Mama Anilea;
Time will tell and it is also a good don for almost all the time.
Tusubiri tu,kwani kesi ya jinai haifi, hukaa hata miaka sitini (kwa mujibu wa Mwakyembe) alipokuwa akiongea na wananchi wa Kyela hapo majuzi.
Mwisho wao tutaujua tu,Magufuli katoa ahadi ya kuanzisha mahakama ya mafisadi kama akiwa Presdo.
Reuben
On Tuesday, September 1, 2015 7:25 PM, 'ananilea nkya' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Ndugu Mokili Juma, Reuben Mwandumbya, Omukunirwa Ireneus, na Wa Sembeye
Nanawashukuruniu sana kwa kusoma hadi mwisho makala yangu niliyoposti jioni ya leo.
Ndugu Mokili Juma, nakushukuru zaidi kwa kunishauri kwamba nipitie makala zangu kwa makini kabla ya kuposti ili kuondoa makosa madogo madogo. Lakini hilo la kumpa mtu mwingine anisomee bahati mbaya sina mtu wa kumpa asome maana niko nje ya nchi—niko mwenyewe. Kadhalika ninaamini kwamba kama ni makosa madogo madogo yasiyo ya kimaudhui msomaji anaweza kusahihisha na kama ni mtu anataka kuitumia kuchapisha gazetini au blog ni vema kuyaondoa makosa hayo madogo madogo.
Nisema kuwa ninapoandika humu hoja zangu ninachojaribu kufanya ni kutoa mchango wangu wa mawazo ili sote tujadili hatma ya nchi yetu kwa kuzingatia ukweli hata kama ukweli huo unaumiza.
Mokili kama umesoma andiko langu vema nimeeleza sababu ya wananchi kupiga kura ya hapana CCM. Kama huafikiani na sababu nilizotoa nawe andika hoja yako tuzijadili hapa maana tunachoshindanisha hapa ni hoja---hoja zilizojikita kwenye ukweli bila woga.
Ndugu Reuben Mwandumbya , Wa Sembeye na Omukunirwa Ireneus.
Kama mnakumbuka Profesa Lipumba awali alisema amemkubali Lowassa baada ya kubaini ufisadi nchini chanzo chake ni serikali CCM na kwamba hata baada ya Lowassa kuachia Uwaziri Mkuu kumekuwa na ufisadi kibao na alitolea mfano ufisadi wa Tegeta escrow. Lipumba alipoachia uenyekiti wa CUF alisema tatizo lake nafsi inamsuta kwa kumpa mtu aliyetoka CCM kugombea Urais kupitia vyama vya upinzani. Lakini kumbuka hata Mwalimu Nyerere alisema upinzani wa kweli utakaowaondolea wananchi umaskini utapatikana pale CCM itakapopasuka. Je kuna ubaya gani mtu aliyetoka CCM kugombea Urais vyama vya upinzani?
Lakini mimi wacha ya Lipumba au Dr Slaa kujiweka pembeni maana hawa wawili nao walikuwa wanataka kugombea Urais kupitia UKAWA.
Swali langu siku zote limekuwa hili: Kama Edward Lowassa ndiye fisadi wa Richmond na mtu hatari Tanzania kwa ufisadi na serikali ya CCM haikuhusika na ufisadi huo wa Richmond wala wa Tegeta escrow ni kwa nini serikali ya CCM haikumpeleka mahakamani Lowassa kwa ufisadi wa Richmond miaka minane imepita sasa?
Ananilea Nkya
E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com
--------------------------------------------
On Tue, 9/1/15, Ireneus Kakuru Mushongi <ireneuskakurumushongi@gmail.com> wrote:
Subject: [Mabadiliko] Re: [wanabidii] WANANCHI WAFANYE NINI WASHINDE UCHAGUZI 2O15
To: "wanabidii@googlegroups com" <wanabidii@googlegroups.com>
Cc: "Wanazuoni@yahoogroups.com" <Wanazuoni@yahoogroups.com>, "mabadilikotanzania@googlegroups.com" <mabadilikotanzania@googlegroups.com>, "Paschally Mayega" <ngowe2006@yahoo.com>
Date: Tuesday, September 1, 2015, 4:21 PM
Mama
Nkya
Hebu weka vizuri hicho
kichwa hapo juu. Kwa kuwa una mahaba na UKAWA sema ama
andika hivi WANAUKAWA TUFANYE NINI ILI TUSHINDE
UCHAGUZI..Sio wananchi hapa kila mtu ni mwananchi bila
kujali itikadi ya chama chake. Unawaambia wananchi wote ama
wana UKAWA tu? Sijaelewa hapa nani mwananchi na na nani sio
mwananchi and are the wananchi against each other..are all
wananchi fighting the common enemy? Wagombea pia bila kujali
vyama vyao na itikadi zao ni wananchi tu!
Sema nani (Mwananchi fulani)
kumshinda mwananchi wa chama fulani... Usifumbe macho au
kufunika uso huku ukidhani huonekani.
Kuwa wazi kama ambavyo umekuwa wazi
baada ya mapinduzi (ya wanaCCM) ndani ya CHADEMA... na
kubadilisha kabisa dhana ya mabadiliko ambayo ndiyo kimsingi
iliijenga CDM na hatimaye kuendelea kuiua dhana hii kadiri
muda unavyokwenda. Watu wanaoijua spidi ya JPM hawatokaa
ndani ya CCM sababu they will be next in a new reformed CCM
hasa baada ya shedding inayoendelea. So lazima wacheze na
opportunities (Diversification). UKAWA ikiwini then they
will safeguard their interests sababu sasa dhana ya ufisadi
sio issue tena huko CDM, the moment ukitumbukia, you are
automatically clean. Hata hawa champions wa Radar, Escrow,
Kagoda, kesho wakifanya Shedding wakahamia UKAWA, they are
auto-cleaned kadiri tunavyoona maana mnajitahidi kuja na
kiLa aina ya strategy za kuwanawisha.
.......na
lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa
limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani,
litakuwa limefunguliwa
mbinguni...... (Mt.16:19)
Kuwa
specific..
Omukunirwa
Ireneus
2015-09-01 17:51 GMT+03:00
'mokili juma' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Sawa dadangu Nkya.
Nimeisoma makala yako ndefu kuhusu "Wananchi wafanye
nini washinde Uchaguzi 2015". Lakini ajabu ukiingia
ndani unaongelea haja ya Wananchi kuiondoa CCM kwa Kupiga
Kura mwaka 2025!!!!!Nakushauri tena,
Tulia dadangu......... Acha jazba!!! Unapoandika makala
jaribu kumpa mtu mwingine mmoja ama hata ikiwezekana, wawili
ili waisome na kufanya masahihisho kabla ya
"kuipost" kwa wasomaji. Badilika
Anna!
On Tuesday,
September 1, 2015 5:26 PM, 'ananilea nkya' via
Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
wrote:
WANANCHI WAFANYE NINI WASHINDE UCHAGUZI
2015?
Na Ananilea Nkya
Mmoja wa watu waliosoma
makala yangu Raymond Mauki, makala niliyoandika kwamba
CCM ilimtoa Edward Lowassa kafara kwa kumpakazia
ufisadi wa Richmond ili chama hicho kidanganye
wananchi kwamba fisadi ni Lowassa na CCM ni chama safi,
amenishukuru kwa mchango wangu kwa taifa kupitia ile
makala. Baada ya kuisoma ameniomba nijubu maswali mawili.
Kwenye malaka hiyo
iiliandika kwa serikali ya CCM ndiyo fisadi wa fedha za
umma na hivyo chanzo cha wananchi wengi hapa nchini kuwa
maskini. Nilitoa mfano wa serikali ya CCM kuwa fisadi
kusimamia wizi wa fedha za umma kwenye akaunti ya Tegeta
Escrow shilingi bilioni 306 mwaka jana 2014. Nilitoa pia
mfano wa ufisadi wa Richmond kwamba ni serikali ya CCM
yenyewe ilihusika lakini walidanganya umma kwamba muhusika
ni Edward Lowassa.
Uthibitisho ni kwamba kama Lowassa ndiye
alikuwa fisadi wa Richmond leo hii angekuwa yuko jela kama
Mramba na Yona. Nilisema pia kwamba hivi sasa nchi
imejaa ufisadi unaofanywa na watawala wa serikali ya CCM
kwa hiyo hata mgombea wa CCM wa sasa John Pombe Magufuli
wanayejidai ni mtu msafi akichaguliwa yerikali yake
italazimika kufanya ufisadi penda asipende. Na yeye
mwenyewe Magufuli amekaririwa akisema kwamba ataika
mfano marais waliomtangulia.
Kwa hiyo nikawashauri wananchi wapiga kura
wakiwepo wanaCCM kwamba kama wanataka nchi yetu iondokane
na ufisadi wa fedha za umma na jeuri ya watawala wa CCM
kujitajirisha huku wananchi wengi wakiwa ni maskini wa
kutupa, na tena watawala hadi kufikia kuwatukana wananchi
masikini kwamba ni malofa na wapumbavu ni lazima
wananchi wafanye mabadiliko—waiondoe CCM madarakani mwaka
huu 2025 kwa kutumia sanduku huru la kura hapo tarehe 25
Oktoba .
Maswali mawili
ambayo msomaji wangu alitaka niyajibu ni haya
ifuatavyo:
Swali la kwanza: Nini mchango wa
wanawake kwenye harakati hizi za leo,unadhani wameamka
kiasi cha kutosha?
Mchango
wa wanawake katika kuleta mabadiliko katika maisha yao
kupitia uchaguzi wa mwaka huu 2015 ni mkubwa na muhimu
sana. Wanawake kwa wingi wao wakijitokeza kusikiliza
kampeni za uchaguzi kisha wakijitokeza kupiga kura na
wakaipigia kura UKAWA wataleta mabadiliko. Hivyo kila
mwanamke aliyejiandikisha kupiga kura, namshauri atunze
kitambulisho chake cha kupiga kura(kichinjio).
Afanye hivyo kwa
kutokukubali kumuonyesha mtu yeyote kitambulisho chake.
Kitambulisho chako ni siri yako (ni silaha yako) ya itunze
kama mboni ya jicho hakuna mtu mwingine yeyote hata kama ni
kiongozi, hata kama ni polisi au mgambo hapaswi kukiona
kitambulisho (kichinjio)n chako. Zaidi hata kama huyo mtu
atakuwa amekuletea zawadi ya kanga, kitende, fulana, sukari,
fedha au chochote kile mwanamke USIDANGANYIKE.
Mimi sina chama chochote cha
siasa nimefungamana nacho lakini nasisitiza wanawake
waipigie kura UKAWA kwa sababu ilani ya UKAWA ina
agenda kuu mbili muhimu zinazogusa maisha ya wanawake moja
kwa moja.
Kwanza UKAWA
wana agenda ya kutoa elimu bure hadi Chuo Kikuu. Hili ni
muhimu kwa sababu elimu ndiyo msingi wa maendeleo yote kwa
mtu binafsi wakiwopo watoto wa kike, familia na taifa
zima.
Pili UKAWA wana
agenda ya kuandika Katiba Mpya inayotokana na maoni ya
wananchi. Moja ya jambo muhimu katika Katiba ya wananchi
ni kuweka uhusiano mpya kati ya viongozi na wananchi.
Katiba Mpya itazuia viongozi kujitajirisha kwa mali za
umma huku mamilioni ya wananchi wakiwepo wanawake
wakitaabika kwa umaskini.
Fedha za nchi zinazotafunwa na watawala
wachache zitatumika kwa mfano kuboresha elimu, huduma
za afya,maji, umeme, kujenga viwanda kuwapatia maelefu ya
watu ajira. Pili Katiba mpya itaweka misingi imara ya
kuhakikisha uwakilishi wa wanawake kwenye vyombo vya
maamuzi unafikiwa asilimia 50/50.
Kashalika Katiba Mpya italeta usawa wa kweli
wa kijinsia nchini na usawa huo utaanza kuonekana dhahiri
uchaguzi wa 2020 kwa kutoa idadi sawa wanawake na
wanaume madiwani kwenye kata na idadi sawa ya wabunge
wanawake na wanaume majimboni. Kadhalika kwenye vijiji na
mitaa mwanamke akiwa mwenyekiti mwanaume atakuwa Makamu
mwenyekiti.
Utaratibu
wa viti maaluma utatumika kwa watu wenye ulemavu peke
yake. Kila aina ya ulemavu itakuwa mbunge mwanamke na
mwanaume. Hayo ndiyo mabadiliko kamili nay a kweli kuhusu
usawa wa kijinsia unaotakiwa Tanania ili nchi yetu na watu
wake waondokane na umaskini.
Katika uchaguzi wa mwaka huu kuna vyama
vinajinasibu eti vimezingatia usawa wa jinsia kwa kuweka
mwanamke mgombea mwenza au mgombea wa Urais. Ni sawa
lakini hiyo ni geresha ya danganya toto kwa sababu kwa
mfumo wa sasa ambapo usawa wa 50 kwa 50 haujawekewa
misingi kwenye Katiba wanawake wanatumika tu kama
wanaume kupitisha sheria na sera za maendeleo za
kunufaisha kikundi kidogo cha watawala wananchi wanaume na
wanawake wakibaki mafukara wa kuputa.
Usawa wa jinsia wa kweli na wa kudumu
hauwezi kufikiwa hapa nchini bila Katiba Mpya ya wananchi
kuandikwa na kuweka misingi ya kutekeleza usawa wa
jinsia kwa vitendo—misingi inayowaondolea wanawake vikwazo
vya kugombea na kushinda sawa na wanaume majimboni na
kwenye kata na siyo viti maalum vya upendeleo—miaka 50
baada ya nchi kupa uhuru.
Kwa hiyo ushuri
wangu kwa wanawake na wale wote wanaofanya kampeni UKAWA
ni kuwaeleza wanawake na wananchi ukweli kwamba wakitaka
mabadiliko ya kweli katika maisha yao wachague UKAWA ndio
waliobeba ajenga ya ukombozi—agenda ya kuwaletea
Watanzania mabadiliko ya kweli yatakayojengwa kwenye misingi
imara –Katiba Mpya iliyotokana na maoni ya wananchi.
Swali la Pili: Watanzania
tufanye nini kuzuia CCM kuiba kura uchaguzi wa mwaka
huu 2015? Mimi napendekeza yafuatayo:
Kwanza: Kila mwananchi mwanamke mwanaume
wakiwepo wana CCM mnaouchukia kuona watu wengi
wanateseka kwa umaskini na watawala wachache wana utajiri wa
kupindukia, kinachotakiwa kama mnanataka uchaguzi wa
mwaka huu uwe ni mwamzo wa kubadilisha maisha ya kimaskini
wanayoishi mamilioni ya Watanzania, ni kutunza
kitambulisho chako (kichinjio) na siku ya kupiga kura
tarehe 25 Oktoba mwaka huu 2015 kwenda kupiga kura kuchagua
UKAWA. Ninaipigia debe UKAWA—umoja unaojumuisha vyama vya
CUF, NLD, NCCR Mageuzi na CHADEMA kwa sababu wana agenda
ya ukombozi wa wananchi.
UKAWA wana
ajenda ya kuandika Katiba Mpya inayotokana na maoni ya
wananchi. Katiba Mpya itaweka misingi mipya ya kuongoza nchi
kuleta mabadiliko-kuondoa umaskinini unaotengenezwa kwa
serikali ya CCM kukwapua fedha za wananchi na jeuri ya
kupora madaraka ya wananchi—yaani CCM kujifanya chama
dola.
Hata kama itakulazimu kusubiri
siku mbili au hata wiki nzima hata mwezi mmoja kuweza kupiga
kura fanya hivyo usikate tamaa. Kakikisha hukosi kupiga
kura maana hakuna ukombozi wenye kuleta mabadiliko
katika maisha ya wananchi wengi ambao hupatikana katika
demokrasia ya vyama vingi vya siasa bila wananchi wenyewe
kushiriki kuleta mabadiliko hayo kupitia sanduku huru la
kura.
Umaskini wa
wananchi ninaouzungumza ni pamoja na ukosefu wa ajira ya
kuwapatia walio wengi wasio watumishi wa umma fedha za
kujikimu. Watumishi wengi wa umma mfano walimu,
madaktari, wauguzi, askari, wahudumu wa maofisa na kulipwa
mshahara isiyokidhi mahitaji ya msingi kama vile chakula,
mavazi na malazi.
Kadhalika kulima kukopwa mazao yao na kutolipwa
kwa muda mrefu. Ukosefu wa barabara vijijini, ukosefu wa
maji, watu kufa kwa kukosa dawa ili hali watawala wachache
wakiugua wao wana haki ya kutumia fedha za umma kwenda
kutibiwa nchi za nje.
Elimu
duni inayosababishwa na shule ambazo si bora hazina
chakula kwa wananfunzi, usafiri, vitabu, maabara na miundo
mbinu mingine muhimu. Shule hazina hazina walimu wenye
ubora na wanaofurahia kufanya kazi zao kwa vile
wanaheshimiwa, kuthaminiwa na kulipwa vizuri.
Vilevile umaskini na kuporw
amadaraka wananchi kunakojidhihirisha kwa vyombo vya
dola hasa polisi kutumika kibabe kunyanyasa wananchi
kama vile nchi yetu bado iko kwenye ukoloni.
Pili: Kila kila Mtanzania
aliyejiandikisha kupiga kura anayeumwa na hali ya umaskini
wa wananchi wengi anapaswa kutunza kitambulisho chake cha
kupiga kura (kichinjio) na asikubali kumuonyesha au kumpa
mtu yeyote hata awe mwenyekiti nyumba kumi, mwenyekiti wa
kitongoji, kijiji, mtaa , polisi , mgambo au mtu yeyote
yule.
Hii ni muhimu maana wapo watu hivi
sasa wanapita nyumba kwa nyumba wakijidai wanafanya
kampeni za nyumba kwa nyumba kumbe ni mbinu za kuwanunua au
kuwadanganya na kuwaogopesha wananchi wanaotaka mabadiliko
ambao Rais Mstaafu Benjami Mkapa amewaita ''MALOFA
NA WAPUMBAVU''.
Lengo la kuwadanyanga au kuwatia woga wananchi
ni ili wasipige kura ya kuwaletea mabadiliko kwa
kuikataa CCMambayo utawala wake umewafanya wananchi wengi
kuwa malofa na wapumbavu huku watawala wa serikali ya CCM
wakijilipa fdha za wananchi na kupata utajiri wa
kukufuru.
Nawashauri
wapiga kura kama ni fedha, nguo, chakula watakuwa
wanaletewa na CCM wakati wanapita kwenye kampeni walizosema
watafanya nyumba kwa nyumba zipokeeni maana pengine hizo
ni zile fedha za wananchi zilizoibiwa mwaka jana 2014 kwenye
akaunti ya Tegeta escrow Benki kuu ambazo nyingine
zilibebwa kwa tandarusi. Ni fedha za wananchi kuleni na
kama ni nguo vaeni ni mali yenu lakini usimpe tena kura
yako maana atarudi tena kwenda kukwapua nyingine na hakuna
kazi yoyote kuwaondolea wananchi umaskini wataifanya
miaka 5 ijayo.
Aidha kila
anayepiga kampeni UKAWA awaeleze wananchi ukweli huu.
Wananchi wakiujua ukweli kuhusu chimbuko la matatizo
yanayowakabili kuwa ni serikali ya CCM kama taasisi
kujihusisha na ufisadi na kuwapora wananchi madaraka,
wananchi wataelewa na watapiga kura kikamilifu kuleta
mabadiliko—kuchagua UKAWA kuendesha serikali tuone
miaka mitano nao watafanya nini kuwaondolea wananchi
umaskini. Wasipotimiza ahadi zao hasa —elimu bure hadi
chuo kikuu na Katiba Mpya uchaguzi wa 2020 watapigwa chini
kupitia sanduku huru la kura . Bila kubadilishana vyama
kwa kuzingatia sera za maendeleo umaskini unaowasumbua
Watanzania wengi hautaondoka nchini.
Tatu: UKAWA viweke mawakala wenye uchungu na
maisha ya mamilioni ya Watanzania. Mawakala ambao
hawahongeki, hawadanganyiki. Mawakala wa UKAWA wanatakiwa
wawe ni watu wanaoweza kuvumilia njaa na wanaoweza kukesha
hadi kazi ya kupiga, kuhesabu kura na kutangaza mshindi
ikamilike. Maana kwenye uchaguzi wakala ukipepesa
ukipepesa macho kidogo tu wajanja wanachakachua.
Nne: UKAWA kuweka mawakala
makini ambao siyo mamluki wa CCM-- watu jasiri (siyo
watu waoga) na wanaojua kusoma, kuandika na kuhesabu na
wenye moyo wa kujitolea kwa faida ya walio wengi
wanaoteseka na maisha duni. Kura ni hesabu kwa mtu
asiyejua kusoma, kuandika na kuhesabu ni rahisi sana
KUDANGANYIKA maana hataweza kusoma na kuelewa
kilichoandikwa.
Tano:
UKAWA kuweka mawakala wenye uvumilivu—mtu ambaye anaweza
kuvumilia njaa ikibidi kukaa bila kula na kunywa kwa
zaidi ya saa 24. Wako mawakala chaguzi zilizopita kwa
kuendekeza ulaji na unywaji wakiwa kazini kwenye vituo vya
kupiga kura, waliagiza vinywaji na vyakula na vinywaji.
Lakini wajanja waliweka kwenye vyakula na vinywaji hivyo
dawa za usingizi. Baada ya kula walijikula na walikuja
kuamka uchaguzi ulikuwa umewisha na kura za mgombea
wao ambaye alikuwa anapendwa na watu amekwishaibiwa kura
zake wakiwa usingizini.
Ninachosema hapa ni kwamba uchaguzi ni wa
mwaka huu ni mapambano ya mamilioni ya wananchi masikini
(wakiwepo wanaCCM wengi tu) na kikundi cha watawala wa CCM
wanaoendelea kujitajirisha kwa kuwa madarakani.
Hivyo mamilioni ya wananchi
wanaoteseka na umaskini wakiamua kuvishinda vishawishi na
ulaghai unaofanywa na watawala wa CCM uchaguzi wa mwaka
huu utaleta mabadiliko kwa mara ya kwanza kuwezesha mfumo wa
vyama vingi kufanya kazi Tanzania. Zaidi fursa ya mamilioni
ya wananchi wanaoishi maisha ya kimaskini kushinda
uchaguzi wa mwaka huu 2015 ni kubwa kuliko wakati
mwingine wowote katika historia ya vyama vingi nchini
kwetu.
Sita: UKAWA
wahakikishe inawaelekeza mawakala wake mambo muhimu ya
kufanya wakiwa kwenye vituo vya kupiga kura. Mambo hayo ni
pamoja na kuhakikisha wanachukua kwa usahihi matokeo
kwenye vituo na kisha wafuatilie kwenye halmashauri
kuhakikisha anayeshinda ndiye anatangazwa mshindi.
Umuhimu wa kufuatilia hadi
matokeo yatangazwe ni kuhakikisha waliopewa mamlaka
kutangaza matokeo ya diwani, mbunge na Rais hawachakachui
matokeo. Umma ukiwa unafuatilia matokeo-wenye kutaka
kufanya mchezo mchafu watauogopa umma. Hakuna kinachoshinda
nguvu ya umma. MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Ninaruhusu Makala hii
ichapishwe na yeyote anayetaka. Lengo ni kuelimishana ili
kuleta mabadiliko . Ukiwa na swali: niandikie: ananilea_nkya@yahoo.com
Ananilea Nkya
E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com
--------------------------------------------
On Sat, 8/22/15, 'raymond mauki' via
Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
wrote:
Subject:
[wanabidii] Re: [Wanazuoni] LOWASSA KAFARA CCM KUJARIBU
KUZUIA MABADILIKO [1 Attachment]
To:
"Wanazuoni@yahoogroups.com"
<Wanazuoni@yahoogroups.com>,
"mabadilikotanzania@googlegroups.com"
<mabadilikotanzania@googlegroups.com>
Cc: "WANA BIDII" <wanabidii@googlegroups.com>,
"Paschally Mayega" <ngowe2006@yahoo.com>
Date: Saturday, August 22, 2015, 5:11 AM
Mama Nkya
nimekuelewa sana
sana na sana, siku zote
nimekuwa nikifuatilia harakati zako
ila
sikujua msimamo wako uko wapi. Nashukuru kwa kuwaambia
watanzania kuwa kila mtu ana uhuru wa kutoa
maoni yake
haijalishi yupo wapi, ana nafasi
gani kwa jamii au yupo
upande gani kisiasa.
Ulichokiandika ni very simple and very
true
hata mtoto wa darasa la nne ataelewa ila cha ajabu kuna
wasomi watakuja kupinga na wanaendeta kupinga
ulichokiandika
tena wakitumia data za uongo
kabisa. Ni ukweli uliowazi kuwa
watanzania
wa leo sio wa mwaka 1995 wa Mrema na nashukuru
yeye mwenyewe amekiri hilo juzi kupitia kituo
kimoja cha
redio(clouds fm), watanzania wa
leo wanahitaji mabadiliko
chanya na
wasipoyapata kwa amani basi watatumia njia
nyingine yoyote japo hatupendi ifike huko.Mama
Nkya, naomba ukipata muda unijibu haya
mawili,
Je, tufanye nini watanzania lei
hii ili kuzuia kabisa
mchezo wa ccm
kutuibia kura zetu kwenye uchaguzi mkuu?
Ukizingatia wameshakiri kabisa watatumia njia yoyote
kushinda ikiwemo goli la mkono.Pili,
nini mchango wa wanawake kwenye harakati hizi
za
leo,unadhani wameamka kiasi cha
kutosha?
Asante
na
ubarikiwe sana,
RAYMOND
MAUKIKIGAMBONI,
DAR ES SALAAM.
From:"ananilea
nkya
ananilea_nkya@yahoo.com
[Wanazuoni]"
<Wanazuoni@yahoogroups.com>
Date:Fri, Aug 21, 2015 at 23:42
Subject:[Wanazuoni] LOWASSA KAFARA CCM
KUJARIBU KUZUIA MABADILIKO [1 Attachment]
[Attachment(s) from ananilea nkya
included below]
LOWASSA
KAFARA CCM KUJARIBU KUZUIA MABADILIKO
Na
Ananilea Nkya
Nimeandika hoja hii baada
ya kusoma na kusikia hoja
zinazotolewa
na baadhi ya Watanzania kwamba eti CHADEMA ,
CUF, NCCR-Mageuzi na NLD -vyama
vinavyounda UKAWA kwa
kumsimamisha
Edward Lowassa kugombea Urais vimepoteza
usafi wa kuongoza mapambano dhidi ya ufisadi.
Ukweli ni kwamba viongozi wa CHADEMA na UKAWA
kumsimamisha
Lowassa kuwa mgombea urais
wamecheza kama Pele. Tena
wanastahili
pongeze kubwa maana walitumia akili kali na
saikolojia ya hali ya juu kubaini kuwa CCM ilikuwa
ilicheza
mchezo mchafu kisiasa kuwatumia
wapinzania kumpakazia
Lowassa ufisadi na
hatimaye CCM kupata nguvu ya kumtoa
Lowassa
kafara ili eti CCM ionekane inajisafisha ufisadi.
Wanaodhani CHADEMA na UKAWA
wamekosea pengine hawajaelewa
kuwa tangu
upepo wa mabadiliko wa kukataliwa mfumo chama
kimoja kuwa madarakani kwa muda mrefu
ulipoanza kuvuma
duniani kote mwishoni mwa
miaka ya 1980, baadhi ya wanaCCM
hawajakubali kwa dhati kabisa ukweli huo na kuamini kwamba
CCM inaweza kupunzishwa kuongoza nchi
angalao kwa miaka
mitano.
Hasa
baada ya Mwalimu Nyerere CCM kuondoka duniani, CCM
imebaki na viongozi ambao hawako tayari
kutumia ujasiri
kuongoza mabadiliko kwa
amani. Baadhi ya vongozi wanaojali
zaidi
maslahi ya wana CCM wachache wanaotumia kauli kama
hirizi kauli aliyowahi kuitoa Mwalimu Nyerere
kuwa bila CCM
imara—Tanzania itayumba
kujidanganya wenyewe na kudanganya
wananchi.
Wanasahau kwamba Mwalimu
Nyerere kama mwanafalsafa na
mwanasiasa
makini alikuwa anatoa maamuzi ya kijasiri kwa
faida ya taifa na wananchi kulingana na hali
halisi ya
wakati husika kwa kusoma upepo wa
wananchi. Kwa mfano
Nyerere aliwahi kusema
CCM si mama yake akimaanisha Tanzania
na
Watanzania ni muhimu zaidi kuliko umuhimu wa CCM kuwa
madarakani.
Mfano Mwalimu Nyerere
mwaka 1992 alionyesha mfano kwamba
maslahi
ya nchi na wananchi ndiyo muhimu kuliko maslahi ya
CCM alipokubali kwenda kinyume na uamuzi wa
wanaCCM wengi
waliokuwa
wamekataaa—mabadiliko—kuanzishwa vyama vingi
nchini ili vyama vibadilishane uongozi wa nchi
--kuharakisha
maendeleo ya wananchi.
Lakini baada ya Mwalimu kuondoka dunaini kila
mwanaCCM
anayechaguliwa kuwa Rais, kwa
kuogopa kulaumiwa kwamba eti
kama CCM
haitachaguliwa kupitia sanduku huru la kura atabeba
lawama za kufanya CCM iondoke madarakani,
serikali zote za
CCM baada ya Mwalimu
Nyerere kuondoka duaniani zimekuwa
zinajihusisha na ufisadi.
Serikali ya CCM imekuwa
ikikwapua kwa wizi wa wazi mabilioni
ya
fedha za umma na kufanya maovu mengine mengi kuhakikisha
CCM haiondoki madarakani. Hivyo chaguzi
zinafanyika kama
geresha tu—kudanganya
wafadhili na mataifa kuwa Tanzania
ni nchi
ya demokrasia ya vyama vingi.
Mfano
uchaguzi wa mwaka 2005 serikali ya CCM chini ya Rais
Mkapa ilikwapua fedha za wananchi kutoka Benki
Kuu Akaunti
ya EPA shilling bilioni 133
ambazo ziliiwezesha CCM kumweka
madarakani
Rais Kikwete.
Mwaka jana 2014 serikali ya
CCM chini ya Kikwete ilikwapua
shilingi
bilioni 306 kutoka akaunti ya Tegeta escrow Benki
Kuu kwa ajili ya kuiwezesha CCM kushinda
uchaguzi wa
serikali za mitaa na uchaguzi
mkuu unaofanyika tarehe 25
Oktoba mwaka huu
2015.
CCM wakishaingia madarakani jambo muhimu
kuliko yote Rais na
serikali yake
analolifanyia ni kubuni ufisadi wa kuipatia
CCM fedha na mbinu nyingine za kuiwezesha CCM ibaki
madarakani uchaguzi unaofuta. Hakuna kazi
muhimu ya
kuwaondolea wananchi umaskini
inayofanyika kwa kiwango na
juhudi
kubwa.
Kwa sababu hiyo, kikundi kidogo cha
watawala, wengi wakiwa
ni kutoka CCM na
familia zao wamejikuta wakinufaika kwa kuwa
matajiri kufuru kwa muda mfupi ili hali
wananchi wengi
wakibaki maskini na mafukara
wa kutupa.
Mfano wabunge (kikundi cha
watu wasiozidi 400) wengi wakiwa
ni
wanachama wa CCM kila mmoja analipwa si chini ya
milioni 10 kila mwezi kama mishahara, wacha
marupurupu na
posho za vikao vya kamati,
posho za safari na mamilioni
mafao kila
baada ya miaka mitano. Lengo wawe na fedha
nyingi za kununua kura za wapiga kura maskini
uchaguzi
unaofuata CCM ibaki madarakani.
Ndiyo sababu kila mwananchi wakiwepo watu
muhimu kama walimu
wa vyuo vikukuu na
madaktari hivi sasa nao wameamua kuwa
wanasiasa.
Zaidi baadhi ya wanaotafuta
madaraka ya kisiasa wanatumia
mbinu chafu
sana ikiwa ni pamoja na ushirikina wa kuuwa
watu wenye ulemavu wa ngozi (albinism) waweze
kupata nafasi
ya kuingia katika kundi la
watawala—kupata utajiri wa
kutisha katika
kipindi cha miaka mitano.
Mfamo Wabunge
waliomaliza muda wao mwaka huu 2015 kila
mmoja ameondoka na kiinua mgongo zaidi ya
shilingi milioni
200. Hii ni kufuru
katika nchi inayojinasibu kuwa ni
maskini
na inapita huko na huko duniani kuomba misaada!
Hata hivyo kwa kadri ufukara unavyoendelea
kuwatafuna
wananchi wengi, na kwa kadri
uelewa wa wananchi
wanaoteseka kwa
umaskini unavyoongezeka kwamba CCM na
utawala wa serikali yake ndicho chanzo cha umaskini wao,
CCM imebaini kuwa haiwezi tena
kushinda uchaguzi kupitia
sanduku huru la
kura kwa kutegemea kete moja tu—kununua
wananchi mafukara peke yake.
Hivyo
katika miaka ya hivi karibuni CCM imeanza kuendesha
siasa za maji taka—kuchafuana wao kwa wao na
hatimaye
wameamua kutoana kafara-lengo kuu
likiwa ni kuzuia wananchi
wasitumie
sandundu la kura kufanya mabadiliko—kuchagua
vyama vingine kuongoza nchi.
Hivyo Rais Kikwete, hata kama ndani ya umungu
wa moyo wake
hakubaliani na CCM inavyotumia
ubabe kukataa mabadiliko
kinyume na asili
ya binadamu, amekuwa akifanya mambo
kutimiza matakwa ya baadhi ya wanaCCM —kujaribu kuzuia
mabadiliko—ili tu kuepuka lawama- amalize
muda wake bila
kuonekana ndiye kasababisha
wananchi kuipunzisha CCM uongozi
kwa
kipindi cha miaka mitano.
Kwa
kufanya hivyo Rais Kikwete amejikuta akiporwa ujasiri
wake aliokuwa nao kama mwanasiasa ambaye
Mwalimu Nyerere
alimuamini.
Kumbuka Mwalimu Nyerere alinukuliwa na gazeti
la Nipashe na
Majira 26/5/95 akisema
baada ya Rais Mwinyi baadhi ya
vijana
ambao alikuwa anaona wana nia ya dhati kabisa na
uwezo mkubwa wa kuongoza Tanzania ni
Benjamin Mkapa, Jakaya
Kikwete na Edward
Lowassa.
Lakini kwa
Kikwete kukubali kuyumbishwa na wana CCM wachache
wasiokubali mabadiliko anaonekana kufumbia
macho utekelezaji
wa kile mwanafalsafa
Mwalimu nyerere alichokisema---kwamba
Watanzania wanataka mabadiliko.
Mfano Rais
Kikwete alipata fursa ya kusimamia mabadiliko kwa
kuandika Katiba Mpya inayotokana na maoni ya
wananchi.
Lakini kikundi kidogo cha
wahafidhina ndani ya CCM
kilimtisha
akajikuta anaweka pembeni ujasiri wake aliokuwa
nao wa kusimamia mabadiliko hayo muhimu kwa
maendeleo ya
taifa hili.
Kama
uamini jiulize ni kwa nini Kikwete aliachia Bunge la
Katiba lililojaa asilimia 80 ya wanachama
likazika Rasimu
ya Katiba ya wananchi pale
Dodoma mwaka jana 2014 -- Rasimu
ambayo
ingeleta Katiba yakuweka misingi ya kuleta
madadiliko Tanzania—mabadiliko ya
kuhakikisha kikundi
kidogo cha watawala
hakijitajirishi kwa ufisadi na kujigawia
mali za umma huku mamilioni ya wananchi wakibaki maskini
na
mafukara wa kutupa?
Baada ya
Kikwete kupoteza fursa ya kuleta mabadiliko kwa
kuandika Katiba Mpya, umma uliofukarishwa
umeendelea
kupata uelewa kuwa CCM na
serikali yake ndicho chanzo cha
umaskini
wao.
Hivyo ili kuendelea kubaki madarakani
serikali ya CCM
imekuwa ikijihusisha na
ufisadi ili ipate fedha za
kuwarubuni
walala hoi wakati wa kampeni za uchaguzi.
Mfano
mwaka 1995 Rais Benjamini Mkapa alijikuta serikali
yake ikifanya ufisadi katika akaunti EPA
(bilioni 122)
zilizotumiwa na CCM
kumuweka Kikwete madarakani.
Ukitafakari utaona kwamba katika ufisadi Tegeta escow,
serikali ya CCM imekapua billion 306 mara tatu
ya ufisadi wa
EPA mwaka 1995 ilipokwapua
bilioni 122 ili kipate fedha
nyingi zaidi
la kuwalaghai wapiga kura mafukara ambao
wameendelea kupata uelewa kuwa CCM inaiba fedha za umma
kununua wapiga kura wakati wa kampeni za
uchaguzi.
Hivyo serikali ya CCM
inayoongozwa na Kikwete ambayo
imeshuhudia
nguvu ya wananchi kudai mabadiliko ikiwa kubwa
kuliko wakati mwingine wowote, inajaribu kila
mbinu chafu na
safi ili CCM ibaki
madarakani baada ya uchaguzi mwaka
huu.
Ndiyo sababu serikali ya CCM kupitia
msemaji wa chama
hicho Nape Nnauye imeanza
kuwaambia Watanzania kuwa CCM
lazima
ishinde uchaguzi wa mwaka huu hata kama ni kwa
kutumia goli la mkono (wizi au lolote lile
chafu).
Zaidi Rais Kikwete amefikishwa
mahali pabaya
kulazimika kubuni
mchezo mchafu kujaribu kuwadanganya
Watanzania kuwa eti CCM na serikali yake ni safi,
haijihusishi na ufisadi unaofukarisha wananchi
isipokuwa
wanachama wachache wa CCM ndio
mafisadi.
Ili kujaribu kutafuta
kujenga uhalali wa CCM kubaki
madarakani
baada ya uchaguzi wa mwaka huu 2015, Kikwete
amejikuta akilazimika kumtoa kafara
Lowassa kwa
kumpakazia ufisadi wa
Richmond.
Wananchi wanauliza kama
Lowassa alikuwa ndiye mhusika wa
Richmond ni kwa nini Spika wa Bunge Anna Makinda
(mmoja
wa watawala wa CCM), hakuagiza
tume ya Bunge iliyoongozwa
na Mbunge wa CCM
Harrison Mwakyembe kumhoji Waziri Mkuu
Edward Lowassa?
Pili wananchi wanahoji kama
CCM haijamtoa Lowassa kafara
kwa
kumbebesha ufisadi wa chama hicho ili kupumbaza hasira
ya wananchi dhidi ya ufisadi wa CCM kwenye
uchaguzi wa
Oktoba mwaka huu 2015 ni kwa
nini Rais Kikwete alikubali
Waziri wake
Mkuu Edward Lowassa ajiuzulu kwa ufisadi wa
Richmond 2008 wakati ufisadi wa kutisha
ulifanywa na
serikali ya CCM kwenye akaunti
ya Tegeta escrow 2014
Kikwete aliwatetea
mawaziri waliogawiwa fedha hizo na Ikulu
ilikuwa ndiyo mtuhumiwa namba moja?
Mimi si
mwanasiasa wa chama chochote cha siasa hapa nchini
ninachoangalia ni chanzo cha umaskini wa
wananchi wengi
Tanzania.
Ndiyo sababu Watanzania wengi nikiwepo mimi mwenyewe kwa
sababu tulipewa habari nusu nusu
zilizotolewa kimkakati na
serikali ya CCM
kuhusu kashfa ya Richmond kumpakazia
Lowassa ufisadi, tulipubwazwa tukaisaidia CCM kumchafua
Lowassa kuwa ni fisadi wa Richmond.
Lakini baadhi ya wananchi walianza kujua
kuna ukweli
uliofishwa kuhusu Richmond pale
TV moja ilipokuwa imemwalika
Lowassa aotoe
yake ya moyoni live siku chache baada ya
kujiuzulu, lakini kipindi hicho cha TV kikafutwa ghafla.
Hata hivyo ukweli huo umekuja kujulikana mwezi
Julai mwaka
huu Lowassa alipotoa hadharani
baada ya kuachana na CCM na
kujiunga na
CHADEMA.
Sasa wananchi
wamefahamu kuwa CCM chini ya serikali ya
Rais Kikwete iliamua kumtoa Lowassa kafara kwa
kumpakazia
ufisadi wa Richmond ili
kuiokoa CCM isiadhibiwe vikali
na wananchi
kwenye sanduku huru la kura –kwa ufisadi
alinawasababishia umaskini na ufukara.
Ndiyo sababu hivi sasa CCM na baadhi ya
wanahabar
wanapakazia CHADEMA na
UKAWA kuwa eti ni mafisadi
baada ya
kumpokea Lowassa (kafara wa CCM) na kumpitisha
kuwa mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania.
Isitosha
hivi sasa kikundi cha watawala wachache wa
serikali ya CCM wanahaha na wanamzonga Kikwete
azuie
mabadiliko kwa mkono kwa kufanya
kila uchafu kupumbaza
Watanzania kwa
kutumia kete ya eti Lowassa ni fisadi wa
Richmond hivyo hana sifa ya kugombea Urais
wa Tanzania,
bali Magufuli ndiye mtu
safi.
Wananchi wenye akili zao wanajiuliza hivi
mwenye kashfa za
kifisadi kati ya Lowassa
na Magufuli ni nani? Ni Lowassa
aliyepakaziwa Richmond au ni Magufuli aliyeongoza
watawala
kujiuzia kwa bei chee nyuma za
umma zilizogarimu wanannchi
mabilioni ya
fedha?
Wananchi pia wanajiuliza kama Lowassa ni
fisadi wa Richmond
ni kwa nini serikali ya
CCM haijamshitaki mahakamani miaka
minane
tangu ufisadi huo ulipotokea?
Hivyo
pengine baada ya Lowassa kutafakari nafsi yake na
kuona kuwa CCM imemtoa kafara asigombee
Urais ili kuzuia
mabadiliko, ameamua
kufanya maamuzi magumu ya kuhama CCM
--kushiriki kuongoza masikini na mafukara wanaotafuta
mabadiliko.
Lowassa ameamua
kutekeleza alichokitabiri Mwalimu Nyerere
kwamba CCM isipokubali kuongoza wananchi wapate
mabadiliko
wanayoyataka—wananchi
watayatafuta mabadiliko hayo nje
ya
CCM.
Ni dhahiri CCM ilipoteza fursa adimu ya
kuongoza wananchi
kwenye kuleta mabadiliko
kwa kuandika Katiba Mpya-- kuweka
misingi ya kukomesha mfumo wa utawala unaowezesha
watawala
kuwa matajiri wa kupindukia huku
mamilioni ya wananchi
wakiwa mafukara na
nchi ikinuka aibu ya umaskini wa
kijitakia ikiwa rasilimali nyingi za asili.
Wanaomchochea Rais Kikwete asikubali
mabadiliko yachukue
mkondo wake, wameunda
timu ya kampeni yanye wajumbe wengi
waliohusika kumpakazia Lowassa ufisadi wa Richmond ili
eti
kwenye kampeni waendelee kumpaka
ufisadi Lowassa, CHADEMA
na UKAWA
wakidhani Watanzania hawana akili ya kutafakari.
Lengo lao ni moja. Wanajua kabisa kuwa kwa
kutumia sanduku
huru la CCM haiwezi
kuchaguliwa. Wanataka kutumia
kisingizio
kuwa CHADEMA na UKAWA imechafuka eti kwa
kumsimamisha Lowassa Urais ambaye CCM
imemtoa karafa –
kwa kumpakazia ufisadi
wa Richmond.
Lakini
baada ya kupata salamu za wananchi kupitia mafuriko
yao kwenye kumtambulisha Lowassa kwamba wao
wanaelewa fisadi
kamili ni CCM, sasa CCM
imeshtuka imeanza kutumia polisi
kuwaadhibu
wananchi. Pengine baadaye itatumia jeshi
kabisa.
Zaidi imeamua kujaribu kampeni za
ardhini -nyumba kwa
nyumba, bila shaka
kutumia mabilioni ya fedha serikali ya
CCM
ilizokwapua Tegeta escrow kununua shahada na kura za
mafukara.
Kwenye
kampeni za nyumba kwa nyumba mtu kwa mtu ndiko
ufisadi mbaya wa kisiasa
unakofanyika—kununua, kutisha na
kuumiza wananchi mafukara.
Swali ni je Watanzania wangapi wapiga kura
watakubali CCM
inapopita majumbani mwao
kuuza shahada zao kwa sukari,
kanga au
fedha hata kama CCM itaamua kumpa kila mpiga kura
shilingi milioni moja?
Ni
mpiga kura gani atakayekubali KUDANGANYIKA kwa
kununuliwa na CCM kwa vijizawadi vya fedha
nguo KUSALITI
mamilioni ya watanzania
wanaoendelea kuteseka kwa ufukara
kila
baada ya uchaguzi kwisha na CCM kubaki madarakani?
Wananchi pia wanauliza je mabilioni ya
escrow yatawanunua
wajumbe wa NEC ili
wavuruge daftari la wapiga kura, au
wachakachue kama uchaguzi wa 2010 au wataharibu daftari
la
wapiga kura, mashine na vifaa vya
kupigia kura, au
kuchelewesha kwa makusudi
kufungua vituo vya wapiga kura
ili
kuvuruga uchaguzi CCM ishinde kwa goli la mkono?
Kadhalika wananchi wanauliza wanaomshinikiza
Kikwete
asikubali mabadiliko wakiona hilo
haliwezekani je watamuua
Lowassa waliomtoa
kafara au viongozi wa CHADEMA na UKAWA
waliompokea Lowassa na kumwezesha kufikia azma yake ya
kujitolea kuwatumikia watanzania ili
kuvuruga uchaguziwa
mwaka huu?
Wananchi wanauliza maswali hayo baada ya
kubaini kwamba
huenda wasiomtakia mema
Kikwete astaafu kwa amani
wamejaribu
kuwalaghai baadhi ya viongozi wakuu wa UKAWA ili
kujaribu kuvuruga UKAWA – lakini UKAWA kwa
vile ni sauti
ya mafukara-sauti ya umma
imeendelea kuwa moto mkali wa
nyika dhidi
ya CCM.
Hivyo binafsi namshauri Rais
Kikwete akubali kuwa baba wa
pili wa Taifa
hili baada ya Nyerere kuondoka. Akubali
kusimamia wananchi watumie sanduku huru la kura kwenye
uchaguzi wa mwaka huu 2015 kupata mabadiliko
ya uongozi
wanayoyataka.
Wananchi wana imani na UKAWA kwamba wakiingia
madarakani
Katiba mpya inayotokana na maoni
ya wananchi itaandikwa.
Huo utakuwa ni mwanzo wa
mabadiliko wanayoyataka
wananchi—kuhakikisha watawala hawajitajirishi
kupindukia
kufisadi fedha za wananchi huku
wananchi wengi wakibaki
mafukara.
CHADEMA na UKAWA wasipotimiza hili na kuonyesha
kwa vitendo maendeleo watakayokuwa
wameyaleta kwa miaka
mitano, ni lazima
wananchi watatumia sanduku la kura
kuwapunzisha.
Ninaamini ni wenye kutetea
maslahi binafsi tu ndiye
atakayemlaumu Rais
Kikwete kwamba eti CCM isipochaguliwa
Oktoba 25, Kikwete atakuwa ni chanzo cha wananchi
kuamua
kuipunzisha CCM kwa miaka mitano.
Nitakuwa wa kwanza kuwapinga watu hao na
kumtetea Kikwete
hata kama ni kwa kuamua
kuingia kwenye siasa kwa kujiunga
na CCM
.
Hakika Rais Kikwete ukisimamia
wananchi wazungumze kuhusu
hatma ya
uongozi wan chi yao kwa kutumia sanduku huru la
kura bila CCM kuingiza mkono mchafu, wewe
mwenyewe
ukistaafu utaishi kwa amani na
furaha huku baadhi yetu
tukikuona kama baba
wa Pili Taifa taifa hili, baada ya
Mwalimu
Nyerere.
Mwisho ninaruhusu yeyote
anayetaka kuchapisha au kutangaza
redioni
natelevisheni niyoyoyaandika hapa TV au kuchapisha
na kuwasambazia Watanzania wote popote walipo
ujumbe huu
afanye hivyo. Wanawaza
kuwasambazia watu mitaani,
kwenyemikutano
ya kampeni, mashuleni vyuoni popote
pale—lengo likiwa moja—sote Watanzania tuujue ukweli
kuhusu ufisadi na mchango wake katika
kuwafanya Watanzania
waishi katika
umaskini. Lakini muhimu kila Mtanzania ajue
hakuna mshindi wa kujisifu—mshindi ni nchi
yetu Tanzania
na Watanzania wote.
MUNGU IBARIKI YANZANIA.
Ananilea
Nkya
E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com
__._,_.___
Attachment(s)
from ananilea nkya | View
attachments on the web
1 of 1 File(s)
LOWASSA KAFARA WA
CCM.docx
Posted by: ananilea
nkya
<ananilea_nkya@yahoo.com>
Reply
via web post
•
Reply to
sender
•
Reply to group
•
Start a New
Topic
•
Messages in this
topic
(1)
Visit Your Group
New
Members
2
• Privacy • Unsubscribe • Terms of Use
.
__,_._,___
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole
responsibility
for any legal consequences
of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree
to this
disclaimer and pledge to abide by
our Rules and
Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to
the
Google Groups "Wanabidii"
group.
To unsubscribe
from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send
Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to
this Forum bears the sole responsibility for any legal
consequences of his or her postings, and hence statements
and facts must be presented responsibly. Your continued
membership signifies that you agree to this disclaimer and
pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message
because you are subscribed to the Google Groups
"Wanabidii" group.
To unsubscribe
from this group and stop receiving emails from it, send an
email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la
'Mabadiliko'.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii:
mabadilikotanzania@googlegroups.com
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Mabadiliko Forum" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
To post to this group, send email to mabadilikotanzania@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania.
To view this discussion on the web visit https://groups.google.com/d/msgid/mabadilikotanzania/CAN5khk7sowgC0R%2Bmyb8awOO85DX3-Bnp66JJ6CP6zLGnLnhXTg%40mail.gmail.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
No comments:
Post a Comment