My Dada,
Watu huvutiwa zaidi kusoma hbr fupifupi ... unapoint ila story ndefu mno... hata mimi nilikuwa kama wewe zamani ila nimeona faida za kufupisha
From: Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Friday, 24 May 2013, 5:56
Subject: Re: [wanabidii] VURUGU MTWARA BAADA YA SERIKALI TAMKO LA SERIKALI KUHUSU GESI
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
Watu huvutiwa zaidi kusoma hbr fupifupi ... unapoint ila story ndefu mno... hata mimi nilikuwa kama wewe zamani ila nimeona faida za kufupisha
Regards,
Mugittu, Zephaniah,
Cell: +255 784 769 481
Fax2Email: 0736605633
Skype: Zephaniah N.N. Mugittu
No matter how high one is talented , business acumen still a necessity
"Poverty is a result of attitude ..."
From: Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Friday, 24 May 2013, 5:56
Subject: Re: [wanabidii] VURUGU MTWARA BAADA YA SERIKALI TAMKO LA SERIKALI KUHUSU GESI
Matanda-wala usijali mimi kuitwa kaka. kuna akina mama warembo lakini ni bisexual wamezaliwa hivyo biologically au ni transgender psychologically. Mwache tu aite atakavyo, unaweza ukamuona mtu kavaa gauni au suruali kumbe-kanyaboya. Ni juzi tu mama bisexual huko china amepata haki yake ya kuolewa. Amefanikiwa kufanyiwa operesheni kuondoa umbile la pili na mchumba kamvisha pete. Hapa Tanzania wanaozaliwa hivyo wapo wengi, hawana msaada, wazazi waliwaficha hivyo hawakufanyiwa upasuaji. Wanateseka na kunyanyasika sana mopaka kubakwa ili kushikishwa adabu eti wajiune na kujitambua kuwa wao ni She sio He. Wapo walioa na kuzalisha naye akiamua anazaa wake. Yaani una watoto mtu kakuzalia halafu nawe una wako umezaa mwenyewe. Bahati ilioje!! Nione ninguunganishe nao uongee nao. Ila unaweza pia kwenda Google kusoma habari za saint wa jina hilo ukaiona na ukaipata. Kuchangia ya Mtwara Ninapenda kuchangia kuwa-nadharia ya education inasema kumuelimisha mtu haimaanishi atafanya ipasavyo. Elimu na kuelimika kukuza ufahamu kuhusu jambo ni muhimu lakini sio mwisho wa tatizo. Umuhimu ni yule anaye elimishwa kubadilika positively kufanya inavyotakiwa. Na ndio maana unaelimisha watu na wanayaona matokeo unayoyasema lakini bado wanafanya watakavyo wao kutokana na mambo mengi-kutokuelimika ndani ya ubongo wao kwa kukubali kwa dhati usemayo; imani potofu iliyojengeka hata usemeje, ushauri wa wengineo (peer influence, wazazi, wazee wa mila, mwenza, ndugu); mila na imani zake na desturi; hali ya kijiologia, sera, upatikanaji/access; livelihoods survival strategies na mengineyo mengi kama sababu. Hivyo baada ya elimu-utekelezaji kuyafikia yasemwayo ni muhimu.Mbinu za uelimishaji na kufikia walengwa directly ni muhimu ili kuepuka matatizo ya mawasiliano ktk kufikisha ujumbe : yaani UJUMBE-njia ya mawasiliano-nani anawasilisha mawasiliano ujumbe....vikwazo...- mpokeaji ujumbe-mrejesho kuwa umefika na umeeleweka. Juzi tu kuna gazeti moja nchini limeandika kuhusu kabila moja huko kusini na masuala ya ngoma za jadi za kumcheza mwali wa kike na kufundisha vitoto mambo ya kikubwa ya ndoa au kujamiiana na jinsi inavyoathiri elimu. Ikatoa takwimu za utoro shuleni na mimba na idadi waliofaulu na ambao hawakufika sekondari. Na hii elimu ndio ufunguo, inapigiwa kelele kila mara mpaka kuanzisha shule ya vidudu ktk kila shule ya msingi na kuanzisha sekondari za kata pamoja na matatizo yake au ya shule hizo. Je, kwani wazazi hawajui hilo? Mbona hawaandamani wakajichoma wenyewe kwa kukiuka sera nzuri ya serikali ya maendeleo yao wenyewe? Nilitolea mfano hapa wa mradi sio Mtwara ila Lindi vijijini jinsi tulivyokuwa tunakaa na kupanga pamoja na kukubaliana. mzee mmoja na mwenzake wakatoa ardhi ekari mia nilisha kuzitaja humu mtandaoni kujengwe hiyo shule ya chekechea baadae ije ijengwe primary school watoto wapate elimu. Funded 100 na familia ya marekani wao wagharimie vinginevyo. Wilaya iliahidi kutoa na kugharimia mwalimu. tukakubaliana waanze kulima shamba la shule (ekari 4 hivi), kuuza mazao kuweka hela bank mpaka hapo shule itakapokamilika watakuwa na hela za madeski, mikeka, vikombe vya uji hela ya kulipa mlinzi na mpishi. 'Hela za nauli kwenda kufungua akaunti Lindi Mjini hatuna, ya akaunti na kupiga picha hatuna; hatutaki viongozi wa kamati ya ujenzi wa shule ya msingi watakula hela' ....Sawa-Ninatoa hela yangu hii hapa mbele ya umma (85,000/= posho ya siku moja) mkafanye tunalojadili, nauli, picha, akiba ya kufungua akaunti. Kisha nikanunua mbegu husika DSM, peleka kupitia mabasi ya Lindi (Sio Mtwara) kusaidia vikundi 2 vya vijana, shule 2 za msingi na hiyo ya chekekea. Shule ya Chekechea kamati ya ujenzi ya kusimamia pia kilimo na mengineyo walioichagua wenyewe--HAIKULIMA. Yakaja maneno mapya. Sio kukataa kamati ya SYMsingi tena.....Tunangojea kwanza shule Ijengwe Ikamilike na mengine mengi ya kutia mtu mwenye nia njema wazimu. Shule imekamilika baana ya mwaka, mkandarasi kaikamilisha ipasavyo-hawakulima, akaunti haina hela, malumbano.... Hapa huyu aelimishwe nini na anaona wasiosoma wanavyokosa ajira au hawajui kusoma na kuandika kama alivyo yeye mzazi hajui hata kusoma kiswahili wenzake wanajua. Anayeoza na kuoa kichanga-haoni matokeo yake. anyway, kasichana kakipata Fistula ataoa mwingine. Umempeleka mtu study tour ambayo husaidia sana ufahamu. inategemea nani kapelekwa, labda wale wasio wa sekta hiyo na wana mahitaji mengine-kupanda ndege, shopping. Kajichagua au kaenda sio Mtarajiwa karudi ...ana mambo yake. Au, kaenda aliyetegemewa lakini amerudi umemuwezesha aweze kutembea kwa walengwa wa mafao ya GAS awafahamishe ipasavyo? hata usafiri wa kutembea vijijini kila kijiji, au kuitisha vikao vya kata na vijiji. Vijiji vingine ni mbali na makao ya Kata watataka kurudishiwa nauli kwa vile kawaita yeye. Anazo hela na usafiri? Hata kama tatizo si nauli-akiwaita wakaja jee watakayoambiwa hawatayageuza (matatizo katika communication of information). naye aliyeona huko Trinidad na Tobago au Ukraine-atasema alichokiona positively? ana uelewa wa kuwakilisha alichoona bila kupaka mafuta na kukigeuza? Muda wa elimu hiyo na matokeo ya ujenzi. Jee waliohudhuria maelezo ni hao ambao wanaandamana? au waliohudhuria ni wazee, vijana hawakuwepo ndio hao wanaandamana maana hawaendaki ktk vikao vya vijiji. au wote wamepata maelezo ya kuelimishwa lakini kama tulivyo waswahili-kuongeza chumvi na kubadili ukweli, matokeo ni vurugu, kutumia baruti za kuvulia samaki na kubomoa madaraja, kukata miti ya umeme ili umeme wa kutoka Kidatu kwa Wavidunda usiingie Mtwara na ktk majumba ya Waheshimiwa viongozi na wengineo. Nao madreva wa magari ya polisi wakija-tunaweka kivumba, barabara asiione auone shimo aanguke wafe askari wote watakaoletwa Ntwara (Tumesikia mitandaoni dreva kasema aliona bahari sio njia!!). Ni kama ile vita ya risasi kugeuka maji na hivi sasa dreva njia aione haipo, akiona kundi la watu askari aone ni tembo akimbie mwenyewe!! SERIKALI YA TZ ina muongozo wa kuangalia athari za mradi na jinsi ya kuwafaidisha walengwa. na hii hufanyika chini ya NEMC na Wizara husika hushiriki kikamilifu. Wakitoa tender kampuni ya nje inayobid lazima iwe na kampuni mwenza au taasisi yenye wataalamu hapa nchini. Hawa wanakwenda kufanya studiez zote na kupanga mpango wa kufaidika na wa kuondoa madhara ya mradi (mitigation measures). Report mbali mbali huandikwa na kuwakilishwa serikalini na donor wa mradi kama yupo au GVT tu. taarifa huandikwa kiswahili na kuthibitishwa na wananchi wakatoa michango yao ktk taarifa hiyo ya mapendekezo kabla ya kuwakilishwa. Wananchi hifikiwa kwa vijiji, vitongoji vya mbali, kata; wazee wa mila na wazee maarufu ke na me kushirikishwa, watumishi wa ugani, masirika binafsi na NGO/CBO zilizopo; vikundi vya wazalisha maji; tourist hotels/companies. yani walengwa ni waliopo eneo hilo na sekta zilizopo formal-informal. kikao cha mwisho kila kundi hupeleka mwakilishi kusikiliza. Kunakuwa na public hearing kieneo vijijini wanafuata mikutano ya hadhara na kuambiwa kisha kukaa vikundi kuandika na walichoandika hutunzwa. wakawakilisha na kuchangia vikundi vyote vilivyopo wake kwa waume, vijana na wazee. Msidanganywe na hearsay, kazi hufanyika, isaidieni serikali na jamii kufanya vya maendeleo sio uharibifu. Unaweza ukasema-HAWANA AKILI kama ikiwa, baada ya kufanya yote ya kuwashirikisha na kuwaelimisha-wanafanya haya wayafanyayo. Au, waliahidiwa vikao, vikaitwa hawakuja wakagoma, sasa wanaharibu hawataki majadiliano.Hawaambiliki na kushaurika-wanaona wanavyoharibu ila wanafanya tu kutaka misifa. Kama inawezekana. Huo mradi uachwe usimamishwe kionekane. Mbona mafuta yapo mengi sana nchini na mafuta hufuatana na GAS. kuna minara mingi ya mafuta toka Ukoloni na hapo Gas haikosi. Huko nyuma, nilitoa mfano wa Mafia Island na milingoti mingi nchini ambapo imefutika maandishi tunadhania ni mnara wa mipaka au bomba la zambia na mingine tunabomoa tunachukua kokoto na nondo. Tunadhania ni mnara wa kuonyesha madini fulani yapo kumbe ni wa mafuta ya ardhini. Nikaweka minara ya Mafia ambayo watafiti tulikuwa hatuijui ila kasichana toka uingereza kilipewa grid reference na baba yake tukaisaka 9bila kibali cha serikali) tukaipiga picha maana baba yake alitaka ajulishwe kama wameanza watanzania kuchimba mafuta au la. lakini utafiti wa Gas ukiendelea mafia 2008 na ipo nyingi kichizi. Angalia kiambata upate kuona jinsi watumishi wa mshahara mdogo wa GVT yako wanavyoteseka maporini, baharini ktk kutekeleza kukusanya mawazo ya wananchi katika miradi mbali mbali. Huu wa kiambata ni mradi wa International airport wa kusaidia usafiri (ambao ni tatizo Mafia) na wa kukusa utalii. Huu utaunganisha utalii ZNZ, Mafia, Arusha, Kilwa, Mtwara-Mikindani. Hivyo sio Mafia tu kulitembelewa ni Mpaka Rufiji-Nyamisati Kilwa Kisiwani-Mikindani-Mtwara. Mafia ni visiwa saba vinavyokalika vyote vilitembelewa na walishiriki kikamilifu. Ila, tishio la kuhusisha watu kidemokrasia ni wale wasioitaka ili wavune mazao (kuvua ndani na Marine Park, kuvuna Mikoko na kuuza mbao na milingoto Uarabuni) ambao walipokuwa wakiondolewa wakaingiza UDINI mabomu ya petroli yakaruka kupambana na askari wa doria wa Marine Park, Idara ya uvuvi na mali asili. watafiti tukiwa chambo ktk shughuli isiyohusu hayo yao lakini tungekufa. --- On Thu, 23/5/13, denis Matanda <denis.matanda@gmail.com> wrote:
|
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment