Nafikiri ndugu Godfrey Mbanyi anachosema tumekishuhudia wengi. Kumbuka Dr. Slaa alivyoshambuliwa bungeni alipoleta hoja ya wizi wa fedha za EPA. Waziri muhusika alipinga kwa nguvu zote na wabunge wengi wa CCM walionekana kushabikia badala ya kufikiri na kutoa maamuzi bila kupoteza muda. Ilichukua muda mwingi kukubali na kutoa maamuzi.
Mfano mwingine ni hoja ya kutaka mabadiliko ya Katiba ilivyopingwa sana na waziri Kombaine na kutetewa na wabunge wa CCM kwamba Tanzania kwa sasa hahitaji kubadilisha katiba na kwamba iliyopo inatosha.Leo hii hao hao ndo wanajifanya machampioni wa hoja za mabadiliko ya katiba. Hii ndo bongo bwana! hivi huwa hamjui kwamba tunakumbukumbu kama hizo. Hoja hata kama ni ya msingi kiasi gani kitu kinachoangaliwa ni nani na anatoka chama gani ili tumsupport na ikibidi tumtukane kama si wa chama chetu. Hadi wapiga kura tunabaki tukijilaumu kwa uamuzi wetu mbovu wa kuwapeleka watu bungeni wasiokuwa na uwezo wa kuchambua hoja bali matusi2013/10/5 Dr. Hamisi A. Kigwangalla <hkigwangalla@gmail.com>
Jovias, Zitto alikuwa kwenye mkutano nje ya jiji la Dar es salaam lakini tutaonana na tutashirikiana kuhakikisha hawagawi vitalu vingine zaidi, walivyogawa vinatosha...tujenge uwezo wetu wa kisheria na kitaasisi kwanza
2013/10/5 Jovias Mwesiga <ngonzy@gmail.com>Hivi sie wasomi wa mabadiliko tunamatatizo ya uelewa. Saizi tunashupaa vile Dr. Hamis kaandika lakini hii kitu ilishaingia humu mabadiliko tupunguzeni ubigwa wa kujadili watu tujadili vitu vya msingi.
Kama kuna kitu cha msingi kakiongelea tukiangalie, SASA nyie wabunge tusaidieni hili. Jana nilisoma Dr. ulikuwa unajaribu kuwasiliana na mheshimiwa ZITTO sijui kama mliwasiliana. Ila kwa ufupi inaonyesha wabunge wetu kama mna meno basi bunge la tanzania halina meno.Huu upuuzi umpitiliza kiasi. Ndugu yangu kakak Kamala utakuwa umeelewa nilipoongelea wasi wangu wa watanzania kuwa na uwezo wa kutumia ubongo.Haitoshi kulalama tu humu nyie wabunge u have to do something about it. Huu si muda wa kutafuta kuonyesha uwezo wa kujua mambo bali muda wa kugeuza giza kuwa mwanga there is no better opportunity to serve Tanzanians than this time tusaidieni kututoa kwenye shimo hili badala ya upuuuzi wa NDIOOO MIA KWA MIYA.Nape hii ndo kazi bora ya chama chako?--2013/10/4 godfred mbanyi <mbanyibg@yahoo.com>
Dr. HK,
Hoja nzuri, lakini mbona wenzenu wa Upinzani wakiuliza mambo kama haya ambayo ni nyeti kwa Taifa , wewe na nduguzo wa CCM mnawazodoa, kuwazomea na kuwakejeli???
Una utashi wa kweli katika hili??
Nauliza tu Mheshimiwa!!!
--------------------------------------------
On Fri, 10/4/13, Dr. Hamisi A. Kigwangalla <hkigwangalla@gmail.com> wrote:
Subject: [wanabidii] Papara za Kugawa Vitalu Vipya vya Gesi asilia: Tumerogwa, ujasiriamali binafsi ama Uzalendo uliopitiliza?
To: "wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>, "mabadilikotanzania" <mabadilikotanzania@googlegroups.com>, afya-club@googlegroups.com
Date: Friday, October 4, 2013, 11:36 AM
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Papara za Kugawa Vitalu Vipya vya
Utafiti wa Gesi Asilia Bila
Sera, Sheria na Kanuni: Tumerogwa, Ujasiriamali Binafsi ama
Uzalendo
Uliopitiliza? (I)
Na Hamisi Kigwangalla,
MB.
Wakati wa kipindi cha bunge la
bajeti, Prof. Sospeter
Mwijarubi Muhongo, Waziri wa Nishati na Madini, aliliarifu
bunge kuwa serikali
ilikamilisha kazi ya kuipitia mikataba ya gesi asilia mnamo
mwezi Novemba 2012 na
akasema kuwa "kukamilika kwa kazi hiyo kumeiwezesha
serikali kubaini maeneo
yanayohitaji kuboreshwa katika mikataba hiyo. Pia, matokeo
ya uchambuzi wa
mikataba hiyo yatasaidia katika uundaji wa sera, sheria na
kanuni za usimamizi
wa sekta ndogo za mafuta na gesi asilia itakayokidhi matakwa
ya watanzania." Kanuni
hii ilinithibitishia jambo moja, kuwa hatuko sawa katika
njia tunayopita
kuelekea kufanya uvunaji wa raslimali hii adhimu na urithi
wetu wa bure; kwamba
hatuna sera, sheria na kanuni, sasa tunaendeleaje kutoa
vitalu vipya kila siku?
Ufahamu wangu mdogo kwenye mambo
haya umeniwezesha kuamini
kuwa sheria ya petroli (The petroleum (exploration and
production) act) ya
mwaka 1980 haikidhi haja ya kuendesha kazi za utafiti na
uzalishaji wa gesi asilia,
na hata biashara ya gesi asilia. Hata nilipoisoma ile sera
mpya ya gesi (draft)
nilibaini wazi kabisa nayo inakiri kuwa hatuna mfumo
madhubuti wa kisheria na
kitaasisi, yaani 'legal and regulatory framework', wa
kuendesha vizuri sekta
hii nyeti.
Prof. Sospeter Muhongo aliwahi
akinukuliwa akisema kuwa
tusipokimbia kuanza kuvuna gesi, majirani zetu watatuwahi.
Kwani gesi inaoza?
Sasa tunavyokimbia namna hii bila kujua tunafaidikaje si
tutajikuta tumefika
kwenye gesi sawa na wenzetu ama tumewawahi lakini
hatuifaidi, kipi bora sasa? Leo
hatuna sera, tunajuaje wajibu wa kila mtu kwenye shughuli za
uvunaji? Ambapo
gesi inachimbwa, watu wenyeji wana haki na wajibu upi?
Masuala ya fidia kwa
wananchi watakaoathirika kwa namna moja ama nyingine
yamekaaje? Wenzetu wa
Kenya wamezuia mafuta yao yasichimbwe mpaka kwanza wawe na
sera, sisi
tunakimbilia wapi?
Wakati tukikiri kuwa hatuna sera,
sheria na kanuni mpya na
za kisasa zinazoweza kukidhi mahitaji ya Taifa ya uvunaji na
uwekezaji kwenye
sekta hii nyeti, hivi majuzi Wizara ya Nishati na Madini
imetoa tangazo la
kualika wawekezaji kwenye 'mkutano na maonesho ya pili ya
Tanzania ya mafuta na
gesi 2013' utakaofanyika Dar es salaam ukumbi wa Mwalimu
Nyerere International
Convention Center kuanzia tarehe 23 hadi 25 mwezi huu
(oktoba), ambapo mzunguko
wa nne wa kugawa leseni za vitalu vya gesi kwenye bahari kuu
na kaskazini mwa
ziwa Tanganyika (The 4th Tanzania offshore and
North Lake Tanganyika
licensing round) utazinduliwa.
Katika tangazo hilo lililotolewa na
Wizara ya Nishati na
Madini kupitia shirika letu la uendelezaji petroli nchini
(Tanzania Petroleum
Development Corporation, TPDC) vitalu saba vyenye ukubwa wa
wastani wa kilomita
za mraba 3000 kila kimoja vitagawiwa kwenye bahari kuu kwa
mtindo wa kuwapa
wawekezaji leseni za utafiti kwa asilimia 100 na vitalu
viwili vitabaki kuwa
mali ya serikali chini ya shirika lake la TPDC ambapo
atatafutwa muwekezaji mshirika
wa kufanya naye utafiti wa pamoja. Vitalu vikigawanywa kwa
mtindo wa kuwaachia
wawekezaji jukumu la utafiti (exploration) maana yake ni
kwamba kuanzia siku ya
kwanza ya utafiti wanaanza kurekodi gharama zao na
wakimaliza na kufanikiwa
kugundua gesi, wanapoanza zoezi la kuivuna na kuiuza sasa
hiyo gesi wanaanza
kukata asilimia si chini ya 70 ya mauzo yote kama gharama
zao. Asilimia 30 tu
inayobaki ndiyo itagawanywa kwa Tanzania kupata asilimia 60
na wawekezaji
kupata asilimia 40. Hii kwa lugha ya kitaalamu wanaita ni
'production sharing
agreement (PSA).' Hapa kuna maswali mengi sana ya
kujiuliza, nani anafanya kazi
ya kuzihakiki gharama wanazoingia hawa wawekezaji ili
watakapokuja kuanza kuzikata
tuwe na uhakika kuwa ndizo gharama halisi walizotumia?
Na katika vile vitalu viwili
ambavyo anapewa TPDC mkataba
utakuwa tofauti kwa kuwa kuanzia mwanzoni shirika letu
wenyewe litaingia kwenye
utafiti hadi uzalishaji na hatimaye mauzo. Na hapa kwa
hakika tutarajie kuwa na
mgao mkubwa zaidi wa faida kwa kuwa tutakuwa tumeshiriki
toka mwanzoni. Na hata
kama mbia wetu akisema ameweka gharama fulani tutaweza
kuzihakiki maana na sisi
tumo. Pia hata uhamishaji wa utaalamu na teknolojia
(technology transfer),
kujenga uwezo wetu wa kiuendeshaji wa zoezi hili la uvunaji
wa raslimali za
gesi asilia na mafuta na hata wa kifedha ni jambo
litakalofanyika kirahisi
katika mtindo huu, na siyo ule wa kuligeuza taifa letu
shamba la bibi kwa
kuwaachia mabeberu waje wavune tu. Huu ndiyo mfumo wa
kufuatwa na nchi yoyote ile
yenye watu wazalendo, wanaojitambua na wanaojua biashara. Na
ambao wako 'serious'
dhidi ya vita ya kupambana na umaskini. Wanaoguswa na shida
za wananchi za siku
hadi siku, wanaoongozwa na utaifa na si na njaa za matumbo
yao.
Leo kampuni ya Statoil ya Norway
aliyegundua visima vya gesi
huko kwenye bahari kuu ya Tanzania ni kampuni inayomilikiwa
na serikali yao kwa
zaidi ya asilimia 67, na imeitajirisha nchi yao. Pia kampuni
kama Petronas ya
Malaysia, National Gas Company ya Trinidad and Tobago
zinafanya kazi kwa
kufuata 'model' ya Norway.
Kwa nini sasa TPDC isiwe
'Statoil' ya Tanzania? Hili ni
swali lenye thamani ya zaidi ya dola za kimarekani milioni
moja. Namtaka Prof.
Sospeter Muhongo, ambaye amekuwa akijinasibu kwa usomi wake
awajibu watanzania.
Aoneshe uwezo wake. Awaambie watanzania elimu yake
imetusaidia nini kuleta
majibu ya swali hili.
Swali lingine lenye kunitatiza na
naamini pia watanzania
wengi linawatatiza ni kwamba, ni kwa nini tunaharakisha
namna hii kuingia
kwenye ugawaji wa vitalu vya gesi ilhali hatuna sera, sheria
na kanuni mpya? Waziri
huyu msomi na mtafiti haoni hatari ya hizi papara zetu
kweli? Haoni hatari ya
kumaliza kugawa vitalu vyote kisha kurudi kinyume nyume sasa
kuanza kuomba
mikataba na wawekezaji irekebishwe kufuata sera, sheria na
kanuni mpya? Na hapo
wanasheria watakuwa wameishaweka vipengele vya kutuzuia
kufanya hivyo
(stability clauses) kwenye mikataba na hatimaye kuishia
kuwapigia magoti
kuwabembeleza tu?
Kila siku tunazungumzia uwazi
kwenye sekta hizi za raslimali
ya gesi, mafuta na madini na Tanzania imesaini mkataba wa
kimataifa wa uwazi
kwenye sekta hizi (Extractive Industries Transparency
Initiative), hivi kuna
uwazi kweli hata kidogo tu kwenye haya maamuzi ya Prof.
Muhongo na maluteni
wake pale Wizara ya Nishati na Madini? Kwanza wanapata wapi
uhalali (legitimacy)
wa kusaini mikataba kwa kutumia sheria ambayo wao wenyewe
wanakiri imepitwa na
wakati na ndiyo maana wameanzisha mchakato wa kutunga sera,
sheria na kanuni
mpya?
Hakuna atakayebisha kuwa ili tuwe
salama ni lazima twende
kwa hesabu sana, kwanza tuwe na mfumo thabiti wa kisheria na
kitaasisi (strong legal
and institutional framework); sasa leo hii ndiyo
tunahangaika kuandika sera, na
kusomesha raslimali watu kwenye sekta hizi, ni lini wataiva
na kuanza kutumika
- miaka zaidi ya mitatu ni lazima ipite!
Prof. Muhongo hivi anazo kweli
takwimu za kodi tulizopata
kutokana na migodi mikubwa ya uchimbaji wa dhahabu? Hana
taarifa kuwa tulianza
kupata kodi pale Rais Kikwete alipoamua kuingilia kati na
kuanzisha mazungumzo
na wawekezaji hawa kufuatia tume ya Jaji Bomani ndipo
tuliposhuhudia wakianza
kulipa kodi ya kampuni (corporate tax) ya asilimia 30? Kabla
ya hapo kila siku
walikuwa wakisema hawafanyi faida na hivyo hawapaswi kulipa
kodi. Leo kuna
kampuni ngapi za uchimbaji wa dhahabu zimefunga migodi yao
bila kulipa hata
shilingi moja na nyingine kulipa miaka miwili hadi minne ya
kurashia rashia tu
kwa 'soni' ili kujijengea mazingira rafiki ya kupewa
kitalu kipya wavune tena
dhahabu? Wakati wimbi la kuingia kwa wawekezaji hawa wakubwa
kwenye migodi ya
dhahabu linashika kasi, kisingizio cha kuwaondoa kwa nguvu
wachimbaji wadogo na
wananchi wenyeji wa maeneo hayo kwenye maeneo yao (kama
wageni kwenye nchi yao)
kilikuwa tuwakaribishe wawekezaji watalipa kodi, watajenga
shule na hospitali,
wataongeza ajira nchini n.k. Hivi ni shule ngapi zimejengwa
kwa mfano na
Resolute pale kwetu Nzega? Wananchi wenyewe wameweza kujenga
shule ngapi kwa
pesa ya kilimo cha jembe lao la mkono tu? Sheria mpya ya
madini ilipokuja
imetusaidiaje sisi kama Taifa? Tumekuwa na sheria nzuri
lakini haina meno
kwenye mikataba ya zamani.
Wawekezaji hawakuleta maendeleo
yoyote ya kupigia mfano,
ambayo hata leo unaweza kuonesha. Hakuna tofauti kati ya
Nzega iliyokuwa na mgodi
mkubwa wa dhahabu na Igunga ambayo haikuwa na mgodi mkubwa
kama ule katika
kipindi hicho hicho – inakuwa bora hata Mwadui ya
Williamson Diamonds kule
Shinyanga ina utofauti na vijiji jirani na hata mjini
Shinyanga kwa wakati ule!
Wawekezaji kwenye sekta ya dhahabu hawakuleta maendeleo kwa
wenyeji
wanaowazunguka wakidai kuwa hawawajibiki kimkataba kufanya
hivyo. Je, tumejipangaje
kwenye sekta ya gesi? Kwa nini tusitulie kwanza,
tukatengeneza sera ya
kuwahudumia wenyeji ( a policy on local content initiatives)
ili 'tuwawajibishe'
wawekezaji, tujue wenyeji watafaidikaje na nchi
itafaidikaje, na wao
washirikishwe kwenye mchakato huo ili twende pamoja?
Kama ilivyo kwa mambo yote
yanayoendelea kwenye gesi, na
kama ilivyokuwa kwenye ile sekta ya madini, usiri wa maksudi
ama wa kutojua
umegubika namna ya wenyeji kufaidika. Tunaambiwa watanzania
wataajiriwa, watauza
bidhaa zao kwenye makampuni ya madini na uchumi wa maeneo
hayo utakuwa kwa
kasi, mchanganuo wa kina wa namna haya yatakavyotekelezeka
umeandikwa kwenye
sera, sheria ama kanuni ipi? Mkakati wa kuwawezesha wazawa
wafanikishe haya kwa
viwango vinavyotakiwa uko wapi? Maana haya makampuni huja na
'viwango' vyao vya
nyanya na vitunguu na vinginevyo, sasa je sisi tumejiandaa
vipi kuwawezesha
wenyeji wafaidike na soko hili jipya na la uhakika?
Je, tuna sera gani ya kutunza na
kutumia mapato yanayotokana
na gesi? Kwa sasa, kwa ufahamu wangu, hatuna. Kwa nini
tusijipange tukatunga
sera, sheria na kanuni safi za kutuongoza, tukajenga mtaji
wa raslimali watu ya
kutosha, tukawekeza mtaji kwenye TPDC yetu ndipo tukaingia
sasa kutafuta 'wabia'
wa kusaidiana nao kutafiti na hatimaye kuwekeza, siyo wa
kuwapa vitalu 'wawekeze!'.
Watanzania tunatamani tuwe na TPDC inayofanana na Statoil.
Je, Prof. Muhongo
yuko tayari kutupa hiyo?
Tukikamilisha mchakato wa kujenga
mfumo thabiti wa kisheria
na kitaasisi kwa njia ya kidemokrasia ya uwazi na shirikishi
tutakuwa tumewapa
uhalali akina Prof. Muhongo na wenzake sasa kufanya maamuzi
ya utekelezaji
yanayofuata sera, sheria, kanuni na mikakati iliyowekwa.
Kwa nini tusijipange kuifanya TPDC
yetu kuwa 'Statoil' (mwekezaji)
kwenye nchi nyingine huko tunakoelekea? Kama tungeliamua
vema huko tutokako, STAMICO
leo ingekuwa tajiri na ingekuwa inachimba dhahabu kama
Ashanti Goldfields Corporation
ya Ghana. Tusikosee tena kwenye gesi.
Tuna haraka gani, na ya nini? Ya
kwenda wapi? Kuhakikisha tu gesi imechimbwa – na kwamba
sisi kufaidika ama
kutofaidika siyo ishu? Kwani kuna umaarufu gani tunaupata
kwa kugawa vitalu vya
gesi vyote leo? Na mwani ni lazima wavigawe vyote hao
waliopo wizarani leo? Tunatunga
sera, sheria na kanuni mpya ili zije zitumike kwenye nini
wakati vitalu vyote
tunagawa leo kwa kutumia sheria ya kizamani? Haya ni maswali
yanayohitaji
majibu kuntu. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo akipenda
anaweza kuja kutukata
kiu yetu ya kujua. Atuelezee kwa kina. Na kama anataka nchi
hii imkumbuke kwa
kushiriki kuijenga afanye uamuzi sahihi - asimamishe ugawaji
wa vitalu vipya
vya gesi, akamilishe mchakato wa kujenga mfumo wa kisheria
na kitaasisi ndipo
aendelee. Ila kama anataka alaumiwe na vitukuu na
vining'ina vyake mwenyewe
aendelee na hii papara yake.
Dkt. Hamisi
Kigwangalla (MB) ni Mbunge
wa Jimbo la Nzega na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Tawala
za Mikoa na
Serikali za Mitaa (TAMISEMI).
--
"Vision is the ability to see the invisible!"
Hamisi A. Kigwangalla, MD, MPH, MBA
P.O.Box 22499,
Dar es salaam.
Tanzania.
Phone No: +255 754 636963
+255 782 636963
website: www.peercorpstrust.org
or www.hamisikigwangalla.com
Email: hamisi.kigwangalla@peercorpstrust.org
or info@hamisikigwangalla.com
Skype ID: hkigwangalla
Blog: blog.hamisikigwangalla.com
--
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
Google Groups "Wanabidii" group.
---
You received this message because you are subscribed to the
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
--
"Vision is the ability to see the invisible!"
Hamisi A. Kigwangalla, MD, MPH, MBA
P.O.Box 22499,
Dar es salaam.
Tanzania.
Phone No: +255 754 636963
+255 782 636963
website: www.peercorpstrust.org or www.hamisikigwangalla.com
Email: hamisi.kigwangalla@peercorpstrust.org or info@hamisikigwangalla.com
Skype ID: hkigwangalla
Blog: blog.hamisikigwangalla.com
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment