Thursday, 6 February 2014

Re: [wanabidii] Maria: Mume wangu aliongopa mahakamani ndoa yetu ikavunja

Mi nasubiri Wanasheria walitolee ufafanuzi jambo hili.

On 6 Feb 2014 07:35, "lucas haule" <kisacha2003@yahoo.com> wrote:
Kama katika nchi hii, kuna wanataaluma watakuwa chachu cha mauaji na ukatili, ni mahakimu. Wanapokea rushwa na kutoa hukumu za kipumbavu kabisa.
Nadhani, tunaweza kuwawezesha Tamwa na wao wakamweka mwanasheria ili kumsaidia mama na watoto.
TAMWA TUWEKEENI NO YA KUCHANGIA.
--------------------------------------------
On Wed, 2/5/14, mngonge <mngonge@gmail.com> wrote:

 Subject: Re: [wanabidii] Maria: Mume wangu aliongopa mahakamani ndoa yetu ikavunja
 To: wanabidii@googlegroups.com
 Date: Wednesday, February 5, 2014, 10:40 PM

 Kitendo cha huyo bwana kuwa
 na mke mwingine ndani ya ndoa nafikiri ni sababu tosha
 kuvunja ndoa ila kinacholeta utata ni mlalamikiwa kujifanya
 mlalamikaji na kufungua kesi ambayo imehukumiwa haraka sana
 kitu kinachoashiria kaharufu ka vijihongo . Ndoa kama hii
 haina sababu ya kuendelea kuwepo ila cha msingi haki
 itendeke katika kugawana mali walizochuma katika kipindi
 chao cha ndoa kikiwemo kiinua mgongo kwa upande wa mwanamke.
 Ebu wanasheria tusaidie inakuwaje mahakama itoe uamuzi wa
 kugawana watoto? Wana maana ya nani amuhudumie mtoto gani au
 ina maana watoto hawa ni wa huyu na wengine ni wa yule.
 Tangu lini mtoto akawa na mama bila baba au kuwa na baba
 bila mama? Sheria kama hii ipo ni vyema ikaangaliawa upya,
 maana inaingilia haki za watoto



 2014-02-06 Joachim
 Mushi <mushijoa@gmail.com>:

 Maria: Mume wangu aliongopa mahakamani ndoa
 yetu ikavunja 
 [caption id="attachment_42717"
 align="aligncenter" width="640"]<a
 href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2014/02/Maria-Tarafa-wa-kwanza-kushoto-akiwa-na-watoto-wake-wanne-aliozaa-na-Ndebile-Kazuri-akiwa-amekaa-kwenye-kifusi-cha-sehemu-ya-nyumba-anayokaa-mumewe-ameibomoa-nyumba-hiyo-ili-kumfukuza-eneo-hilo..jpg"><img
 src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2014/02/Maria-Tarafa-wa-kwanza-kushoto-akiwa-na-watoto-wake-wanne-aliozaa-na-Ndebile-Kazuri-akiwa-amekaa-kwenye-kifusi-cha-sehemu-ya-nyumba-anayokaa-mumewe-ameibomoa-nyumba-hiyo-ili-kumfukuza-eneo-hilo..jpg"
 alt="Maria Tarafa (wa kwanza kushoto) akiwa na watoto
 wake wanne aliozaa na Ndebile Kazuri akiwa amekaa kwenye
 kifusi cha sehemu ya nyumba anayokaa, mumewe ameibomoa
 nyumba hiyo ili kumfukuza eneo hilo."
 width="640" height="424"
 class="size-full wp-image-42717" /></a>
 Maria Tarafa (wa kwanza kushoto) akiwa na watoto wake wanne
 aliozaa na Ndebile Kazuri akiwa amekaa kwenye kifusi cha
 sehemu ya nyumba anayokaa, mumewe ameibomoa nyumba hiyo ili
 kumfukuza eneo hilo.[/caption]

 [caption id="attachment_42718"
 align="aligncenter" width="584"]<a
 href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2014/02/Bw.-Ndebile-Kazuri.jpg"><img
 src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2014/02/Bw.-Ndebile-Kazuri.jpg"
 alt="Bw. Ndebile Kazuri anayedaiwa na aliyekuwa mkewe
 kuiongopea mahakama." width="584"
 height="480" class="size-full
 wp-image-42718" /></a> Bw. Ndebile Kazuri
 anayedaiwa na aliyekuwa mkewe kuiongopea
 mahakama.[/caption]

 <strong>Nkasi,
 Rukwa</strong><strong>NOVEMBA</strong>
 18, 2013 Mahakama ya mwanzo, Namanyere, Wilaya ya Nkasi
 iliamua kuvunja ndoa ya Ndebile Kazuri na Bi. Maria Tarafa
 wote wakazi wa Kijiji cha Isale Mji mdogo wa Namanyere
 wilayani Nkasi Mkoa wa Rukwa. Ndoa hiyo ambayo hadi mahakama
 inaivunja ilikuwa na watoto wanne, yaani watoto wawili
 wakiwa na miaka 9 na 7 huku wengine wawili wakiwa na miaka 3
 na mwingine mwaka mmoja.

 Mume ndiye aliyeenda mahakamani kufungua kesi akiomba
 kutengana na mkewe akidai anatabia mbaya hivyo hawezi
 kuendelea kuishi naye. Kazuri anaomba mahakama itengue ndoa
 hiyo akiwa tayari na mke mwingine ambaye anaishi naye
 tofauti na Bi. Tarafa.

 Bi. Tarafa anasema shauri hilo lilifunguliwa Oktoba 22,
 2013 na Novemba 18 mahakama baada ya kuridhika na sababu
 zilizotolewa na mlalamikaji na bila kumpa nafasi ya
 kujieleza mlalamikiwa iliamua kuvunja ndoa hiyo. Bi. Tarafa
 katika mahojiano na mwandishi wa makala haya alipotembelea
 Wilaya ya Nkasi kwa msaada wa Chama cha Wanahabari Wanawake
 (TAMWA); anasema sababu zilizotolewa na mumewe mahakamani
 kuomba ndoa ivunjwe si za kweli japokuwa mahakama iliridhika
 na kuamua kuvunja ndoa yao na kuwagawa watoto.

 Anasema chanzo cha mumewe kuamua kuvunja ndoa hiyo ni
 pamoja na yeyé kudai mahitaji yake na familia yao kwa
 mumewe ambaye kipindi hicho alikuwa tayari amemtelekeza bila
 huduma hizo huku akiishi na mwanamke mwingine aliyezaa naye
 pia.

 "…Hadi anafungua kesi hiyo kuomba ndoa
 itenguliwe alikuwa tayari amenitelekeza maana alikuwa hatoi
 chochote kwangu licha ya kuwa naishi na watoto wake, alikuwa
 hanihudumii hata nikiumwa nilikuwa nikiishi kwa kutegemea
 kilimo mimi pamoja na watoto wangu…alinitelekeza
 kihuduma tangu Oktoba 2012."

 "…Hata mazao ambayo yalipatikana baada ya
 mimi kulima na wanangu nayo alikuwa akiyasimamia yeyé na
 wakati mwingine kumnufaisha zaidi mke mwenzangu na familia
 yake zaidi yangu mimi ambaye ndiye niliteseka
 kiuzalishaji," anasema Bi. Tarafa katika
 mazungumzo.

 Anasema mbali na unyanyasaji huo pia alikuwa akipigwa
 sana na mumewe mara kwa mara kwa sababu zisizokuwa na
 msingi. "…Kuna wakati nilikuwa mjamzito wa
 miezi nane alinipiga hadi nikaenda kulazwa aliniumiza sana
 kiuno pamoja na shingo, lakini mbali na kuniumiza kiasi
 hicho aligoma kabisa kunipeleka hospital ili niweze
 kutibiwa. Walilazimika kuja wazazi wangu ambao walinipeleka
 hospitali na kulazwa. Baada ya mimi kulazwa yeyé alikamatwa
 na polisi na kufunguliwa mashtaka kutokana na kitendo
 alichokifanya," anasema Bi. Tarafa.

 [caption id="attachment_42716"
 align="aligncenter" width="480"]<a
 href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2014/02/wake-Ofisa-Ustawi-wa-Jamii-wa-Halmashauri-ya-Wilaya-ya-Nkasi-Oscar-Mdenye.jpg"><img
 src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2014/02/wake-Ofisa-Ustawi-wa-Jamii-wa-Halmashauri-ya-Wilaya-ya-Nkasi-Oscar-Mdenye.jpg"
 alt="Ofisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya
 Nkasi, Oscar Mdenye," width="480"
 height="510" class="size-full
 wp-image-42716" /></a> Ofisa Ustawi wa Jamii
 wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi, Oscar
 Mdenye,[/caption]

 Anabainisha kuwa baada ya kumuomba sana mke wake
 aliingiwa na huruma na kufuta kesi ili waende wakayazungumze
 kinyumbani na wazee wa pande zote ili kutafuta suluhu, hivyo
 aliridhia na kufuta kesi hiyo. Kikao cha wazee kilimuamuru
 kulipa gharama na muda kwa wazazi wangu ambao walilazimika
 kusafiri kutoka kijijini kwao na kuacha shughuli zao na kuja
 kuniuguza mimi zaidi ya wiki moja hadi hali ilipokuwa
 nzuri.

 Pamoja na hali hiyo mateso kihuduma kwangu yaliendelea
 alikuwa hatoi chochote kutoka kwa mkewe mwingine anayeishi
 naye kuja kwangu kwa ajili ya wanae. Wakati mwingine
 aliwafukuza wanangu kukanyaga kwa mkewe huyo mwingine, licha
 ya watoto hao kuwa wakimsaidia kazi nyingine. Anasema mtoto
 wangu mmoja ndiye aliyekuwa akichunga ngombe ambazo ambazo
 zinainufaisha zaidi familia ya mke mwenzake, lakini wao
 hawapati hata maziwa ya ng'ombe wanapokamuliwa.

 "Nilivumilia nikachoka siku moja nikamfuata na
 kumwambia kama ataendelea kuwatenga wanangu ki-huduma hata
 mifugo ambayo wao ndio wachungaji basi nitawazuia kuchunga
 ng'ombe hizo maana zinawanufaisha wao pamoja na mke
 mwenzangu lakini sio mimi na watoto wangu ambao ndio
 wachungaji.

 Hapa napo alinipiga sana na kudai kwanini ninawazuia
 watoto wangu kuchunga ng'ombe za baba yao, alisema
 watoto lazima wachunge maana watakapotaka kuoa ukubwani
 watatumia ng'ombe hizo kama mahari hivyo siwezi
 kuwazuia…mgogoro uliendelea. Ndipo nilipoamua
 kumshtaki kwa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Isale
 'A', anasema.

 Bi. Tarafa anasema hata siku anaenda kujifungua mtoto
 wa nne ambaye ni wa mwisho kuzaa na Kazuri alilazimika
 kuwafungia watoto wake ndani usiku na kwenda hospitali
 mwenyewe. "…Nilipoanza kuhisi uchungu nilituma
 watoto wakamjulishe kuwa hali yangu ni mbaya hivyo naitaji
 msaada nipelekwe hospitali, aligoma kabisa kuja, majirani
 wakamfuata tena wao akagoma ndipo walipokuja mama na kaka
 yangu na kunipeleka wao hadi hospitalini nikajifungua salama
 mtoto wake wa nne," anasema.

 Baada ya kujifungua manyanyaso yaliendelea alifikia
 hatua ya kunitaka mimi na watoto wake niondoke pale kwake na
 niende kuishi kwa wazazi wangu eti akidai atakuwa
 akinihudumia kulekule. Mimi nilikataa nikamwambia siwezi
 kuondoka na mzigo wa watoto na kwenda nao nyumbani
 kwetu. 

 Anabainisha kuwa Novemba 18, 2013 baada ya mvutano na
 yeye kukiri kuwa yupo tayari kuachana na mume huyo iwapo
 atapata haki zake na watoto, mahakama ilivunja ndoa hiyo na
 kuamuru aondoke na watoto wawili bila kueleza namna
 watakavyo pata huduma toka kwa baba yao.

 Alisema mahakama iliamuru watoto wa miaka 7 na 9
 watabaki kwa baba yao na yeye kuondoka na wawili wenye miaka
 miaka chini ya saba. Aliongeza kuwa Mahakama iliamuru apewe
 magunia 9 ya mahindi kati ya 10 ambayo tulilima pamoja na
 bati 7.

 "…Mume wangu alidanganya kuwa hatuna mali
 pale mahakamani, mimi nikaeleza ni uongo kwani tuna
 ng'ombe zaidi ya 127, buzi 30, nyumba mbili pale
 kijijini Isale pamoja na hekari zaidi ya 70 za
 ardhi…hawakunisikiliza pale mahakamani. Ukweli ni
 kwamba tunamali hizo ambazo tulichuma tukiwa wote,"
 alisema Bi. Tarafa.

 Mwandishi wa habari hii amebahatika kupata nakala ya
 hukumu ya kesi hiyo, ambayo kweli haikuonesha namna watoto
 wanaobaki kwa mama watahudumiwaje na baba yao licha ya
 kuamuru kuwa watabaki na mamayao. Hata hivyo
 akizungumzia mvutano huo, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya
 Wilaya ya Nkasi, Ramadhan Rugemalira anasema mama huyo
 anahaki ya kufungua kesi nyingine ya madai kuomba mgawanyo
 wa mali na matunzo kwa watoto endapo hakuridhika na hukumu
 iliyotolewa kwa shauri hilo.

  "…Anachotakiwa kuomba mahakamani kwa
 sasa ni mgawanyo wa mali, kwamba katika kesi yao ambayo
 mahakama ilivunja kuna mali ambazo mahakama haikuzizungumzia
 kabisaa lakini na mimi (mke) ninahaki na mali hizo,
 unaona…ataleta ushahidi kama ng'ombe hao wapo
 kama kuna ardí na nini…hivyo huyo mwanaume ataitwa
 na kesi kusikilizwa," anafafanua Rugemalira.

 Hata hivyo, Hakimu Rugemalira anasema huenda mtoa
 hukumu wa mwanzo aliteleza kwa kitendo cha kutoainisha namna
 watoto wanaobaki kwa mama watalelewa vipi na baba
 (kihuduma). Anasema pamoja na hayo bado mama huyo anahaki ya
 kufungua madai mengine kudai haki hizo.

 Anasema Bi. Tarafa anaweza kufungua kesi ya madai kudai
 matunzo ya watoto pamoja na mali ambazo mahakama
 haikuzizungumzia kabisha wakati wa kesi ya msingi ya kuvunja
 ndoa yao. Anaongeza kuwa au mama huyo anaweza kukata rufaa
 mahakama ya wilaya kupinga hukumu ya awali kwamba
 hakuridhika na kitendo cha mahakama kumpa watoto bila ya
 kueleza namna ya watakavyo pata gharama za matunzo toka kwa
 baba.

 "…Anaweza kuleta shauri mahakamani
 akilalamika kwamba katika ndoa yetu iliyovunjwa kuna mali
 ambazo mahakama haikuongelea kabisa, na mali hizi katika
 kuzichuma na mimi ninauhusika, basi ataleta ushahidi
 mahakamani kuthibitisha uwepo wa mali hizo na walichuma wote
 kisha mahakama itamwita huyo mwanaume na kesi kusikilizwa
 ikiridhika basi mali hizo zitagawanywa," anasema
 hakimu Rugemalira.

 Mwandishi wa makala haya alizungumza na Kazuri
 aliyekuwa mume wa mama huyo kujua anazungumziaje juu ya mali
 ambazo mkewe anazilalamikia, yaani ng'ombe 127, nyumba
 2, mbuzi  30 na ardhi hekari 70. Katika majibu yake
 anasema mali hizo zinazolalamikiwa alipewa na babayake mzazi
 amshikie wakati anaanza maisha hivyo bado ni mali ya
 babayake ambaye alidai yupo hadi sasa. 

 Pamoja na madai hayo uchunguzi uliofanywa na mwandishi
 wa makala haya umebaini baba yake na Kazuri (kwa jina Kazuri
 Moshi) ni marehemu na alifariki dunia tangu mwezi Machi 2004
 na mali zake kugawiwa kwa watoto wake wote wenye haki ya
 kupata akiwemo Kazuri mwenyewe.

 Hata hivyo mtalaka wake Kazuri akifafanua zaidi juu ya
 mali anazolalamikia; anasema walipewa ng'ombe 65 za
 urithi toka kwa baba yake na Kazuri, lakini wamezizalisha
 hadi kufikia ng'ombe zaidi ya 127. Aidha anabainisha
 licha ya mifugo hiyo wanamiliki mashamba na nyumba mbili
 lakini anashangaa mzazi mwenzake anamdhulumu zote.

 Kwa upande wake Ofisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya
 Wilaya ya Nkasi, Oscar Mdenye, akizungumzia sakata hilo
 anakiri kumfikia. Anasema Bi. Tarafa alifika katika ofisi
 yake akilalamika kutoridhika na uamuzi wa mahakama.
 Alilazimika kutembelea familia hiyo zaidi ya mara moja
 Kijijini Isale na kufanya mazungumzo ya kina na pande
 zote.

 Anasema kwa maoni yake baada ya kuchunguza amegundua
 kuna utata juu ya sababu zilizotolewa mahakamani hadi
 kuvunjwa ndoa hiyo. Anasema kwa kuzingatia sheria nyingi
 kama Sheria ya Mtoto (2009), Sheria ya Ndoa (1971), Sheria
 ya Kanuni za Adhabu (1937) na zinginezo; pamoja na mikataba
 ya kimataifa iliyoridhiwa na kusainiwa na taifa ni vyema
 kila mtu, kwa nafasi yake mzazi/mlezi, mahakama, polisi, na
 maofisa Ustawi wa Jamii pamoja na vyombo vingine kuona
 Ustawi na maendeleo ya mtoto ni jambo muhimu. 

 Anabainisha kuwa; Sheria ya Ndoa (1971) fungu 113 (2),
 inaeleza uwezo wa Mahakama kutengua/kubadili amri yake ya
 kutengana iwapo itatosheka kwamba amri hiyo ilitokana na
 maelezo ya kupotosha au yasiyo na ukweli.

 "…Mahakama inaweza kuangalia upya taarifa
 ya sababu za kuachana (wizi na kiburi) ambazo Kazuri
 aliwasilisha mahakamani kwa kuwa zinaonesha hazina ukweli na
 zinahitaji ushahidi na uhuru wa kujitetea. Kwa kufanya hivyo
 mahakama itakuwa imempa Tarafa fulsa ya kufungua kesi ya
 madai na hivyo kupata mstakabali wa ustawi wa watoto wote
 wanne," anasema Mdenye.

 Kiongozi huyo wa ustawi wa jamii anasema;
 alivyofuatilia kwa kina mzozo huo amebaini  Kazuri
 alimpa mimba mtalaka wake akiwa darasa la sita 2003/2004,
 hivyo kumpotezea fulsa ya kusoma, lakini leo anamwacha
 solemba (mtelekeza na watoto) kirahisi tu bila kukumbuka
 makosa yake ya nyuma. 

 "Kikubwa zaidi Sheria ya Ndoa (1971), kifungu 114
 kinaeleza uwezo wa mahakama kutoa amri ya kugawana mali za
 waliooana. Mahakama itazingatia masilahi ya watoto, na
 itatazama usawa katika ugawaji. Pia kifungu 136 (1)
 kinaeleza uwezo wa Mahakama kuzingatia nasaha za maofisa wa
 ustawi na wengineo husika."

 Anabainisha kuwa Kazuri hajafanya hivyo badala yake
 amebomoa hata nyumba ya vyumba viwili aliyokuwa akiishi
 mtalaka wake na watoto na alipoulizwa kwa nini anafanya
 ukatili huo alijibu amebomoa ili mkewe na watoto waende
 kuishi kwa bibi yao yaani mama mkwe wake.

 Kimsingi nashauri sote tuache mawazo mgando kama ya
 Kazuri ambaye anazungumza kwa kujiamini kana kwamba ni jambo
 jema. Nina mengi ya kusema juu ya mzozo huu ambao Kazuri
 anaonekana kukosa utu, lakini sina uwezo wa kupinga amri ya
 mahakama. Tuiachie kwa kuwa ndio chombo cha mwisho cha
 uamuzi kwa tatizo hili," anasema Mdenye.

 <strong>*Imeandaliwa na www.thehabari.com kwa
 kushirikiana na TAMWA</strong>
 --
 Joachim Mushi, Mhariri Mkuu wa gazeti tando la
 Thehabari.com


 Mail address:-
 mushi@thehabari.com/
 jomushi79@yahoo.com/
 info@thehabari.com


 Mobile:- 0717
 030066/ 0786 030066/ 0756 469470
 Web:- www.thehabari.com  

           http://joemushi.blogspot.com




 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.


 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.






 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to
 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.



--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

0 comments:

Post a Comment