Friday 26 April 2013

[wanabidii] MIAKA 49 YA MUUNGANO. MASWALI SITA

¤Kwenye kuingia mkataba wa Muungano, kwa nini Nyerere alimshirikisha mwanasheria wake Roland Brown wakati Karume alimpa mwanasheria wake Wolfgang Dourado likizo ya muda kwenda nchini Uganda wakati Karume hakuwa msomi ukiachia uzoefu wa kazi ya ubaharia pamoja na umaarufu wa kucheza mpira?

¤Hati ya Muungano ilikuwa na mambo 11. Hivi sasa yamefikia 23 kutokana na kuongezwa na Nyerere taratibu kwa kupitia decree. Je, Karume alijua kuhusu uwepo wa decree kwenye katiba?

¤Mkataba wa Muungano uliridhiwa na Bunge la Tanganyika (tena weekend). Kwa nini Bunge la Zanzibar (Baraza la Mapinduzi) halikuwahi kukutana kuridhia? Je, Muungano ni halali?

¤Karume hakutaka muungano wa serikali mbili. Ilikuwaje Nyerere akakomaa?

¤Kama lengo la Muungano ni regional integration (as opposed to Kwame Nkurumah's notion), kwa nini Muungano wetu haukuongezeka tena tokea 1964 (e.g. Kwa ku-include nchi za jirani e.g. Mozambique au Zambia? Je, ni kwa sababu waliona matatizo makubwa kwenye muungano wetu (kama Ethiopia/Eritrea, Sudan/South Sudan, Gambia/Senegal).

¤Kwa mazingira ya hivi sasa ambayo uwezekano wa kupata rais mzanzibar kuzidi kuwa mdogo, je, muungano unaweza kudumu miaka mingi mingine?

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment