Sunday 15 December 2013

[wanabidii] JWTZ INUNUE HISA KWENYE MIRADI MIKUBWA

Ndugu zangu ,

Jeshi la nchi jirani ya Rwanda yaani RPF limenunua Hisa kwenye kampuni kubwa ya mawasiliano nchini Afrika Kusini ya MTN pia imenunua kampuni kadhaa katika nchi nyingine kama sehemu ya kuboresha kipato cha jeshi hilo la Rwanda .

Hapa kwetu sijawahi kusikia Jeshi likijishugulisha na shuguli za uwekezaji mkubwa au kwenye biashara za ushindani kama wa simu za mikononi , migodi ya dhahabu na Kilimo .Niliwahi kusikia moja ya mchuchuma ambayo ilileta kelele kidogo .

Ni vizuri Jeshi letu kuachwa liwekeze kwenye maeneo mengine yenye faida kwa Jeshi hilo kwa kununua hisa kama kwenye kampuni za simu , migodi ya dhahabu , kwenye vitalu vya gesi na hata kwenye utafiti .

Tunasikia kwa mfano uwekezaji katika gesi ni gharama sana , hivi jeshi linashindwa kuwekeza huko mpaka tuombe mikopo mikubwa mikubwa ? Jeshi linashindwa kuuziwa vifanda na mashamba makubwa kwa ajili ya kuwekeza kweli ?

Hawa vijana wanaoajiriwa kwenye majeshi yetu kila siku wanaenda huko kufanya nini kama hawatumiki kwenye shuguli nyeti na muhimu kwa taifa kama hizi ?

Jeshi lianze kutafuta fedha lenyewe za kujiendesha na kidogo litapewa toka serikali kuu .

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

0 comments:

Post a Comment