Friday 12 April 2013

[wanabidii] Unawaza nini kuhusu suala la kuchinja nyama machinjioni

Wapendwa, kuna suala limeibuka la akina nani wanastahili kuchinja nyama mpaka maaskofu kutoa tamko? Hivi karibuni Umoja wa Makanisa ya Kikristo Jijini Mwanza, umetoa tamko kali kwa kuwataka waumini wa dini hiyo kutokula nyama yoyote iliyochinjwa wa Waislamu.

Tamko hili limetolewa mwisho wa mwezi uliopita na Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Victoria Nyanza (DVN), Boniphace Kwangu, mbele ya viongozi wa madhehebu mengine, katika kikao cha pamoja kilichoketi kwenye moja ya majengo ya Kanisa la Kwa Neema Jijini Mwanza.

Kauli hiyo ya viongozi wa kiroho imekuja siku chache baada ya kuibuka mgogoro mkubwa baina Waislam na Wakristo juu ya nani mwenye halali ya kuchinja nyama hasa maeneo ya Machinjioni.

Mbali na Umoja huo wa madhebu ya Kikristo jijini Mwanza, unaojumuisha Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC), Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), na Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT), umetangaza pia kusudio la kuufikisha mgogoro huo Mahakamani, ikiwa ni pamoja na kuitaka Serikali itafsiri kisheria ni nani hasa kati ya Waislamu na Wakristo mwenye mamlaka ya kuchinja nyama.

–Vyombo mbali mbali vya habari Tanzania

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment