Mimi ninaongea kwa ujumla sio Lowasa tu na wengineo ila wewe unadhani nampinga mheshimiwa. Ninasema-akili tunazo, macho tunayo, kuna kila kitu tanzania lakini tupo hapa tulipo kutokana na hulka zetu. Kubadili hulka sio rahisi rahisi ni kubadili tabia sisi ni hulka!! Mbona hatujaona mabadiliko majimboni kwenu wagombea-mfano Monduli utokako wewe Team yake mheshimiwa.
Nenda popote TZ -kuna utata mkubwa katika maendeleo yetu binafsi kwani matendo yetu wananchi na viongozi wetu na watumishi ugani ni tata na sehemu kubwa -mbweteko. Na niliweka mfano wa ofisi ya kijiji sio mbali na DSM ni jirani tu kuna Mto Ruvu, kuna msitu wa hifadhi wanaweza kuomba magogo ya mbao wilayani; niliweka magogo yaliyokatwa hapo msituni jirani ni msitu wa kijiji but potected. Ofisi imezungukwa na chaka la miti na kuna udongo wa bure na si mbali sana kuna mto na maji ya bure. Ofisi matundu makubwa kuta za udongo zimebomoka, ipo wazi, faili za kijiji na nyingine za kesi za watu zinakaa majumbani kwa viongozi. Nilisema-Diwani kapelekwa na wachina huko China kuona maendeleo yeye na timu ingine ya bongo kwa kuwa kuna shamba kubwa wachina wanataka kuliomba serikalini limerudishwa kwa Rais. Part of benefit sharing ni kujipendekeza kwanza kwa wananchi waikubali kampuni gani inapokwenda kuomba ridhaa yao hapo na kukubaliana mafao. wamepanda ndege
kwenda China! wameona mataa, wamerudi-wanajaa vitambi tu. Kwanza watumishi ugani wote hawakai katani kwao wanakaa mijini na hawaendi huko. Ukitaka kwenda nao kikazi uwape usafiri, nauli na posho ya kutwa. Ni Kaya yao na eneo lao la kazi, ila uwalipe na umewasaidia kufika kazini na kufanyanao kazi kutwa (Fukuza kazi hawa). Kila mtumishi wa serikali akae eneo lake la kazi na utendaji wake upimwe na sasa waajiriwe kwa mkataba akipofanyakazi za matokeo-tchao asepeshwe. Hebu angalia hiyo picha vyandarua 2 kimoja ndani ya banda na kingine nje wamefunikia kuku. Kiongozi wa nyumba kumi, kitongoji na kijiji yupo na watumishi ugani hupita hapo na tulipita nao wakaona. Tatizo.
Nimeongea sana kuwepo vyuo mbali mbali nchini ambavyo sio mfano. Unafika chuo cha mainjiania ujenzi-rooms za maabara yao zimeanguka ceiling boards na ngazi za kufika madarasani zimebomoka concrete imekatika nao ni maijinia ujenzi-mazoezi hufanyia wapi? Hatujiulizi. Unafika chuo cha wasomi wa mazingira-chupa zimezagaa kila kona na wao hukatiza hovyo na kuharibu bustani za chuo, vyoo vinafurika lakini wanazomea mambo ya waste water management, sewerage disposal and treatment, pollution, water and env management. Nguo za akina dada zipo dampo nyuma ya bweni kunguru wanaruka nazo, mbwa wanasambaza! Bongoland hiyo. Medical school-kunguru anaruka hovyo na maplasenta na makadava yapo dampo!
Ninaongea kuhusu kuwepo vyuo mbali mbali mapaka VETA, vya Maendeleo Jamii, Kilimo na Ufugaji lakini viongozi hawavitumii wakaomba na kusaidia vijiji vyao tata vikawa pilot study and demo areas. Hapo Monduli kuna Ranchi ya mifugo jirani tu, Ipo USA River; kuna boreholes toka mkoloni zipo zinaweza zikafanyiwa rehabilitation wakanywa maji safi na wakahamasishwa kufuga kisasa sio kuhamahama na kuharibu mazingira na uchumi wa wengine na wa nchi. wanakunywa maji machafu yenye uchafu wa kila aina nao matajiri? Mbuzi au kondoo 5 sawa na ng'ombe mmoja. Tajiri achangie ng'ombe masikini mbuzi-wanaweza kujipatia maendeleo. usione Mmasai kavaa lubega-yupo humo mwenye degree-twende makwetu tukahamasishe mabadiliko iwe Masaini au Ukwereni, Umakondeni na Uzaramoni. Kote kuna kila kitu lakini sisi sikio la kufa. ukipata hela ni anasa, kuoa, kuzaa sana, wake wengi na michepuko ndio sifa. Kwa nini tuwe na mapigano kila siku, kuuana na kutiana vilema kama viongozi
wachaguliwa wangefanya kazi na kutekeleza majukumu yao? Ninakuuliza-wasukuma wanalisha mchele nchi nzima mpaka 25% ya uliwao Kenya. Lini aliwakaribisha mifugo yake ile angalau robo eka eti ana birthday yake?
Lini Mmaasai anayelima Naitolia, Kitwai A, Loliondo-Engerosambu akawaweka ndama na mama ng'ombe anayenyonyesha shamba la mahindi na la maharage meusi (ngwara) eti wale ekari moja ili apate maziwa mengi? lakini atatoka mfugaji Monduli, Manyara au toka Mwanza hadi Tunduru, Mbeya, Rufiji akalishie mifugo yake elfu 5 ekari 10 usiku mmoja na mchana aipitishe mashambani akihapa na apige wakulina (na siku hizi ukiwa mwanamke unabakwa). hii ni makusudi (calculated) na viongozi wa watotkako wanawaangalia na waendako wanakula rushwa. Irrigation systems donor funded zimekufa au kuharibiwa vibaya na wafugaji (Malolo-fika kupitia Ruaha Mbuyuni na Ruvu Bagamoyo). Mifugo imezagaa. utajiri wa mifugo au wa mpunga, nazi, mikorosho lakini tunaishi katima umasikini. Makogo ya mikoko yanakatwa na kupelekwa uarabuni (Rufiji), Mikorosho na minazi kibao lakini mzawa huyo afanyae hivyo anaishi katika kijumba cha udongo na fito unamchungulia. Ardhi nzuri sana Mkuranga, misitu
natural kibao, mikorosho na minazi na mabwawa ya maji-lakini nyumba unamchungulia ipo wazi. Chandarua alichopewa kupunguza malaria amefunikia kuku wasiliwe na mwewe. Extension staff yupo anapita hapo au tena ni jirani tu na zahanati na ofisi ya kijiji tunawaachia (Tunaogopana au ni vipofu!). Kwanza mmiliki wa bara wanywayo pombe watu kijijini hapo ni VEO na mchezo wa pool ni wa Diwani watoto na vijana hucheza pool kuanzia saa 2 asubuhi hakuna kwenda shule au shamba.
Hali kama ya Monduli na utajiri-haiwezekani kukaa kutegemea WFP kulisha watoto wetu shule eneo ambalo toka ukoloni ilikuwa bread basket ya ngano, shayiri etc mazao ya baridi na ukame. Matajiri tunawatumiaje kuushika uchumi na wapo mpaka wa kimasai? Wapo wenye hotels, majumba ya fahari, magari na mamia ya mifugo-utata ni wealth ranking kwa Social Class kuwa ni mifugo sio cash money, mijengo ya kisasa na elimu. Au kuwa wake wangapi unao na watoto sio maendeleo yanayoonekana. kisha sifa yetu ni kusema ili tuendelee lazima mashamba yaondoke miji midogo (kibaha) na katika cities (Dar, Mwanza, Mbeya etc). Hivyo sasa unajenga Kibaha city, Handeni City, Mkuranga city (mashambani) na kuongeza kigamboni City (kuondoa viazi na mihogo iliyokuwa ikilimwa), Kawe, Bunju city (Cities without farms bali lami na terazo sakafuni. Hii itaongeza changudoa watoto na vishoga). Nenda machimbo ya madini-ni uharibifu wa mazingira kwa wachimbaji wadogo wadogo, uchafuzi, umalaya,
ulevi-kisha kulalama tunaonewa.
Fika visiwani kwenye historia-majengo yanaporomoka lakini wasanii mihela wapo, matajiri mihela wapo hawavinunui wakawekeza wakakwamua vijana. Mibaba vifua miraba minne ipo barabarani inatembeza chupi za mitumba. Matajiri wenye mihela huchukua maeneo ya viwanda na kujenga hall za arusi na sherehe sio kufufua viwanda na mashamba ya kulisha viwanda na mikopo walipewa. Tuna macho, tuna mihela lakini tunajimaliza wenyewe kisha kulalama. Wafugaji wahamaji wanalalama kuonewa lakini ni uhurugani uzurure nchi nzima na maelfu ya mifugo kilomeka mamia na maelfu ukipita ukilishia mashamba na kuharibu mazingira na kupiga/kuua wasio hatia? Pia mkulima-umebweteka hulimi kiendelevu na hata kuuza mazao mabichi upate pesa ya p[ombe. Wakipewa mafunzo na kuanzishiwa vikundi wapate mikopo-vikundi hufa kwa kugombea madaraka, ufisadi, kuchukua mikopo na kutoroka bila kulipa kuziacha familia zao na kuua umoja kwa mzunguko wa hela kutofanikiwa. Wakipewa mifugo ya kisasa kopa
ng'ombe/mbuzi lipa mnyama huyo-wanaibiana mifugo. Wakipanda miwa as outgrowers, au kupanda miti ya miwati na ya kahawa-huchomeana misitu kukomoana. Tija inabaki kuingiza wahamiaji haramu, rushwa kutoka wanasiasa, majungu, maandamano! Tumeoza, tubadilike na kila kiongozi mchaguliwa katika Kata na majimbo awe mfano eneo lake au jimboni kwake. Tumechoka kudanganywa kuwa -fulani ndio jibu la mabadiliko ikiwa sisi wenyewe tupo kama TUFE hatukubali na hatupo tayari kubadilika.
Kichekesho cha waTZ ni kuwa-Hata mpira tunataka kocha ndio afanye mazoezi sio sisi wachezaji kujituma. Simchukii Lowasa ila ninaona kuna mushikeri wanatudanganya, hatuoni ukweli kwa wanayoyaongea viongozi. Mifano mizuri majimboni kwao ipo kwa wachache na sio baadhi ya hao ambao wanaona wao ndio jibu. Mbona makwao jibu hilo halipo na kuna kila kitu? Kaeni Jangwani kwenu Monduli msizagae kuja kwetu kilosa. Tuliuawa 90% na mjerumani sasa tutakufa kwa kukataa kuonewa na wamasai wajao kututesa kipindi hiki cha uhuru. Ndio maana tupo kupambana na kupigana kufa na tusiposaidiwa-tutatangaza mkoa wa Morogoro kuwa Nchi ndani ya TZ iwe na liwe (Swela) na kuhakikisha-tunawaondoa wafugaji wote hao ndugu zako. Mliwekwa ndani ya wildlife conservation area mlisema hamlimi, lakini mnakaribisha wageni, mnazidisha mifugo inayofanya degradation kisha mnadai maeneo zaidi. Punguzeni mifugo. Ng'ombe mmoja anatakiwa ale square acre 5 huko semi arid area za Arusha, Ngorongoro,
Manyara etc. Ardhi haiongezeki. Tubadilike. Mwekezaji akitunza eneo lake vizuri-mnavamia eti mnaonewa mnakatazwa msilishie-mpanga ktk lodge ni kufuga? Hata wanyama pori hupunguzwa (live harvesting) na kuacha sustainable levels. Ninyi hampunguzi mifugo na kufuga kisasa why-Lowasa ndio jibu la sisi kuendelea kuzagaa!! Mbona hamjabadilika miaka yote hiyo nayo yupo ni milionea? Tutaamini vipi kushuka mabadiliko kama ninyi huyu huyko atokako bado mpo ktk senchari ya 9?
Bye for good!! Nisamehe bure, ila Usinichokoze tena nisije nikaamua kutangaza nia na agenda ikawa -kila mtu akae kwao/kwake na ajihusishe na uchumi sustainably mwisho wa kuzurura hovyo na kuhamia kusiko kwenu ni sasa unless umenunua ardhi na una hati miliki!! Kufuga ng'ombe ni kulingana na size ya ardhi ya binafsi au ya jumla. Ukizidisha-zinataifishwa na kuuzwa unafunguliwa bank account hela zinawekwa baada ya kutozwa kodi ya uharibifu mazingira. Kuoza mtoto wa kike mahari mwisho millioni 4 au ng'ombe 4 na umri wa kuoza au kuoa.kuolewa ni miaka 18+ na kuoa mwisho wake 4 kwa kibali cha maandishi ya wake waliotangulia. Hii itasaidia watu kujali maendeleo kuliko ubinafsi wa kulimbikiza mifugo tu au wake na watoto makumi na malaki ya vijukuu na vitukuu kumaliza ardhi na kuleta migongano.
--------------------------------------------
On Wed, 24/6/15, 'Lesian Mollel' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Subject: Re: [wanabidii] LOWASA KIZAAZA,(BODA BODA WAPINGA JARIBIO LA KUTAKA KUDHULUMIWA UJIRA WAO)
To: "'Hildegarda Kiwasila' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Wednesday, 24 June, 2015, 1:42
Mimi sion issue hapa kiwasila at all
hii pekee haitosh kumdisqualify lowasa,monduli iko mbali
kimaendeleo lakin hakuwez kuchange koote....
Ukiwa unaenda kibaha tu hap mbele kiluvya utaona nyumba
kibao za tope does it mean mnyika hfai' kawasila hakimungu
juz nilikua natembelea walum kuwapa loan zetu,nafanya kaz
taasis moja ya kibenki ya serikali nilipofika shule moja
ndugumbi nikakuta darasa la tano nje wamekaa chini wote na
mwalim kaakaa kat kati anasimamia halafu mtihank,shuke ya
magomeni kat kati ya mjin,dada usijifanye mzungu bana
watanzania kibao maisha bado.....nilikua kijijin kwa pinda
na pengo madarasa kibao wako chini,hakuna road,hakuna
maji,hakuna hata umeme au hata mirad kama hy ya wfp,usiseme
as if mimi ni wa mjini nakuambia hv bora jangwa la monduli
kuliko maeno yenye kila aina ya resources lakin hakuna kitu
lakin nyie mnamshambulia edwad tu kila kukicha,why not
pinda,why not wasira or even membe jamaniii....
Mondule wamejitahid
By the way utafiti sjui report skuisoma sana coz sion dat
bring data here kupima maendeleo kimajimbo kwa kila mtangza
nia ndipo tujudge watu si mkurupuke tu na data fake hpa
thats just a small biased report to show negative side
of lowasaa,mmmmmh mtahukumiwa
Acha dada as researcher argue with analytical data,do
comprison,do not bias pleease
Mollel
Team lowasa,who never go back easily with poor logics
Lesian
'Hildegarda Kiwasila' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
wrote:
>Salum, Zawadi hi hapa ya Lesian Mollel Mmaasai Team
Lowasa imeambatishwa. Tunachosema tu ni kwamba: Vijiji na
majimbo yetu yana matatizo mengi ambayo yanatatulika kwa
sisi kujituma kuwahamasisha ndugu zetu. Wabunge wengi
wamegombania katika maeneo ya makabila au chimbuko lao.
Kijijini kwako kukoje kama kwingine mbali. Ni cha mfano?
Hawana matatizo ya majengo ya shule, vyoo , nyumba duni,
uharibifu mazingira, kuchomeana mashamba kwa wivu eti
utavuna sana miwa au miti ya mbao. Kunywa maji machafu na
uharibifu mazingira ya mito, maziwa, bwawa. Kuchangia
maendeleo budi zamani tukisomeshwa bure na hela za nchi za
kikomunisti au za marafiki zetu wakishindana. Sasa ni wao
hawataki wanataka tujigharimie kwa gkodi zetu hakuna dezo
tena. Kama umeshindwa kuonyesha mfano jimboni-utaonyeshaje
kitaifa? kama umeshindwa kama Diwani-utawezaje ukiwa mbunge?
Tujisahihishe tusiahidi Mana ya Jangwani waliyopewa
waisraeli. Hebu angalia hapa Kango zawadi ya Mollel.
> Tunayoyaongea ni haya sio kumchukia mtu-hapana.
Tunataka tuchague kwa vidhibiti vya utendaji tuone angalau
mifano ya jimboni kwako. Kama ni gesi, madini-mbona tanzania
yapo mengi? Mafia tulikuta visima vya mafuta ya petroli
minara yake ya toka 1956 na hayajachimwa na alituletea grid
reference msichana wa kizungu toka UK ambaye baba yake
alikuwa administrator huko. Tukatumia GPS tukafika. tuna
mengi sana nchi hii-ubinafsi tu na uvivu, uongo, visasi,
kutokujituma na kutokuona mbali, kutaka rahisi rahisi;
ubishi na ushindani usiotija, kubweteka-hata football
tunashindwa-kisa KOCHA. Kocha ndio acheze afunge magoli,
akukimbize ufanye mazoezi usijali sana michepuko na pombe!
Fukuzeni hata kocha kumi inakula kwetu tu kufungwa
daima-hatujitumi!! Na hivyo-hata tubadili Rais mia-kama
hatujitumi na kukubali ukweli, kuwa wabunifu, waaminifu ktk
kutumikia jamii; kupenda kuendeleza makwetu sio kuiba na
kuleta vya wenzetu tutumie makwetu-tutarudi nyuma daima.
>
>Inaumiza kuona-tuna kila kitu lakini tupo hapa tulipo
tunategemea ajaye atuletee! Nao baadhi wanatoa ahadi ya
kutuletea sio kutuburuza, kukamata kufunga na kurejesha hela
za mikopo waliopewa kufufua viwanda na mashamba wakajenga
nyumba wanazopangisha kwa midola. Kuhakikisha kila mwananchi
anashughuli ya kufanya, kijijini ana nyumba na choo bora na
anajituma. Mijini tuondoe hawa vijana na mijibaba kibao
barabarani inatembeza vitu na bidhaa kutandaza njiani. Wenye
hela wafungue mashamba, kujengwe nyumba na processing
industries wawe huko sio barabarani mbona maduka ya vifaa
hivyo yapo? Tunahitaji Rais zaidi ya Dictator wa nchi
jirani.
>
> On Mon, 22/6/15, 'salumkango' via
> Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
> wrote:
>
> Subject: Re:
> [wanabidii] LOWASA KIZAAZA,(BODA BODA WAPINGA JARIBIO
LA
> KUTAKA KUDHULUMIWA UJIRA WAO)
> To:
> "'Hildegarda Kiwasila' via Wanabidii"
> <wanabidii@googlegroups.com>
> Date: Monday, 22 June, 2015, 12:51
>
> Dada Hildegard huwa unaongea
> ukweli mpaka watu
> wengine wanachukia. Lkn
> pia ni mmoja kati ya wanawake jasiri
>
> mnaoweza kutetea hoja zenu kwa vielelezo sahihi
visivyo
> shaka ndani yake.
>
> Mungu akubariki sana
>
>
>
> Sent from
> my Samsung Galaxy smartphone.
>
>
> -------- Original message
> --------
> From: 'Hildegarda
> Kiwasila' via Wanabidii
> <wanabidii@googlegroups.com>
>
> Date:22/06/2015 11:15 AM (GMT+03:00)
>
> To: wanabidii@googlegroups.com
>
> Cc:
> Subject: Re:
> [wanabidii] LOWASA KIZAAZA,(BODA BODA WAPINGA
> JARIBIO LA KUTAKA KUDHULUMIWA UJIRA WAO)
>
>
>
>
>
> --
>
> Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>
>
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
>
>
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
> Utapata Email ya
> kudhibitisha ukishatuma
>
>
>
> Disclaimer:
>
>
> Everyone posting to this Forum bears the sole
> responsibility
> for any legal consequences
> of his or her postings, and hence
>
> statements and facts must be presented responsibly.
Your
> continued membership signifies that you agree
> to this
> disclaimer and pledge to abide by
> our Rules and Guidelines.
>
>
> ---
>
> You received this
> message because you are subscribed to the
>
> Google Groups "Wanabidii" group.
>
>
> To unsubscribe from this group and stop
> receiving emails
> from it, send an email to
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
>
> For more options, visit
> https://groups.google.com/d/optout.
>
>
> --
> Send
> Emails to wanabidii@googlegroups.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
>
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
> Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to
> this Forum bears the sole responsibility for any legal
> consequences of his or her postings, and hence
statements
> and facts must be presented responsibly. Your
continued
> membership signifies that you agree to this disclaimer
and
> pledge to abide by our Rules and Guidelines.
> ---
> You received this message
> because you are subscribed to the Google Groups
> "Wanabidii" group.
> To unsubscribe
> from this group and stop receiving emails from it, send
an
> email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
> For more options, visit
> https://groups.google.com/d/optout.
>
>--
>Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>
>Kujiondoa Tuma Email kwenda
>wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
>Disclaimer:
>Everyone posting to this Forum bears the sole
responsibility for any legal consequences of his or her
postings, and hence statements and facts must be presented
responsibly. Your continued membership signifies that you
agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules
and Guidelines.
>---
>You received this message because you are subscribed to
the Google Groups "Wanabidii" group.
>To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
>For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
No comments:
Post a Comment