Tuesday, 2 June 2015

Re: [wanabidii] Yaliyojiri Ukumbi wa Hyatt Regency: Frederick Sumaye atangaza nia kugombea Urais

Mi naona hata hilo la walimu ameshindwa kujibu alichofanya ni kukimbia swali na hata hilo la rushwa pia kalikwepa kwani hata waziri mkuu ni mkubwa

On Jun 2, 2015 9:12 PM, "'ELISA MUHINGO' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Swali la Katiba lilimshinda kujibu au hakulielewa? Kalikwepa?
--------------------------------------------
On Tue, 6/2/15, 'mpombe mtalika' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] Yaliyojiri Ukumbi wa Hyatt Regency: Frederick Sumaye atangaza nia kugombea Urais
 To: "ELISA MUHINGO' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Tuesday, June 2, 2015, 5:46 PM





 Waziri mkuu mstaafu muda huu
 anatangaza nia akiwa katika
 ukumbi wa Hyatt Regency Dar es salaam, huku akiwa na kauli
 mbiu 'UONGOZI BORA,
 KOMESHA RUSHWA, JENGA UCHUMI'. Anasema huwezi kukemea
 rushwa na halafu na wewe
 upo ndani ya rushwa.

 Anaongelea mafanikio katika
 katika kipindi yuko madarakani
 ikiwemo televisheni ya taifa, uboreshaji elimu ya msingi.
 Anasema leo badala ya
 sekondari nayo kupanda ndio hio imeshuka.



 Anaongelea sera ya ubinafsishaji, anasema sera hio ilikuwepo
 kabla ya uongozi
 wa Mkapa. Hivyo wao walikuwa watekelezaji na hawawezi
 kulaumiwa. Ubinafsishaji
 kama sera ni kitu muhimu na ni vizuri ilifanyika. Mashirika
 zaidi ya asilimia
 45 yamenunuliwa na watanzania, mengine kwa ubia na wageni na
 asilimia ishirini
 pekee yalinunuliwa na wageni kwa asilimia 100.



 Nimekumbana na mambo magumu katika miaka hio kumi ikiwemo
 ajali ya MV Bukoba na
 ajali ya treni, ukame wa mwaka 1997. Niliunda kamati ya
 kushughulikia jambo
 hilo na kuchimba visima zaidi ya 300 Dar es Salaam. Mambo
 magumu yalinikomaza
 katika uongozi. Mvua za El nino zilifata baada ya ukame,
 ilikuwa hali ya hatari
 lakini tulijikwamua na tuliendelea na kazi wa kujenga taifa
 letu. Kifo cha baba
 wa taifa, mimi sikulala siku tatu nzima hata kwa nusu saa,
 sijawahi kuona
 kipindi cha amani kama kili, polisi waliripoti hata uhalifu
 haukuwepo.



 Wakati waziri mkuu, sikuweza kusikia watu wanapigana,
 asubuhi nisiwepo pale,
 leo wakulima na wafugaji wanapigana miezi sita sasa. Mfano
 mgogoro wa waancholi
 na wahadzabe.



 Huwezi kuzungumzia amani wakati watu wana njaa, tatizo la
 uchumi, watu
 wanaangalia takwimu badala ya uhalisia. Tunatakiwa
 tuendeleze kilimo, hata
 wakati wa Nyerere tulileta matrekta lakini tuliendelea?
 Kuleta matrekta ni
 jambo jema sasa nitalima heka 50, lakini uwezo wa mbegu heka
 3 na kupalilia
 heka 3.



 Eneo lingine muhimu ni masoko, lazima kiendelezwe katika
 ukubwa wake. Wakulima
 watauza kwa bei ya hasara na bei ikiwa vizuri hawana tena
 mazao. Leo viwanda
 vya sukari, hatuwezi kuingiza sukari kutoka nje bila kodi,
 lazima tulinde
 viwanda vyetu vya ndani. Mazao yetu yote, kama tutakua na
 juhudi za kusindika
 mazao, hili tatizo la ajira ambalo tunapiga nalo kelele
 sana, litapungua. Pia
 pengo kati ya walionacho na wasio nacho litapungua.



 Nimeona shule binafsi wanafanya vizuri, wanataka wazipunguze
 nguvu, ongeza
 juhudi nawe umfikie. Katika miaka miwili au mitatu
 tutapunguza kwa kiasi
 kikubwa wanaoenda nje.



 Rushwa na ufisadi, hili jambo sina utani nalo. Ukituhumiwa
 kwa rushwa ndani ya
 wiki moja unachunguzwa na wiki mbili mahakama imekuhukumu na
 kama ni viboko
 unapokea kabisa.



 Nawashukuru ndugu zangu waandishi wa habari, nimezungumzia
 Dar es Salaam na
 naamini mtafikisha nchi nzima ili tumpokee rais Kikwete
 kijiti ambae amefanya
 vizuri. Kama kuna maswali pia niko tayari.



 Matangazo haya yalikuwa yanarushwa na ITV, Star TV, Mlimani
 TV, Radio free
 Africa, radio one ila bahati mbaya sehemu kubwa ya nchi
 umeme hamna ikiwemo
 mikoa mitano

 =========

 MASWALI

 Tanzania Daima: Katika
 awamu hio ufisadi mwingi ulitokea, uuzwaji NBC,
 EPA, Radar Kiwira Kama mshauri mkuu wa rais na mtendaji



 Mwananchi: Umenukuliwa
 mara kwa mara kuwa ikitokea ameteuliwa mla rushwa
 kupitia CCM wewe utajitoa



 Mariam Mziwanda, gazeti la
 Uhuru: Kabla hujaachia uongozi wa uwaziri
 mkuu ulitajwa kama kiongozi unaemiliki mali nyingi, kupitia
 fursa hii



 MAJIBU



 Swali la Kwanza

 Kwanza kama waziri mkuu naweza kumshauri wa rais, Ameziita
 kashfa lakini mimi
 siziiti kashfa. Kama NBC ni ubinafsishaji wa kawaida. Sijui
 watu wanatoa wapi
 taarifa kuwa walikuwa wanapata faida, regulator wa benki
 zote ni BOT hivyo ndio
 ana taarifa sahihi. Hakuna kwamba tuliuziana benki hotelini
 Hizo zingine zote
 zinafanana, Radar na ndege ya rais, unatakiwa utofautishe
 maamuzi ya serikali
 na kama kuna ufisadi, nchi ilikuwa haina radar. Katika
 ununuzi ule kama kuna
 mtu alifanya foul anatakiwa akamatwe, ilimradi imethibitika
 mtu alifanya ovyo
 ni jukumu la serikali kumkamata sio Sumaye,



 Swali la michezo ni muhimu ni ukosefu wa muda ndio maana
 sikuigusa ila katika
 kitabu changu cha sasa mtaiona.



 Mimi na wala rushwa ni maji na mafuta, nitatoka ndio lakini
 naamini chama
 changu hakiwezi kuchagua mla rushwa. Sitegemei kutoka kwa
 sababu hawatachagua
 mla rushwa.



 Sasa Mariam, muda unatoa jawabu, mimi leo watanzania
 wananijua, watoto wangu
 mnawajua wanafanya kazi za kawaida za serikali. Mtikila
 ambae alinituhumu mambo
 mengi sana, baadae akasema watu wasafi nchi hii ni Sumaye,
 Warioba na
 Mwakyembe. Hela nyingine ambayo nilipata nilisomesha
 waandishi wa habari nyie
 mnajua. Mimi nina moral authority kwa muda mrefu.



 Kuhusu nani tishio katika mbio za urais, hakuna hata
 mmoja.



 MASWALI

 Pendo: Katiba mpya
 kuna mkwamo, ukipata ridhaa unawaahidi nini wananchi
 ambao maoni yao yametupwa



 Mtanzania: Uumekua
 unaongelea umiliki wa ardhi bila faida, wewe
 unatuhumiwa kumiliki maeneo makubwa na mengine
 hayajaendelezwa



 Radio Iman:
 Umezungumzia vipaumbele vingi, walimu wana kilio cha muda
 mrefu tangu wewe ukiwa madarakani kuhusu stahiki zao



 Kubenea: Nyumba za
 serikali ziliuzwa wakati uko madarakani, tamko lako!



 Mimi sidhani tatizo ni katiba, tatizo ni usimamizi wa
 sheria, kwa mfano
 kiongozi mla rushwa, katiba haikupi fursa ya kumuhukumu?
 Tatizo sio katiba,
 hatuhitaji li-document likubwa kama tuliloliandika.



 Swala la ardhi, wapo
 watanzania wengi tu wana ardhi kubwa kuliko mimi,
 haya mambo yanakuzwa tu, nimeshindwa kuendeleza baadhi ya
 maeneo kwa sababu
 sijapewa hati bado. Hela ya kujenga kibanda Dar unaweza
 kununua ardhi kubwa
 sana mikoani.



 Swala la kuboresha walimu, tulifanya hayo na msiwe na
 wasiwasi nalo kwa upande
 wa mafao.



 Nyumba za serikali ni uamuzi wa serikali, sababu yake kubwa
 ilikuwa ni nini,
 kwa sababu ungozi wa Mkapa ulikuwa ni uwazi na ukweli.
 Kamati ilisema nyumba za
 serikali ni nyingi mno hivyo pesa nyingi zinaingia
 kuzikarabati. Tulikua kwenye
 ubinafsishaji, mashirika yalikuwa na nyumba nyingi, nyumba
 nyingi tuliamua
 kuziondoa. The highest bid secured, tulijaribu kutetea hata
 ma-general managers
 lakini ilishindikana.



 Rushwa ni rushwa, mtu hata uwe mkubwa namna gani, yani mnipe
 Urais nimshindwe,
 hakuna mkubwa kuliko Rais, wote nitawashughulikia.

 ndugu
 nawasilisha tuwachambue hawa watangaza nia mmoja baada ya
 mwingine tuwajue na udhaifu wao







 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

No comments:

Post a Comment