Monday, 12 May 2014

Re: [wanabidii] UKAWA wanapigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar?

By implication UKAWA inapigania uhuru wa Zanzibar na Tanganyika ambayo ndiyo maoni ya watanzania yaliyofanyiwa utafiti. Wanapinga udhalimu unaoletwa na wapinga demokrasia wanaotaka kuendelea kuitafuna nchi kwa kisingizio cha serikali 2


2014-05-12 7:11 GMT+03:00 'Fred Hans Kipamila' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Prof. Shivji ana ajenja ya siri au ametumwa na watu fulani aongee kwa maslahi yao. Rasmu ya sasa ilivyo ndiyo msimamo wa Shivji ulivyo. Ukisoma maabdiko mengi ya Prof. Shivji huko nyuma anaushangaa muundo wa muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar (kwa mfano, The Legal Foundation of the Union). Watu hawa wanabadili ajenda iliko mezani ya kujadili rasmu ya katiba wanatangaza utengano. Hii ni mbinu mpya ya kubadili maada ili wananchi wawaone wenzao wanataka kuvunja muungano.
Nimeshangazwa na kauli za katibu wa CCM kule Zanzibar, anasema maalimu Sefu ajiuzuru nyadhifa zake kama hataki muundo wa serikali mbili! Ni jambo la kushangaza kusikia maneno haya toka kwa kiongozi mkuu wa chama tawala, anamwambia Sefu amwandike barua rais wa Zanzibar kuomba kujiuzuru. Sefu kawekwa na katiba ya Zanzibar na si kwa huruma ya CCM wala Shein. Anachotakiwa kufanya Kinana kama kweli anao ubavu ni kuwaambia Wazanzibar katiba yenu haifai tuichane maana inawaweka madarakani wapinzani wa CCM.
Huyu mtu hana jipya na ziara zake ni za kupoteza muda tu kama si kwa ajili ya posho. Ndiyo maana alipowaita mawaziri walioteuliwa na Mwenyekiti wake ni mizigo, Mwenyekiti hakumjali wala kumjibu alimpuuza tu. Kama yeye aliamini katika alichokisema ziarani ambacho mwenyekiti wake alikipuuza alistahili kujiuzuru, lakini hawezi kwa vile anazihitaji posho zaidi kuliko kukijenga chama.
Maalimu Sefu yupo pale kwa mujibu wa katiba ambayo imeiondoa Zanzibar chini ya mamlaka ya Muungano, huwezi kumwambia Sefu jiuzuru bila kwanza kuifuta katiba yenyewe. Hakuna mwenye ubavu wa kumwondoa Maalimu madarakani pasi kuivunja katiba ya Zanzibar kwanza. Tujadili hoja iliyoletwa mezani ambayo ni rasmu ya katiba tusibadili hoja kwa manufaa ya matumbo yetu. Wala hakuna sababu ya kuzungumzia juu ya katiba ya Zanzibar, tuliwaona wakiitengeneza kwa umakini na kwa mshikamano wa ahli ya juu, wakajiwekea wigo wa kutulizwa na mtu juu ya mambo yao tukanyamaza. Hata alipotokea mwendawazimu kutuonyesha njia kwamba wamejiondoa kimya kimya tukasema mwendawazimu huyo tusimsikilize. Leo kinana anataka kujitia madaraka juu ya mambo ya Zanzibar amechelewa.
--------------------------------------------
On Sun, 5/11/14, 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: Re: [wanabidii] UKAWA wanapigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar?
 To: hamisznz@gmail.com, wanabidii@googlegroups.com
 Date: Sunday, May 11, 2014, 12:07 PM

 Mimi sioni kama ukawa wanapigania
 uzanzibari na utanganyika ila wanataka bunge la katiba
 lijadili rasimu iliyoletwa kwao na tume. Hisia ya
 utanganyika hazikuletwa na tume bali tume ilizikuta kwetu.
 Zimekolezwa na katiba ya sasa ya zanzibar ambayo kimsingi
 ilivunja muungano kwa kukinzana na katiba ya muungano. Hii
 ndiyo inafanya watu makini kumshangaa shivji. Inakuwaje
 asielewe tume. Marekebisho ktk mapendekezo ya tume nje ya
 mfumo wa shirikisho ni kuibembeleza zanziba ikubali kurudi
 kwenye serikali isiyo kama ya sasa ila kama ya 1964 na ya
 Tanganyika iwe vile. Hii itaimarisha muungano. Kinyume chake
 serikali 2 ni sawa kuufutilia mbali muungano.

 ----------
 Sent from my Nokia Phone

 ------Original message------
 From: Abdalah Hamis <hamisznz@gmail.com>
 To: <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Saturday, May 10, 2014 4:46:47 PM GMT-0700
 Subject: [wanabidii] UKAWA wanapigania uhuru wa Tanganyika
 na Zanzibar?



 KATIKA mada aliyoitoa Machi 31, mwaka huu wa 2014 kwa vijana
 wa vyuo vikuu
 jijini Dar es Salaam, pamoja na mambo mengine, Profesa Issa
 Shivji
 alionyesha wasiwasi kuwa mapendekezo ya Tume ya Mabadiliko
 ya Katiba kuhusu
 muundo wa Muungano wa Serikali tatu yangeibua hisia za
 utaifa wa Tanganyika
 na Zanzibar.

 Maoni haya ya Profesa Shivji yalipingwa na Tume yenyewe
 pamoja na watu
 kadhaa, tena kwa maneno makali yaliyomshambulia Profesa
 Shivji binafsi na
 kuachana na hoja zake. Wakosoaji wa Profesa Shivji walienda
 mbali zaidi na
 hata kumtuhumu kwamba amenunuliwa na Chama cha Mapinduzi
 (CCM).

 Utamaduni wa kutuhumu watu kununuliwa umeanza kuota mizizi
 na kugeuka kuwa
 ugonjwa wa kitaifa katika nchi hii. Kwamba kila mtu asiye
 mwanachama wa CCM
 anapaswa kutoa maoni yasiyofanana na msimamo wa CCM. Ole
 wako utoe maoni
 yako ambayo kwa bahati nzuri au mbaya yakaendana na maoni na
 msimamo wa CCM
 basi unaingizwa kwenye orodha ya watu walionunuliwa na chama
 hiki. Huu ni
 udhaifu mkubwa sana katika ujenzi wa hoja. Hata hivyo, hii
 si hoja yangu
 kwa leo.

 Hoja yangu ya leo ni kwamba kile kilichoonekana kwamba ni
 hofu ya Profesa
 Shivji sio hofu tena bali ni jambo halisi na la kweli
 kabisa. Tayari hisia
 za utaifa wa Tanganyika na Zanzibar zimekwishaanza
 kujitokeza waziwazi.
 Sasa watu wanavaa fulana za Tanganyika na katika mitandao ya
 kijamii watu
 wanajivunia utanganyika na sio utanzania tena.

 Pengine hizi mbwembwe za kuvaa fulana na kujipaka rangi za
 bendera ya
 Tanganyika hazitishi sana kama maneno niliyoyasikia Zanzibar
 katika
 mikutano ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA). Kwa kiasi
 kikubwa, na kwa
 tafsiri yangu, viongozi wa UKAWA huko Zanzibar walijikuta
 wakipigania uhuru
 wa Zanzibar na Tanganyika badala ya kupigania Serikali
 tatu.

 Sijui viongozi hawa kama walikusudia kufanya jambo hili au
 walijikuta
 wakilifanya tu kutokana na mazingira na mihemko ya kisiasa
 iliyokuwepo pale
 Zanzibar. Ili kuweka vizuri hoja yangu, naomba niwanukuu
 viongozi wawili wa
 juu wa UKAWA.

 Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA na UKAWA katika mkutano
 wa Aprili 30,
 2014, pamoja na mambo mengine, alinukuliwa na gazeti la moja
 la kila siku
 la Mei mosi, 2014 akiwaeleza wananchi wa Zanzibar kuwa:
 "Ni jambo la hatari
 katika mchakato wa Katiba ya wananchi kuwa na woga au
 hofu…Lazima tuwe
 tayari kuwaonyesha watawala kuwa tuna umoja imara,
 tunapigania mataifa huru
 ya Tanganyika na Zanzibar".

 Katika mkutano huo huo, Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA na
 mjumbe muhimu wa
 UKAWA, Tundu Lissu, alinukuliwa na gazeti jingine la kila
 siku la Mei mosi,
 2014 akiwaambia wananchi kuwa: "Kwa sababu Zanzibar
 haijawa huru na
 Tanganyika haijawa huru na ukitaka kujua ukweli wa hili
 angalia vitabu,
 kuna jina Tanganyika limefutwa ili kuitawala Zanzibar, sasa
 inabidi tuseme
 ili kuleta uhuru wetu". Lissu aliendelea kusema;
 "Zanzibar inatakiwa kuwa
 mamlaka kamili".

 Baada ya kutafakari maneno haya na muktadha mzima wa
 mikutano ya UKAWA huko
 Zanzibar nimejiuliza swali moja muhimu: Je, UKAWA
 wanapigania uwepo wa
 Muungano wa Serikali tatu au uhuru wa Tanganyika na
 Zanzibar?

 Pamoja na kuunga mkono umoja wa vyama vya upinzani kwa
 ujumla wake hasa
 katika muktadha wa kuimarisha upinzani nchini, jambo ambalo
 tumeliombea
 miaka mingi, nalazimika kuhoji dhamira ya UKAWA katika
 mazingira ya Katiba
 mpya. Ukichunguza kwa makini maneno ya Mbowe na Lissu
 unaanza kupata jibu
 kwa nini CHADEMA na CUF waliokuwa maadui wa kisiasa hadi
 juzi kiasi cha
 kushindwa kusimamisha mgombea mmoja wa ubunge huko Chalinze
 dhidi ya
 mgombea wa CCM, ghafla wamegeuka marafiki wa kisiasa bila
 hata makubaliano
 rasmi yenye ajenda ya wazi.

 Kimsingi CHADEMA sasa wanapigia debe sera ya CUF, ya
 Zanzibar huru yenye
 mamlaka kamili pengine bila wao kujua. Inajulikana enzi na
 enzi kwamba CUF
 hawataki Muungano uliopo; wanataka tu ushirikiano wa
 kijirani wa kawaida
 kama ulivyo katika nchi zingine za Afrika kama vile Jumuiya
 ya Afrika
 Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo kwa Nchi za Kusini mwa
 Afrika (SADC)
 au ile Jumuiya ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS). Lakini
 zote hizi ni
 ushirikiano tu na wala sio Muungano. Ndio maana CUF wanataka
 Zanzibar iwe
 na mamlaka kamili kuhusu mambo yote nyeti, ikwemo uraia,
 uhamiaji, fedha,
 bandari, mambo ya nje na kiti Umoja wa Mataifa na wanajua
 fika kwamba
 ukishayatoa mambo haya katika Muungano huna haja ya kuwa na
 Muungano tulio
 nao.

 Kwa hiyo wenye akili tunajua kwamba CUF hawataki Muungano
 kwa sababu huwezi
 ukataka Muungano na hapo hapo ukataka mamlaka kamili. Hakuna
 Muungano wa
 namna hiyo duniani bali ni ushirikiano wa kijirani.

 Sasa kama hivyo ndivyo, je CHADEMA nao sasa hawataki
 Muungano? Na je, huu
 Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ni umoja wa watu
 wasiotaka Muungano?
 Kama hivyo ndivyo, kwa nini wasiweke wazi matakwa yao ili
 waweze kujulikana
 hivyo na wapate wafuasi kwa sababu hizo? Vinginevyo,
 viongozi wa UKAWA wana
 wajibu wa kutuelimisha wanamaanisha nini wanaposema
 wanapigania uhuru wa
 Tanganyika na Zanzibar? Uhuru huu wanaupigania kutoka koloni
 gani?

 UKAWA wanasema kwamba wanapigania Rasimu ya Tume ya
 Mabadiliko ya Katiba.
 Lakini Rasimu ya Tume hiyo inapendekeza Muungano imara na
 kwa maoni ya tume
 pengine imara zaidi kuliko hata huu uliopo. Rasimu
 haiongelei uhuru wa
 Zanzibar au Tanganyika na wala haiongelei habari za mamlaka
 kamili ya
 Zanzibar kama walivyohubiri wao huko Zanzibar. Hivyo basi
 UKAWA hawawezi
 kutafuta uhalali wa ajenda yao kwa kujificha katika rasimu
 ya tume kwa kuwa
 wanajua rasimu hii inaungwa mkono na walio wengi.

 Kwa hiyo wasiwasi wangu ni kwamba, kupitia ndimi zao huko
 Zanzibar, ni wazi
 kwamba UKAWA wanataka uhuru wa Tanganyika na Zanzibar. Kwa
 maneno mengine
 hawataki Muungano au wanataka Muungano lege lege utakaojifia
 wenyewe mbele
 ya safari.

 Wosia wangu ni kwamba UKAWA wanawajibika kuweka msimamo wao
 wazi na kututoa
 wasiwasi baadhi yetu tunaopenda Muungano imara bila kujali
 aina ya muundo
 na ambao tunaanza kutishwa na kauli zao.
 - See more at:
 http://www.raiamwema.co.tz/ukawa-wanapigania-uhuru-wa-tanganyika-na-zanzibar#sthash.W1y6hDst.dpuf

 --
 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

 Kujiondoa Tuma Email kwenda
 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
 Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

 Disclaimer:
 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 ---
 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.
 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

 --
 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

 Kujiondoa Tuma Email kwenda
 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
 Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

 Disclaimer:
 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 ---
 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.
 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment