Friday 8 March 2013

[wanabidii] Kenyatta kuitawala Kenya

Hadi usiku wa manane kwa saa za Afrika Mashariki, Uhuru Kenyatta alikuwa amemwacha Raila Odinga kwa kama milioni nzima huku zilizobakia zikiwa hazina dalili za kuziba pengo hilo.
 
Shughuli itakuwa imekwisha kufikia asubuhi kwani kuna uhakiki tu unaofanyika sasa, na Uhuru amevuka 50% na watu wake makini wamekuwa wakisherehekea kwenye chuo kikuu kimoja.
 
Hongera Wakenya kwa kufanya uchaguzi kwa amani ukiondoa ule upuuzi wa ki-al Shabab/al Qaeda wa Mombasa ulitokea alfajiri ya Jumatatu.
 
Tanzania, sasa ni zamu yetu: Ama tuwe kama Kenya ya 2007/08 au tuwe kama tunavyodhaniwa.
 
Kila dalili inaonesha kwamba tutakuwa Kenya ya 2007/08 - kazi kwetu!
 
Matinyi.

0 comments:

Post a Comment