Godfrey, Mimi nimekanusha taarifa kwamba Membe alisemwa kwenye mkutano huo, na kwamba Dr Kigwangallah alisema Mkuu wa Mkoa aondolewe kwa sababu ya uhusiano mbaya na Shehe na kuashiria udini. Dr Kigwangallah alipendekeza viongozi wakuu wa Serikali Mtwara wawajibishwe, - yaani kamati nzima ya Ulinzi na Usalama. Lakini pia Munde hakuwepo kwenye mkutano, sijui angeongeaje mambo hayo, Hawa Ghasia naye hakuchangia hoja yoyote. Kwa kweli uzushi wa namna hii unania ya kuchafua kabisa. Sijui namna ya kuthibitisha hili labda, lakini nasema mbele ya Mungu kwamba huu ni upotoshi mbaya na aliyeandika kama anasoma maneno haya Mungu amsamehe na ampe moyo mpya aache kuchafua wenzake kwa sababu yoyote, hata kama ni mbio za 2015 huu siyo ustaarabu. Hivi kwa nini JF waandishi wengi hasa wale wanaotukana na kuleta maneno ya kuchafua na kuchonganisha wanaandika wakiwa wameficha identity?, na moderators wa JF wanaona sawa tu.. Nawaomba moderators wahamasisheni watu wenu kuwa wao halisi.. Aliyeileta makala hii Wanabidii na Mabadiliko awaambie ukweli kwamba habari hiyo ilikuwa imepotoshwa kwa kiwango siyo cha kuvumilia. Mtu huyo anihitajika kushitakiwa kabisa, japokuwa ni taabu kujua identuty yake.. Naomba nikurejeshe kwenye makala hiyo iliyotoka JF (angalia mandishi mekundu hapo chini - ni ya uongo kabisa). Wapo wabunge wengine wanaosoma ujumbe huu wanajua niyasemayo ni kweli tupu kwa vile Mungu ndiye aongozaye. Hata mwandishi wa ujumbe huo anajua moyoni mwake kuwa aliandika kwa nia mbaya tena akiwa ameficha identity. Godfrey washauri moderators wa JF waondoe post hiyo ya uongo na ya kupaka matope, lakini pia waweke ulazima wa watu kutumia true identy zao, vinginevyo Great THINKERS will always be Great MONGERS Mungu akubariki Ngw'izukulushilinde ================================ Dr. Hii habari imekaaje? imejadiliwa sana Jamii Forum unaweza kutusaidia > kutupa maelezo. > > REF: Wabunge wa CCM > wamemrarua waziri wa mambo ya nje Bernard membe kuwa ni kinara wa Fujo na > vurugu > zinazoendelea mtwara, wa Kwanza > kuchangia alikuwa ni mbunge wa newala ,alisema membe ni mtu hatari na ni > kirusi > Ndani ya chama kwani anamtumia mbunge mtwara mjini murji na misikiti > kumchafua > waziri wa serekali za mitaa Hawa Ghasia, Baada ya munde alifuata Hawa > Ghasia > ambaye naye alimshtutumu Membe kuwa anamfitini kwa kumtumia murji ,na murji > kupiga misikiti anaendesha mkakati kupitia misikiti ,''vurugu za mwezi > January > nyumba yangu pamoja na ya Mhe Anna Abdala zilichomwa moto Mhe mwenyekiti > Jana > tena wamechoma nyumba yangu na ofisi za chama moto nimefanya utafiti > nimegundua > ni waziri mwanzagu ndie anaenifitini kwa wananchi wa mtwara hii ni hatari > sana > kwa mustakabali wa chama na Taifa kwa Ujumla' > > Waziri Ghasia alienda mbali zaidi kwa Kusema Kama investment > membe anazo za kutosha mtwara lakini hazichomwi wala hazirushiwi mawe,hii > inasikitisha ,Wakati Huo Huo mbunge wa nzega Dk kigwangallah > ameitaka serekali imuondoe mkuu wa mkoa wa mtwara Simbakali kwakuwa Hana > mahusiano mazuri na mashekhe na ili mkoa Huo utulie aondolewe mkotoliki > apelekwe > muislamu. > > Alexander ==================================== --- On Sat, 5/25/13, Nicomedes Kajungu <nicomedes76@gmail.com> wrote:
|
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment