Thursday 21 March 2013

[wanabidii] Taarifa ya Kufukuzwa kazi Wafanyakazi Waandamizi 7 wa Wizara ya Ujenzi, TBA

Yah:  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Wizara ya Ujenzi na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) imewafukuza kazi na kusitisha mikataba ya Wafanyakazi Waandamizi saba wa Wizara na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa tuhuma za ubadhirifu na utendaji kazi mbovu.

 Hatua hiyo ni sehemu ya dhamira ya Wizara ya Ujenzi ya kusafisha Wakala zake na  kuongeza ufanisi.

Katika nyakati tofauti Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi amekuwa akipokea tuhuma za vitendo vya ubadhirifu miongoni mwa watendaji waandamizi katika Wakala zinazotoa huduma chini ya wizara hii.

Kufuatia tuhuma hizo Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alifanya ukaguzi maalum katika ofisi za  TBA Mkoa wa Dar es salaam na Katibu Mkuu wa wizara Balozi Herbert E. Mrango na Mtendaji Mkuu wa TBA Arch. Elius Mwakalinga waliunda Kamati za kupitia taarifa za CAG na taarifa nyingine. 

Kamati hizo zimeweza kubaini kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa taratibu za fedha, manunuzi na uendeshaji.  

Maafisa waliofukuzwa kazi ni pamoja na Bw. Charles Gabriel Lyatuu ambaye alikuwa ni Meneja wa TBA mkoa wa Dar es Salaam; Bw. Ladislaus I. Kapongo aliyekuwa Mhasibu Msaidizi (TBA mkoa wa Dar es Salaam) na Bi. Agness F. Chambo aliyekuwa Mhasibu Msaidizi (TBA mkoa wa Dar es Salaam).

Aidha, kwa Mkurugenzi wa Biashara na Fedha Bibi Yona Orida na Injinia Charles Makungu ambaye alikuwa ni Mkurugenzi wa Miliki wameondolewa katika nafasi za uongozi  walizokuwa nazo TBA.

Hatua zaidi zilizochukukuliwa ni kuwashusha vyeo Meneja wa Mkoa wa Pwani Bibi Esteria M. Nyamhanga na Bw. Samwel C. Samike ambaye alikuwa ni Meneja wa TBA mkoa wa Mbeya.

Hatua hizi zimechukuliwa kunatokana na watendaji hao kuhusishwa na tuhuma za ubadhidilifu ambazo zimebainika kufanyika katika taasisi hiyo. Maeneo ambayo yamebainika kuwa na ukiukwaji mkubwa ni pamoja na kufanya malipo kwa kutumia mikataba isiyosainiwa na pande zote,  kufanyika malipo kinyume na taratibu za manunuzi na hata malipo kufanyika kwa fedha taslim kinyume na taratibu. 

Aidha, eneo la manunuzi ya viwanja kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya TBA pia yameonyesha kuwa na vitendo vya ubadhilifu na ukiukwaji wa taratibu.  Vipo viwanja vilivyobainika kununuliwa nje ya taratibu, baadhi ya nyaraka kuonyesha ukubwa tofauti na ule uliolipiwa, kununua maeneo yasiyofaa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Serikali, kuongeza bei na kufanyika kwa malipo kabla ya mikataba kusainiwa.

Hatua zilizochukuliwa ni muendelezo wa juhudi za Wizara za kuhakikisha kuwa maeneo yote yanayoashiria kuwa na utendaji ulio nje ya maadili yanafuatiliwa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria na taratibu za utumishi wa umma.

Aidha, ili kuboresha ufanisi katika Wakala hivi karibuni waliteuliwa Mameneja wapya 15 wa TEMESA katika mikoa mbali mbali hapa nchini ikiwa ni pamoja na kuwahamisha vituo mameneja wengine.

 Kwa upande mwingine, ajira za Watendaji katika vituo vyote vya mizani tayari zimetangazwa na kwa sasa kazi ya kupitia maombi yaliyowasilishwa inakamilishwa ili kuhakikisha kuwa watendaji wasio waaminifu hawapati nafasi katika maeneo hayo ambayo yamekuwa yakilalamikiwa kwa vitendo vya ubadhirifu.

Wizara itaendelea kuchukua hatua za aina hii pale ukiukwaji wa sheria na taratibu za utumishi wa umma utakapobainika.

Taarifa hii imetolewa na;

M.S. Ntemo

MSEMAJI WA WIZARA YA UJENZI

Source: http://www.wavuti.com/#ixzz2O9n1fy00

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment