Saturday 5 October 2013

[wanabidii] Uchambuzi

Diego Costa anaweza kuichezea  Hispania

Na Olle Bergdahl Mjengwa,

 

MSOMAJI, mchezaji anayewashangaza wengi msimu huu ni mchezaji maarufu wa Atletico Madrid, Diego Costa.

 

Nikiandika makala hii, Diego Costa amefunga mabao nane katika mechi saba katika ligi ya Hispania. Wiki hii mechi za kufuzu Kombe la Dunia zinachezwa.

Kinachowashangaza  wengi ni kwamba Diego Costa aliyezaliwa na  kukulia Brazil, na mwenye miaka 24 ,  hajawahi kucheza mechi ya mashindano dhidi  ya timu ya taifa ya Brazil. 

 

 Mchezaji huyo ameishi  Hispania tangu mwaka 2007. Ana uraia ya Kihispania pia. Kwa hiyo, mchezaji huyo anaweza kuichezea timu ya taifa ya Hispania.

 

Sheria za FIFA zinasema  mchezaji akicheza mechi moja ya ushindani na timu moja ya taifa, mchezaji huyo atabidi kuichezea timu hiyo katika kipindi chake chote cha kucheza mpira. Lakini, Diego Costa amecheza mechi moja tu na timu ya taifa ya Brazil na ilikuwa mechi ya kirafiki dhidi ya Italia mwaka huu.  Kwa hiyo, Diego Costa bado hajacheza mechi ya ushindani na Brazil, na kwa hiyo anaweza kuichezea timu ya taifa ya Hispania.

 

 Lakini, chama cha soka cha Brazil hawataki Hispania kumwita Diego Costa kucheza mechi za kufuzu Kombe la Dunia akiwa na Hispania. Diego Costa alipata uraia wa Hispania mwaka huu, lakini chama cha soka cha Brazil wanaamini mchezaji huyo ni Mbrazili na wamewambia FIFA kwamba Costa hajacheza mechi ya ushindani na timu ya taifa ya Brazil kwa sababu hawana mechi za kufuzu kwa kuwa  fainali za Kombe la Dunia zitachezwa Brazil mwakani.

 

FIFA wameamua kwamba Diego Costa hata ruhusiwa kucheza mechi za kufuzu fainali za  Kombe la Dunia wiki hii na wiki ijayo, na haruhusiwi kuichezea timu ya taifa ya Hispania wala ya Brazil mpaka FIFA wakimaliza utafiti juu ya suala hilo, na hivyo wataamua kama Diego Costa anaruhusiwa kuichezea timu ya taifa ya Hispania au hapana.

 

Vyombo vingi vya habari vinaamini kwamba FIFA watamruhusu Diego Costa kuichezea timu ya taifa ya Hispania, na kwamba  mchezaji huyo amemwambia Del Bosque, kocha wa timu ya taifa ya Hispania kwamba anataka kuichezea timu hiyo. Bila shaka, Hispania wanahitaji mchezaji kama Diego Costa. Timu ya taifa ya Hispania kwa muda  mrefu hawajakuwa na mshambuliaji anayefunga mabao mengi  katika timu ya taifa na timu ya klabu.

 

Hispania wamebaki na mechi mbili tu za kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia. Na wana nafasi kubwa kuchukua nafasi ya kwanza katika kundi lao, hivyo,   watafuzu kucheza fainali za  Kombe la Dunia. Lakini, Costa atakosa mechi hizi. Hata hivyo, naamini kwamba kama Costa ataendelea kuwa katika hali nzuri ya kimpira, basi, mchezaji huyo atachukua nafasi katika kikosi cha kwanza cha Hispania kama anaruhusiwa kuichezea timu hiyo.

 

Brazil na Hispania walikutana katika fainali ya kombe la mabara mwaka huu. Hispania walifungwa mabao matatu kwa bila. Labda Hispania na Brazil watakutana katika fainali ya Kombe la Dunia mwakani. Del Bosque anajua kwamba kama Diego Costa anaichezea timu yake, basi, Hispania watalipiza   kisasi.  

 

-      MWISHO-

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

0 comments:

Post a Comment