Thursday 7 March 2013

[wanabidii] Mwanamme Jiulize, Ni Lini Mara Ya Mwisho Ulifungua Daftari La Mtoto Wako?

Ndugu zangu,
Siku hii ya Kimataifa ya Wanawake haifai ikapita bila kujadili masuala ya msingi yenye kumhusu mwananmke na mahusiano yetu; wanawake na wanaume hususan kwenye kusaidiana malezi ya watoto wetu.

Kwa mwananme, mara nyingi jukumu la kumlea mtoto anamwachia mwanamke, haya ni mapungufu. Haitoshi tu kwa mwanamme kuacha hela ya chakula na mboga nyumbani. Kuna kufuatilia maendeleo ya watoto, ikiwamo shule.

Nitoe mfano, jana nikiwa hapa Morogoro kamanda wangu mmoja amenipigia simu akiwa nyumbani Iringa kuniomba nimsaidie na kazi yake ya shule kuhusu historia. Ananitegemea pia kuwa ni msaada kwake kwa mambo ya shule. Hivyo, ikanibidi niwaombe radhi wenzangu kuwa nisingekuwa nao baada ya saa kumi na mbili jioni kwa vile nahitajika nirudi nilipofikia na kuanza kazi niliyopewa na mwanangu. Kumsaidia kufafanua masuala ya historia.

Hoja yangu hapa, ni kuwa wanaume, pamoja na majukumu yetu mengi, tuna wajibu wa kutenga muda nyumbani walau wa kuwauliza watoto wetu juu ya maendeleo yao ya shule. Kuyaangalia madaftari yao pia.

Na hapa mwanamme uanze kwa kujiuliza; Ni lini mara ya mwisho umeliangalia daftari la mtoto wako? Au ni kazi uliyomwachia mkeo tu?

Happy International Women Day!
Maggid Mjengwa,
Msamvu.
0788 111 765
http://mjengwablog.co.tz/

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment