Wanambadiliko, Nimekerwa na mjadala huu, unaotokana na uongo wa dhahiri kutoka Jamii Forum na naandika maneno haya kwa nguvu ya Roho wa Mungu ili msema uongo na aumbuke mbele ya Mungu. Inasikitisha na kukarahisha kuona uongo unaotungwa Jamii Forum ili kuchafua watu. Unaweza kuwadanganya watu kwa muda, lakini kifo kitakuumbua. Dhahiri Maneno yanayominishwa kusemwa na Dr Kigwangallah si yake, wala hakuyasema mkutanoni. Tuliokuwepo mkutanoni Dr Kigwa hakusema chochote kuhusu Membe bali alisema habari ya viongozi wa seriklai wa Mtwara (kamati ya Ulinzi na Usalama, mkoa na wilaya waondolewe kwa kushindwa kutekeleza wajibu wao wa kulinda amani ya eneo hilo. Mapendekezo hayo yaliungwa mkono na wabunge wengi. Bernard Membe yeye hakuongelewa kabisabali Hawa Ghasia na Murji mbunge wa Mtwara mjini, waliotuhumiwa nawabunge wengi kuwa ndiyo chanzo cha mgogoro huo. Ukiosma habari hiyo Jamii Forum inaonekana imeandikwa na mtu kwa kuficha identity akilenga kumchafua Membe na Kigwangala, na nadhani ni agent wa kundi jingine la urais. Nchi hii uongo umekuwa silaha ya kwenda mbele. Bahati mbaya sana uongo ni silaha mfilisi ya shetani ambayo mwishoni huumbuka. Hii ni janga kwa taifa, propaganda za kuchafuana na kutukanana zinachefua na kukarahisha, lakini uongo wa JF utajitenga siky moja. Mungu atende kazi yake. Tumwombe Mungu Shetani yule lusifeli wa kale ashindwe, na nchi yetu ivuke salama 2015 Mungu awabariki wote Ngw'izukulushilinde --- On Fri, 5/24/13, paul lawala <pasamila292000@gmail.com> wrote:
|
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment