Mkurugenzi wa Fadhila FM Redio, Br. Edwin Mpokasye akiwakaribisha washiriki katika ufunguzi wa warsha ya Maadili na kuandika Habari za Jinsia na Migogoro kwa waandishi wa habari wa Redio za Jamii iliyofanyika Masasi mkoani Mtwara.
Mkurugenzi wa Fadhila FM Redio, Br. Edwin Mpokasye akikabidhi risala aliyoitoa kwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi Farida Mgomi wakati wa hafla fupi ya ufunguzi wa warsha hiyo.
Mshauri na Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO Bi. Rose Haji Mwalimu akitoa ufafanuzi kuhusu madhumuni ya warsha hiyo inayoendeshwa chini mradi wa Democratic Empowerment Project (DEP) unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na kutekelezwa na UNESCO. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Bi. Farida Mgomi.
Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Bi. Farida Mgomi, akitoa hotuba ya ufunguzi wa warsha ya Maadili na kuandika Habari za Jinsia na Migogoro kwa waandishi wa habari wa Redio za Jamii iliyofanyika Masasi mkoani Mtwara.
Mshiriki wa warsha Hassan Hassan kutoka Kituo cha Redio Micheweni FM, Pemba, akiwasilisha kazi ya kikundi kazi.
Pichani juu na chini ni washirki kutoka Redio Jamii za Micheweni, Mtegani, Zenji, Pangani na Fadhila waliohudhuria warsha ya siku 10 iliyofanyika kwenye kituo cha Redio Fadhila FM Masasi.
Mshauri na Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO, Bi. Rose Haji Mwalimu akiendesha mafunzo ya Jinsia kwa washiriki wa warsha ya Kuandika Habari za Migogoro Kimaadili kwa waandishi wa habari wa Redio za Jamii iliyofanyika Masasi mkoani Mtwara.
Mshiriki kutoka Pangani FM Redio, Abdilhali Shukuran (kushoto-mwenye shati nyeupe), akichangia mada ya Jinsia na Uchaguzi wakati Mkufunzi wa mafunzo hayo Bi. Rose Haji Mwalimu akimsikiliza kwa makini.
Picha ya pamoja ya washiriki wa warsha pamoja na mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Bi Farida Mgomi (wa pili kulia).
Zainul A. Mzige,
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
No comments:
Post a Comment