Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) inapenda kuufahamisha umma kuwa kuanzia tarehe 1 Juni, 2013, SUMATRA ilianza kutoa leseni za kusafirisha abiria kwa magari yenye uwezo wa kubeba abiria kuanzia 7 hadi 14 (kama ya NOAH).
Hatua hii imefikiwa na SUMATRA ili kuimarisha udhibiti katika sekta hii ya usafiri ambapo huduma ya usafirishaji abiria kwa kutumia mabasi madogo yanayobeba abiria kuanzia 7 hadi 14 yanatoa huduma bora, salama na yanakidhi viwango.
Aidha hatua hii imekusudiwa kusaidia wamiliki kufanya biashara ya usafirishaji kwa weledi na ufanisi zaidi na
Hatua hii imefikiwa na SUMATRA ili kuimarisha udhibiti katika sekta hii ya usafiri ambapo huduma ya usafirishaji abiria kwa kutumia mabasi madogo yanayobeba abiria kuanzia 7 hadi 14 yanatoa huduma bora, salama na yanakidhi viwango.
Aidha hatua hii imekusudiwa kusaidia wamiliki kufanya biashara ya usafirishaji kwa weledi na ufanisi zaidi na
mdhibiti kuwasimamia watoa huduma hao na hivyo kuimarisha shughuli za udhibiti ili kuwa na usafiri bora na salama kwa wananchi wa Tanzania.
Ili kufanikisha utoaji leseni kwa ajili ya usafirishaji wa abiria, wamiliki wa magari hayo ambayo yanajumuisha
magari aina ya NOAH wameelekezwa kuzingatia yafuatayo:
SUMATRA itatoa leseni ya usafirishaji wa abiria baada ya mmiliki wa gari husika kukamilisha matakwa yote yaliyotolewa hapo juu.
Tungependa wananchi na wadau kwa ujumla waelewe kwamba, leseni ni nyenzo muhimu ya udhibiti.
Faida za leseni ya usafirishaji ni pamoja na:
Hivyo tunatoa wito kwa watoa huduma kukata leseni ya usafirishaji ili waweze kufaidika na faida zilizotajwa hapo juu.
SUMATRA imekuwa ikifanya kazi karibu sana na Jeshi la Polisi kama msimamizi mkuu wa utekelezaji wa Sheria hapa nchini. Pale ambapo taarifa za Polisi zinapothibitisha ukiukwaji wa sheria, hatua za kisheria huchukuliwa na mdhibiti (SUMATRA).
Kutokana na hali hii tunapenda kuwafahamisha wamiliki wa mabasi madogo ya abiria 7 hadi 14 na umma kwa ujumla kuwa SUMATRA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani watafanya ukaguzi kwa magari yote yasiyo na leseni za usafirishaji ili kuhakikisha mabasi yote yanayotoa huduma ya usafiri kwa umma yana leseni halali ya usafirishaji abiria na kufuata Sheria, Kanuni na Masharti yote yaliyobainishwa katika leseni hiyo.
Ni vyema wamiliki wa vyombo vya usafiri hususan wa mabasi madogo kuzingatia na kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo kwa ajili ya maslahi ya muda mrefu na yenye tija kwao kama watoa huduma na kwa sekta ya usafirishaji abiria hapa nchini.
Kwa kushirikiana tunaweza kuwa na usafiri bora na salama!
Imetolewa na:
Meneja Mawasiliano
SUMATRA
Juni, 2013
Ili kufanikisha utoaji leseni kwa ajili ya usafirishaji wa abiria, wamiliki wa magari hayo ambayo yanajumuisha
magari aina ya NOAH wameelekezwa kuzingatia yafuatayo:
SUMATRA itatoa leseni ya usafirishaji wa abiria baada ya mmiliki wa gari husika kukamilisha matakwa yote yaliyotolewa hapo juu.
Tungependa wananchi na wadau kwa ujumla waelewe kwamba, leseni ni nyenzo muhimu ya udhibiti.
Faida za leseni ya usafirishaji ni pamoja na:
Hivyo tunatoa wito kwa watoa huduma kukata leseni ya usafirishaji ili waweze kufaidika na faida zilizotajwa hapo juu.
SUMATRA imekuwa ikifanya kazi karibu sana na Jeshi la Polisi kama msimamizi mkuu wa utekelezaji wa Sheria hapa nchini. Pale ambapo taarifa za Polisi zinapothibitisha ukiukwaji wa sheria, hatua za kisheria huchukuliwa na mdhibiti (SUMATRA).
Kutokana na hali hii tunapenda kuwafahamisha wamiliki wa mabasi madogo ya abiria 7 hadi 14 na umma kwa ujumla kuwa SUMATRA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani watafanya ukaguzi kwa magari yote yasiyo na leseni za usafirishaji ili kuhakikisha mabasi yote yanayotoa huduma ya usafiri kwa umma yana leseni halali ya usafirishaji abiria na kufuata Sheria, Kanuni na Masharti yote yaliyobainishwa katika leseni hiyo.
Ni vyema wamiliki wa vyombo vya usafiri hususan wa mabasi madogo kuzingatia na kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo kwa ajili ya maslahi ya muda mrefu na yenye tija kwao kama watoa huduma na kwa sekta ya usafirishaji abiria hapa nchini.
Kwa kushirikiana tunaweza kuwa na usafiri bora na salama!
Imetolewa na:
Meneja Mawasiliano
SUMATRA
Juni, 2013
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment