Atang'oaje Camera Sulle kama ziikiwa juu ya highest point pande 4 za paa au ghorofa? Mbona Ulaya ambako kuna kila aina ya teknolojia hawang'oi? Maana itabidi kwanza apande juu ya paa au aingie ndani huko computer room azime system na hapo inabidi aingine ndani ya fence na jengo au apande ilipo camera aifunike-juu ya jengo!! Kama majengo ya jirani nayo yana Camera-atazima camera ngapi? Wizi umekua kiteknolojia na wenye mali, majengo nao wakue na milingoti ya umeme/simu barabarani nao police was usalama barabarani, JWTZ watumie hizi teknolojia waweke camera katika milingoti barabarani au majengo yao. Hivi wakitumia google camera muda walipochoma hawatoona huyo mwanga akienda eneo hilo? Usalama wa nchi unakuwaje mpaka kituo cha police kinavamiwa, nyumba ya Mbunge, mahakama etc hakuna hata camera ya solar kama umeme hakuna, betri zipo pia za alternative power? mbona twacheza na usalama? Hata hao FBI wakija-watapiga ramli kwa manyaunyau kujua issue wakati vya kuweka vidhibiti vya monitoring usalama hatuna? Au vipo hatujui ni siri? Sasa tunawasakaje miezi na miaka kama tunavyo na bado hatuwajui? Watu wamejaa ubinafsi kwani utaona hata kule wanakopigana ambako dini ni moja-wanawake na wasichana wanabakwa sio tu kuuawa. Familia nayo inawaua kwa hadhi ya familia wakijua wamebakwa. Sasa, Janjaweed wa N. Sudan anambaka msichana S. Sudan huku mbakaji anasali kutwa mara 5 na anapigana kwa jila la Allah! Jee hapa DINi ipo wapi na anabaka? Vitoto vidogo visichana vyeusi Sudan ya Kusini vimebeba vitoto vya kiarabu ktk umri mdogo kutokana na kubakwa! Au anapigana Afghanistan, Syria, Mali-anabaka na kuua anarusha jambia anatoa roho ya mtu na anaua akimtaja Allah!! Mungu gani anakutuma ufanye hivi? Hii haiji akilini kama haya ni mapigano ya KIDINI-ni ubinafsi tu wa binadamu. Ni kama ile ya Mbagala unachoma moto, unaingia kanisani unaiba vifaa unapeleka nyumbani (Unampeleka Yesu unamkaribisha home kumtoa kanisani). Maana vifaa vya kanisa la Yesu umepeleka nyumbani huku umechoma moto kanisa lakini umebeba vitu umeiba. Hii ni Njaa. Ila-mambonde hayo ya Mbagala, Mkuranga, Pugu, Kisarawe huyaoni ukalima na kupata chakula kutwa upo barazani utaranta wa Manchester, simba , yanga, makanisa na uonevu. ukienda Kisiju ardhi bwerere msukuma anahamia na mifugo, kulima na kukuuzia mihogo; mikorosho ipo ktk majani na mabonde ya chepechepe yameota magugu msukuma kaingia anayakausha na mifugo. Anakata miti anauza mkaa anakupa gunia 2 za mkaa uuze; analima mihogo na viazi na kukupa lita ya maziwa daily unaona umeukata. Jitume na somesha. Hakuna dini inayoruhusu uue na ufanye uchafu kwa jina la Mungu. Hawa wachomao makanisa au mahekalu ni njaa tu, bangi na unga umewaharibu akili. Pamoja na kuwa kuna uwezo wa kutengeneza magobore vijijini lakini wapiganaji wakiona hawapati silaha, chakula na misaada yoyote, hawawekewi hela bank na hao wanaowatuma labda wataacha. labda ukiripua kanisa-bank transfer ya mamilioni inaingia bongo account unaganga njaa. Haya yaangaliwe. Ufike wakati nchi za ulaya sisipokee wakimbizi, isiwauzie silaha nchi za africa na bara la Asia, UN iache kwenye nchi zipiganazo zijimalize zenyewe bila misaada labda wataacha. Faida gani miji ya Somalia, Syria kuwa maghofu? gharama ya miaka/karne ya kujenga miji hiyo ya maghorofa kama Libya, Syria na sasa kubomoa. Vizazi vijavyo vinavuta moshi wa sumu-watakuja kuzaa watoto vilema tu. wataijenga tena Syria kwa miaka mingapi? Kwa kumuua mwana maendeleo Gadafi-wamepata nini Libya mbona hakujatulia? wamemuonea tu kijana wa watu ambae alikuwa mwanamapinduzi halisi. Ya Gadafi imeumiza sanasana. laana yake wataibeba maisha yao yote. Mnataka nini watanzania wakati mnaona wenzetu wanavyokimbia na kuacha watoto na wazazi nyuma, anatupa mizigo hajui aende wapi. porini kuna simba, fisi chui watakutafuna. Ubakaji congo HIV/AIDS kila askari kutokana na ubakaji na kila kaya watu wameambukizwa. Ubakaji kwa sasa sio limited kwa wanawake tu-si tunawasikia wasemavyo ni wamama na wababa. tena bora wamama wanapata huduma wababa wanakufa kisaikolojia kujitokeza na kubata huduma. Ndio mwataka haya yote? PUMBA Tupu vichwa vyetu tumendau mapambano ya kivita na kuuana badala ya kujenga nchi. Tu wavivu, hatuna malengo ya maisha yetu. penye kila kitu unakuta tumebweteka ni malumbano kisiasa na kutokuzingatia matumizi endelevu ya raslimali, visingizio kibao. Kichefuchefu. Nchii hii inataka dictator kuliko Kagame. kama unataka uchaguliwe uwe Rais 2015, usiahidi kutuachia tubweteke-ahidi kuwa utahakikisha kila mtu anafanyakazi, anasoma shule zenye karakana za ujuzi sio kusoma nadharia tu; uwekezaji utatoa direct benefits`kwa vijiji asilimia kadhaa na kutakuwa na auditing vijijini hadi kitaifa; watu watazingatia matumizi endelevu ya ardhi na raslimali zake pende wasipende mpaka kufuga kisasa sio kuzurura na kuathiri mazingira na kilimo; upunguzaji mifugo kuzingatia uwezo wa ardhi itakuwa ni LAZIMA; kutumia vifaa vya kisasa kwa wachimbaji wadogo wadogo na kutumia protective gear LAZIMA au ulazwe ndani na kuchimba madini ni kwa kuunda vikampuni na kuviandikisha ili mpate mikopo. Hii itapunguza uharibifu mazingira, uchafuzi wa maji na uharibifu afya na mikopo itatolewa na kufirisiwa wakilewea pombe wasichimbe madini.Biashara ni kuzingatia misingi yake na mahala palipo ruhusiwa sio kujaa barabarani mpaka mkandarasi anashindwa kuchonga barabara muda unapita tumejitandara na vibanda vyetu hatuondoki kiasi kwamba hata kupiga mitaro ya maji anashindwa. ahidi uzalishaji mali na nidhamu ya utendaji wa kikazi, mazingira na mipango ardji mijini na vijijini. Kusiwe na kuzurura vibaba limebeba sidiria na sumu ya panya kutwa anatembea kilometa 5-50. Angekuwa Ruangwa valley angetumia nguvu hii kulima ekari ngapi? fungua mashamba ya JKT, wape trekta, jenga mabanda na mahema tuwasombe tukalime huko, packaging ya mazao, dege la jeshi linakuja linazoa, yanashushwa KIA yanakwenda kuuzwa nchi zenye njaa. Ukikutwa unazurura mjini ukamatwe. Masoko yalipo mitaani yanafikika. Tuwaondoa hawa wa barabarani wakae mahala walipotengewa ili wakandarasi wafanye maendeleo ua ukarabati miundombinu ikamilike on-time. Bajaji na bodaboda kupita njia ya miguu na biashara kupangwa njia za kupita watu ikishughulikiwa nasi wahusika tukizingatia nidhamu zinazotakiwa hizi chuki za kijinga za kupigana na maofisa afya, mgambo, polisi zitakwisha ili tufanye ya maendeleo. Kuchoma moto makanisa sio solution ya matatizo tunayoyaanzisha wenyewe. --- On Sun, 19/5/13, Emmanuel Sulle <esulle17@gmail.com> wrote:
|
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment