Hayawi hayawi mwishowe yanukia,
Wanasema akufukuzaye hakuambii toka, hii ni tabia ya viumbe waitwao binadamu, yalianza huko nyuma ya kutaka kujivua gamba, mara ikaonekana ikiwa kweli watavuana magamba wataumizana, na pengine ambaya angedhlika zaidi ni mwanzisha mada. Hrakati za kutafuta kuungwa mikono pande zote za nchi zikafanyika, na mwishowe kwa taratibu walizojiwekee CCM zikafuata, kunafununu ini bidi kutumia njia tata, kwenye hesabu inaitwa prove by induction, au tumia ushawishi kuonyesha kwamba 2+3=6. Muda wa kukusanya karatasi za wathaniwa ukawadia, zikasahihishwa na wakapatina watano ambao kwa namna nyingine kwa mfumo wa kishule utasema walio wakali darasani. Hapo ndipo kiswahi huwa kinachanganya kidogo, watu hao wanaoitwa wakali utashaangaa waweza kuwakuta hata hawapendi kuongea sana darasani na wala si wachokozi, sasa ukali wao sijui unatoka wapi? Bila shaka ilitafusliwa moja kwa moja toka kwenye neno "sharp" maana yake ncha kali, basi kama ni hivyo kweli wenye ncha kali wakateuliwa kuingia dulu ya pili na hapo mwenye ncha kali zaidi ya hao tano akapatikana.
Hata hivyo kati ya walioachwa kuna wengi njia zilizotumika kuchagua wenye ncha kali zaidi zilikiukwa, lakini sisi hayo hayatuhusu sana, wao wanataratibu zao zilifuatwa hazikufuatwa hilo siyo letu, wameleta mtu mmoja wa kuwawakilisha, sasa bado upande mwingine wenye nguvu karibu sawa na waliokwisha kuchagua jembe lenye ncha kali nao wateue jembe ikiwezekana lenyemakali sawa au ikiwezekana lenye makali zaidi. Kisha wabwage shambani tuone nani atakuwa akilima madongo mbakubwa makubwa na mwisho wa siku nani atakuwa amelima eneo kubwa kuliko mwingine.
Na mwishowe tutalinganisha kwa mavuno waliyofikisha nyumbani, maana mtu unaweza ukaivisha mazo vizuru ukaja ukashindwa kuyavuna.
0 comments:
Post a Comment