Nijuavyo mimi, fani ya uhandishi wa habari ina maadili yake. Lakini kama huyu mwandishi wa habari amelipwa au amewezeshwa ili kuandika propaganda hapo ndipo maadili yanapoharibika na tunapoteza mwelekeo kabisa.
Waandishi wa habari watafanya kazi kwa uhuru iwapo watajilipa wenyewe. Kwa namna khali ilivyo sasa sijui kama ndugu zetu watakuwa na uhuru na utashi wanaotakiwa kuwa nao. Inafika mahala wanakubali hata vitu ambavyo sio vyenyewe, ili mradi mwenye mbwa kasema. Uhuru wa fikira utatoka wapi? Nawaza kwanguvu tu!
From: LINGONET Lindi <lingonetlindi@yahoo.co.uk>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Saturday, May 25, 2013 11:03 AM
Subject: Re: [wanabidii] Ujumbe Muhimu kwa Wadau wa Habari
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Saturday, May 25, 2013 11:03 AM
Subject: Re: [wanabidii] Ujumbe Muhimu kwa Wadau wa Habari
wandugu vurugu za mtwara zimetawaliwa na habari za kishabiki sana ,nadhani hii ni moja ya mambo yanayokoleza sintofahamu katika kadhia yote ya gesi kusini mwa tanzania ,kwa bahati mbaya hata serikali imejiingiza katika kutumia propaganda kukabiliana na yanayojiri mtwara ,iliyofikia kuandaa vipindi maalumu kwa ajili ya kueneza uongo ili wananchi wa kusini waonekane ni wahalifu,waziri mkuu alikwenda mtwara akaongea na wananchi na kufikia makubaliano amabyo mpaka leo hajayatekeleza inayomwia vigumu tena leo kwenda mtwara kwa sababu hana majibu ya maswali atakayoulizwa kufuatia makubalano yao. lakini turudi katika vurugu za tarehe 22/5/2013 wananchi walibaki majumbani mwao ama kutekeleza wito wa vipeperusi au kwa hofu ya vurugu na biashara zote zilifungwa,ni askari tu waliokuwa wanaranda mjini na kupiga mabomu ya machozi bila ghasia zozote,kitendo kilichoamsha makundi ya vijana kuwarushia mawe kama hujuavyo katika jambo lolote kuna watu wanaoshabikia fujo,lakini la msingi walioanzisha vurugu ni polisi,baada ya kuzidiwa na gari ya kurusha maji ya kuwasha kushindwa kufanya kazi,wanajeshi waliingia kusaidia na maeneo yote ambayo jeshi waliwajibika hakukuwa na madhara makubwa kama yale ambayo polisi walikuwepo kwa kukamata wanaume na kuvunja maduka na kupora vitu,kwa bahati mbaya sana vyanzo vya habari vilizusha taarifa zisikuwa na ukweli na kueleza kuwa daraja la mikindani limevunjwa na huwezi kuingia mtwra jambo ambalo si sahihi,siku ya pili ya tarehe 23/5/2013 ndipo polisi walipofanya fujo kubwa sana katika maemeo ya magomeni,chipuputa,mangowela mdenga na tandika.maeneo yote ya madukani shangani railway ambayo wanajeshi walikuwepo hakukuwa na vurugu kwa vile wanajeshi walikuwa wanafanya kazi bila kupora mali wala kuingia majumbani kuwachomoa watu. hivyo dhamira yangu hapa ni tujitahidi kueleza hali halisi ilituweze kupata muafaka huku tukijitahidi kuondoa tabia ya wananchi kufanya vurugu wakati wakudai haki na kuwa na jeshi la polisi linalofanya kazi kwa mujibu wa taratibu na sheria wakati waandishi wa habari kama huna chanzo cha habari usizushe taarifa ambayo inaweza kuharibu amani yetu,mwandishi amekimbia fujo amejificha kuogopa kupigwa lakini anasema daraja limevunja bila kuona haya ndio mambo yanayozidisha sintofahamu
|
0 comments:
Post a Comment