alienda mto kagera kujenga daraja, anasema amin aliondoka mwenyewe hapa kuna mapungufu ya habari, anasema wakati majeshi yanavuka mpaka alienda makao makuu dar kuweka mambo sawa napo kuna taarifa hazijakaa sawa, mwandishi awahoji na wengine kama balozi mahiga na gen gemoghe.
2016-05-20 21:55 GMT+03:00 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
He he he he! Aya ya ya ya
--------------------------------------------
On Fri, 5/20/16, 'mpombe mtalika' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Subject: [wanabidii] Jenerali Kiwelu: Nilimnyima Sokoine siri za kijeshi vit
To: "ELISA MUHINGO' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Friday, May 20, 2016, 8:28 PM
Asema katika Vita ya Kegara udhibiti wa mawasiliano na
taarifa ulikuwa wa kiwango cha juu.
Raia
Mwema: Hali ilikuwaje kule eneo la mapambano wakati wa vita
ya Kagera?
Jenerali
Kikwelu: Kazi ilikuwa ngumu sana. Maana vijana wangu
waliokuwa
kule mbele, wale askari wa JWTZ walikuwa katika nusu
morali, maana
ukishatoka kwenye mstari wa mbele ukarudi nyuma morali ya
vita
inapungua. Kwa
hiyo kazi ya kwanza ilikuwa kuwajenga
kisaikolojia.
Kazi ya pili ilikuwa ni kupata reinforcement
(kuongeza
nguvu) kazi ambayo niliyomwachia Ernest Mwita Kiaro, hata
CDF naye
alikuja akakaa mahala fulani pale Bukoba (jirani), kwa hiyo
Dar es
Salaam tulimpa kazi Mwakalindile ndiye aliyekuwa anakaimu
kama Chief of
Staff, halafu Kiaro, chifu wa mgambo kazi yake ilikuwa
kukusanya mgambo
wote nchini, akina Mwakalindile ni kukusanya JKT, Polisi na
Magareza,
wote walikuja kule.
Ninaposema
kulikuwa na changamoto kubwa sana
ni kwamba hawa askari hata siku moja hawakuwahi kuwa eneo la
vita ama
eneo la mafunzo ya kivita kwa pamoja. Kwa hiyo, ilikuwa kazi
kubwa,
ndiyo maana ikatuchukua muda pale kabla hatujaruka daraja,
ilikuwa ni
lazima nifanye mafunzo ya pamoja ili kuwaweka watu (askari
kutoka
Magereza, Polisi, Mgambo na JKT) waweze kufanya kazi
pamoja.
Lengo
ilikuwa kuondoa fikra za kitabaka vitani, kuachana na mambo
ya
huyu mgambo au JKT. Kwa hiyo nilianzisha range ya kupiga
silaha, mtu
unampa risasi kumi anapiga zote wash out (anakosa kulenga
shabaha),
maana sisi (jeshini) tuna kitu kinaitwa bull, inner, outer
n.k… sasa
huyu unampa risasi zote anapiga wash out, tunampa nyingine,
akipiga ile
target namwambia umepiga bega (target hasa ni kifuani kwenye
moyo au
kichwani) sasa wakati mwingine ukimpa risasi tano… mbili
anapiga ndani,
nikasema sasa wameiva.
Kwa
hiyo ilikuwa ni mafunzo ya msingi. Kwa mfano, ukiwa porini
na ndege ya adui inakuja ufanye nini.
Unaulizwa ukiona ndege ya adui inatoka kule wewe unakwenda
wapi? Namna
gani mnaweza kusonga mbele, mnajihami vipi na namna gani
mnaweza
kupumzika kwa sababu askari hawezi kupumzika chini ya kivuli
cha mti.
Sasa baada ya mafunzo hayo ya pamoja, tukaridhika askari
wetu wameiva,
tukaanza kusonga mbele kutoka Katoro hadi tukafika karibu na
mpakani,
tukaweka kambi ambayo mpaka leo ipo pale, nyuma ya
Mtukula.
Raia
Mwema: Labda ungeeleza kuhusu Daraja la Kagera kushambuliwa
na adui?
Jenerali
Kiwelu: Daraja hili wakati nimefika tu, kutoka kupewa ile
amri
(ya kwenda vitani)… nimefika Kaboya, siku hiyo hiyo jioni
nikatoka
kwenda kutazama daraja. Nikafika darajani upande wa kulia
kama unakwenda
Mtukula umbali wa kilomita moja, nikaliona daraja ambalo
baada ya
dakika 15 nikiwa pale likalipuka, kwa hiyo sikuweza kuwahi
kuweka askari
pale darajani.
Wakati nafika pale na mtu mmoja anaitwa Kanali
Kitete tunatazama…nataka sasa kufanya mbinu namna gani
nitavuka daraja
ili majeshi yangu yakae upande mwingine.
Basi
nikarudi zangu
Kaboya kwa ajili ya kuanza kufanya mkakati mwingine maana
pale daraja
limekwishavunjwa, nikaripoti daraja limevunjwa…hakuna
daraja kuanzia
sasa. Ndipo tukaanza mipango mingine kuhusu daraja, tukaleta
madaraja ya
muda na mtu mmoja anaitwa Brigedia Rajabu ndiye aliyekuja
na vifaa
hivyo kutoka kikosi chetu cha uhandishi na tukamweka sehemu
ya umbali wa
kama kilomita tano kutoka kwenye daraja, ndipo alipofanya
mafunzo yake
ili baadaye kufunga daraja la muda.
Raia
Mwema: Ilichukua muda gani hadi kufanikisha daraja hilo la
muda?
Jenerali
Kiwelu: Unajua kuna wanazungumza kwa ushabiki mambo ya vita
tu
wakati hawajui chochote kuhusu vita, watu hawa mimi nawaita
majitu,
hawajui maana ya vita. Wapo wengine wanafikiri jeshi hii la
Tanzania
lilikuwa tayari kwamba unakwenda tu kwenye vita, sasa
ukiwaambia kwamba
jeshi hili tulipokwenda kwenye vita tulikuwa na mchanganiyo
wa watu wote
hawa, halafu pia kuleta vifaa vya kuvuka daraja,
kuwafundisha namna ya
kuweka daraja, kuleta vifaru, ndipo wataona ugumu wa kazi
iliyokuwapo.
Pale
ni lazima uwe na nguvu ya kutosha kuhakikisha kwamba mkiruka
(daraja) hakuna kurudishwa nyuma. Kama nilivyotangulia
kusema wale
askari wetu waliokuwa kule awali, walikuwa wachache na
walivurumishwa na
adui kiasi cha morali yao kuwa chini kivita, kwa hiyo
ilikuwa ni lazima
nihakikishe sasa watu wangu ni imara, vifaa viko.
Tulikuwa
tunafanya mipango na ukaguzi pamoja na makamanda wangu,
akina Jenerali
Marwa, Jenerali Luhanga, Mayunga, Walden… tunakwenda hadi
tunafika pale
kwenye daraja kwa sababu Idi Amin alirudisha majeshi yake
(Uganda)
akiamini kazi imekwisha. Sasa tulikuwa na makamanda wangu
hao tunakwenda
pale kupanga mikakati, lakini, swali kwamba wapi tupite
(kuvuka daraja)
na lini sikuwaambia.
Hakuna
mtu aliyejua hata Edward Sokoine
(aliyekuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya Mwalimu Nyerere)
alikuja
akaniuliza …. sasa General nafikiri tumechelewa sana
kuruka (daraja),
sasa unaruka lini na unapitia wapi?
Nikamwambia
hiyo ni siri ya
kijeshi… akasema hata mimi? Nikamwambia ndiyo mzee. Kwa
hiyo mimi
nilikuwa napita kando ya ule mto kwa gari hadi Murongo,
halafu watu
wanapiga mabomu kila sehemu lakini hawajui tunaruka wapi
kupitia wapi..
.tuliweka watu (askari) hadi eneo la Kakunyu huku Bukoba
Vijijini, kwa
hiyo kuna ambao walijua tunaruka kupitia huko. Hatimaye
nikaona sehemu
ya kuruka ni pale pale walipovunja (daraja), lakini
sikuwaambia
wapiganaji wetu.
Sasa
imefika siku ya kuruka, ndani ya saa 24.
Nikawaita makamanda wangu nikawaambia sasa inabidi turuke
kwenda
kumshambulia adui, vifaa na kila kitu tayari, na askari kama
tulivyofanya mafunzo wako tayari. Makamanda wakasema
tunangoja tu amri
yako, nikasema amri itatoka, wakauliza na kutaka niwaambie
tunaruka
kupitia eneo gapi, nikasema nitawaambia.
Ilipofika
saa tano usiku
nikawaambia makamanda… Marwa utakuwa katikati, Mayunga
ukiruka tu
unakwenda kushoto kuelekea eneo la Mbarara, Walden ukiruka
tu unaelekea
eneo la Minziro, Luhanga ukiruka tu unafuata njia ya Marwa
halafu
makamanda wengine watakuwa tayari kusubiri lolote (reserve).
Baada ya
maelekezo hayo nikawataka waende kuwaambia askari wao kwamba
tunaruka
leo (usiku huo), nikamwita Mhandisi Mkuu Rajabu na kumwambia
utatandaza
daraja lako (juu ya mto) saa nane usiku…akafanya kazi
hiyo.
Saa
nane usiku mpaka kufika saa tisa kuelekea saa 10 (takriban
saa mbili
hivi mfululizo) vikosi vikaanza kuruka kwa mujibu wa amri ya
operesheni
(operation order) ilivyotamkwa. Ilikuwa bahati mbaya
nilipoteza askari
mmoja tu pale wakati wa kuvuka daraja.
Baada
ya hapo tulifanya
mashambulizi, kazi ya kwanza ilikuwa ni kukamata eneo.
Nimeeleza kazi
niliyopewa nilitakiwa kurudisha heshima ya nchi hii na
heshima ya nchi
ni kurudisha mipaka yetu pale ilipokuwa awali na hivyo
tukahakikisha
tumefika Mtukula, wengine wamefika Minziro na wengine
mpakani na Uganda
kule.
Sasa jukumu la msingi la kurejesha mipaka ya
nchi likawa
limekamilika na Rais Julius Nyerere akaja kule na akasimama
eneo lenye
kilima pale na tukamweleza kwamba sasa mzee kazi ya kwanza
uliyotutuma
tumeimaliza, mipaka yetu sasa iko salama, akasema vizuri
lakini huyu
"mshenzi" huyu ametuharibia mambo mengi sana si bado
yuko kule (nchini
mwake), basi kazi bado haijakwisha.
Ndipo tukaingia hatua ya
pili, maana sehemu ya kwanza ya ukombozi wa nchi yetu ikawa
imekwisha
ikafuata hatua hiyo ya pili ambayo ni kumwadhibu
adui. Raia
Mwema: Je, baada ya kazi hiyo ya kwanza kukamilika
ulirejeshwa kwenye nafasi ya Mnadhimu Mkuu (Chief of
Staff)?
Jenerali
Kiwelu: Pale kilichofanyika ni kwamba baada ya kumaliza ile
kazi ya awali, tukaingia sasa kazi ya kuandaa na kutekeleza
operesheni
ya kuvuka mpaka ambayo ni tofauti na opereshani ya kumwondoa
adui
nyumbani kwako.
Sasa
unakwenda nyumbani kwake lazima uwe na
mkakati, sambamba na nguvu ya kutosha kwenda kwake, kwa hiyo
rais
ikabidi afanye utaratibu wa kumtafuta kamanda wa kuingia
Uganda, mimi si
ndiye niliyekuwa Chief of Staff na mkuu wa majeshi akiwa
Twalipo ambaye
naye hayuko makao makuu, kwa maana hiyo akiwa huku mbele
(vitani) kule
makao makuu hakuna maandalizi yoyote, nani anaanda nini…
nani anafanya
nini.
Kwa
hiyo ilibidi nirudi Makao Makuu ya Jeshi Dar es Salaam
na pale (vitani kuelekea ndani ya Uganda) nikamkabidhi
Msuguri, mimi
nakamwambia nakwenda (makao makuu) kukufanyia kazi ya
kuandaa vifaa,
wewe kazi yako ni kwenda ndani kumwadhibu Idi Amin. Nikarudi
makao makuu
nilikuwa na mtu mmoja alikuwa Naibu Waziri wa Ulinzi,
Kanali Bakari,
basi tukafanya kazi na Bakari, tunkaenda hadi nchi za nje
kutafuta
nguvu…. zana za kivita.
Wako
marafiki walitusaidia, sina sababu ya
kuwataja sana lakini kati ya nchi rafiki tulizokwenda ni
pamoja na
Urusi, China, Korea na Bulgaria. Ikabidi tukusanye vifaa na
ndipo hapo
wananchi walichangia mambo mengi sana, wapo waliojitolea
magari yao,
vyakula, mifugo kama ng'ombe ili kuwawezesha wapiganaji
wetu kule mstari
na hatimaye Msuguri akuvuka mpaka akiwa na uhakika wa nguvu
za kutosha
na uangalizi huku nyuma anakotoka.
Raia
Mwema: Kwa wakati huo wewe
ndiye uliyekuwa makao makuu Dar, sasa uliwezaje kudhibiti
link
(viunganishi vya taarifa) za silaha mlizopata kutoka nje ya
nchi?
Jenerali
Kiwelu: Kwanza wakati nikiwa pale Kagera tulikuwa
tumedhibiti
sana uvujaji wa taarifa. Unajua kuna mkutano mmoja mkubwa wa
kimataifa
ulikuwa unaendelea pale Arusha uliokuwa umehusisha nchi
nyingi huku vita
pia ikiendelea na hao washiriki wa mkutano hawakujua
chochote
kilichokuwa kikiendelea nilidhibiti uvujaji wa taarifa,
viongozi wengine
tuliwapa amri maalumu hakuna kufika kwenye eneo la vita na
wala kupewa
taarifa yoyote, ni kama tulivyokuwa tunapambana kuwasaidia
kule Msumbiji
siku moja tukakuta mzee mmoja wa kizungu kule Tunduru anayo
redio
ameijichimbia ndani, kumbe alikuwa anawasiliana kwa maana ya
kupeleka
taarifa, tukamkamata.
Hata pale Karagwe, tulikuwa na watu fulani
pale ambao ni kanisa fulani sitaki kuwataja nao pia walikuwa
na redio ya
mawasiliano, ukiona utafikiri mtu anapiga kinanda kumbe
anapeleka
taarifa, kwa hiyo tukafunga njia zote za mawasiliano,
nikasema hakuna
mawasiliano ya aina yoyote na taarifa zozote kwenda Ikulu
nitapeleka,
tulihakikisha taarifa hazivuji vinginevyo tusingeweza kuvuka
pale.
Raia Mwema: Vipi kuhusu Yoweri Museven (Rais wa
sasa wa Uganda), alikuwa sehemu ya mapambano?
Jenerali
Kiwelu: Museven yeye alitokea huku nyuma kapitia Karagwe
kalala kijijini pale wakati Mayunga amekwishavuka mpaka,
akaungana na
Mayunga, ukweli ni kwamba Jeshi la Tanzania na chini ya
Luteni Jenerali
Mayunga ndiye aliyekabidhiwa kazi ya kupita Mbarara na
kutoka hapo
kuelekea Kampala, na wengine wakapita Minziro kwenda
kuungana kule.
Museven hakuwa na jukumu la kuongoza ni kama alisaidia mambo
kadhaa
yakiwamo masuala ya taarifa.
Raia
Mwema: Vipi kuhusu uteuzi wako kuwa mkuu wa mkoa?
Jenerali Kiwelu: Baada ya vita, tukawapokea
vijana kutoka Uganda pale
Bunazi, nikafanya kazi ya kuwasambaza na kuwarudisha kule
walikotoka,
wengine Ruvuma, Kigoma na maeneo mengine ya nchi.
Tukahakikisha wamerudi
na kupewa haki zao.
Baada ya kumaliza pale Bunazi, nikarudi Dar
es Salaam kwenye kitengo changu cha Mnadhimu Mkuu, sasa
makamanda wote
wakawa wamerejea kutoka vitani. Ikabidi sasa jeshi lipangwe
upya….unajua
watu walikwishaonja kutoa roho za watu huwezi kucheza nao
hivi hivi,
ikabidi sasa tupangane upya.
Namna
gani jeshi litakavyoendeshwa
na kwa hiyo, Amiri Jeshi Mkuu akapanga upya…akasema sasa
wewe bwana
umemaliza kazi hii nakushukuru…sasa nataka kukupa kazi
nyingine…nikamwambia sawa, nipo tayari kwa kazi yoyote,
akaniambia
utakwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, nikamwambia naenda
lakini hii kazi
sijawahi kufanya sasa ukiona nafanya vibaya uniite, na mimi
nikiona
kuna tatizo nitakuja.
Kwa hiyo nikaenda zangu Tanga ndipo wakati huo
yakafanyika mabadiliko, Twalipo akatoka pale akawa Waziri wa
Ulinzi,
Msuguri akawa Mkuu wa Majeshi halafu na Jenerali Kombe akawa
Mnadhimu
Mkuu, tukaendelea.
Raia
Mwema: Nini hasa unachojivunia katika wadhifa wako wa Mkuu
wa Mkoa wa Tanga?
Jenerali Kiwelu: Tanga kuna mambo mengi. Lakini
moja kubwa ni kwamba
pale Tanga wale Waswahili wangu wa Tanga ni wavivu, hawakuwa
watu wa
maendeleo. Sasa walikuwa wanakaa pale kwenye nyumba zao za
nyasi mjini,
nikawaambia sikilizeni hatuwezi kuishi hivi…mtu lazima
afanye kazi na
mjiwekee kipato na mtengeneze nyumba.
Wakauliza tunatengenezaje
na hatuna mashamba kwa ajili ya kutupatia kipato? Nikafanya
uamuzi,
nikaenda barabara ya kuelekea Muheza kuna mashamba ya mkonge
pale na
hapakuwa na mtu anayelima, nikasema nitachukua haya mashamba
na wala
sikuuliza ni ya nani.
Nikawaambia
nyie mtakwenda kulima pale na
kutakuwa na mabasi asubuhi na jioni ya kwenda na kurudi
shambani, na
kwamba wakishavuna watapata chakula lakini nikataka
watengeneze nyumba
zao na watoto wasome kwa kipato watakachopata.
Nikamwambia ofisa
husika apime viwanja, lakini nikawaambia nyumba zao
wasizivunje
isipokuwa wajenge kuta kwa kuzizunguka na baada ya kufika
hatua ya
kupaua, wanaweza kuvunja nyumba za ndani yake za nyasi,
ndivyo nyumba
nyingi za Tanga zilivyojengwa kwa wakati huo.
Nilikaa
pale kwa
miaka nadhani mitatu tangu mwaka 1980 kisha nikahamishiwa
Rukwa ambako
nako pia kuna mambo mengi niliyofanya. Uzuri wa Rukwa watu
wa kule ni
wachapa kazi lakini tatizo lao walikuwa wanachapa kazi bila
utaratibu.
Nikawaambia msilime tu mahindi ya kutosha nyumba yako tu
bali limeni kwa
malengo ya kupata kipato. Nikawataka walime kwa utaratibu,
wajue
masuala ya mbegu, maandalizi ya shamba.
Lakini
haikuwa kazi
rahisi kwa sababu ilibidi tutengeneze kitu kama shule
kijijini kwa ajili
ya kumfundisha mtu kulima, kuandaa shamba, kupanda,
kupalilia hadi
kuvuna, ni miezi minne…watano amevuna ameweka kwenye
kihenge, anakuwa
amefaulu. Sasa mtu anapokuwa anajifunza kulima alikuwa
akijifunza kilimo
cha kisasa, kupanda kwa mistari, kutumia mbolea, kutumia
dawa za
kudhibiti wadudu na baada ya kuvuna, ajue namna ya kutunza
mazao.
Sasa
katika kuandaa mashamba wengine walikuwa wanatumia majembe
madogo
ya kukokotwa kwa ng'ombe na wengine majembe ya mkono,
uongozi ngazi ya
mkoa ilibidi tufanye utaratibu na tulifanikwa kwenda kununua
majembe
kutoka Zimbabwe ya kukokota kwa ng'ombe na ya kupandia.
Niliomba fedha
nikapewa za mbegu ambazo kule hakuna, nikaagiza mbegu kutoka
Kenya
lakini hazikuwa zinatosha, nikaenda kwenye wizara (ya
kilimo) natafuta
mbegu nako hakuna.
Lakini
nikaona sio siku zote kwenda kutafuta
mbegu, nikaanzisha shamba la mbegu eneo la Mlundikwa, mwaka
wa pili
tukawa sasa tunaweza kupata mbegu zetu na tukajua namna ya
kuziweka
katika madaraja ya ubora.
Sasa
baada ya kuwa na uhakika wa mbegu
tukaingia hatua ya matumizi ya majembe ya ng'ombe,
tulipomaliza mwaka wa
kwanza na wa pili, ule mwaka wa tatu tukafaulu na kupata
mazao mengi,
maana nia yangu pale ilikuwa ni kupata mavuno mengi ili
kushindana na
wenzangu wa mikoa mingine ya kilimo, na ikibidi hata
kuwazidi lakini kwa
manufaa ya watu wangu hasa katika kuongeza kipato chao mara
dufu au
zaidi.
Raia Mwema: Kwa hiyo kuwapo kwako Rukwa
kulisababisha mkoa
huo kuwa miongoni mwa mikoa mingine mikubwa ya kilimo kama
Mbeya,
Ruvuma na Iringa?
Jenerali Kiwelu: Kwanza mimi nikiwa kule
nilijua Mbeya ambako nilikuwa napita pale, Iringa na Ruvuma
ndio
iliyokuwa mikoa mitatu mikubwa na mashuhuri kwa kilimo,
ikiitwa "The Big
Three". Nikasema hawa hawawezi kuwa Big Three na mimi
napita mikoa yao,
changamoto yangu ya kwanza nikasema lazima niingie pale
kwenye orodha
ya Big Three ili tuwe Big Four.
Raia
Mwema: Baadaye ulipelekwa kuwa Mkuu wa Mkoa Kagera, hali
ilikuwaje kule?
Jenerali
Kiwelu: Unajua ule Mkoa wa Kagera unafafana hali ya hewa na
mikoa kama Mbeya, Kilimanjaro na Arusha, mimi sehemu ya
asili ni
Kilimanjaro ambako mazao ni pamoja na kahawa na migomba kule
nako mazao
ni hayo hayo, tofauti iliyokuwapo ni kwamba kule Kilimanjaro
tulikuwa
tunalima kahawa aina ya Arabika sasa Kagera ilikuwa nafasi
yangu ya
kujifunza kilimo cha kahawa aina ya Robusta, ikawa lazima
niwainue wale
wakulima tuone tunafanya vizuri zaidi. Sasa kule kwa sababu
wengi ni
wabishi kweli kweli wanataka lazima waone vitendo kwa mfano,
ikabidi
niwe na shamba la mfano na hata sasa baada ya kustaafu bado
naendelea na
kilimo kwenye shamba langu.
Chanzo Raia Mwema.
Maoni Yangu
Tumeeona
jinsi Generala Kiwelu alimvyomnyima Sokoine taarifa za vita
kwa kumwambia ni siri ya kijeshi na Sokoine pamoja na
wadhifa aliokuwa
nao aliheshimu hilo hakutaka zaidi ya jibu
alilojibiwa.
Hivyo
basi wanasiasa wetu wa kizazi hiki waige mfano wa Sokoine
kwa kuheshimu
vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kutotaka kila kitu
kuwa wazi
ikiwemo eti kwa kuwa wao ni wabunge au wanasiasa wapo kwa
niaba ya
wananchi hapo watakuwa hawavitendei haki vyombo vyetu hivyo
kwani
vinafanya kazi kubwa ya kuhakikisha tuna kuwa na amani
pamoja na
uturuvu.
Hata huko Marekani na ulaya huwezi kukuta
wanasiasa
wanataka mambo ya jeshi na vyombo vingine vya ulinzi na
usalama kuwekwa
hadharani kama wa hapa kwetu wanavyotaka ili wapate umaarufu
wa kisiasa.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
No comments:
Post a Comment