Monday 20 May 2013

Re: [wanabidii] KUTOKA TANGA - Makanisa mawili yachomwa moto


Nimekuelewa. Poa.
Ila unapojiripua, ukakatika miguu bila ya kufa ukakaa hai, hao waliokutuma na Imani iliyokuganda hawakusaidii/haikusaidii. Unabaki unasota saidia baba, saidia mama!! Walioahidi kuilipa familia yako kama utafanikiwa kujiripua, kuua na kufa-wanalala mbele- hawalipi hela. Hii tumeisoma katika magazeti na taarifa mbali mbali nayo ipo. Hao mabikira saba utapewa kweli na peponi hakuna ngono? Hakuna aliyekwenda peponi akarudi anyway akatueleza kama huko kuna ngono hadi hao mabikira saba iwe issue.

Zipo dini duniani za waumini kutembea bila ya kuvaa nguo na ktk mahekalu kuharibu vichanga kwa ngono. Nao wana Mungu wao na Imani yao inayotaka kutembea bila ya nguo iwe haki ya binadamu na kuabudu lolote kwa Imani yako iwe haki. Dini ni OPIUM, Imani ndio kitunguu saumu chake.

Hata Kinjikitile Ngware aliwaambia watu wake kuwa bunduki ya mzungu itageuka maji na akiipiga ikalia semeni 'Maji' tutashinda na vita ya Maji maji ikamaliza watu na ni mfano mmojawapo wa Imani.

Magazeti yanatangaza Imani za waganga na waganga wa kienyeji hufanikiwa kurubuni watu wakaamini na kuuana, kuua albino, kuchomeana nyumba kwa imani ya kichawi.Utajiri wa harakaharaka bila masharti, hela za jini chuma ulete, dawa ya kupasi mtihani ukawa wa kwanza hata kama umefeli, kumshika mume asitoke na akupe kila utakacho; dawa ya kufuta kesi mahakamani; kufanikiwa maishani, dawa ya biashara (sio usome ujasiriamali- no).  Issue ya Imani ni tatizo hasa kama Imani yenyewe ni POTOFU.

Na ndio maana nikahoji-unapoua unataja allah, unaingia nyumba ya mtu adui yako unamkomoa kwa 'kubaka akina mama, visichana, akina baba'-Imani  ya Allah na kwenda uwinguni ipo hapa? Huu ni Ubinfasi, dini na Imani yake 'Kisingizio'.

Hebu ona Mzee Karume alivyouawa Msikitini-Nyumba ya Mungu. Ona kazi aliyofanya. Majumba aliyoanzisha kama ya Libya yamemaliziwa juzi baadhi yake miaka yote yalikaa hivyo maendeleo aliyokuwa ameanzisha. Ona Libya-wamepata nini na imani uisemayo? Ona Misri. ilikuwa mfano. Imesomesha madaktari wapo dunia nzima, utalii masaa 24 maduka Cairo hayafungwi usiku, mchana. Sasa hebu ona. Rais aliyeingia alivyo mkali kukemea na kutawala kimabavu ili awaweze. Bado hayajaisha pamoja na kuua na kuuana. Watu wasio na hatia unawaua, umasikini palepale au kuongezeka.

Kwani vita inachagua. Kama Boko Haram na Janjaweed na wengineo ni Imani ya uwingu inawasumbua-mbona jamaa zao wakipata nafasi ya kukimbia nchi nchi wakimbiliazo ni zile zenye katiba ya 'msalaba?' Hii ndio ninahoji kama ukristo ni tatizo kwao. Chakula cha kuganga njaa kinatoka huko misalabani na mpaka sasa wamefikia kulisha watu chakula cha mifugo. Bora mtu asife ale hiki cha mifugo kisicho madhara kuliko afe kabisa kwa kukosa kula na unawaona wamepanga foleni. Imani ndio inaponza lakini mifano mbona mingi kama hata ya Kibwetere-Uganda na ya nchi ambazo sasa ni maghofu? Unaona hasa kama imani imewababaisha, nchi maghofu na kila mtu anatengeneza hela zake na kuvamia misafara kupora ili kuishi; kuvamia walimu wanaofundisha wasifundishe na huwakata mikono wakabaki nchini na vilema wengi wakakosa nguvu kazi. Kama issue ni Imani-na kwenda kwa Mungu, kwa nini ukisha kuua unajificha hujitokezi uuawe hadharani ili uende mbinguni? unajificha na ukikamatwa unaweka mawakili huku ukiwa umeua au kuhusika na kuchoma hekalu. Unakana hatia? Hii ni imani ya Mungu au UBINAFSI. Ungejitokeza ukasema ni mimi, nipigeni risasi-wewe unakana japo umehusika. Hata rais wa Liberia aliyeua alikana pia Idd Amin, Sembuse Boko-Haram. Hawaui kwa kujionyesha ili nao wafe waende peponi. DINi Kisingizio-ubinafsi tu. Na ndio maana Mungu kajificha, angejitokeza aseme ukweli wangeaibika wengi kuona kuwa wanachoamini si Kweli, wameongezea chumvi kwa tamaa zao. Kila roho inahaki ya kuishi na kumcha Mungu, Usiue, usizini. Dhambi ya kuua kwa makusudi -haina msamaha.

Tulinde Amani Yetu TZ, tupendane bila ubaguzi. Tuchape kazi ili tuondoe visingizio vya aina yote vitakavyofanya kuoneana. Hii ndio hoja kuu yangu-Adios Amigo!!

--- On Mon, 20/5/13, alexander chipalazya <chipalazya@yahoo.com> wrote:

From: alexander chipalazya <chipalazya@yahoo.com>
Subject: Re: [wanabidii] KUTOKA TANGA - Makanisa mawili yachomwa moto
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Monday, 20 May, 2013, 19:19

Kiwasila,
Hao wachoma mahekalu hawaogopi CCTV nitofauti sana na vibaka, maana wao wanasukumwa na IMANI.  Ndio maana inakua vigumu kushughulikia Boko Haramu, Taleban, Al-qaeda, na Alshababu. Wako tayari kufanya lolote kwa gharama yoyote maana wanaitetea 'IMANI'. Kumbuka wengine wamefundishwa na kushika, 'Ukiua kafiri unaenda ahela na ukijilipua na kuuwa walei na maaskofu utapewa zawadi ya mabikra ahela. Ni imani za jinsi hii ndio zinawafanya watu wasiwaze mara mbili kufanya mauaji yasiyo elezeka.
Alexander


From: Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Monday, May 20, 2013 3:00 PM
Subject: Re: [wanabidii] KUTOKA TANGA - Makanisa mawili yachomwa moto


Angalia faida ya CCTV cameras na ya Video Camera na Camera za Kawaida ktk kufichua uovu. Jamaa kafumaniwa, lakini gari la kumpokea kutoka gholofa la juu liliitwa kumpokea. jee sisi tuna magari namna hii ya vono? uliziona gari za Police USA Boston kulikotokea mripuko ni ya kutisha na kiusalama hali ya juu. Maendeleo kiuchumi na mabadiliko kijamii yaje na maendeleo kiteknolojia.

Pili-Wazo: Kama mpira wa yanga na simba siku moja umeingiza milioni mia tano- si tunaweza kuchangia maendeleo sio kuangalia mpira tu? Makanisa, misikiti inaweza kuleta maendeleo ya jamii zao kwa kuchangia au kufanya au kuandaa mashindano ya namna hii kama ya ushindani wa Simba na Yanga kukusanya mapato ya kujenga na kuongezea michango ya waumini. Twachangia arusi (send in, send-off) na mipira. Twaweza. Chuki na kuchomeana mahekalu why?

Tumejenga kwa miaka 50 bado tupo hapa-tuanze kubomoa inakuwaje tena. Wivu wa elimu ni pamoja nawe kusoma sana, wa maendeleo ni wa wewe kuiga kuyatafuta. Mbona michango ya arusi mikali sana? vipi ukiwa msikitini/kanisani kuchangia shule ya vidudu, zahanati, kisima cha maji. Pili, kila kanisa au msikiti-uwe na borehole ya maji kutoka huduma. Kila msikiti mkuu kikata uwe na shule ya vidudu au ya Msingi na kila wa wilaya shule ya msingi, kimkoa kila dini/dhehebu iwe na secondary na high school moja na kitaifa Chuo Kikuu, hospitali ya Kitaifa. Kila dhehebu linachangia wenyewe kwa toa ndugu au sadaka. Lawama itakwisha. Kila dhehebu linagharimia mfumo wake wa mahakama ambao unatambulika kitaifa kwa ajili ya rufaa ikitakiwa.Vyeti vya ndoa vimekwisha kutolewa kwa madhehebu yote vinatambulika na GVT. Ni mambo madogo tu yakiwa coordinated na walezi kimadhehebu kupata TOT training-Tutapeta kama tutajituma. Maana-hata kwenye dini moja wanapigana anyway na vita haiishi, vilema kila kona hawana msaada, wanateseka. Why tuwaige Alexander?




--- On Mon, 20/5/13, alexander chipalazya <chipalazya@yahoo.com> wrote:

From: alexander chipalazya <chipalazya@yahoo.com>
Subject: Re: [wanabidii] KUTOKA TANGA - Makanisa mawili yachomwa moto
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Monday, 20 May, 2013, 11:54

Kiwasila inauma sana, hakuna maendeleo katika ubinafsi. 

Huu ushauri wako nimuhimu...'Ufike wakati nchi za ulaya sisipokee wakimbizi, isiwauzie silaha nchi za africa na bara la Asia, UN iache kwenye nchi zipiganazo zijimalize zenyewe bila misaada labda wataacha. Faida gani miji ya Somalia, Syria kuwa maghofu? gharama ya miaka/karne ya kujenga miji hiyo ya maghorofa kama Libya, Syria na sasa kubomoa'

Nafikiri UN ikifanya hivyo watu watatia akili. Haingii akilini nchi kama somaliland kutotawalika maana ni kabila na dini moja. Hawa siasa kali wanataka kusilimisha dunia nzima, ila sasa hata mahala ambapo nchi nzima ni islam hakuna amani.
Alexander

From: Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Monday, May 20, 2013 5:23 AM
Subject: Re: [wanabidii] KUTOKA TANGA - Makanisa mawili yachomwa moto


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment