Tuesday 4 June 2013

Re: [wanabidii] KONGAMANO LA WAISILAMU JIJINI DAR, Sheikh Ponda aunguruma, Awasihi waisilamu kuwa na umoja, Nuru inakaribia.


Nijuavyo mimi-Kazi au wajibu wa serikali ni kuongoza na kuwezesha. Kuna Katiba halafu vitu vya misingi (principles) zilizomo ktk Katiba huingia katika Sera. sera hutekelezwa kwa kuundiwa Mikakati ya Sekta (strategies) ambazo huwa na mpako kazi wenye malengo, shughuli na viashiria na bajeti ambayo hupitishwa na bunge. Halafu yote hayo principles na sera hulindwa na Sheria ya sekta hiyo husika-mfano Haki za binadamu (sheria ya ndoa, mirathi; sheria ya mtoto etc). Kuna sheria ya ardhi nayo hutaja haki; sheria ya misitu, wanyamapori, marine parks, bahari na uvuvi; mifugo; madini; mazingira; maji; usafi wa mazingira, afya, uraia etc.

Lakini waswahili husema-unaweza kumswaga Punda mpaka mtoni ila huwezi kumlazimisha-kunywa Maji. Weka sera, mikakati na Vision (Dira) zake; weka sheria mfano sheria itambue uwepo wa imani wa kuabudu na dini tofauti hata za kimila; itambue na ardhi ya kimila. Kwa Mtanzania (binadamu) vyote hivi vinapinda au kupindishwa.

Unamuongoza mtu na kumwambia-elimu ni ufunguo wa maisha-soma usiozeshe mapema; ukimwi unaua usiwe na mpenzi zaidi ya mmoja (sikio la kufa anaoa mitala eti dini inaruhusu na ana vimada na wakezake wana mabwana pia); panda mti ukatapo mti (anachimbua mti hadi mizizi) hapandi; fuga mifugo kisasa, punguza mifugo unaharibu mazingira unayotegemea umezidisha beyond carrying capacity kwamba ardhi haiongezeki bali watu na wanyama huongezeka. Unaweka ni nvyuo vya  kilimo, vya mifugo na mifano ya mifugo na kilimo cha mazao, unawapeleka study tour, una extension staff wa kuwaelekeza. Watakaoiga 1 kati ta 10 na huyo mmoja watamuibia. Kuwa na mingi ni cultural definition ya wealthy class hiyo ndio priority. Unawaeleza kuwa -Eneo hili ni la kulima mtama mtama sio mahindi ukilima utakosa chakula-Lima mtama na ufuta ni almasi uuze ununue mahindi na mchele. Analima ekari na ekari za mahindi na mpunga-anakosa kabisa. Kisha-serikali haitujali kutupa chakula cha misaada cha njaa-kila mwaka atalima hilo hilo bado. Na wale wamabondeni-mafuriko hadi kila mwaka na kupoteza familia na mali-sihami au nitahama nikilipwa fidia-alikuambia nani ukae bondeni? wakipewa kiwanja na mabati wajenge-anauza plot na mabati na hema linachoka linaishia anakuwa na tabu zaidi-anarudi bondeni. Mifano michache ya kuwajibika. Jee uwachape fimbo watu wazima? uwafunge-jela kubwa kiasi gani unayo na kuweza kuwalisha daily? Pita vijijini uone-utalia kama unaipenda nchi yako.

Unaambiwa usivue kwa baruti unaharibu mazalia ya samaki-miamba na mazingira yake; vua kwa nyavu tundu kubwa-hataki; chandarua kuzuia malaria, lalia daily-anaokotea chupa tupu, anafunikia mchicha-halalii anaogopa kupungua nguvu za ulijari. unamwelimisha, kumuwezesha, kuweka vikoba, mikopo, leseni za wazawa vheap-hajiungi kkt vikundi; anaua albino na kukata watu viungo atajirike sio mikopo usemayo na kujiunga. Umfanye nini?


Haki zako ni wajibu wako pia. Huwezi kudai haki ikiwa hutimizi wajibu. Serikali ni nani?
Mfanyakazi serikalini ni mwanao, nduguyo, jirani yako. Ni yule unayetoa kodi akalipwa ujira, akawa mwizi wa mali ya umma katika umri mdogo maana anapenda anasa, anayemlipa fidia anayebomolewa nyumba ipite barabara kizee wa watu anatakiwa alipwe milioni 20 yeye anampa milioni 2. anayetoa plot moja kwa watu zaidi ya mmoja; anayefungua zahanati akapeleka dawa za CHF huko na akikamatwa unamuwekea wakili na mnajazana mahakamani kusikiliza kesi. Ni yule anayempa mimba mwanafunzi akiwa bosi halafu mzazi unafuta kesi unachukua kitu kidogo. Hapa nawe ni serikali maana unatakiwa usimamie utendaji bora kama mwananchi na sheria ya ubakaji ipo ale miaka 35 wewe unakubali kupokea milioni 5 na huitumii kimaendeleo. Unapompigia kura kiongozi anayeshutumiwa kwa ufisadi, udini, ukabila na anashinda kura-haki yako na wajibu wako umeuharibu na umeharibu majukumu ya viongozi na watawala wa serikalini ambao wanausimamizi mwema hawapendi uovu. Ukimlinda mtumishi kibaka hata awe mumeo, mkeo, mwanao unaona anafanya magendo, ananunua magari kibao kazi kaanza jana-unaficha mwizi hutimizi wajibu wako. Kwani serikali ni nani na raia ni nani? Mbona mkuu wa wilaya, mratibu kata, bwana/bibi kilimo ni mume/mke na ndugu wa mtu? Mbona wakikosea nyumbani hatuwaweki kitako kifamilia au kimila wajirekebishe mpaka wanafungwa? Tunalindana. Mbona ukeketaji wasichana unaendelea ndani ya familia Kisiri-tunakiuka haki na sheria iliyopo baba na mama na ndugu? Yatima anadhulumu nani na sheria iliyotungwa ba serikali kuhusu mirathi ipo? serikali ni wewe, mimi (Raia) na walioajiriwa na kuchaguliwa, viongozi wa mila na dini, wote tunawajibika. Kiongozi uwe mfano Jimboni kwako  kwanza na kijiji chapo kiwe super tuje tujifunze huko sio kupiga kelele tu bungeni, vijijini maeneo yako kila kitu kipo hakuna lolote ufanyalo kuhamasisha kikaonekana. Tukifika 50% hawana vyoo, maji wanakoga hapo hapo, kufua na kuchota. wakichanga elfu 2 kijiji chote kila mtu utapata hela za kuchimba borehole kadhaa ukaweka handpumps-hufanyi hivyo ila-maandamano! ushindwe na ulegee kiongozi wa namna hiyo.
kama mtumishi wa umma na wa GVT- Wajibika

Raia asipozingatia sheria mfano ya ujenzi, viwanja vinapimwa, anabananisha nyumba na kuziba njia eti anaganga njaa-mji unakuwa makorokoro. Kisha moto ukiwaka, njia ya kupita kuzima moto hakuna-inakula kwake. anapata hasara na asipojirekebisha-utawaka kila mara na kumrudisha kimaendeleo. anaona hapo jirani kunauzwa gas, kuna pharmacy na viripuka, kuna kuranda mbao na vyumbi la mbao, yeye hapo jirani anaweka welding ya vyuma inayorusha cheche za moto. haoni au haujui moto? Mtu mzima aonyeshwe mifano mingapi ya moto na kufa mbona anaiona. kiziwi na kipofu. Ikija timu ya kubomoa-wanatoka na mapanga, pakiungua-serikali haina wajibu kwa raia, haitimizi wajibu wa usalama kwa raia wake? Kichwa hicho kizima?

Nawashangaa hata wanawake, mume au bwana kabaka mwanae wa kuzaa au mtoto wa kambo-msameheni mume wangu, tutakula wapi. Hili kwanza ni kosa lake la kwanza. anafanya mbinu kufuta na kukana ushahidi atoao mtoto, wanahonga wapimaji watoe vithibitisho sivyo. doctor wa awali kaandika alibakwa na uthibitisho, wa majuu anaonyesha vingine kinyume. haangalii kuathirika kwa mtoto ila pensi na kula ambapo anaweza kujitegemea. Na mume akitoka hapo-anawakimbia anahamia mbali.

Mjini Shule-tunasomeshana kila mtu na msimamo wake, wangu ni huu.


--- On Tue, 4/6/13, Rashid Maalim <rashid.o.maalim@gmail.com> wrote:

From: Rashid Maalim <rashid.o.maalim@gmail.com>
Subject: Re: [wanabidii] KONGAMANO LA WAISILAMU JIJINI DAR, Sheikh Ponda aunguruma, Awasihi waisilamu kuwa na umoja, Nuru inakaribia.
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Tuesday, 4 June, 2013, 12:51

Hivi  rafiki  yangu unaweza kuniambia   unavyo jua  wewe  Kazi na  wajibu  wa  Serikali  kwa  Raia  wake?


2013/6/4 Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>


Nimekupata Rashid Maalim lakini- Ila ninasema, tunayo mifano mizuri nchini-Tuige wachaga wanajituma!! Hawa, hawachagui kazi na wana ushindani.
Usiniambie mzalisha kahawa (mchaga) anasomesha ila Mkusuma wa Mwanza mwenye ng'ombe 100, mbuzi 500, kondoo 50 na kuku kibao, samaki anavua kisha hasomeshi anaoza tu ili aongeze mifugo kuwa anaonewa. Vivyo hivyo kwa wafugaji wengine ambao wingi wa mifugo yao inatutesa wilaya mbali mbali wanasafiri huko na huko kulisha mashamba, watoto hawasomi kuwa-wanaonewa!! 

Msukuma amevuna dhahau toka ukoloni akija nazo DSM kabla ya Uhuru akijaza ktk Chupa kama vile anapeleka uji kwa mgonjwa muhimbili.  Wahindi, Waarabu, Baniani, Goa, Bohora, Baluchi wametajirika kwa dhahabu crude ya kutoka Mkoa wa mwanza wakiwa na viwanda vya usonara mijini gold nzito ya ulaya imesingiziwa.  Walioweka maduka ya dhahabu na waliokuwa na utajiri mkubwa wengi wameweza kuwa na maduka makubwa, viwanda kutokana na madini haya halafu vipusa pamoja na memo ya tembo. Operation Uhai ilirudisha nyuma matatiri wengi hasa Waarabu wa Tanga, Kilosa, Dar na Morogoro kwani vipusa viliwatajirisha sana malori ya mizigo na biashara zao zililala.

Niambie msukuma kajenga viwanda vipi kwa dhahabu na almasi aliokuwa akiuza kwa mlango wa nyuma? Huyo kaongeza ng'ombe, wake na watoto.

Goa, Mwarabu, Mhindi au Wajamii ya Asia wamepeleka kwao vito kupitia nduguzao huko wanauza dhahabu nzito makwao na wana maduka makubwa. Enzi hizo airport husachiwi sana mama wa kihindi anazivaa ndani na nje anapeta.

Mmasai anashindwa nini kuendelea? Akichangia mbuzi mmoja tu ni mchango mkubwa wa kujenga madarasa lakini mkulima atauza mahindi magapi apate 50,000/= lakini unalimbikiza mifugo utajiri halafu watoto wanasoma chini ya mti? Donors wamejitolea sana kwao na unakuta wamehama na shule ipo tupu. Kusomea chini ya miti inakuwaje wakati mifugo kibao, udongo hauuzwi na mbao za miti unapata kibali halmashauri? Unamlaumu nani kama huna kipaumbele ktk elimu?

Tembelea mazingira ya Pwani-coastal areas uone walivyobweteka.

Kama elimu ilibagua wakati wa ukoloni-sasa ukoloni bado upo? Kama husomeshi na mtoto hapendi kusoma na humshauri au kumlazimisha-utabaki hivyo hivyo kulalama. Utawaona wa jirani yako wanapeta. Havidondoki kama mvua.

Makabila yaliyopendelewa na Nyerere kwa vile ni madogo au traditionalists kubadilika wasome-akachukua watoto wao kupeleka kusoma ulaya-wamebaki huko huko hawakurudi. Waliorudi wamerudi na wake wazungu ambao bongo wameona tabu wamerudi nao tena ulaya. Sawa na kusomesha mtoto UDSM akaamua harudi kijijini akakuacha solemba unakufa pekee ktk poverty. Akija home-anauza mashamba na mali nyingine anarudi dar.

Ona wivu hata ukiwa nyuma ili uige wale wa maendeleo nawe uendelee. Unajionea mwenyewe wa kutokuwa na malengo, mipango na juhudi halafu unakaa kutwa-tulionewa, bado tunaonewa, nchi mbaya etc kisha jani mpaka mlangoni hata kupalilia huoni ni cha maana. Mvua inanyesha tope limejaa, nyasi na makuti yapo-tunaonewa!! Ukuta upo wazi mtu anaweza kukuchungulia. Choo uwa upo wazi, kubanda cha choo kifupi ila nje miti mirefu kibao huezeki wala kukandika nyumba-Tunaonewa!! Unakula embe unatupa kokwa wala huipandi ila mwanzako akiipanda wewe kuvuna kwa mwenzako unakuwa wa kwanza-Tunaonewa. Hata kupanda mwembe na mpapai nje ya nyumba? Tuwaige hao wachaga na pia wapemba kibiashara na wakinga wamekuja juu kujituma. Waha nao na Wakurya wanakuja juu sana sasa.

Elimu ndio ufunguo wa maisha. Tukiwa Ulaya masomoni  kwa scholarship tukiwaona wenzetu wa huko wakiteseka kusaka hela wajilipie shule.Pilikapilika nyingi ktk kupata hela na scholarship wao kiduchu kulipiwa na mashirika. Anakuja shule lakini anaanza kazi kuanzia asubuhi, au akitoka shule na usiku. Kufagia barabara, kuosha vyombo hotelini, dreva wa taxi au bus, maktaba au mpishi cafeteria fulani, muuza beer bar. Sisi hapa university students wetu hawawezi haya. kuosha vyombo tu nyumbani tatizo. Kuchangia arusi si tatizo elimu tabu. Kulipa kiingilio cha mpira poa milioni 500 zinapatikana siku moja mpirani. Kuchangia hivyo secondari kwa mwaka kiwilaya zipatikane ili mabweni yajengwe-impossible.

Ukitaka bure utapata-lakini Kodi lazima iwe kubwa-ipae juu hakuna kuepuka kama ilivyo ulaya. Kodi yao kwa kila kiuzwacho na bado hakuna free services. Jee tutaweza na sisi ni watu wa mission town? Maana hata hiyo Ulinzi shirikishi kuletwa kusaidia usalama wa jamii imekuwa balaa-rushwa tupu hao vijana. Kukwepa kodi ndio sala yetu. Dhuluma kibao mpaka ndani ya familia na mtu anaweka wakili anashinda kesi huku kadhulumu!! Ndio maana hatutoki hapa tulipo ktk umasikini.

Bongoland kulalamika na shutuma ndio donda ndugu. Bure dunia nzima kwa sasa hakuna. Ajira directly ukimaliza shule hakuna. Soma, jenga uwezo, jiajiri uwe mkristu, mwislamu, Budha, Bohora, Ismailia whatever!!
Ukitaka bure-uwe mtumwa wa anayekupa. Kuchangia maendeleo ndio sera ya sasa kidunia maana hakuna cha bure toka dunia ya nje. Kingine ni kufaidika na raslimali zilizopo hivyo budi tusitunze ili uwekezaji utufaidishe. Ukijenga-usibomoe eti umekasirishwa. Na ukisha kubomoa unapata nini hasira zikisha kuisha.

Sheik Ponda (Mwanaume mzuri mwenye macho na lips nzuri-anapendeza) anasema NURU itakaribia!! lakini utaipata NURU tu ikiwa kama utahangaikia kujiendeleza sio kwa kukaa kitako ukisubiri kishuke. Cheap politics au mafunzo duni ndio unampa mtu kumwambia hivi, unampa mtu  tamaa ya fisi kumbe-utoke jasho, uihangaike, ukihangaikie ukipate, ukitumie sustainably. Ninafunga sala. hii. Bye.

--- On Tue, 4/6/13, Rashid Maalim <rashid.o.maalim@gmail.com> wrote:

From: Rashid Maalim <rashid.o.maalim@gmail.com>
Subject: Re: [wanabidii] KONGAMANO LA WAISILAMU JIJINI DAR, Sheikh Ponda aunguruma, Awasihi waisilamu kuwa na umoja, Nuru inakaribia.
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Tuesday, 4 June, 2013, 9:19

Baaada  ya  story  yako ndefu  ishu  ni kwamba ,hakuna  ambaye  anakataa  kusoma  wala  hakuna  jamii isopeleka  watoto  wao  shule ,ila  tatizo ni kwamba  serikali  haitaki  kutafutia ufumbuzi  matatizo  ambayo mengi yake  ni  matokeo ya  historia mfano Elimu .Elimu  ya wakati wa mkoloni ilibagua  watu  kiasi kwamba  kuna baadhi ya makabila na dini wakanufaika  kuliko wengine  kama wachaga,na wahaya.Mpaka  leo hii ukiangalia  vizuri  kielimu  ni hawa ndio wako mbele  .Tatizo la elimu au  umasikini  si waislamu tu  bali ni matokeo  ya historia  ambayo  serikali makini ilitakiwa  kuyasawazisha  .Lakini  mpaka leo zaidi ya propaganda  na kuaacha  majukumu yake ya msingi wa  jamii yake  inawaachia  jamii nyingine kujibu  maswala yake



2013/6/3 Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>

Tunaisemea jamii inayounda Taifa na Serikali. Ina matendo na mitazamo inayohitaji pia kubadilika ili zifanikiwe.

Kama dini ni away of Life, je ina maana mtu anasali kutwa hafanyi kazi? Watu watakupa mifano kuwa, kama mtu mfano yupo Chuo Kikuu na dini ni a way of life anasali in a routine way kutwa, kucha. Hii itamfanya kwa mfano akimaliza vipindi saa kumi na mbili jioni anakwenda kusali maombi kuanzia (mkristu huyo) saa 12 jioni hadi asubuhi (mikesha). Akirudi kesho darasani anasinzia, hajamaliza assignment na anajipa stress za zamisha. Huyu atafeli mitihani asipoangalia. Mwingine anarudi asubuhi kutoka mkesha (mke wa mtu) anakuta mtoto alizidiwa homa usiku akafariki. Housegirl hakuwa na uwezo wa huduma zaidi. Baba naye alilala nje kwa kimada kutokana kwamba mama daima yupo mikesha ya kusali na kuwajibika na familia na mumewe kudogo. Ndoa inavunjika hapo.

Kama ni wa kusali sala 5- as a way of life,  ni kusali kutwa na kufunga biashara au huduma ya kiofisi kila baada ya masaa fulani bila ya kuacha msaidizi. Kama ni mfanyakazi wa bank-madirisha yote yamefungwa kasoro labda moja na foleni ndefu sana-utakosa wateja watajiunga na bank ingine. Kama ni hotel-mwekezaji ataleta wahudumu wengine hata wa kutoka nchi jirani (malawi, Kenya, zambia) kuepuka misururu ya wageni reception mtu wa mapokezi yupo nyuma stoo ya hoteli anasali au kaenda kusali nje ya jengo. Mwekezaji au tajiri hatokubali kukosa wateja mtu anasubiri apokelewe au kupata chakula masaa kitu kidogo hakiji. Ni mifano ya kuonyesha-serikali haitotelemsha kama mvua.

Budi kugangamala na kutafuta mibadala ili kujiajiri kiufanisi au kuajiriwa na kufanyakazi kwa ufanisi. Ni mifano hai na halisi bongoland kwa madhehebu ya wakristu na waislamu na tunayaona katika nchi yetu na za wenzetu.

Sali sana lakini soma sana na pata ujuzi-zalisha sana. Tunza mila ya kabila lako lakini tendea haki wengine sio unasema amefariki au amehama lakini kumbe umemuoza na umemtorosha hapo katika umri mdogo hasomi au umemuozesha unamchanganya kimajukumu kijana shule haipambi.
Ni mifano halisi tunayokumbana nayo katika kupanga mipango shirikishi, IEA, SEA ya kuangalia watafaidikaje na miradi. Baadhi ya desturi hizi hukatisha tamaa wenye nia nzuri na kusaidia maendeleo.
 
--- On Mon, 3/6/13, Rashid Maalim <rashid.o.maalim@gmail.com> wrote:

From: Rashid Maalim <rashid.o.maalim@gmail.com>

Subject: Re: [wanabidii] KONGAMANO LA WAISILAMU JIJINI DAR, Sheikh Ponda aunguruma, Awasihi waisilamu kuwa na umoja, Nuru inakaribia.
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Monday, 3 June, 2013, 10:20

 Hivi katika  nyinyi kuna hata  mmoja  msemaji wa  serikali hapa?Maana malalamiko  yametupwa kwa serikali na  ushahidi wakutosha,sijui mnamsemea nani  nyinyi.Na pia  wote tunatofautiana  Imani  kati  yetu  kuna  kwao  dini ni  part  time   au ni kitu  cha kufanya  wakati hauna kazi  wakati  wengine  ni way of  Live  kwa hio  tusigeneralise mambo kwa mtazamo  wako


2013/6/3 Fred Hans Kipamila <fhkipamila@yahoo.com>


--- On Sun, 6/2/13, Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk> wrote:

From: Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>

Subject: Re: [wanabidii] KONGAMANO LA WAISILAMU JIJINI DAR, Sheikh Ponda aunguruma, Awasihi waisilamu kuwa na umoja, Nuru inakaribia.
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Sunday, June 2, 2013, 6:54 PM



Matatizo mengi ya kuonekana dini fulani au kabila fulani linabaguliwa au kuonewa yataisha kama makabila na madhehebu hayo yatakazania elimu ya darasani yenye kupatia wanafunzi life skills. Sio kusoma dini tu. Pia, yatakuwa na malengo ya kujiendeleza kwenda na wakati. Mfano sio kuzurura na mifugo, kuchimba madini na kuoza visichana kuongeza mifugo uonekane tajiri-bali kufuga kisawa wachache bora, kuuza mazao yao, kusomesha na kuleta maendeleo ya familia. Kuwa na familia ndogo ya wafanyakazi waliojiri na kuajiriwa. Mungu nipe na mchele mkononi!! yaani-Sala ziende na ufanyaki kazi productively kwa maendeleo yako. Culture iende na maendeleo sio kinyume chake.

Muhimu dini yoyote kwa karne hii ni kuondoka utumwani. Ule uliokuja na waeneza dini walioitumia kutunyonya. Budi kuhimiza waumini kujituma, sio kukaa barazani tu, sio kuwa na mikesha ya sala bila ya kufanyakazi au kushinda kutwa unakwenda kusali sio kuzalisha mali. Ukisha kusali tumbo linataka kitu.

Wanadini/waumini wahimizwe kuchangia maendeleo yao-sio kujenga mahekalu ya dini ya mamilioni. No, hii haitoishi. Wakiwa katika Ibada-waelimishwe umuhimu wa kuchangia wajenge shule, zahanati, huduma za maji hata kuanzisha Vikoba na bank za kidini kupata mikopo kuepuka bank binafsi zinazotoza riba kubwa; kuwa na vituo vya malezi ya yatima, wazee, wenye ukoma, na walemavu wengine wasiotakiwa majumbani wananyanyaswa.

Kutetea haki za binadamu, vijana, wanawake. Iwe marufuku kikabila, kidini kuzuia wasichana wasisome na kuwaoza ktk umri mdogo. Kupunguza ndia za wake wengi maana husaidia kuambukiza Ukimwi, virus wanaosababisha cancer za uterus na maradhi mengine kwa wababa, kuwa na familia kubwa masikini yenye watoto wengi.


kila mtu wa dini popote alipo ajue kuwa havitoshuka kama mkate waliopewa waisrael jangwani enzi za Musa, havitoshuka kama mvua bali kwa kutafutwa kwa kazi ngumu kwa kutumia raslimali zilizopo. Hata kama utachukua madaraka-fahamu dunia kwa sasa haitoi tena misaada ya bure ili utoe huduma bure kwa wananchi wako, ni kwa kufanyakazi kodi igharimie aidha maendeleo au huduma utakazo kutoa bure. Bure kutoka China, England, Russia, USA imekwisha.

Ukitoa mchango kanisani au msikitini-itumike kuhudumia hekalu na maendeleo ya jamii. Mchango wa 15,000/- kutwa moja kwa hekalu la dini lililojaa waumini ni sawa na kichekesho ambapo waumini hao wana daladala, maduka, mahoteli, migahawa, mikarafuu, korosho, pamba, kahawa, minazi, wauza samaki, madini. Kutoa kwa moyo michango ktk mahekalu kutasaidia kulipia maendeleo ya waumini. Kwa wakristu madhehebu mbali mbali misa moja inafika laki 1 hadi 7. inategemea kanisa ni la mjini, kijijini, City na lina misa ngapi. per day michango ya matoleo kanisa lingine hupata 4-10 million ambazo zinalisha mapadri na masista, huduma za umeme, maji; kugharimia mashule, zahanati, ujenzi mbali mbali nao hupata michango maalum mpaka harambee. Dhehebu kuwa na Colleges, Universities na wasomi wa kuendesha miradi ya dhehebu, kuajiri wataalamu, kuwa na vitega uchumi ili kupunguzia mzigo waumini ndio fashion ya sasa ulimwenguni. Wabongo waangalie haya sio kutegemea vije tu au dhehebu ligharimiwe na GVT kupitia hela za walipa kodi ambao sio waumini wa dhehebu hilo. Ni pale tu dhehebu lina Zahanati, Hospitali kubwa ambayo hutoa huduma ndio inapata madaktari, wauguzi na health kit inayotolewa na wizara ya afya kwa sababu inatoa huduma na kupunguza mzigo kwa GVT kujenga service ya namna hiyo hapo. haina haja ya GVT kujenga another hospital ambapo e.g. Aga Khan, KCMC zipo au zinaongezea huduma zaidi ya Muhimbili au kuipunguzia mzigo. Kama ni mahakama ya kidini-kila dini inao mfumo wake wa mahakama ijigharimie vyote ila mikopo ya Vyuo vikuu-hata wale waendao Universities za Dini wanapatiwa.

Tuungurume tu Kidini, kimadhehebu, kikabila kuonekana tunaonewa na serikali au jamii lakini tunayaharibu wenyewe sehemu kubwa mfano-raslimali zipo ila  tumebweteba wavivu tupo barazani kutwa. Mama akienda shamba asindikizwe na kijana au asiende pekee wakati baba anavua na anaweza kwenda mwenyewe ila haruhusiwi kutoka;  au wasichana hawapewi kipaumbele kusoma na elimu dunia haipewi kipaumbele; mzazi hatumii kuuza mifugo kusomesha au kuchangia ujenzi wa shule kwa kuuza mbuzi mmoja au kutoa 20,000/= kwa mwaka lakini analewa daili au anaoa na kuhonga daily zaidi ya hizo. Hana kipaumbele cha elimu. watoto watasomaje chini ya mti wakati miti mnakata mbao unapeleka nchi jirani, miti mnachoma mkaa. kijijini mnafyatua tofari za kuchoma mnauza na kujengea na kijiji kina mafundi wa kienyeji pia wajengao nyumba za tope au za tofari za aina zote? Kuwaje hakuna harambee ya kufyatua tofari mkajenga darasa moja kila mwaka? Aibu na excuses za kijinga. Eti unakwenda Dar au China unasafirisha mitumba mpaka kijijini mbali porini ukitumia malori ya mizigo au kukodi. Kwa mbinu hiyo-huwezi kusafirisha mchele kutoka huko kuja dar-mchele hauna soko kijijini kwa vile hakuna barabara/miundo mbinu! Mitumba kafa ulaya maroba kibao-imefikaje; madela toka uarabuni na maembe ya kutoka Sudan na S. africa yapo kilombero gulioni, Iringa Mjini au Makete remote area? Kituko bongoland! Kumbe miundombinu si issue hapa!! Shule zipo-haendi shule na akienda hana daftari lakini baba kutwa anavuta sigara pakti na kunywa viroba!


Kama ni kikabila tunaoa na kuoza vichanga visisome, au tunaharibu mazingira kwa kulima na kufuga unsustainably. Mengi tunayolaumu yapo chini ya uwezo wetu. Ifike kila dhehebu mwalimu wa dini wa chekechea awe naye na cheti cha form 4 ambayo kwa sasa ukitaka ajira ya kufagia ofisini au kupika chai ni cheti cha form 4. Shekh au Padri awe angalau na degree asiwe na cheti cha dini tu-awe msomi muona mbali aongoze wengine. Kwa wakristu hii sio tatizo. Padri, Sister ni Msomi sio wa dini tu na elimu ya darasani.

DINI ZIWE NA DIRA YA ELIMU DUNIA PIA INAYOTOA AU KUELIMISHA LIFE SKILLS NA KUWAWEZESHA WAUMINI KUWA NA PROFESSIONAL SKILLS ILI KUJIAJIRI AU KUPATA AJIRA. Tukitegemea vizuke kama mvua-tutakaumizana na kuoneana daima, tutapigana na kuuana kwa kushukiana. Mpe mwanao elimu akasome shule yoyote uionayo bora. Una maduka, biashara ushindwe nini kusomesha umuweke auze duka tu; afuge tu, avue samaki tu. Somesha aweze kuuza duka kibiashara, kununua bidhaa bongo asafirishe nchi za nje. Wahindi wameweza kuwa na viduka hadi vikawa viwanda na kuexport na kuwa na miradi Kenya, Canada etc. Waafrika tuige na tuige Wachaga kibiashara ua uwekezaji. Tutapigana na kuwa wakimbizi maporini maana hatuna pa kukimbilia nchi jirani nako kunawaka.


--- On Sun, 2/6/13, mngonge <mngonge@gmail.com> wrote:

From: mngonge <mngonge@gmail.com>
Subject: Re: [wanabidii] KONGAMANO LA WAISILAMU JIJINI DAR, Sheikh Ponda aunguruma, Awasihi waisilamu kuwa na umoja, Nuru inakaribia.
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Sunday, 2 June, 2013, 18:47

Ukifuatilia typology ya kueneza uislam katika pwani ya Afrika mashariki utagundua kwamba kulikuwa na tatizo lililofanywa na waarabu katika mikakati ya kueneza uislam.  Walipokuja wamissionari wakawa na mikakati iliyoziangalia jamii za kiafrika na kuweza kujipatia wafuasi kiulaini. Kama ni shule waarabu ndo wa kwanza kuzianzisha hapa kwetu lakini zilishindwa kuimarika kama za wenzao ambao waliokuja baadaye.

Wawe waarabu au wazungu hakuna aliyekuja na lengo moja tu la kueneza dini kama dini, walikuja na lengo jingine ambalo ni uchumi. Tatizo watu wengi tunalibeba tatizo hilo la kihistoria na kuliingiza katika jamii ya kizazi kingine kwa namna tunavyotaka liwe badala ya kuangalia ualisia tangu zilipoletwa kwetu. Ni vyema watu wakaisoma historia vizuri tangu mwanzo wa ujio wa dini hizi maana ukianzia mbele lazima kutakuwepo mkanganyiko


On Sun, Jun 2, 2013 at 7:29 PM, richard bahati <ribahati@gmail.com> wrote:
Sheikh Ally Basaleh nae hakusita kuwaambia serikali kuwa kwenye daladala waliopanda watanzania kuna watu wamevaa ndala na kuna wengine wamevaa buti wenye ndala wanakanyagwa ndio maana wanasema! Kwahiyo badala ya kufanya hasira na kuchukua maamuzi ya nguvu bora wawasikilize wanaosema wanakanyagwa.....................

http://goldentz.blogspot.com/2013/06/kongamano-la-waisilamu-jijini-dar.html

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment