Wednesday 2 October 2013

Re: [wanabidii] KUB Freeman Mbowe Vs NS Job Ndugai: Kushindwa kwa Uongo baada ya kweli kufahamika!

Dr. HK

Unajua si kila mtu kwa hali ilivyo anaweza kusema kitu akaeleweka kwa watu jinsi wanavyochochewa na kujenga hofu kwa watu bila hata woga au aibu.

Sisi tulioko mikoani tunashangaa watu wana naadharia tofauti kabisa na motion hii uliyofafanua na kwamba sasa wanaamini kuwa KUB kaonewa.

Mtu kama wewe ukisema unakubalika siyo kama wasio na majina. Msikae kimya nchi hii brother ikiwaka moto hata nyie mtaungua pia.

Kuna.watu wana mtizamo safi lakini kama kawaida kwenye msafara wa mamba na kenge wamo ambao kwa mtizamo wangu ndio.wengi. Wamefaulu kuvuruga akili za vijana wetu kwa maslahi yao binafsi. Siku wakipata nchi watawaaacha solemba wakilamba midomo na.kilalamika afadhali ya jana na.watakuwa wamechelewa.

Jitahidini.sana kuweka sawa.hya.mambo.kabla.hayajingia katika hatua ambayo hayawezi kurekebishika bro.

Uwe na.siku njema.

Sent from Yahoo! Mail on Android



From: Dr. Hamisi A. Kigwangalla <hkigwangalla@gmail.com>;
To: wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>;
Subject: Re: [wanabidii] KUB Freeman Mbowe Vs NS Job Ndugai: Kushindwa kwa Uongo baada ya kweli kufahamika!
Sent: Wed, Oct 2, 2013 7:08:38 AM

Ezekiel,

Ni kweli lakini wapo wenye wajibu wa kutoa maelezo hayo sema hawatoi tu. Mimi nimeandika kwa utashi wangu kwa faida ya kuweka sawa kumbukumbu tu.


On Wed, Oct 2, 2013 at 9:03 AM, ezekiel kunyaranyara <ekunyaranyara@yahoo.co.uk> wrote:

Dr, HK

Maelezo haaya yaaanaeleweka na yanaweka ukweli bayana lakini mnachhelewa sana kuyatoa hadi sumu inaenea kabisa katika vichwa vya watu. Sijui kama mnaweza kiondoa kirahisi sumu hii.

Sent from Yahoo! Mail on Android



From: fadhil fadhil <fadhil.fadhil96@gmail.com>;
To: <wanabidii@googlegroups.com>;
Subject: Re: [wanabidii] KUB Freeman Mbowe Vs NS Job Ndugai: Kushindwa kwa Uongo baada ya kweli kufahamika!
Sent: Tue, Oct 1, 2013 6:02:02 PM

Nashukuru kwa ufanuzi, tatizo letu wengi wetu hatujui kanuni za
mijadala ya bungu huwa tunakurupuka kama alivyokurupuka mhe. Mbowe,
Siku za nyuma niliwahi kusema Katika wabunge wa Upinzani Bungeni,
Namkubali Zito na kafulila na Machali wa NCCR huwa hawana kawaida ya
kukurupuka

On 10/1/13, Dr. Hamisi A. Kigwangalla <hkigwangalla@gmail.com> wrote:
> KUB Freeman Mbowe Vs NS Job Ndugai: Kushindwa Kwa Uongo baada ya kweli
> kufahamika!
>
> *Imeandikwa na Dkt. Hamisi Kigwangalla, MB*
>
> * *
>
> Leo nimeamka na mzuka wa kuandika. Kwanza nasukumwa na kuandika kuhusu
> ukweli, zaidi kwa kuwa nafurahia kuandika maneno yanayofanana na yale
> yaliyosemwa na mwandishi nguli wa Kiswahili, babu yangu Shaaban Robert,
> ambaye kazi zake hazitokuja kufubaa vizazi na vizazi, nikizifananisha na
> zile za William Shakespeare, mwandishi mashuhuri wa mashairi na fasihi
> simulizi wa Uingereza ya karne ya 16. Lakini pia nafurahi kuandika kuhusu
> dhana ya ukweli ambayo mimi daima naisimamia na nitaifia itapobidi.
>
> Hayati Shaaban Robert anaandika hivi katika kitabu chake cha Kusadikika:
> 'Msema kweli huchukiwa na marafiki zake. Nikipatwa na ajali kama hiyo,
> sitaona wivu juu ya wale wawezao kudumu na marafiki zao siku zote. Siwezi
> kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya
> milele itakayotokea pale uongo utakaposhindwa.'
>
> Nimeazima hekima hizi kutoka kwa Shaaban Robert kwa lengo la kutaka
> kuzungumza ukweli, maana ukweli una tabia nyingi sana na kubwa niipendayo
> mimi ni ile ya kutobadilika badilika. Ukweli hubaki ukweli hata kama
> utaishi miaka dahari, utabaki kuwa kweli tu. Nimependa leo kujadili jambo
> hili kwa sababu kwanza lilileta aibu kubwa kwa bunge letu, pili mijadala
> iliyofuatia baada ya jambo hili ilileta taswira ya kuonewa na kukandamizwa
> kwa upinzani kwa kuzibwa mdomo, na tatu kwa kuwa iliongeza nguvu kwa
> wapinzani bungeni kudumu katika kususia kushiriki mjadala wa hoja ya
> muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba iliyokuwa ikijadiliwa. Yote haya
> naona yanapelekea kutuondoa kwenye mtindo wa 'muafaka' wa pamoja kwenye
> mchakato wa kuandika upya katiba yetu tuliokuwa tukiendelea nao.
>
> Nitaomba nitumie kanuni za bunge kujenga hoja yangu. Nianze na ile kanuni
> ya 60 (1.) ambayo inatoa maelekezo ni wakati gani mbunge atapata muda wa
> kusema bungeni, inasema: ' Mbunge akitaka kusema bungeni anaweza:- (a)
> kumpelekea spika ombi la maandishi; (b) kusimama kimya mahali pake; na (c)
> kutumbukiza kadi ya elektroniki.' Mhe. Mbowe aliposimama bungeni alitumia
> kanuni hii kwenye ile fasili ndogo ya (b). Lakini ukisoma kanuni hiyo hiyo
> ya 60 ile fasili ya pili inasema 'isipokuwa kwamba, Mbunge yeyote hataanza
> kuzungumza hadi aitwe na spika ama kwa jina ama kwa wadhifa wake na
> kumruhusu kusema…' Hivyo Mhe. Ndugai (NS) alimuona Mhe. Mbowe lakini
> hakumruhusu kusema, na kwa mujibu wa kanuni hii alikuwa kwenye mamlaka ya
> kuamua aidha kumruhusu ama kutomruhusu.
>
> Mbowe anataka kuzungumza baada ya hoja kuafanyiwa maamuzi, anazungumza nini
> tena? Anataka kura zipigwe kwa mara nyingine ya pili tena ama anataka
> kuanzisha upya mjadala wa hoja iliyofungwa? Anasimama kwa kanuni gani,
> maana kanuni ambayo ingeweza kumpa fursa ya kuzungumza ilikuwa ni ile ya
> 'kuhusu utaratibu' tu, lakini kwa mujibu wa taarifa rasmi ya majadiliano ya
> bunge (hansard) za siku hiyo, aliposimama Mhe. Mbowe (KUB) hakusema 'kuhusu
> utaratibu'. Kanuni ya 68 (1.) inasema hivi: 'Mbunge anaweza kusimama wakati
> wowote na kusema maneno *"kuhusu utaratibu"*, ambapo Mbunge yeyote ambaye
> wakati huo atakuwa anasema atanyamaza na kukaa chini na Spika atamtaka
> Mbunge aliyedai utaratibu ataje kanuni au sehemu ya kanuni iliyokiukwa.'
> Kwa mujibu wa taarifa rasmi za majadiliano ya bunge (hansard), Mhe. Mbowe
> (KUB) hakutamka neno hili na kwa maana hiyo hakukusudia kulielekeza Bunge
> kuhusiana na kanuni yoyote ya bunge iliyokiukwa. Na pia hakukuwa na Mbunge
> yeyote yule aliyekuwa akisema kwa wakati ule hivyo matumizi ya kanuni hiyo
> hayakuwa 'warranted'.
>
> Aghalabu angeweza kutumia kanuni ya 63 (3.) inayoruhusu Mbunge yeyote yule
> kusimama na kutamka maneno 'kuhusu utaratibu'  kama angekuwepo Mbunge
> anayesema kwa wakati ule, lakini bahati mbaya sana hakuwepo Mbunge yeyote
> aliyekuwa akisema wakati ule. Kumbukumbu rasmi za bunge (hansard)
> zinaonesha kuwa ndiyo kwanza tulikuwa tumemaliza kupiga kura na Mhe. Ndugai
> (NS) ndiyo alikuwa amemuita tu Mbunge wa Vunjo, Mhe. Augustino Lyatonga
> Mrema azungumze, naye hakuwa amezungumza lolote lile. Kipengele hiki cha
> kanuni hii huwa kinatumika bungeni kwa ajili ya kumkosoa Mbunge aliyesema
> uongo ili kuweka kumbukumbu sawia. Kwa kuwa hakuna aliyekuwa amesema lolote
> lile, maana yake hakukuwa na taarifa za uongo zilizosemwa bungeni na
> yeyote, hivyo kipengele hiki hakikuwa na nafasi. Hivyo kanuni hii pia
> isingeweza kutumika kumpa ulazima wa yeye kupewa fursa ya kusema bungeni
> kwa wakati ule.
>
> Kanuni nyingine ambayo ingeweza kumpa nafasi ya kuzungumza ilipaswa kuwa
> ile ya 'taarifa'; hii ni kanuni ya 68 (8.) ambayo inasema: 'vile vile
> Mbunge yeyote anaweza kusimama mahali pake na kusema *"taarifa"* na kwa
> ruhusa ya Spika, atatoa taarifa au ufafanuzi kwa Mbunge anayesema….' Jambo
> la kwanza Mhe. Mbowe (KUB) hakusema neno hili, kwa mujibu wa taarifa rasmi
> za bunge (hansard) na la pili hakukuwa na mbunge mwingine aliyekuwa akisema
> wakati ule hivyo hakukuwa na mtu yeyote ambaye alihitaji taarifa ya Mhe.
> Mbowe.
>
> Kilichokuwepo bungeni kwa wakati ule ni kuwa, bunge lilikuwa limemaliza tu
> kuifanyia kazi na hatimaye kuifanyia uamuzi hoja ya Mhe. John Mnyika (Mb.)
> iliyotaka kura zihesabiwe na ikapita na hivyo kura zilihesabiwa.
>
> Nimeitazama kanuni ya 68 (7.) labda kama ilitumika, lakini wapi! Kanuni hii
> inasema: 'hali kadhalika, Mbunge  anaweza kusimama wakati wowote ambapo
> hakuna Mbunge mwingine anayesema na kuomba *"mwongozo wa Spika" * kuhusu
> jambo ambalo limetokea bungeni mapema, ili Spika atoe ufafanuzi kama jambo
> hilo linaruhusiwa au haliruhusiwi kwa mujibu wa kanuni na taratibu za Bunge
> na majibu ya Spika yatatolewa papo hapo au baadaye, kadri atakavyoona
> inafaa.'  Kwa bahati mbaya sana Mhe. Mbowe (KUB) pia hakutumia kanuni hii,
> kwa kutotamka maneno haya kama ambavyo taarifa rasmi za majadiliano bungeni
> (hansard) za siku hiyo zinavyosema.
>
> Kumpa nafasi ya kusema Mhe. Mbowe ingekuwa ni sawa na kudharau Bunge zima
> ambalo lilikwishafanya maamuzi kwa njia ya kura kuhusiana na hoja ya kutaka
> uamuzi wa kukataa hoja ya Mhe. Mnyika ufanywe kwa njia ya kura. Wakati
> naandika hapa nimefanya utafiti wa kutosha kwa upeo wa macho yangu na uwezo
> wangu na nimejiridhisha kabisa, bila shaka yoyote ile kuwa, hakukuwa na
> nafasi yoyote ile ya kikanuni ya kutoa fursa ya Mbunge yeyote yule
> kulijadili jambo ambalo lilikwishafanyiwa uamuzi na bunge zima. Na kama
> Mhe. Mbowe (KUB) alikuwa anataka kuleta mezani hoja mpya hakukuwa na sababu
> ya kuwa na wasiwasi maana tayari Mhe. Ndugai (NS) alikwishaingiza kwenye
> kumbukumbu kuwa alikwishamuona, na kwa mujibu wa kanuni za bunge angempa
> nafasi ya kusema baadaye. Katika hali ya kawaida, Mhe. Mbowe (KUB) alipaswa
> kukaa chini na kusubiri ni wakati gani angeitwa apewe fursa yake ya kusema.
> Hakuna kumbukumbu yoyote ile inayosema kwamba Mhe. Mbowe (KUB) alikuwa na
> hoja ya dharura na hata baada ya bunge hatujashuhudia jambo lolote lile la
> dharura lililotokea.
>
> Kanuni ya 5 ya bunge inampa Spika mamlaka ya kuwa na maamuzi ya mwisho
> kwenye jambo lolote kwenye mijadala ya Bungeni, na hii ni kwa mujibu wa
> ibara ya 84 ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania. Pia kanuni hiyo
> hiyo ya 5, ile fasili ya (4) mpaka ya (6), inatoa fursa kwa Mbunge yeyote
> ambaye hakuridhika na uamuzi wa kiti (NS kwa niaba ya Spika) kukata rufaa
> dhidi ya uamuzi huo. Hivyo, badala ya Mhe. Mbowe (KUB) kulazimika
> kung'ang'aniza kiti kimpe nafasi ya kusema bungeni angeweza kukaa
> akasubiria kufuata utaratibu wa kukata rufaa unaowekwa na kanuni hii.
>
> Kwa heshima ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni na kwa kuzingatia ukweli kwamba
> katika mfumo wa demokrasia yoyote ile iliyokomaa, sauti ya wachache ni
> lazima ipewe fursa ya kusikika zaidi kuliko hata ya wengi. Pengine ni dhana
> hii iliyopelekea Spika kuamua kumpa haki ya kwanza ya kusema Kiongozi wa
> Upinzani Bungeni kila mara anapokuwa ameonesha nia ya kufanya hivyo kwenye
> hoja yoyote ile bungeni. Pia pengine ndiyo maana KUB amekuwa akipewa
> kipaumbele cha kuuliza swali la kwanza kwenye kipindi cha maswali ya papo
> kwa papo kwa Waziri Mkuu. Pengine. Lakini kwa mujibu wa kanuni za Bunge
> zinazotumika sasa, sijaona mahali popote pale kwenye kanuni hizi ambapo KUB
> anapaswa kupewa nafasi ya upendeleo kwenye kusema bungeni. Sijaona. Napata
> hisia kwamba pengine KUB alitaka kujifananisha na KUB wa Bunge la
> Uingereza, ambaye ana mamlaka tofauti na KUB wa bunge letu.
>
> Rai yangu kwa watanzania wenzangu wote ni kuwa, tuepuke tabia ya kupuuza
> ukweli na kuatamia uongo. Ama kushabikia uongo. Kufanya hivyo ni kuchukua
> hatua za haraka kuelekea kuondoa mtangamano wa kitaifa na kuvuruga amani,
> upendo na mshikamano wetu. Watanzania tuwe makini tuepuke vitendo vyote
> vinavyotishia kulegalega kwa tunu hizi. Tusikubali kuacha mbachao kwa msala
> upitao. Tutakuja kujuta tukiendelea kuushadadia uongo na kufurahia matunda
> ya zao la uongo la muda mfupi , kisha siku kweli ikidhihiri tutaambulia
> aibu na majuto na masikitiko ya milele.
>
>  Ukweli una hii tabia nyingine ambayo mimi naihusudu sana; hii ni ile tabia
> ya kuwa ukweli haupendi kupuuzwa puuzwa. Ukweli unapenda usemwe na utatoa
> faida yake, na ukipuuzwa tu siku moja utadhihiri na itakuwa tumechelewa.
> Huu ni ushauri wangu wa wazi kwa watanzania wenzangu wote kuwa tudumu
> kwenye ukweli bila kutazama itikadi zetu na tusiupuuze ukweli kwa kuchelea
> aibu ya muda tukajinyima faida ya kudumu itokanayo na kweli.
>
> Yeyote atakayeamua kufuatilia kanuni zetu za bunge na akasoma kumbukumbu za
> taarifa rasmi za majadiliano ya bunge, naamini, atakubaliana na mimi kuwa
> hakuna uonevu uliokuwepo, wala hakuna mabavu yaliyotumika katika kumnyima
> nafasi ya kusema bungeni Mhe. Mbowe (KUB). Tunatofautiana hisia lakini
> ukweli kwa faida ya ukweli utabaki pale pale.
>
> Dkt. Hamisi Kigwangalla, MB ni Mbunge wa Jimbo la Nzega na pia ni
> Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za
> Mitaa (TAMISEMI). Ni mhitimu wa Digrii ya Udaktari wa Tiba za Binadamu,
> Shahada za uzamili kwenye Afya ya Jamii (MPH) na kwenye Usimamizi wa
> Biashara (MBA). Kwa sasa anaandika tasnifu yake ya digrii ya Uzamivu(PH.D.)
> kwenye Afya ya jamii (mifumo ya usawa na uchumi wa afya).
>
>
> --
> "Vision is the ability to see the invisible!"
> Hamisi A. Kigwangalla, MD, MPH, MBA
> P.O.Box 22499,
> Dar es salaam.
> Tanzania.
> Phone No: +255 754 636963
>                +255 782 636963
> website: www.peercorpstrust.org or www.hamisikigwangalla.com
> Email: hamisi.kigwangalla@peercorpstrust.org or info@hamisikigwangalla.com
> Skype ID: hkigwangalla
> Blog: blog.hamisikigwangalla.com
>
> --
> Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha
> ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal
> consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be
> presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to
> this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
> ---
> You received this message because you are subscribed to the Google Groups
> "Wanabidii" group.
> To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an
> email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
> For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
>

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.



--
"Vision is the ability to see the invisible!"
Hamisi A. Kigwangalla, MD, MPH, MBA
P.O.Box 22499,
Dar es salaam.
Tanzania.
Phone No: +255 754 636963
                +255 782 636963
website: www.peercorpstrust.org or www.hamisikigwangalla.com
Email: hamisi.kigwangalla@peercorpstrust.org or info@hamisikigwangalla.com
Skype ID: hkigwangalla
Blog: blog.hamisikigwangalla.com 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

0 comments:

Post a Comment