Saturday 25 May 2013

Re: [wanabidii] NIMEAMUA KUKANUSHA: KIGWANGALLA NA UDINI WAPI NA WAPI?

Dada Anna, ndo maana ninawaomba na kuwasihi wenzetu wa kwenye media wawe makini watusaidia kufanya kazi yetu vizuri zaidi
Sent from my BlackBerry® smartphone from Vodacom Tanzania

From: anna nyanga <luguanna@yahoo.com>
Sender: wanabidii@googlegroups.com
Date: Sat, 25 May 2013 04:02:05 -0700 (PDT)
To: wanabidii@googlegroups.com<wanabidii@googlegroups.com>
ReplyTo: wanabidii@googlegroups.com
Subject: Re: [wanabidii] NIMEAMUA KUKANUSHA: KIGWANGALLA NA UDINI WAPI NA WAPI?

Sasa, hawa waheshimiwa Wabunge watafanya kazi saa ngapi? kama kila mara ni kuandika taarifa kwa umma? tena sio za kuleta maendeleo ila kukanusha tuhuma na uzushi!
 
Where are we heading to!!!!
 
Raisi mtarajiwa nimetulia hapa, wanapigana vijembe tu wao!
 
From: salum mkango <salumkango@yahoo.com>
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Saturday, May 25, 2013 10:19 AM
Subject: Re: [wanabidii] NIMEAMUA KUKANUSHA: KIGWANGALLA NA UDINI WAPI NA WAPI?

 
Mhhhh!!!!! 2015 kazi ipo. Kama mbinu chafu zimeanza mapema namna hii, sijui muda ukifika itakuwaje. Haya wengine yetu macho na masikio.

From: denis Matanda <denis.matanda@gmail.com>
To: wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Saturday, May 25, 2013 11:00 AM
Subject: Re: [wanabidii] NIMEAMUA KUKANUSHA: KIGWANGALLA NA UDINI WAPI NA WAPI?

Jiunge na winning team kaka! Hahahahaaaaaaaaaa


2013/5/25 Dr. Hamisi A. Kigwangalla <hkigwangalla@gmail.com>
OFISI YA MBUNGE
JIMBO LA NZEGA
Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla (Mb.)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 
Kufuatia taarifa za uzushi zinazosemekana zilitokana na kikao cha wabunge wote wa CCM (CCM party caucus) zilizoenezwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari na haswa kwenye mtandao wa kijamii na watu wenye nia ovu ya kutaka kuharibu jina zuri la Mhe. Mbunge wa Jimbo la Nzega, Dkt. Hamisi Kigwangalla (Mb.) kwa kuchafua taswira yake na heshima kubwa aliyojijengea kwa muda mrefu kwenye jamii, tumeelekezwa kutoa taarifa hii yenye lengo la kukanusha na kuweka kumbukumbu sawia kwa lengo la kuuelewesha umma.
Kwanza, anasema Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla (Mb.), hana tabia za kuwagawa watu kwa matabaka ya itikadi zao, dini ama makabila yao. Anasema msingi huu wa kuishi kwa kushirikiana na kupendana anautoa nyumbani kwao Nzega alipozaliwa na kukulia, kwa babu yake aliyekuwa Sheikh na muasisi wa Taasisi ya kiislam ya Nusratul qadiriyya (zawia) ambayo ilikuwa na wafadhili wakuu wakristo na kila mwaka walikuwa wakishiriki kwa hali na mali kwenye maulid na dua nyingine mbalimbali; miongoni mwa walezi na wafadhili hao ni pamoja na Hayati Chief Humbi Ziota, Mhe. Lucas Lumambo Selelii (Mb. Mstaafu wa Nzega na Katibu wa Makanisa ya Pentekoste Mkoa wa Tabora), Mhe. Steven Maziku Kahumbi (Mb. Mstaafu wa Bukene), Hayati Mhe. Mzukila (Mb. Mstaafu wa Nzega) – ambao walikuwa ni wa dini ya kikristo. Ni msingi huo uliomfundisha yeye kuwa mstari wa mbele kwenye kuunga mkono jitihada za watu wa dini zote na hata wasio na dini katika shughuli zao za kuendeleza imani zao ama kufanya shughuli za maendeleo bila kuingilia uhuru ama itikadi zao. Ni katika msingi huo huo amekuwa akishiriki kujitolea kujenga makanisa, misikiti na hata kuchangia kazi za wasanii wa kwaya mbalimbali bila kubagua kwa misingi ya udini. Watu wa Nzega ni mashuhuda kwa hili. Na zaidi ya hapo, Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla (Mb.) hawezi kuwa wa mstari wa mbele kuhamasisha ubaguzi wa kidini, jambo ambalo kila siku analipinga hadharani, na kwamba yeye binafsi ana Ndugu wa damu wenye wazazi wa kikristo, na waliooa ama kuolewa na wenza wenye dini ya kikristo na kuzaa watoto na wajukuu wa dini ya kikristo. Na pia si muumini wa kutafuta umaarufu kunuka unaotokana na kuwagawa watu kwa hoja dhaifu na mfu kabisa za udini.
Pili, Mhe. Hawa Ghasia (Mb.) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), HAKUWEPO KABISA kwenye kikao, hivyo  yote yanayosemwa na wazushi hawa ni ya uongo na hayana msingi wowote. Maana Mhe. Ghasia, asingeweza kumshambulia Mbunge Mwenziye ilhali hakuwepo kabisa kwenye mkutano huo.
Tatu, Mhe. Munde Tambwe Abdallah (Mb.), HAKUZUNGUMZA hata mara moja. Hivyo yote yanayosemwa dhidi yake ni uzushi na uongo wa kupindukia.
Nne, Mhe. Bernard Membe (Mb.) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ni rafiki yake mkubwa na wa karibu sana na kama ingetokea akasemwa kwa nia ya ubaya ama kumharibia sifa na yeye akiwemo kwenye kikao hicho, bila shaka yoyote ile angesimama kumtetea. Hivyo hili la Mhe. Membe kusemwa, halikuwepo na ni UONGO wenye nia ovu ya kuwagawa wanaCCM katika makundi "hasimu ya kulazimisha" ambayo hayapo.
Tano, anawataka watu wenye mradi wa kumchafua wakome mara moja maana mradi huu ni dhahiri kabisa haujawalipa mpaka sasa na kamwe hautowalipa. Kama ni vita za Urais ama Ubunge basi wasubiri 2015 watapambana. Taarifa hizo za kizushi zilizosambazwa na namna zilivyowekwa ni wazi kabisa zinalenga kumchafua Mhe. Bernard Membe (Mb.), ambaye ni rafiki yake wa karibu na anatajwa tajwa kuwa na uwezekano wa kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015, na kwa maana hiyo haihitaji akili ya Albert Einstein kubaini kuwa ni nani aliye kazini kwenye hili. Ametutaka tuwaambie hao watu kuwa yeye hayuko tayari kamwe kumuunga mkono mgombea wao, mwenye tuhuma za kifisadi, ambazo hazikwepeki na hazisafishiki, mwenye tamaa ya mali na madaraka isiyokoma na kwa kuwa yeye siyo mnafiki, analiweka wazi hili. Na kwamba kama ikitokea kweli Mhe. Bernard Membe (Mb.) akachukua fomu ya kuwania Urais yeye Mhe. Dkt. Kigwangalla atakuwa tayari kumuunga mkono na kumfanyia kampeni ya kufa na kupona kwa kuwa anaamini katika usafi na uzalendo wake, umakini wake na uwezo wake wa kazi. Na kwa kuwa anaamini kuwa kama Mhe. Membe atakuwa Rais, basi nchi itakuwa kwenye mustakabali mwema.
 
Anawasishi wanahabari kusimama kwenye weledi na kuacha kuandika mambo ambayo hawana uhakika nayo na bila hata ya kuwahoji wahusika.
 
Taarifa hii imetolewa leo Tarehe 24/Mei/2013 na;
TeamHamisiKigwangalla
Ofisi ya Mbunge,
Jimbo la Nzega.


--
"Vision is the ability to see the invisible!"
Hamisi A. Kigwangalla, MD, MPH, MBA
P.O.Box 22499,
Dar es salaam.
Tanzania.
Phone No: +255 754 636963
                +255 782 636963
website: http://www.peercorpstrust.org/ or http://www.hamisikigwangalla.com/
Email: hamisi.kigwangalla@peercorpstrust.org or info@hamisikigwangalla.com
Skype ID: hkigwangalla
Blog: blog.hamisikigwangalla.com 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
mailto:wanabidii%2Bunsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mailto:wanabidii%2Bunsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 



--
Wasalaam,
 
Denis Matanda,
Mine Planning Supt,
Tanzania.
 
" Low aim, not failure, is a crime"
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 


0 comments:

Post a Comment