Sunday 12 May 2013

Re: [wanabidii] Mh Zitto sijakuelewa

Mngonge
Kama hujui nakushauri ukae kimya kama wenzako tunavyofanya siku hizi.





Walewale.



From: mngonge <mngonge@gmail.com>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Saturday, May 11, 2013 1:31 PM
Subject: Re: [wanabidii] Mh Zitto sijakuelewa

Uzoefu unaonyesha tatizo lipo kwa waislam wenyewe zaidi kuliko serikali. Kwani tatizo ni nini kama waislamu wote kwa ummoja wao wakaamua kuunda ummoja mwingine ambao unakubaliwa na pande zote, na kuiambia serikali kwamba ndicho chombo wanachokitambua
?
Nasema tatizo lipo kwa waislam wenyewe kwa sababu vipo vikundi vyenye sera ambazo wanajua fika ni zao wenyewe na wala hawakubaliani na wenzao. Vikundi hivi ni vidogo lakini vina nguvu kuliko waislam wote na ndivyo vinavyolalamikia BAKWATA. Hadi unaonekana kama mchezo wa madaraka zaidi kuliko haki za waislam. Ilifika mahali misikiti ikaanza kutekwa na vijana na kuwaweka pembeni wazee. Kijana unateka msikiti ambao hujui ulijengwa namna gani hadi ufike hapo ulipo kwa sababu gani? kama siyo kwamba kuna harufu ya vifedha vya kuwaamasisha vijana ni nini? Waislam kuweni macho na watu hawa wenye malengo yao lakini wanataka kutumia mgongo wa uislam. Mambo gani ya kugombania madaraka kwenye huduma za imani?


2013/5/7 Juma abdallah <juma.abdallah@huawei.com>
Paul;
Mi sikuisikiliza huo mchango wa Zitto ila kama kaongea hivyo yuko sahihi kabisa na huo ndo ufumbuzi sahihi.Kwa muda mrefu serikali imeng'ang'ania kuitambua Bakwata pekee kama chombo cha kusemea waislamu wote wakati Bakwata hakikubaliki na asilimia kubwa ya waislam.Matokea yake serikali inapokuwa imekubaliana na Bakwata katika utendaji na maamuzi yanayohusu waislam,matatizo yanaibuka kwa waislam kupingana na maamuzi hayo.Ukweli ukubalike kwamba si waislam wote wanaongozwa na Bakwata,kuna vyombo vingine na kwa serikali kukataa kuvitambua matatizo haya ya mkaranganyiko wa makubaliano utaendelea milele.Ifike mahala taasisi nyingine zitambulike Zitto yupo sahihi.
Ushauri wangu usichanganye mambo,UAMSHO si taasisi ya Kiislam ina mambo yake haiusiani na waislam,pili unaposema vikundi vya kigaidi na kuusisha uislam unapoteza muelekeo na kuwa kama umekurupuka au taja taasisi ya Kiislam unayoiona wewe ni ya Kigaidi..Taasisi za Kiislam na Mihadhara ni vitu tofauti jipange unyooshe maelezo,unachanganya habari.
//Maoni yangu binafsi.
 
From: wanabidii@googlegroups.com [mailto:wanabidii@googlegroups.com] On Behalf Of paul chilewa
Sent: Monday, May 06, 2013 8:06 PM
To: wanabidii blog
Subject: [wanabidii] Mh Zitto sijakuelewa
 
Nimekusikiliza ukichangia budget ya mambo ya ndani, mwanzoni nilikuelewa uliposisitiza umuhimu wa viongozi hasa wa kisiasa kutoa matamko yanayo wagawa wananchi hasa kuwagawa kidini,ulichonichanganya ni pale ulipo sema serikali inakosea kuongea na BAKWATA kwani sio chombo kinachokubalika na waislamu wote,inawezekana ni kweli kutokana na utafiti wako lakini pengine unguzitaja taasisi nyingine zilizo omba kuongea na serikali sikakataliwa na ni kwa masuala yapi kwani kama sijakosea nadhani ni serikali hiyohiyo iliyoongea na waislamu ambao sio BAKWATA na kuwapa chuo cha TANESCO kama sija kosea na kuwa chuo cha kiislamu Tanzania.Mimi nadhani ungetoa mfano wa tasisi hizo badala ya kuitaja BAKWATA kutokubalika na kuacha kutaja taasisi nyingine zilizonyimwa haki hiyo ya kuongea na serikali.Vilevile unaposema serikali isijihusishe na masuala ya kidini hukufafanua najua muda  wa dakika tano hautoshi lakini nivizuri ukawaeleza watanzania kujihusisha kivipi ili tupate tafsiri sahihi.Mimi binafsi serkali kusaidia taasisi ya kidini kama ya kiislamu kupata eneo la kutoa huduma za kijamii kama elimu(Chuo cha kiislamu ni sahihi) lakini kwa uendeshaji dini pengine inaweza isiwe sahihi.Nahisi badala ya kusaidia kutatua tatizo wewe ndio unamwaga petroli Mh tueleze hata muamsho na vikundi vingine vya kigaidi navyo vipewe nafasi mimi binafsi nadhani sio sahihi,Mwisho tuambie grievancies unazotaka serikali kushughulikia nizipi au ni zile tunazosikia kila siku kwenye mihadhara?
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 


0 comments:

Post a Comment