Huko Wazo Hill-Itakuwa kuna mtu mkubwa mmojawapo binafsi au yupo ndani ya kiwanda cha saruji kwa sasa anataka kupora hizo nyumba na maeneo hayo ili ajenge chuo, secondary au maghorofa ya kupangisha ajilie kuku. Serikali isipoangalia itaingia katika migogoro mingi ya ardhi kwa sasa na hadi baadae. Mfano-mashamba ya mikonge ambayo hayalimwi na baadhi ya wananchi wameruhusiwa kulima mazao ya chakula bila ya kujenga nyumba au kupanda mazao ya kudumu kama minazi etc. Wananchi ktk baadhi ya maeneo ya mashamba haya yaliyokuwa GVt estates wamejenga nyumba za kudumu, wamepanda minazi, miembe etc na wameishi miaka mingi. Watoto wao wanafahamu au kufikiria ni customary land yao. Pia, waliokuwa wakiishi ktk nyumba za mikonge toka ukoloni ambao bado wapo na nyumba za NHC ktk townships, za railway station bado karne wamo na wazazi wamefariki ila familia za watoto na wajukuu wamo na wanadhania ni nyumba/mali ya mzazi wao. Mamlaka ya minazi, kahawa, TZRS zina facilities ambapo tume tunaishi tumejisahau. Wapo ambao maeneo yalikuwa ya makampuni kama Benanco Kunduchi wameuza kwa watu binafsi ambao wamejenga nyumba. Utaona wanabomolewa lakini anatokea mtu tapeli anapauza tena, muhusika anakuja kubomolewa tena na tapeli ameondoka amekwisha kula hela. Maeneo ya mashamba ya katani mfano Mbwewe-Segera-Mwakiyumbi, Hale-Tanga kuna baadhi ya vijiji vimepewa maeneo ya mashamba ya katani na GVT kwa ajili ya makazi na kilimo. Lakini unakuta wenyeji badala ya kulima mashamba na kutumia ardhi kujenga nyumba ya kudumu yake-anauza maeneo yote kunajengwa nyumba anakosa shamba la kulima. Yupo kijijini lakini hana shamba la kulima. Aliyekuja kununua si mkazi ametoka mbali amejenga nyumba amepangisha. Anarudi tu kukusanya kodi toka huko atokako. Naye huyo mwenyeji alikuja manamba toka ukoloni kazeekea hapo alitoka Mbeya, Songea harudi tena kwao na ardhi kauza akijifanya ataondoka arudi kwao, anajikuta kamaliza hela. Au hata kama akienda kwao, baada ya muda anarudi anajikuta huko kwao hajakuzoea tena anaona tabu au roots zilikwisha kupotea hana msingi wa maisha, anarudi anajikuta ni masikini kijijini ambapo kuna raslimali ambapo yeye alimaliza kuziuza. Anaanza kujenga barabarani na kuja kuvunjiwa tena. Wapo waliopimiwa barabarani enzi za ujamaa vijijini wakitolewa vitongoji vya mbali na kupangwa kama train barabarani ili kuwa karibu na huduma za jamii. Hivi sasa nyumba zote hizo zina X kuonyesha zinataka zibomolewe. Hapo walipangwa na GVT. Italiwa wangapi nchi nzima. Land use planning na land evaluation na mipango kisiasa tulikotokea ilikuwa ina vision fupi sasa-tatizo la fidia kila kona. Ktk baadhi ya mashamba ya katani yenye katani nzee na misitu wamehamia wafugaji na mifugo yao ambayo nayo inakula mazao ya wanaolima ktk mashamba ambayo yapo idle. Pale ambapo Mikonge hiyo ipo ambapo wananchi wameruhusiwa kulima mazao ya chakula ktk ya mistari ya mkonge wakisaidia kufanya usafi wa shamba, sio wote wanatumia nafasi hii nzuri. Baadhi hupanda mazao yasiyomea vizuri kutokana na ardhi ilivyo na ukame na hawashauriki kuwa usipande mahindi bali ufuta na mtama. Uza haya mazao ununue mahindi kuliko kupanda mahindi ukose kabisa kila mwaka na msimu-haipambi, hakieleweki. lakini miaka ya karne za nyuma ulikuwa unapita unaona mtama mrefu na ufuta hiyo Chalinze-Mbwewe na sasa kuna mtama mfupi na ulioliwa na ndege-hataki. Sasa-mahindi ni luxury food. Na viongozi wa vijiji wala rushwa waliouzia wafugaji mashamba ya mamlaka ya katani etc ambao wamelipa hela za rusha na kuhamia humo msituni-tatizo lingine la mapambano baadae. Mtoa rushwa na mpokea rushwa wote manzamane. Elimu kwa umma kuhusu ardhi, kuzingatia sheria ya ardhi ni muhimu kwani kutakuja kujiingiza katika umasikini mkubwa kwa kubomolewa ikiwa unanunua kwa rushwa, kuibia watu mali na kujenga pasipo ruhusiwa; kustaafu kulipwa mafao na kubakia hapo ukaja kutesa watoto watakapokuja kufukuzwa ktk nyumba ya mwajiri. Tanzania ipate onyo pia ktk mipango miji kuhakikisha ramani ya mipango miji inazingatiwa na environmental management ethics. Watu wanajenga 100% ya plot kuweka mzigo ktk ardhi na huduma, kubananisha magengo kiasi kwamba moto ukiwaka hakuna pa kupita kuzima na hatuna helikopta ya zima moto. bado hata baada ya majengo kuungua wananchi wanakuwa blind-wanarudia kujenga hivyo hivyo kubananisha majengo na kuchanganya matumizi yasioruhusiwa kuchanganywa-duka la sawa jirani na saluni na welding workshop ya vyuma itoayo cheche, nyama choma restaurant jirani na duka la mitungi ya gas na duka la madawa ya kilimo na mifugo na jirani na transfoma ya umeme etc. Tunaona bali ni vipofu. Majanga yakitokea-lawama. Unaona kuna ujenzi wa nyumba ya ghorofa-unapanga biashara hapo chini na kupaki gari. Likiporomoka jiwe au bamba zito la simenti na kukukata mguu, kuvunja gari-inakula kwako kwani hukuona? Tukielekezwa-sugu, viziwi. Siasa zimetujaa kuliko utendaji na uthubutu wa kukemea haya ktk maeneo yetu. Moto utaendelea kuwaka mijini na gharama zitaendelea kutumaliza, kubomoleana na kesi mahakamani hazitakwisha na zitamaliza muda na resources chache tulizonazo. --- On Sat, 8/6/13, Abdalah Hamis <hamisznz@gmail.com> wrote:
|
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment