Tuesday 9 April 2013

Re: [wanabidii] Uchambuzi Wa Habari: Viboko Shuleni Au La, Ni Mjadala Wa Aibu!

Wizara imekosa mwelekeo(vision) ya kuleta mabadiliko katika elimu nchini. Watendaji wakuu hawasomi na hawajifunz, bali wanakuwa "reactive" Hainiingii akilini kuwa waziri anaona viboko ni suhulu ya vijana kuwa na adabu na tabia njema.
 
Makongo
 
----------------------------------------------------------------
Japhet Maingu Makongo
Director, Ubunifu Associates Ltd
P.O. Box 32971, Dar es Salaam,
TANZANIA
Website: www.ubunifu.co.tz, info@ubunifu.co.tz,
Tel: +255 22 2762027, Mobile:+255 754 571 256

From: Maggid Mjengwa <mjengwamaggid@gmail.com>
To: mabadilikotanzania <mabadilikotanzania@googlegroups.com>; wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Tuesday, April 9, 2013 10:59 PM
Subject: [wanabidii] Uchambuzi Wa Habari: Viboko Shuleni Au La, Ni Mjadala Wa Aibu!



Ndugu zangu ,

Moja ya habari kubwa leo ni hii;

"Serikali imesema itarudisha adhabu ya viboko kwa wanafunzi shuleni ili kujenga nidhamu na kujituma.Akizungumza Dar es Salaam jana wakati akizindua tovuti ya www.shledirect.co.tz inayowezesha wanafunzi kujisomea kwa njia ya mtandao, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo ilisema kuondolewa kwa adhabu ya viboko shuleni kumewafanya wanafunzi wengi kukosa nidhamu na wakati mwingine kujifanyia mambo kienyeji.

"Wasipotandikwa mambo hayaendi, nilipokuwa mwalimu mkuu nilikuwa nawatandika kweli ndiyo maana shule yangu ilikuwa ikiongoza Mkoa wa Mbeya hivihivi hawaendi..." alisema huku akishangiliwa na wageni waalikwa." ( Mwananchi, Aprili 9, 2013)

Nionavyo;

Tunarudi nyuma miaka 50 badala ya kwenda mbele. Kuna wengi kama mimi tusioamini, kuwa, kumchapa mwanafunzi bakora ni kumsaidia kujenga nidhamu na kujituma.

Kinyume chake, kama ni nidhamu, utamjengea nidhamu ya woga na kufanya yale ambayo anadhani unataka ayafanye na si kuwa ayafanye kwa faida yake na jamii hapo baadae.

Viboko vinamfanya mwanafunzi asijiamini na hata akose uwezo wa kudadisi. Bado nakumbuka, kuwa nikiwa Darasa la Tano ilinitokea nikachapwa bakora darasani kwa kosa la ' kumdadisi sana mwalimu'. Mimi nilitaka kupata ufahamu zaidi lakini mwalimu aliniona nimekosa nidhamu.

Habari hiyo ya kwenye Mwananchi inazungumzia mpango wa kurudisha sheria ya adhabu ya viboko wakati kimsingi watoto wetu wanachapwa viboko mashuleni kila kukicha.

Wanafunzi kukosa nidhamu na kutokufanya vizuri kwenye masomo inachangiwa na mambo mengi. Tuanze kuyaangalia hayo kwanza kabla hatujawahamasisha walimu wakate bakora za miti ya mipera kuwachapa watoto wetu.

Na kwa Waziri mwenye dhamana kuonyesha kushabikia watoto kuchapwa bakora si kitu kingine bali ni jambo la kusikitisha sana. Na mjadala wa kama watoto tuwachape bakora au la, katika wakati tulio nao, ni mjadala wa aibu- A shameful debate!

Maggid Mjengwa,

Iringa.

0788 111 765
http://mjengwablog.co.tz/
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 


0 comments:

Post a Comment