Sunday 5 May 2013

[wanabidii] AHADI KUMI ZA TANU

Tujikumbushe Ahadi 10 za TANU:

1. Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja.
2. Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote
3. Nitajitolea nafsi yangu kuondoa umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
4. Rushwa ni adui wa haki. Sitapokea wala kutoa rushwa.
5. Cheo ni dhamana. Sitakitumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
6. Nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote.
7. Nitashirikiana na wenzangu wote kuijenga nchi yetu.
8. Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
9. Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa TANU na raia mwema wa Tanganyika na Afrika.
10.                 Nitakuwa mtiifu na mwaminifu kwa Rais wa Serikali ya Tanganyika.

Ahadi hizi tungezitekeleza hata 25% tungekua mbali. 

0 comments:

Post a Comment