliyowasilishwa kwa Rais Julius Nyerere, mwezi Machi mwaka 1982, ikiwamo kuhakikisha Kiswahili na Kiingereza ndizo ziwe lugha rasmi za kutumia kufundisha katika ngazi zote ili kuwezesha Tanzania kwenda sawa na mataifa mengine. Kwa kuwa sitaki kujadili kazi na utekelezaji wa tume, kwa ujumla sitakwenda mbali zaidi ya hapo kwa kuwa iko siku nitaandika juu ya utekelezaji wa maoni ya tume hiyo kwa wakati muafaka.
Mkapa na mapendekezo ya ya Makweta

Alipoingia madarakani Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, mwaka 1995 alianza kutekeleza kwa vitendo maoni ya Tume ya Makweta kwa kubuni Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) na Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES).

Kwa wale wanaojua watakumbuka kuwa MMEM ililenga kupanua nafasi za shule za msingi na kuboresha mazingira ya shule ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa vitendea kazi huku MMES, pia ikiwa na lengo hilo kwa shule za sekondari.

Ili kutekeleza azma yake kwa ufanisi mkubwa Rais Mkapa kama kiongozi wa nchi alielekeza kuwepo kwa awamu ya kwanza ya mipango hiyo yaani MMEM na MMES, ambapo awamu ya pili iliangukia katika serikali ya awamu ya nne.
Kikwete na ujenzi wa shule za kata

Baada ya Serikali ya Awamu ya Tatu kukamilisha kazi yake na kukabidhi kijiti cha kuongoza nchi kwa Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais Jakaya Kiwete, Novemba 2005, Edward Lowassa aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, huku Waziri wa Elimu akiteuliwa Magareth Sitta na Naibu wake akiwa Mwantumu Mahiza (wote hao wakiwa ni walimu).

Mwezi Machi mwaka 2006 kulifanyika mkutano wa watendaji wa serikali katika Hoteli ya Blue Peal, Ubungo jijini Dar es Salaam.

Katika mkutano huo, kama ilivyo kwa ratiba ya wakubwa Lowassa baada ya kufungua mkutano husika iliwadiwa wakati wa kunywa chai, Naibu Waziri wa Elimu Mahiza, alifanya kile kinachoitwa ujasiri kwa kumwomba Waziri Mkuu wakati huo kumsikiliza kidogo ili amweleze shida yake kwa niaba ya waziri wake.

Katika maeelezo yake Mama Mahiza alimwambia Lowassa kuwa; "Sisi katika Mkoa wa Dar es Saalam tuna shida, tuna watoto waliofaulu lakini hawana nafasi ya kuendelea na masomo sasa tunaomba kutoa wazo la kuwapatia nafasi lakini inahitaji ushauri wako mheshimiwa."

Baada ya maelezo hayo na ufafanuzi wa kina kidogo, Lowassa alimtaka Waziri na timu yake kufika ofisini kwake kesho yake saa nane mchana ili wamweleze kwa undani ni mikakati gani waliyokuwa nayo kuhakikisha watoto hao wanaendelea na elimu ya sekondari, baada ya kufaulu lakini hawawezi kusoma kutokana na ufinyu wa nafasi za sekondari kipindi hicho.

Nataka niweke wazi kuwa wakati huo, Mkoa wa Dar es Salaam ulikuwa na shule za sekondari za serikali tatu tu. Leo mkoa huo una shule za sekondari 112.
Ufaulu ulikuwa ni watoto 33,775 sawa na asilimia 71.2 kati ya 47,459 waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2005 ufaulu uliotokana pia na maboresho ya MMEM huku MMES yakiwa bado hayajatekelezwa vya kutosha kwenda sambamba na ongezeko la ufaulu.

Kati ya wanafunzi 33, 775 waliofaulu ni watoto 25,457 tu ndio waliopata nafasi ya kuendelea na masomo hivyo kufanya wanafunzi 8,300 kukosa nafasi ya kuendelea na masomo. Sitaki kueleza kwa undani mjadala uliokwepo kabla ya Mahiza kumvaa Lowassa kuhusu hali hiyo lakini nitagusia tu kwa ufupi.

Kabla ya Naibu Waziri Mahiza kumvaa Lowassa, aliwaita wabunge watatu wa majimbo kupitia CCM Mkoa wa Dar es Salaam ambao wote bado wapo, Abbas Mtemvu Jimbo la Temeke, Iddi Azan Jimbo la Kinondoni na Mussa Azan Zungu Jimbo la Ilala, na kuwaambia hali halisi kuwa watoto zaidi ya 8,000 wamefaulu lakini wamekosa nafasi ya kuendelea na elimu ya sekondari na hapo, Mahiza akawaeleza kuwa atamvaa Lowassa kumpa wazo la kuondokana na tatizo hilo.

Jibu la Lowassa kwa Mahiza
Baada ya maelezo hayo ya Mahiza kwenye chai, walipotoka hapo walikwenda moja kwa moja kujifungia ofisini yeye na wataalamu karibu wote wa ngazi ya juu hadi usiku wa manane, na kuingia tena alfajiri kwa ajili ya kuandaa kile ambacho Waingereza wanakiita "paper" ya kwenda kwa Waziri Mkuu Lowassa saa nane mchana.

Takwimu zinaonesha kuwa saa 8 kamili mchana Magret Sitta, Mahiza na watalamu wao walitinga kwa Lowassa kuwasilisha paper ya nini tatizo na ni nini wanachotaka kufanya kukabiliana na tatizo.

Walichowasilisha kwa Lowassa
Kwanza walitoa takwimu za ufaulu wa wanafunzi wa shule za msingi kwa nchi nzima wakiainisha kila mkoa kuanzia waliofanya mtihani, waliochaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari na waliokosa nafasi kutokana na ukosefu wa shule za sekondari.

Pili walitoa takwimu maalumu kwa Mkoa wa Dar es Salaam peke yake kutokana kuwa na idadi kubwa zaidi huku serikali nzima ikiwa katika Jiji hilo kubwa Afrika Mashariki. Walitumia mfano wa Dar es Salaam kutaka kujenga hoja yao ambayo kiini chake kilikuwa ni Mahiza kutaka kufanya mambo mawili.

Jambo la kwanza alilopendekeza Mahiza kwa Lowassa ni kuomba kubadilishwa kwa sheria ili Wizara ya Elimu na Ufundi iruhusiwe kutumia fedha za MMES awamu ya pili (MMES 2) kujenga shule mpya za sekondari kwa haraka ili wanafunzi wote waliokosa nafasi waendelee na masomo badala ya fedha hizo kutumika kuboresha shule za zamani na kuwalipia ada watoto wanaotoka katika kaya masikini.

Pili alipendeleza wananchi wachangie kufyatua matofaili na kukusanya mawe, halmashauri za wilaya zichangie usafiri huku serikali kuu kupitia MMES 2 ikipeleka fedha kwa ajili ya mabati, saruji na misumari kukamisha madarasa hayo.

Wakati huo MMES awamu ya pili ilikuwa na lengo la kujenga shule 1,600 katika kipindi cha miaka mitano nchi nzima hatua ambayo bado isingesaidia kutatua tatizo kubwa lililokuwa limekumba taifa kwa wakati huo licha ya idadi hiyo kuwa ndogo mno kwa mahitaji ya nchi.

Mahiza alipata ujasiri huo kwa kuwa wakati huo alikuwa amemaliza kujenga shule ya sekondari ya sayansi kuanzia kidato cha tano hadi cha sita, ikiwa na vitu vyote Bagamoyo, kwa mfumo wa ushirikiano kati ya serikali na wananchi hivyo alikuwa na uzoefu kuhusu kile alichopendekeza kwa Lowassa.

Shule kama hiyo aliyojenga Mahiza zilitakiwa kujengwa katika kanda zote 11 za
elimu nchini japo leo sitaki kujadili kama zipo kweli au imebakia hiyo ya Mahiza peke yake.

Kutokana na 'paper' hiyo Lowassa aliguswa na mpango huo na kutoa ruhusa kwa Wizara ya Elimu kuanza kutekeleza mpango huo japo ilimchukua muda mrefu kumwelewa Mahiza.

Kwa ufupi huo ndio mwanzo wa ujenzi wa shule za sekondari za kata, sasa swali langu la msingi hapa ni je, kati ya Mahiza kwa maana ya Wizara ya Elimu na Lowassa, nani aliyeanzisha shule za sekondari?

Nataka Lowassa atuambie ukweli kuhusu hili na akiwa kama mkristo mzuri atubu katika hili. Lakini pia awaombe radhi Watanzania kwa kujitwalia sifa isiyomhusu bila kuwataja wahusika wakuu.

Lowassa angesema kuwa yeye ni miongoni mwa watendaji wa serikali walioshiriki kuhimiza ujenzi huo wala isingekuwa shida na wala nisingediriki kushika kalamu yangu inayopatika kwa nadra siku hizi kutokana na kubanwa na majukumu mengine ya kitaifa, kuandika juu ya hili.

Najua, natambua na nasema wazi kuwa mwaka 2007 baada ya Bunge la mwezi wa pili, Lowassa kama Waziri Mkuu alimsaidia Rais Kikwete kuratibu mgawanyiko wa mawaziri wote nchi nzima kusimamia uamuzi wa Wizara ya Elimu kuhakikisha shule hizo za kata zinakamilika na watoto wote waliofaulu kupata nafasi ya kuendelea na masomo wanapata fursa hiyo.

Uamuzi huo pia ulitokana na malalamiko kutoka kwa wabunge wengi kuwa watoto wamefaulu hawana pa kwenda, mimi nilikuwepo bungeni na anayenipinga akachukue hansard (kumbukumbu rasmi) za Bunge na orodha ya waandishi wa habari waliokuwapo wakati huo bungeni.

Lakini nikimnukuu Lowassa na mpambe wake namba mbili Frederick Sumaye, ambaye alikuwa waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 10, alisema wazi kuwa hakuwa na nguvu ya kufanya lolote ndio maana walishindwa
kufanya mabadiliko wanayotaka sasa.

Sasa swali langu kwa Lowassa kama kweli hiyo ndio hali halisi kumbe hata usimamizi wa mawaziri kwenda mikoani ilikuwa amri ya Rais Kikwete na si yeye?
Na kama sivyo basi yeye Lowassa na Sumaye watueleze wazi kuwa kama walikuwa na mamlaka makubwa ya kuanzisha vitu kama hivyo na vikafanikiwa kumbe yale yote wanayodai walishindwa ilikuwa ni uzembe wao, hivyo Lowassa hafai kuwa Rais kwa kuwa alishindwa?

Na kama sivyo basi, mafanikio ya shule za kata tumpe Mwantumu Mahiza/ Wizara ya Elimu na Rais Kikwete kama kiongozi wa nchi, aliyetoa kibali cha kubadilishwa kwa sheria, taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za MMES -2. Mimi nasubiri Ikulu ya sasa kabla ya kuingia Rais mpya, basi Rais Kikwete ampe Mahiza tuzo ya ubunifu na kutekeleza maoni ya Tume ya Makweta vinginevyo mnaficha ukweli wa historia.

Tusisahau kuwa moja ya pendekezo la Tume ya Makweta ambayo Mahiza alisaidia ubunifu katika utekelezaji ni upanuzi wa elimu juu yaani vyuo vikuu kuanzia mwaka 1990. Kazi hiyo imefanyika na leo kila mmoja anashuhudia nafasi ya elimu ya juu. Sasa tunapigania ubora wa elimu na si nafasi ya elimu.

Nimalizie makala yangu kwa kusema tufanye siasa kwa lengo la kuomba ushindi lakini tuwaambie Watanzania ukweli tukimhofia Mungu tunayemtaja kuwa yuko pamoja nasi kila siku, kwani iko siku tutajibu kila neno tunalotamka.

Tusisahau kuwa kadri tunavyotumia udhaifu wa Watanzania walio wengi kutojua kufanya utafiti wa mambo muhimu na kuwaaminisha uwongo kama huo kwa maslahi ya kwenda Ikulu, ndivyo tunavyozidi kubomoa taifa badala ya kujenga kwa kuwa
tutakuwa na wananchi wengi wasiojua ukweli kuhusu nchi yao na matokeo yake ni kukosekana kwa uzalendo kwa kuwa hawajui historia halisi ya mambo mbalimbali ya kimaendeleo yanayowahusu.

Siasa za uwongo, za ubinafsi kama hizi ndizo zinatufanya tuamini kuwa Kenya na Uganda wanatuzidi kwa kila kitu jambo ambalo si kweli. Nimeshuhudia mara nyingi wataalamu kutoka Kenya na Uganda wakitiririka Mamlaka ya Mawasiliamo Tanzania (TCRA) kuja kujifunza vitu na mbinu mbalimbali kuhusu uendeshaji masuala ya mawasiliano na teknolojia mpya hapa kwetu.

Nimeshuhudia vijana wa Tanzania wakibuni mbinu za kisasa jinsi ya kutumia teknolojia kama Maxmalipo inayoongoza, lakini leo ukimuuliza kijana wa Tanzania kuhusu ubunifu huo, atakwambia ukitaka kujua mambo mengi kuhusu teknolojia nenda India au Afrika Kusini. Kisa kajazwa uongo na wanasiasa wanaojitafutia ufalme. Tuache siasa za uongo tuseme ukweli, tujenge taifa madhubuti kwa maslahi yetu sote. –

Chanzo Raia Mwema
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


Read More :- "Re: [wanabidii] Lowassa akikumbuka kutubu, atasema na hili"

[wanabidii] UBA’S ODUOZA WINS CEO OF THE YEAR AWARD AT INVESTMENT SUMMIT IN NEW YORK

Habari za asubuhi,


Tafadhali pokea CODES hapa chini


<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/09/Mr.-Phillips-Oduoza-GMD-CEO-UBA-Plc.jpg"><img class="aligncenter wp-image-146659" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/09/Mr.-Phillips-Oduoza-GMD-CEO-UBA-Plc.jpg" alt="Mr. Phillips Oduoza, GMD-CEO, UBA Plc" width="552" height="552" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Group Managing Director and CEO, UBA Plc, Mr. Phillips Oduoza.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Group Managing Director and CEO, UBA Plc, Mr. Phillips Oduoza has emerged the 2015 Ai Socially Responsible Investment (SRI) 30 CEO of the year at this year's 8th annual Ai CEO Investment Summit.  This is the second time he is winning the award after winning it first in 2013.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>He was named the winner from a long shortlist that included Nassef Sawiris, CEO, Orascom Construction Company, Sifiso Dabengwa, CEO, MTN Group, SA, Guillaume Roux, CEO, Lafarge Africa, Segun Agbaje, CEO, GT Bank, Graham Clark, GMD, Dangote Sugar and Ben Kruger/Sim Tshabalala, Co-CEOs, Standard Bank. The event took place in New York at the sidelines of the UN General Assembly.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Africa investor (Ai), is a leading international investment and communications group based in South Africa. Every year it organises the institutional investment summit as a platform for public and private sector leaders in Africa to dialogue with global counterparts on ways to invest and grow businesses in Africa. As an integral part of the summit, Ai also hosts the investment and business leadership awards to reward exceptional business practices, economic achievements and investments across Africa, whilst recognising the institutions and individuals improving the continent's investment climate.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>At the summit and awards ceremony attended by over 250 of Africa's most prominent and influential business, government and development finance leaders, as well as five African Heads of State, the UBA CEO won the Ai SRI CEO of the Year award in recognition of his exceptional achievements over the last year which according to the summit organisers, is an "inspiration for business and government leaders working to raise Africa's investment profile".</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>The judging panel considered excellent leadership skills, enhanced organisational image, innovation and originality as well as alignment with the millennium development goals (MDGs) in choosing the Socially Responsible Investment (SRI) 30 CEO of the year.  Speaking on the award, Oduoza who has twice been recipient(the first time in 2013), said: 'as Africa's global bank, The United Bank for Africa, UBA, has operations in 19 African countries and 3 global financial centres -  New York, London and Paris, serving over 9 million customers. This award validates our efforts over the years in building a solid pan-African banking business that is profitable, sustainable and socially responsible. I dedicate it to all UBA people: customers, staff and other stakeholders in Africa and across the globe". </strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Other recognitions at the ceremony include: Venture Capital/Private Equity Award won by the Abraaj Group, whilst Institutional Investor of the Year and Investment Promotion Agency of the Year went to Public Investment Corporation of South Africa (PIC) and Centre de Promotion des Investissementsen Côte d'Ivoire (CEPICI) respectively. The Leadership in Sustainable Investment in Africa Award went to the Bill and Melinda Gates Foundation.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/09/Uganda-Pres-GM-USA.jpg"><img class="aligncenter wp-image-146660" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/09/Uganda-Pres-GM-USA.jpg" alt="Uganda Pres + GM USA" width="631" height="419" /></a></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Uganda President Yoweri Museveni with General Manager USA.</strong></em></span></p>
&nbsp;


KAWAIDA

Mr. Phillips Oduoza, GMD-CEO, UBA Plc

Group Managing Director and CEO, UBA Plc, Mr. Phillips Oduoza.

Group Managing Director and CEO, UBA Plc, Mr. Phillips Oduoza has emerged the 2015 Ai Socially Responsible Investment (SRI) 30 CEO of the year at this year's 8th annual Ai CEO Investment Summit.  This is the second time he is winning the award after winning it first in 2013.

He was named the winner from a long shortlist that included Nassef Sawiris, CEO, Orascom Construction Company, Sifiso Dabengwa, CEO, MTN Group, SA, Guillaume Roux, CEO, Lafarge Africa, Segun Agbaje, CEO, GT Bank, Graham Clark, GMD, Dangote Sugar and Ben Kruger/Sim Tshabalala, Co-CEOs, Standard Bank. The event took place in New York at the sidelines of the UN General Assembly.

Africa investor (Ai), is a leading international investment and communications group based in South Africa. Every year it organises the institutional investment summit as a platform for public and private sector leaders in Africa to dialogue with global counterparts on ways to invest and grow businesses in Africa. As an integral part of the summit, Ai also hosts the investment and business leadership awards to reward exceptional business practices, economic achievements and investments across Africa, whilst recognising the institutions and individuals improving the continent's investment climate.

At the summit and awards ceremony attended by over 250 of Africa's most prominent and influential business, government and development finance leaders, as well as five African Heads of State, the UBA CEO won the Ai SRI CEO of the Year award in recognition of his exceptional achievements over the last year which according to the summit organisers, is an "inspiration for business and government leaders working to raise Africa's investment profile".

The judging panel considered excellent leadership skills, enhanced organisational image, innovation and originality as well as alignment with the millennium development goals (MDGs) in choosing the Socially Responsible Investment (SRI) 30 CEO of the year.  Speaking on the award, Oduoza who has twice been recipient(the first time in 2013), said: 'as Africa's global bank, The United Bank for Africa, UBA, has operations in 19 African countries and 3 global financial centres -  New York, London and Paris, serving over 9 million customers. This award validates our efforts over the years in building a solid pan-African banking business that is profitable, sustainable and socially responsible. I dedicate it to all UBA people: customers, staff and other stakeholders in Africa and across the globe". 

Other recognitions at the ceremony include: Venture Capital/Private Equity Award won by the Abraaj Group, whilst Institutional Investor of the Year and Investment Promotion Agency of the Year went to Public Investment Corporation of South Africa (PIC) and Centre de Promotion des Investissementsen Côte d'Ivoire (CEPICI) respectively. The Leadership in Sustainable Investment in Africa Award went to the Bill and Melinda Gates Foundation.

Uganda Pres + GM USA

Uganda President Yoweri Museveni with General Manager USA.




--
Zainul A. Mzige,
Operation Manager,
MO BLOG,
+255714940992.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
Read More :- "[wanabidii] UBA’S ODUOZA WINS CEO OF THE YEAR AWARD AT INVESTMENT SUMMIT IN NEW YORK"

[wanabidii] Top Headlines: India calls Pakistan 'prime sponsor of terrorism', asks it to vacate PoK

Times of India
Daily Newsletter | Thursday, October 01, 2015
fbtwittergoogleplus
TOP HEADLINESMORE »
India calls Pakistan 'prime sponsor of terrorism', asks it to vacate PoK
Bluntly calling Pakistan a ''prime sponsor of terrorism,'' India on Wednesday asked Islamabad to vacate the part of Kashmir it has occupied, virtually laying down a new paradigm for any resolution of the issue.
PM rides Gandhi wagon to woo Africa leaders
This Gandhi Jayanti, PM Narendra Modi will rekindle Mahatma Gandhi’s Africa connection to reach out to African leaders ahead of the third India-Africa Forum Summit from October 27-29.
Nirbhaya teen radicalized in juvenile home?
Central intelligence agencies have expressed concern that the juvenile involved in the 2011 Delhi High Court blast may be trying to indoctrinate the teen, found to be in conflict with law in the 2012 Nirbhaya gang-rape case, for joining jihad.
CITIESMORE »
Kolkata: Doctors alarmed by ‘mixed malaria’
Is the Plasmodium vivax — the protozoa that triggers benign malaria — turning virulent and acquiring the characteristics of the more potent falciparum parasite that causes cerebral malaria?
Kolkata: Tagore’s Jorasanko abode in tatters
Rabindranath Tagore may be the most celebrated author at home and abroad, but Jorasanko Thakurbari, the building that stands witness to the bard’s formative years, is in dire straits.
AIADMK councillor murdered in public in Chennai
In a bloody reminder of the politician- land mafia nexus, an AIADMK councillor was murdered in front of his house at Mannurpet near Ambatture Industrial Estate on Wednesday.
TECHMORE »
Apple's India sales target: 12L iPhones in one quarter
Apple is gearing up for a blockbuster opening of new iPhone devices in India as it targets to sell 12 lakh devices in the October-December quarter, nearly equivalent to its total sales for whole of last year.
5 devices unveiled at Google event
Here's a look at the five devices Google unveiled today
Google unveils Nexus 5X, Nexus 6P smartphones
Google Nexus 5X with 5.2-inch screen will cost $379, whereas Nexus 6P with 57-inch display will be available for $499; both will be up for preorder starting next week.
SPORTSMORE »
Rohit predicts India to become world's best fielding unit
India's Ajinkya Rahane pouched a record number of catches - 8 - in a Test match, overtaking Yajuvindra's seven against England in Bangalore.
Ranji Trophy: Can Gambhir-Jadeja change Delhi's fortunes?
Surprisingly, Ishant lost his place in the 15-man Delhi squad for not responding to phone calls and text messages from chief selector Vinay Lamba.
N Srinivasan moves SC accusing Anurag Thakur of perjury
N Srinivasan on Wednesday moved the Supreme Court accusing the BCCI secretary Anurag Thakur of committing an offence of perjury before the top court.
BUSINESSMORE »
India bright spot in slowing global economy: IMF chief
Global growth will be likely weaker this year than last with only a modest acceleration expected in 2016, International Monetary Fund chief Christine Lagarde said on Wednesday, and reiterated that India remains a bright spot.
WTO cuts 2015 trade growth forecast
WTO on Wednesday lowered the global trade growth forecast for 2015 to 2.8%, from 3.3% projected in April, adding to the already gloomy sentiment for Indian exporters.
Jabong's Jan-June losses soar 46%, in talks for sale
Rocket Internet-backed fashion e-tailer Jabong saw its losses widen at a time when it's been put on the block for a possible sale.
ENTERTAINMENTMORE »
Bollywood’s Prem returns with Sonam
Prem Ratan Dhan Payo sees the return of Salman Khan’s most-loved character, Prem. It also marks the reunion of Sooraj Barjatya and Salman after a gap of 16 years.
Pic: Harbhajan-Geeta's wedding invite
We were the first to tell you about Harbhajan Singh and Geeta Basra’s wedding details in our September 6 edition, titled 'Elaborate 5-day Punjabi wedding for Geeta-Harbhajan, reception in Delhi'.
Bollywood's most desirable single men
While Shahid Kapoor is now taken, and ruling heartthrob Ranbir Kapoor is already with Katrina Kaif, we take a look at the most desirable single men left in Bollywood today.
Other Newsletters from TOI:
Breaking News | Digest | Tech | Entertainment | Movie Reviews | Life & Style
Unsubscribe | To manage your newsletter subscription settings, click here.
Copyright 2015 Bennett Coleman & Co. Ltd. All rights reserved. For reprint rights: Times Syndication Service
Read More :- "[wanabidii] Top Headlines: India calls Pakistan 'prime sponsor of terrorism', asks it to vacate PoK"