Kugombea Urais kuwe na umri wa mwisho. Vijana wataingia lini? Kuna nini huko madarakani hata uwe mzee unataka bado ugombee kama Mugabe? hivi Africa ina nini? Mbona watu hupenda madaraka sana kuliko kuwa chini na utajiri wao kusaidia maendeleo. Ningekuwa na hela na ni mbunge tajiri, ningerudi jimboni kwangu nikakaa huko na kukufanya heaven katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi, kielimu wengine wakaona wivu na kuiga mfano. Na ningechaguliwa mpaka ninakufa kuingia kaburini. huenda wasingenizika bali kunikausha tu na kuniweka kwenye kioo wanitazame daima niwe Mungu wao. Badala ya kung'ang'ana kwenda juu-rudini chini majimboni mkawawezeshe na hiyo mihela kama kweli ipo. Mbona tunaona wafugaji watoto wanasomea chini ya mti na wamevaa lubega, mifugo inatolewa huko inakwenda nchi nzima watu wanachapwa viboko bila sababu wakati wenye mahela wapo lakini hawachangii maendelehini endelevu makwao? Mnawasifu utajiri, umahili wa kazi au utendaji. Huko vijinini kwao kulikoni? Kuna kilimo na ufugaji wa 600 AD, kinyesi mpaka mlangoni mpaka serikali inawalazimisha kunywa dawa wa vkuzuia upofu kupunguza vilema na wengine kulazimishwa kula za matende kuzuia neglected tropical diseases ambazo desturi na tabia zetu ndio zinaziweka. Mtu wanawake 10 (na wa mtandao pia wapo) kuambukizana ukimwi tu hii; watoto 100 wajukuu 300 karne hii?? Mbunge yupo wapi? Kisha bi mkubwa kucha kuchapa wake wenza wadogo!! karne hii! Vijisenti hivyo na mihela ya utajiri mbona hajiweki piped water schemes au majosho na dip za mifugo ili waweze kutulia wasiharibu maendeleo kwingine na wafuge kisasa, kulima kisasa? Mbona visent havitumiki kuunganisha wajasiriamali jimboni vijana kibao mpaka kelele zipigwe kitaifa? why? Tuonyesheni mfano mlipo kuwapa misaada na mikopo wajiajiri hao vijana na wastaafu katika kilimo cha mazao ya kuuza, mboga, matunda, tree (asali) and livestock products. Wakanunua label wakafunga mazao kupakia JK Nyerere au KIA na label ya TZ sio ya Kenya. Hao watendaji mbona hatuwaoni ktk haya bali ni kelele za ajira kwa vijana, wasomani wamalizao vyuo, hawa na waleetc? Mbona hawayafanyi kwao tukaiga kama tumuonavyo mzee Mengi na Mitaji ya Vikoba, vilema etc? Sifa iende na utendaji sio ufokeaji au matangazo ya maneno vitendo vichache. Tuonacho ukifika vijijini maeneo ya wasifiwa ni kinyesi mpaka mlangoni cha mifugo; kwa wakulima ardhi kipara haitoi mazao kinyesi kipo cha bure hapeleki shambani. Analima kilimani bila kupiga makinga maji. Nyumba ukuta wazi unamchungulia ndani na udongo hanunui maji ya mabwawa yapo hata ya visima vya kienyeji. Kaezeka makuti/nyasi hakufunga kikamilifu upepo mdogo ukija paa linaondoka. Kaishi miaka 70 hapo alipo au zaidi lakini nyumba ipo wapi hana hata miti ya kuzuia upepo mkali usimuathiri na miti ya kivuli au matunda kuzunguka nyumba hana bali huenda kukata miti ya shule waliyopanda wanafunzi kinyemela usiku apate mijengo. Kwake nyumba ipo uchi hana na akiokota mbegu akizitupa tu zitaota kama zilivyoota shule kupangea mstari unaopendeza. Diwani, mbunge wapo hapo kijijini!! waziri ndio kwao Kata hiyo. Sifa ziwe za maendeleo kikazi na pale alipo awe mfano. Hii ikiwa kigezo kelele na maandamano yasiyo tija yataisha-Yeye amefanya nini kwake maana mengi yanawezekana pale tulipo ila tu vipofu pia tupo ambivalent. Umaarufu wa ubweteubwete ujue hao wanaokusifu wanaangalia matumbo yao-survival. Wanaopima kwa vigezo-wataacha kukupigia KURA. Yatakushangaza uje ulio kilio cha mbwa mdomo juu. Watakushangilia jukwaani na kujazana lakini hawatokupa KURA. Mifano imeshatokea huko nyuma wabongo kuzukuma gari, kumbeba mtu juu kwa juu etc. Kwenye kupiga KURA hawapo. --- On Sat, 9/3/13, hkigwangalla@gmail.com <hkigwangalla@gmail.com> wrote:
|
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment