Thursday 17 October 2013

Re: [wanabidii] Utafiti: Wasio na elimu waongoza kumpenda Rais Jakaya Kikwete

Mngonge,

Kwani kwenye utafiti huu waliohojiwa walihojiwa by phone ama face to face?  Walichaguliwa kwa taratibu gani?

Courage


2013/10/18 mngonge <mngonge@gmail.com>
Utafiti huo ulitakiwa useme watanzania wengi wanampenda Kikwete kwa sababu watanzania walio wengi wana elimu ya darasa la saba au chini. Japo nina wasiwasi na design, sample size na namna walivyopick respondents (sampling procedure) kama ni appropriate. Kwa hali tuliyonayo sasa hata hao wenye darasa la saba na kushukachini wamekwishashtuka si rahisi kupata majibu kama hayo. Rais ni kiongozi wa taifa zima hivyo utafiti unaohusu maoni ya raia juu ya utendaji wake lazima uhusishe sample kubwa na iwe na uwakilishi mzuri kwa kila cluster/strata.


2013/10/16 Abdalah Hamis <hamisznz@gmail.com>
Na Goodluck Eliona, Mwananchi

Ripoti mpya ya utafiti imebaini kuwa asilimia kubwa ya Watanzania wenye elimu ya darasa la saba na wale wasiosoma, ndiyo wanaokubaliana na utendaji kazi wa Rais Jakaya Kikwete.

Ripoti ya utafiti huo iliyopewa jina la 'Namna Watanzania wanavyouangalia utendaji kazi wa Bunge na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania' ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Asasi ya Afrobarometer, inaonyesha kuwa asilimia 77 ya waliokosa elimu ndiyo wanamuunga mkono Rais Kikwete.

Afrobarometa ni Asasi ya Kimataifa inayojumuisha taasisi tatu za Institute for Democracy ya Afrika Kusini, Ghana Centre for Democratic Development ya Ghana na Political Science Department ya Chuo Kikuu cha Michigan cha Marekani.

Mtafiti Msaidizi wa Afrobarometer, Stephen Mwombela akisoma ripoti hiyo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alisema asilimia 72 ya wale walioishia darasa la saba ndiyo wanamuunga mkono Rais.

Wakati asilimia 23 ya watu wasiosoma ndiyo hawamkubali Rais na asilimia 28 ya wale walioishia darasa la saba, pia hawaridhishwi na utendaji wa kiongozi huyo.

Mwombela, hata hivyo, alisema utafiti huo uliohusisha watu 2,400 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaonyesha kuwa idadi kubwa ya wasomi wa kiwango cha sekondari na kuendelea wanaunga pia mkono utendaji wa Rais, lakini siyo kwa kiwango cha juu kama wale ambao hawajasoma.

"Asilimia 60 ya waliosoma elimu ya sekondari na kuendelea wanaunga mkono utendaji wa Rais, lakini 40 hawakubaliani na utendaji wake," ilisema taarifa ya matokeo ya utafiti huo uliofanyika kati ya Mei hadi Juni mwaka jana.

Matokeo ya utafiti huo yanatofautiana na yale ya mwaka 2008, ambayo yalionyesha kuwa wasomi walikuwa wanamuunga mkono Rais kwa asilimia 92.

Pia katika matokeo ya utafiti huo wa mwaka 2008, ulionyesha kuwa wasiosoma walimuunga mkono kiongozi huyo kwa asilimia 92.

Imani ya wananchi kwa Rais

Ripoti hiyo ilisema pia imani ya wananchi kwa utendaji wa Rais imeshuka hadi kufikia asilimia 74 kwa mwaka jana, tofauti na asilimia 94 ya mwaka 2005 wakati aliposhika wadhifa huo.

Pia utafiti huo uliodhaminiwa na Taasisi ya Utafiti kuhusu Kuondoa Umaskini (Repoa) umebainisha kuwa imani ya wananchi kwa Rais imeshuka kutoka asilimia 88 mwaka 2008 hadi asilimia 74, huku idadi ya watu wasiokubaliana kabisa na Rais ikiongezeka kutoka asilimia 11 mwaka 2008 hadi asilimia 26 mwaka 2012.

 

Imani kwa Bunge

Wananchi wengi pia wameonyesha kutokuwa na imani na mwenendo wa Bunge, kwa kulipa asilimia 76 mwaka 2012, idadi yao ikishuka kutoka asilimia 83 ya mwaka 2008.

Imani ya wananchi kwa Bunge imeshuka katika kipindi hiki ambalo liko chini ya Spika Anne Makinda, ambaye alichukua uongozi mwaka 2010 wakati mwaka ule wa 2008 lilikuwa chini ya Samuel Sitta imani ilikuwa juu. Taarifa hiyo pia inaeleza kuwa watu wanaoishi vijijini ndiyo wanaoridhishwa zaidi na Bunge kwa kupata asilimia 63, ikilinganishwa na wakazi wa mijini ambao ni asilimia 60.

Pia imebainika kuwa wananchi wa Zanzibar wanaridhishwa zaidi na utendaji wa Bunge kwa asilimia 64, tofauti na wananchi wa Tanzania Bara ambao wanaridhishwa kwa asilimia 61.

"Watu waliokuwa wanakubaliana na utendaji wa Bunge mwaka 2003 walikuwa asilimia 31, lakini mwaka 2012 idadi iliongezeka hadi asilimia 61," alisema Mwombela wakati akiwasilisha matokeo ya utafiti huo unaofanyika kwa mara ya tano nchini Tanzania.

Hata hivyo, Mwombela alisema kuwa wananchi wengi bado wanafurahishwa na utendaji wa Mahakama, lakini idadi yao imepanda kutoka asilimia 73 kwa mwaka 2008 na kuwa asilimia 74 mwaka 2012.

Akichangia baada ya ripoti hiyo kuwasilishwa, Dk Abel Kinyondo, alisema kuwa matokeo ya utafiti huo hayajaonyesha kuporomoka kwa imani kwa Rais badala yake yameonyesha uhalisia.

"Inawezekana imani kwa Rais haijashuka, badala yake imekaa katika hali yake, kwa sababu kitu gani alikifanya 2008 watu wakampenda sana, ambacho leo hii hajakifanya hadi wasimpende?" alihoji Kinyondo. Kinyondo alionekana kushangazwa na namna Rais alivyoweza kupata asilimia 71 wakati nchi inapita katika kipindi kigumu cha rushwa na ufisadi.

Mwakilishi kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Victor Kimesera alisema utafiti huo una kasoro kadhaa ikiwa ni pamoja na kumtaja Rais kuwa ndiye mwakilishi pekee wa Serikali wakati kuna viongozi wengine wengi. "Kwa upande wa Rais walitakiwa kuhoji viongozi wengi zaidi kwa sababu Rais siyo kiongozi pekee yake katika Serikali," alisema.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Fedha, Dk Jonas Kipokola alisema kama utafiti huo ungefanyika Mei hadi Juni mwaka huu, huenda matokeo yangekuwa tofauti. "Siwezi kusema yangekuwaje, lakini yasingekuwa hivyo yalivyo," alisema Kipokola.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

0 comments:

Post a Comment