Sunday 19 May 2013

Re: [wanabidii] Kumbe udini una mkono wa nje!

Sasa si aukate huo mkono? Ningefurahi rais wetu kipenzi angesema majasusi wetu wameshadhibiti huo mkono.
Kama kuna mkono wa nje je miguu, kiwiliwili kichwa moyo fijo na ini viko wapi?

Na itakosekanaje kuwepo mikono ya nje ilhali siku hizi FBI ni kama kikosi mojawapo hapa nchini?

Tanzania hoiiiiiiiiyeeeeeeee!


From: Mobhare Matinyi <matinyi@hotmail.com>
To: Wanabidii googlegroups <wanabidii@googlegroups.com>; Mabadiliko <mabadilikotanzania@googlegroups.com>
Sent: Sunday, May 19, 2013 8:49 PM
Subject: [wanabidii] Kumbe udini una mkono wa nje!

Rais Kikwete: Udini unaoibuka una mkono wa nje
 
Dodoma. Rais Jakaya Kikwete amebainisha kuwa vurugu za kidini na kisiasa zinazotokea nchini, zina uhusiano na watu wa nchi za nje.

Alitoa kauli hiyo jana kwenye ibada maalumu ya kuwekwa wakfu kwa Askofu Mkuu wa Sitta wa Kanisa Anglikana Tanzania, Dk Jacob Chimeledya.

Rais Kikwete alikuwa mgeni rasmi kwenye ibada hiyo iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu.

"Wanaohamasisha vurugu hizo ni watu wenye uhusiano ya karibu na watu wa nje ambao mambo yakiharibika nchini watakuwa wa kwanza kupanda ndege, ilhali wakiendelea kutoa matamko ya uchochezi wakiwa nje ya nchi wakati wengine wakiendelea kuumia," alisema Kikwete.
 
Endelea: http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Udini-unaoibuka-una-mkono-wa-nje/-/1597296/1856798/-/10s0m89/-/index.html
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 


0 comments:

Post a Comment